JAMANI DADA MARTHA... LOOO! (9)

Zephiline F Ezekiel
Mtunzi: 2jiachie

SEHEMU YA TISA
ILIPOISHIA...
Mama Anna akapeleka mkono wake mmoja na kushika maiki akiashiria utayari wake uko wapi.

Roi naye akaunganisha hisia, wakabilingishana mpaka wote wakawa hoi, wanahema tu. Mama Anna akavuta mpira uwanjani,

JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈

ENDELEA...
mchezo ukaanza kupigwa huku ushangiliaji ukiwa mkubwa kwa pande zote mbili.

Maneno yote, mama Anna aliyatumia, Roi akawa kama amepungukiwa akili, alisema yasiyosemwa.

***

Martha alipoona muda unakwenda aliamua kutoka tena akiamini, Roi alishaziona funguo na sasa atapitia nyumbani kwake ili wakutane.

Alipanda Bajaj tena mbele ya wale wapangaji wenzake.

Ile anapotea tu, yule mpangaji aliyepigiwa simu na mama Anna akamtumia meseji mama Anna...

“Martha katoka hapa tena, nahisi anakuja hukohuko.”

Mama Anna hakupata nafasi ya kuisoma meseji hiyo kwani wakati inaingia ndiyo kwanza yeye alikuwa katikati ya mashambulizi uwanjani akitafuta ushindi na alishatangaza kwamba anakaribia kuupata.

Hata alipoupata, Roi hakumwachia ili na yeye apate pointi yake moja ili kusiwe na wa kumzidi nguvu mwenzake. Mama Anna alitumia ufundi kidogo tu, Roi akawa akihangaika mpaka jasho jembamba likamchuruzika, ambapo mama Anna alilimudu kuliondosha kwa taulo.

***

Martha alifika nje ya nyumba na kumpigia simu Roi. Simu iliita kule chumbani, Roi kwa vile alishashinda, akatoka kwa mama Anna na kuiwahi...

“Du! Wajina wako anapiga,” alisema.

“Sasa. Anaweza kuwa nje?” aliuliza mama Anna...

“Inawezekana,” alisema Roi lakini hakuipokea simu hiyo.

Mama Anna naye akakumbuka, simu yake akaifuata, akakutana na ile meseji. Alipoisoma, akamwonesha Roi...

“Martha katoka hapa tena, nahisi anakuja hukohuko.”

Roi alitumbua macho pima, akasimama akiwaza, akasema...

“Kwa hiyo yupo nje hapo?”

“Ndiyo maana yake,” alijibu mama Anna.

Martha alishangaa simu ya Roi kuita bila kupokelewa kwani si kawaida yake.

Akaenda kwenye kile kiduka cha jirani...

“Dogo hujambo?” alimsalimia muuzaji.

“Sijambo.”

“Eti, huyu kaka anayekaa hapa huwa anafika muda gani?”

“Mh! We ni nani kwani?”

“Mgeni wake.”

“Kutoka wapi?”

Tanga.”

Muuza duka huyo alimkodolea macho Martha akiwa anaonekana haamini kama alitokea Tanga. Tanga bila hata kibegi cha nguo!!

“Kwani namba yake ya simu huna?” aliuliza muuza duka huyo.

“Nampigia hapokei. Nikasema nije hadi hapa ili kama anakuja muda huu nimsubiri kama si muda wake nikatafute gesti ya kulala.

Muuza duka huyo alijua kuna kitu kilimfanya Roi asipokee simu. Na kitu hicho si kingine ni jamaa huyo kuzama ndani na mwanamke mwingine aliyekuwa amekaa kwenye benchi nje ya duka lake.

Kwa hiyo uamuzi ulikuwa kwake. Aseme ukweli au adanganye.

Moyoni mwake aliona Roi mwenyewe alitakiwa kuwa muwazi katika mipango yake kuhusu wanawake. Si vizuri kugonganisha...

‘’Mimi nimemwona kaingia ndani muda si mrefu,’ alisema muuzaji huyo.

Martha akashangaa...

“Kwa miguu?” aliuliza.

“Na gari.”

Martha alitupia macho kwenye geti na kubaini kwamba, ni kweli gari linaweza kuwemo ndani halafu mtu aliye nje asilione...

“Aliingia na nani?”

“Mwanamke mmoja hivi. Alimsubiri kwa muda mrefu hapohapo nje.”

“Mwanamke mmoja hivi! Kavaaje?”

“Huyo mwanamke kavaa haya magauni yenu ya siku hizi, marefu mpaka miguuni, amelaza nywele kwa nyuma, mweupe kiasi, ana figa namba nane.”

Kwa haraka sana, Martha alimuweka kichwani mama Anna kwani anakumbuka ndiye aliyevaa hivyo inavyosemwa.

