AISEE KUMBE RAHA (6)
JINA: AISEE KUMBE RAHA Mwandishi: Pablo SEHEMU YA SITA ILIPOISHIA... ‘’Mmmmh mbona sikuelewi simu yangu unaifanyia vipii??’’chiku akanitandika swali lingine lililosababisha mwanaume nianze kujichekesha huku majasho bado yakiendelea kunitiririka ‘’H..amna baby narushaa nyimboo’’ ‘’mmmh Pablo unarusha nyimboo kwenye simu ya torchii’’…………………… SASA ENDELEA... Swali la chiku likazidi kuniogopesha na mwanaume nikajuta nikishikwa na aibu baada ya kuangalia ile simu ilikuwa ni nokia ya torch ambayo ilikuwa haina uwezo wa kurusha simu.nilimuangalia chiku ambaye alikuwa tayari kashaanza kujiweka sawa sawa kwa kuvaa nguo ya ndani na harakaharaka akanyanyuka na kuanza kunisogelea taratibu huku akiwa na wasiwasi ambao ulikuwa ukinipa wasiwasi na mimi ambaye ile chiku ananifikia karibu ndipo neno delete likimaanisha kufuta likaonekana katika macho yangu ambayo haraka na mimi nikakibonyeza lakini kabla hata sijamaliza kuangalia kama messeji imefitika chiku alikuwa kashafika na kunipokonya simu yake kwa hasi…