NILIFANYA MAPENZI NA MAITI 20 ILI NITAJIRIKE (3)

Zephiline F Ezekiel

SEHEMU YA TATU
TULIPOISHIA...
Baada ya dakika arobaini, basi likaanza kuingia ndani ya kituo kikubwa cha Ubungo, huko, idadi kubwa ya watu ilinishangaza, haikuwa kama Morogoro, watu walionekana kuwa wengi huku wengi wao wakionekana kuwa bize wakifanya mambo yao.

JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈

SASA TUENDELEE...
Niliteremka na mwanamke yule kuondoka, sikuwa na pa kwenda, begi langu mikononi, kwa sababu humo kulikuwa na watu wengi, wa rika zote tena mbele nikiona kuna mikeka, nikasema pia ua, ilikuwa ni lazima na mimi niishi humohumo, hata kwenda huko nje, sikutaka kabisa, kama kula, nitakula humohumo, kama kufanya biashara, acha nifanye humohumo, ila kutoka ndani ya kituo cha Ubungo, nisingeweza, kwani hata kama ningetoka, ningekwenda wapi? Sikuwa na sehemu, hivyo kuishi humo niliona kuwa sulkuhisho. Na humohumo ndipo ningepata huo utajiri.

Nilipokuwa nikiingia ndani ya kituo hicho, moyo wangu uliniambia kwamba inawezekana nilikuwa peke yangu ambaye sikuwa na makazi, niliamini kwamba unapoingia usiku basi watu hao wote wangeondoka na kuelekea nyumbani kwao hivyo kubaki peke yangu kumbe kile nilichokuwa nikikifikiria hakikuwa sahihi kabisa.

Muda ulizidi kwenda mbele, ilipofika saa moja usiku, badala ya watu kupungua ndiyo kwanza walizidi kuongezeka. Nilijiuliza kilichokuwa kikiendelea ni kitu gani lakini nikashindwa kufahamu chochote kile. Mabasi kutoka mikoani yaliendelea kuingia kwa zamu, nilichoka sana, nilihitaji kulala lakini sikujua wapi pa kulala kwani kila sehemu niliyoiangalia pale kituoni ilikuwa na mizigo ya watu hivyo kuwa na wakati mgumu.

“Wewe dada!” nilimsikia mwanaume mmoja akiita nyuma yangu, nilipogeuka, macho yangu yakagongana na macho ya mwanaume huyo.

“Abee..” niliitikia, akanisogelea.

“Wewe ni mgeni mahali hapa?” aliniuliza huku akiwa amenikazia macho.

“Ndiyo!”

“Umetoka wapi?”

“Morogoro!”

“Unaitwa nani?”

“Naitwa Zakia!”

Kwa jinsi nilivyomwangalia mwanaume yule, nilijua tu kwamba alitaka kunizoea na kulikuwa na kitu kingine alichokihitaji kutoka kwangu. Kiukweli nilifanya mambo mengi mabaya, yasiyopendeza mbele ya jamii lakini wakati mwingine nilitakiwa kuyafanya hayo kwa sababu hali niliyokuwa nayo kipindi hicho, ilinilazimu kufanya hivyo.

“Utalala wapi sasa?”

“Sijajua, sina ndugu yeyote yule…” nilimjibu.

Kwanza akaonyesha tabasamu pana, lilinishangaza lakini kitu nilichokumbuka, mwanaume huyu alifanya kama alivyofanya Mudi kwamba kama sina ndugu, basi yeye angejifanya ndugu ila mwisho wa siku alihitaji penzi.

Akaniambia twende sehemu kuzungumza, kwanza niliogopa lakini sikuwa na jinsi, ningefanya nini na wakati nilihitaji msaada mkubwa kutoka kwake? Hivyo nikakubaliana naye. Tukaenda sehemu, ilikuwa pembeni ya duka moja la vinywaji, pale niliona kukiwa na mikeka zaidi ya thelathini ikiwa imekunjwa, sikujua ilikuwa ni ya kazi gani.

“Unajua mpango mzima wa kulala humu?” aliniuliza swali.

“Kulala humu? Kwani kuna watu wanalala humu?” nilimuuliza huku nikionekana kushtuka.

“Ndiyo! Wanakodisha mikeka na kulala, saa kumi na mbili wanairudisha..” aliniambia.

“Wanakodisha wapi?”

“Hapa kwangu…ukitaka nitakupa…”

“Wanakodisha kwa shilingi ngapi?”

“Elfu moja, ila wewe, nitakufanyia bure kabisa…” aliniambia.

Jibu lake lilinipa uhakika juu ya kile nilichohisi juu yake. Sikutaka kukataa, nilikuwa na uhitaji mkubwa wa kukaa jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuutafuta utajiri hivyo nilikubaliana naye. Akanipa mkeka na kunionyeshea sehemu ya kulala, nikaenda, nikautandika na kulala huko.