“Huyo ni mama Anna tu. Yaani kumbe...mh! Yaani mama Anna na Roi ni wapenzi? Mbona siamini. Wameanzaje kwanza?”

Martha aliinua simu yake akampigia mpangaji mmoja na kuzungumza naye...

“Hivi unaweza kuamini mama Anna alipotoka hapo kumbe amekuja nyumbani kwa yule mtu wangu?”

“Kweli?”

“Kabisa. Nimepewa ushahidi wote.”

“Kwa hiyo?”

“Wamo ndani na geti limefungwa.”

“Mh! Mama Anna naye bwana. Ana maana gani sasa kufanya hivyo kwa mtu wa karibu kama wewe?”

“Ndiyo hapo sasa. Mimi leo sitoki hapa getini. Nipo tayari hata kulala hapahapa,” alisema kwa uchungu Martha na kukata simu.

***

Roi na mama Anna walikuwa chumbani sasa, kitandani, wakigalagazana kwa mahaba mazito huku mwanamke huyo akilia kilio cha uongo ili kumkoleza zaidi mwanaume huyo pale kitandani.

Wote walikuwa wamelegea macho kwani kwa mama Anna yeye alishajua jinsi ya kumnasa Roi huku yeye Roi akiwa hoi bin taaban.

Simu ya mama Anna iliita mpaka ikakata, ikaita tena mpaka ikakata, ikaita tena...

“Mh! Hiyo simu itakuwa ya umuhimu kwangu,” alisema Roi na kumtaka mama Anna aipokee...

“Hakuna lolote, haina umuhimu wowote, ngoja niizime tu,” alisema mama Anna akiifuata.

Kabla hajaizima aliangalia missed calls akakuta mbili na zote ni za wapangaji wenzake, akahisi kitu. Akampigia wa kwanza...

“Vipi mama nanihii...”

“Mwenzangu, Martha yupo getini. Kasema ana ushahidi umo ndani kwa jamaa yake na hatoki mpaka kesho asubuhi.”

Palepale mama Anna alikata simu, akamwangalia Roi. Naye Roi akamuuliza...

“Vipi kwani?”

“Martha yupo getini. Lakini ishu si hiyo bali amejua mimi nimo ndani, eti ana ushahidi.”

Roi alikumbuka kwamba, atakuwa ameambiwa na muuza duka ambaye alishuhudia kila kitu...

“Mmh! Atakuwa ameambiwa na muuza duka. Loo! Sasa?”

“Hata sijui. Kwani wewe hofu yako ipo kwa kiasi gani?” mama Anna alimuuliza Roi.

“Mimi sina wasiwasi wowote ule. Nimeamua kuwa na wewe japo kibinadamu nitakuwa nimefanya makosa makubwa, kumuumiza mtu jambo ambalo silipendi katika maisha yangu,” alisema Roi kwa sauti ya upole.

Alitoka kitandani, akavaa. Mama Anna naye akatoka kitandani, akamfuata kwa nyuma yeye akiwa amejizungusha upande wa kanga. Walifika sebuleni, wakaangalia kwa nje kupitia nafasi ya matundu ya ukuta wa fensi. Walimwona Martha amesimama dukani akizungumza na muuza duka.

Sura ya Martha ilitafsiri uchungu wa maumivu ya kutendwa. Ikawa kama imejikunja, Roi akahisi huruma...

“Martha... Wajina wako anaumia sana. Sasa itabidi nikutoe kiaina. Pita mlango wa nyuma, nenda mahali hapo nyuma kuna baa, kakae.”

“Mh!” Aliguna mama Anna, akatoa wazo...

“Sawa lakini turudi chumbani, nipe haki yangu kwanza ndiyo nitoke, siwezi kutoka hivihivi wakati uliishaanza kunipandisha mzuka wangu na mzuka wangu ukinipanda mimi akili zinachanganyikiwa kabisa.”

“Kuhusu hilo tu, twende sasa hivi.”

Walikwenda chumbani ambako Roi aliikuta simu yake ikiendelea kuita kwa namba ya Martha.

Mama Anna alikimbilia moja kwa moja kwenye kitanda huku akitupa kanga chini.

Alipokuwa juu ya kitanda akakaa mkao wa mechi tayari akijua anatakiwa kutoka ndani ya nyumba hiyo lakini moyoni alihakikisha anatoa mapigo ambayo, Roi anaweza kuamua asitoke tena na Martha kama kulala nje ya geti alale tu.

Roi, kuona mkao wa mama Anna alichanganyikiwa. Kama paka aliyeona panya. Akaenda kitandani kwa staili ya kuruka kama golikipa wa timu maarufu ya Ulaya...puu!!

Palepale alianza kuserebuka na mchezo huku mama Anna akimwangalia kwa hisia kali kama vile alikuwa akitumbuliwa jipu.

Mama Anna aliamua kujilegeza kabisa hivyo alitoa ushirikiano wa hali ya juu bila kuonesha dalili hata ya chembe kwamba kuna jambo hakubaliani na Roi...

“E...eti baby,” aliita Roi...

“Niambie baba...”

“Unaweza kuhama pale?”

“Kuhamia wapi baba angu?”

“Nitakaposema mimi?”

“Naweza ndiyo mume wangu.”

Roi kuitwa mume ndiyo kabisa, akajikuta anawewesekea uwanjani na kelele za mahaba kama vile yeye ndiye mama Anna.

***

Kule nje, Martha alitawala benchi la nje ya duka, mawazo yake yalikuwa usahihi wa mama Anna kuwepo au kutokuwepo ndani ya nyumba ya Roi...

“Ina maana kumbe niliposema nilimsikia mama Anna akimwita Roi baby nilikuwa sahihi? Lakini hawa walikutana wapi mpaka wakafahamiana?

“Kwa pale nyumbani hapana, haiwezekani. Lini kwanza? Na ilikuaje? Siku zote, Roi anakuwepo wakati ambao na mimi nipo, akitoka kurudi usiku...

“Halafu pia mbona si muda mrefu, Roi kaja kwangu! Hawa huenda wanajuana kabla ya hapa. Itakuwa hivyo, wanajuana kabla ya hapa,” aliwaza moyoni Martha akijihisi unyonge f’lani hivi.

“Lakini wewe Mangi utakuwa unamjua vizuri sana huyu kama anayeishi hapa. Hivi, ni mwadilifu kiasi gani?” Martha alimuuliza muuza duka...

“Nani, Evender?” muuza duka aliuliza naye...

“Kwani huyu kaka mwenye nyumba hii anaitwa Evender?”

“Ndiyo.”

“Mh! Siyo Roi?”

“Mh! Mi silijui jina la Roi, namjua kama Evender.”

Martha alianza kuingiwa na wasiwasi zaidi. Akahisi huenda Roi kujiita Roi alimwingiza mkenge. Na kama ni kweli halafu mpaka wameingia kwenye uhusiano hakusema ukweli wa jina lake, Martha alianza kuona kumbe alikutana na mwanaume tapeli...

“Labda ni jina la mtaani,” alisema Martha na kuomba Mungu iwe hivyo.

Mara mzee mmoja mteja aliwasili dukani hapo na kumwangalia sana usoni Martha...

“We binti kama nakufahamu,” alisema mzee huyo...

“Mimi sikufahamu.”

“We siye mdogo wake Benard?”

Ni kweli, Martha ana kaka yake anaitwa Benard. Ni machepele ile mbaya...

“Kweli Benard ni kaka yangu,” alisema Martha...

“Sasa je? Sasa Benard ni rafiki wa mtoto wangu, Mawazo. Akili zao kama sawasawa. Mimi nilikuona siku moja tu pale Kituo cha Polisi Urafiki wakati kaka yako na Mawazo walipowekwa ndani...”

“Kweli, nimekumbuka,” alisema Martha akiwa amemkumbuka mzee huyo ambaye umri ulikwenda sana...

“Haya! Mimi naishi nyumba ile ya tatu kutoka hapa. Hapa umefuata nini sasa?” aliuliza mzee huyo huku mkono wake mmoja ulioshika noti ya shilingi mia tano ukiwa umeshaingia kwenye dirisha la kuhudumiwa dukani hapo...

“Nina shida na kaka mmoja anaishi nyumba hiyo yenye geti jekundu,” alisema Martha huku macho yake yakielekea kwenye nyumba ya Roi...

“Nani, Ismaili?” aliuliza mzee huyo.

“Kwani anaitwa Ismaili?”

“Ee... ndiyo jina lake,” alisisitiza mzee huyo huku na yeye macho yake yakitua kwenye geti la nyumba hiyo.

Martha na muuza duka wote wakabaki wametumbua macho...

“Au wewe unamsema mwingine?” aliuliza Martha...

“Jamani! Kwani kwenye nyumba hiyo kunaishi watu wangapi? Si mmoja tu, kijana kijana hivi...mweupe, ana gari lina rangi ya kijiko cha chai ‘silva’.”

“Ee...” alikubali Martha...

“Ndiyo, anaitwa Ismaili. We alikwambia anaitwaje?”

“Mimi namjua kwa jina la Roi...”

“Mh! Roi tangu lini? Yule anaitwa Ismail Twalib Mussa.”

“Mimi namjua kwa jina la Evander,” alidakia kijana muuza duka.

“Hakuna bwana. Anaitwa Ismail.”

Mara, gari jeusi lilifika na kupaki getini kwa Roi, wakashuka wanaume wawili, wakiwa wamevaa suti nyeusi. Wakatembea kuelekea pale dukani. Wakasalimia wote kisha mmoja wao akauliza...

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi

Chapisha Maoni