Maisha yangu mapya yakaanza ndani ya kituo hicho, nilishinda nikiwa huko, sikutoka kwani mambo mengine nilikuwa nikiyafanya humohumo ndani. Mwanaume huyo aliyeitwa Dickson akanitafutia biashara ya kuuza ya kuuza magazeti, kweli nikaanza kuifanya na kuingiza kiasi kidogo cha fedha, hichohicho ndicho nilichokitumia kwa matumizi mengine.

Dickson alinionyeshea upendo wa ajabu, alionekana kuwa miongoni mwa wanaume waliokuwa na uvumilivu mkubwa. Hakuniambia suala lolote la kimapenzi, wakati mwingine nilikuwa nikijiuliza sababu ya yeye kunisaidia, kwa nini mimi? Je hali ingeendelea hivyohivyo au mwisho wa siku angebadilika.

Mwezi wa kwanza ukapita, nilikuwa nikiendelea kuishi ndani ya kituo hicho na kwa kweli sikuwa nimetokea. Ninayokuandikia hapa unaweza ukashangaa lakini ukweli ulikuwa huo. Ulipoingia mwezi wa pili, Dickson akashindwa kuvumilia, akaniambia ukweli kwamba alikuwa akinipenda na alitaka kunioa.

“Kunioa mimi?” niliuliza.

“Ndiyo!”

“Hapana! Haiwezekani…”

“Kwa nini?”

“Dickson, nipo tayari kwako kwa kila kitu isipokuwa mambo mawili tu,” nilimwambia pasipo kumuonea aibu.

“Mambo gani?”

“Sitaki unioe na sitaki uzae nami, ila mengine yote ruksa…” nilimwambia bila kupepesa macho.

Akatabasamu kidogo na kuniangalia kwa macho yaliyoonyesha kama mtu aliyetaka nirudie kauli zangu. Hakuniambia kitu zaidi ya kuondoka kuendelea na shughuli zake huku mimi nikiendelea kuuza magazeti.

Ilipofika usiku, akaniita alipokuwa akilala na kunitaka nimpe kampani kwani usiku huo ulikuwa na baridi kali hivyo nikakubaliana naye na kwa mara ya kwanza kukutana naye kimwili. Moyoni sikuumia, sikujuta kwani tangu nimeingia Dar es Salaam ndiye aliyeonekana kuwa msaada wangu mkubwa.

“Zakia…” aliniita kwa sauti ya uchovu.

“Abee mpenzi…”

“Nataka uwe tajiri kama unavyosema, upo tayari?” aliniuliza huku akiuweka mkono kifuani kwangu. Kabla ya kujibu, nikaachia tabasamu pana.

“Nipo tayari!”

“Kweli?”

“Ndiyo mpenzi! Nimesafiri kutoka Morogoro kuja hapa kwa ajili hiyo tu…” nilimwambia.

“Basi subiri..kesho kuna mtu atakuja, mwambie kila kitu,” aliniambia.

“Anao utajiri?”

“Hana ila ukitaka, anakupa?”

“Kweli?”

“Hakika!” aliniambia huku akiongeza tabasamu usoni mwake. Nikawa na uhakika wa kuuupata huo utajiri.

Nilikaa pale Ubungo na kuanza kumsubiria Dickson ambaye aliniambia asingechukua muda mrefu mpaka kurudi mahali hapo. Kama nilivyokwambia kwamba nilikuwa na presha kubwa, hakukuwa na kitu kingine nilichokifuata jijini Dar es Salaam zaidi ya utajiri tu, hivyo kuniambia kwamba angerudi akiwa na mtu ambaye angenifanya nitajirike, kwangu ilikuwa furaha tele.

Nilikuwa na presha kubwa, kila wakati nilikuwa nikiangalia saa yangu, hakukuwa na siku ambayo niliona mshale wa dakika ukienda taratibu kama siku hiyo, nilikuwa na presha kubwa na kitu nilichokitaka kwa wakati huo ni kuonana na huyo mtu na kumwambia kile nilichokitaka.

Baada ya kusubiri kwa saa tatu ndipo Dickson akarudi huku akiwa na huyo mtu. Alikuwa mwanaume mtu mzima, mwenye ndevu nyingi ambaye alionekana kuwa wa kawaida sana kiasi kwamba nikashangaa, iweje mtu huyo anipe mimi utajiri na wakati yeye mwenyewe alionekana kuwa mtu wa kawaida sana.

Wakati nikijiuliza hayo yote, mwanaume huyo, hata kabla ya kuzungumza nami, akatoa tabasamu pana usoni mwake, tabasamu lililoonyesha matumaini makubwa kwamba nisiwe na wasiwasi kwani tayari nilipata nilichokitaka.

“Naitwa bwana Hassani Mudi…” alijitambulisha huku akiniangalia kwa uso wenye tabasamu hilo pana.

“Naitwa Zakia…” nilimwambia, na mimi nikatoa tabasamu pana vilevile.

Dickson akaanza kuniambia kwamba huyo ndiye alikuwa mtu aliyeniambia kwamba ningepata utajiri kupitia yeye, nilipomwangalia, bado nilikuwa na maswali mengi ambayo yote hayo hayakuwa na majibu yoyote yale.

Huyo mzee akaniambia niende naye pembeni kwani suala ambalo nililitaka halikuwa la kulizungumzia juujuu, ilitakiwa tutulie sehemu na aniambie kila kitu, nikakubaliana naye hivyo Dickson kutulia pembeni akitusubiri.

“Kweli unataka kuwa tajiri?” lilikuwa swali lake la kwanza kuniuliza.

“Ndiyo!” nilimjibu huku nikionekana kumaanisha nilichomwambia.

“Kweli?” aliniuliza.

“Ndiyo!”

“Sidhani kama unataka utajiri…” aliniambia.

“Kweli tena, nataka kuwa tajiri…” nilimwambia kwa sauti yenye msisitizo kabisa.

“Zakia, huna moyo, huna moyo, unaonekana tu…”

“Moyo ninao, nipo tayari kwa lolote lile.”

Niliposema hivyo, yule mzee akaanza kucheka sana, sikujua alikuwa akicheka nini, sijui kama alifurahishwa na jibu langu au la. Nilibaki nikimwangalia kwa mshangao, yeye mwenye aligundua kwamba nilikuwa nikijiuliza mengi kuhusu kicheko kile.

“Eti una moyo! Moyo gani na wakati unaogopa hata mende?” aliniuliza.

“Siogopi mende…nimetoka Morogoro mpaka hapa kwa ajili ya kutafuta utajiri tu, jua kwamba nina kiu ya kuwa tajiri, nipo tayari kufanya lolote ili nipate huo utajiri,” nilimwambia.

“Hata kuua?” aliniuliza.

“Sidhani, ila nikiambiwa kwamba nikimuua huyu napata utajiri, nitaua tu, sitokuwa na budi,” nilimwambia.

Nilichokuwa nikikiongea, nilimaanisha kutoka moyoni mwangu, kwa wakati huo nilikuwa tayari kwa lolote lile, kiu kubwa ya kuwa tajiri ilikuwa imenikamata. Mzee Hassani akaniambia kwamba jioni ya siku hiyo angenifuata hivyo nijiandae kwani kuna sehemu nilitakiwa kwenda naye, hilo halikuwa tatizo, nikakubaliana naye, akazungumza kidogo na Dickson kisha kuondoka, ndiyo kwanza muda huo ilikuwa saa saba mchana.

Aliniacha na mawazo tele, kichwa changu kilivurugika kabisa, wakati mwingine nilikuwa namuamini huyo mzee kwamba angenifanya kuwa tajiri mkubwa lakini wakati mwingine nilikuwa na wasiwasi kwamba asingeweza kufanya hivyo.

Kama kweli yeye alikuwa akitoa utajiri, kwa nini yeye mwenyewe hakuwa tajiri? Kama alikuwa akitoa utajiri, kwa nini Dickson hakuwa tajiri na wakati alikuwa rafiki wake wa karibu? Kila nilichojiuliza, nikawa na uhakika kwamba inawezekana mzee huyo alikuwa muongo.

“Dickson…unamuamini kweli huyu mzee?” nilimuuliza Dickson.

“Ndiyo!”

“Kweli atanisaidia?”

“Sana tu…kuna marafiki zangu kama watano, kawasaidia na sasa hivi ni matajiri wakubwa hapa mjini,” aliniambia.

“Sasa kama yeye anatoa utajiri, kwa nini na wewe asikupe? Au hutaji kuwa tajiri?” nilimtupia swali.

“Nataka!”

“Sasa kwa nini hujamwambia akupe?”

“Basi tu, nataka utajiri ule wa kuutafuta kwa nguvu zangu ili baadaye niwe na ushuhuda jinsi nilivyosota,” aliniambia huku macho yake yakionekana kuwa na jambo lililojificha.

Sikutaka kujali sana, nilichokuwa nikikiangalia ni maisha yangu tu kwani kwenye ridhiki za kuwa na maisha mazuri, Mungu aliwapa wale waliokuwa na kiu kubwa kama niliyokuwa nayo kipindi hicho.

Basi baada ya saa kadhaa, mzee Hassani akarudi mahali hapo na kukutana naye. Akanichukua na kuanza kuondoka naye mahali hapo. Kumbuka kwamba kwa kipindi chote tangu nifike Dar es Salaam sikuwa nimetoka ndani ya kituo kile, hivyo kutoka humo ndipo nikaanza kuona mazingira halisi ya jiji hilo.

USIKOSE SEHEMU IJAYO

Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi

Chapisha Maoni