
Mtunzi: Nyemo Chilongani
SEHEMU YA TATU
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
Bila kunificha akaniambia kwamba hanipendi, tena nisifikirie kuwa naye hata kidogo. Unadhani niliumia, walaaa! Shamila alikuwa msichana mrembo, kusema kwamba sikustahili hata kutembea naye kwangu mimi ilimaanisha kuwa nitafute pesa, nikipata nimtafute.
JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈
ENDELEA...
Kulipa kisasi kwa Issa ilihitaji nguvu kubwa, haikuwa kirahisi kama ilivyokuwa ikionekana, ilikuwa ni lazima nipambane kuhakikisha napata maisha mazuri kama watu wengine, halafu ndiyo nimfuate.
Wanawake waliendelea kufurika Kariakoo, walikuwa wengi mno tena waliokuwa wakipendeza kupit kawaida. Sikuacha kuwasalimia, kila siku niliamini kwamba ili uwapate wanawake wazuri basi hukutakiwa kuwahofia hata kidogo.
Siku ziliendelea kukatika, niliendelea kuwasiliana na Aisha na kuonana naye sana. Alinipenda, si kwamba nilikuwa mzuri ni kwa sababu niliwahi kufanya naye mapenzi.
Nilimzoea, kikafika kipindi akayajua maisha yangu, hata alipokuwa akija na kumwambia kwamba sina pesa, hakuwa akilalamika kwani nilimwambia kila kitu na akatokea kunikubali kwa maisha niliyokuwanayo.
Mishemishe zangu za kumtafuta Shamila hazikukoma, kila siku nilimwambia maneno yale yale kwamba nilimpenda lakini hakutaka kunielewa hata kidogo.
Nilipoona nimeshindwa, nikasema si kesi kama nikiamua kumfuatilia mdogo wake Halima ambaye alikuwa akifika hapo mara chache sana.
Nilijipanga na kusema kwamba ni lazima nimfuate msichana huyo kama tu angekuja Kariakoo kutembea kama alivyofanya. Nikawa mzee wa kucheza karibu, sikutoka maeneo husika kwa kuwa niliamini muda wowote ule Halima angeweza kufika mahali hapo.
Baada ya wiki ndiyo akafika, nilimsalimia na kuendelea na mambo yangu. Sikuwa na presha, nilijua ningemkamatia wapi hivyo nikaanza kupiga misele lakini macho yangu yalikuwa pale dukani.
Ilipofika majira ya saa nane mchana nikamuona akitoka, sikutaka kumfuata moja kwa moja, alikuwa akienda kwenye kituo cha daladala za Kimara hivyo nikapitia kule Big Bon na kwenda kumsubiri kwa mbele.
Nilimuona akija, nikasimama sehemu wanapouza magazeti na kutulia hapo, alipopita tu nikamsogelea na kumshika mkono, alishtuka, akageuka na kuniangalia.
“Edward...” aliniita huku akiachia tabasamu.
“Pole kwa kukushtua jamaniiii!” nilimwambia huku nami nikiachia tabasamu.
“Usijali!”
“Leo mbona mapema?”
“Nawahi chuo, nimeanza jana na ndiyo maana naondoka mapema!”
“Ooh! Msomi wangu! Ningependa nikusindikize!” nilimjaribu.
“Wapi?”
“Chuo! Au sisi ambao hatujasoma hatutakiwi kuingia huko?” nilimuuliza kimatani.
“Hahaha! Acha utani! Nashukuru Edward!” aliniambia.
“Kushukuru kwako kunamaanisha nini? Kwamba naruhusiwa?” nilimuuliza.
“Noooo! Hauruhusiwi! Shemeji yako atakuona!”
“Kwani mimi si joka la kibisa, ananiogopea nini?” nilimuuliza.
“Hahaha! Una maneno wewe!”
“Basi sawa. Nashukuru kwa kuniruhusu kukuleta mpaka hapa kituoni, uwe na masomo mema,” nilimwambia.
“Nashukuru!”
Akaingia ndani ya daladala na kuondoka zake. Alionekana kufurahia pasipo kujua kwamba kwenye zile hatua kumi za kumuumiza Issa hiyo ilikuwa hatua ya kwanza. Nikarudi kuendelea na ishu zangu kama kawaida.
***
“Paaa! Paaa! Paaa...” nilisikia milio ya bunduki kutoka mbali kidogo na mahali nilipokuwa.
Ilikuwa ni majira ya saa kumi alfajiri, kila mlinz aliyekuwa mahali hapo alikuwa akiogopa, milio ile ya risasi ilionekana kabisa kuwa bunduki nzito, japokuwa tulitakiwa kulinda mahali hapo, walinzi wakaanza kukimbia.
Mimi sikukimbia, haimaanishi kwamba nilikuwa na nguvu, hapa, ni kwa sababu sehemu ambayo nilikuwa ilionekana kuwa salama zaidi.
Wote walikimbia na kubaki peke yangu na kilrungu changu. Kwa mbali nikaanza kumuona mzee fulani akikimbia, alivalia kanzu huku mkononi akiwa na mfuko wa nailoni.
Niliogopa, kwa jinsi alivyokuwa akikimbia ilionekana kama mtu aliyekuwa akiogopa kitu fulani na nyuma yake kulikuwa na watu waliokuwa wakimfuatilia.
Nilitoka nilipokuwa na kusogea kule alipokuwa. Mara milio ya risasi ikaanza kusikika tena, mzee yule akaanguka na kutulia.
Nilitetemeka, sikujua kilichokuwa kikiendelea. Ghafla nikawaona wanaume wawili, sikuweza kuaona vizuri usoni kwa sababu ilikuwa usiku na hata hivyo walivalia vinyago usoni ambavyo niliviona baada ya kupita sehemu iliyokuwa na taa.
Wakamsogelea yule mzee ambaye alikuwa akiugulia maumivu pale chini, kitu cha kwanza kilikuwa ni kuuchukua mfuko wake alioushika lakini cha pili kilikuwa ni kutaka kumpiga risasi.
“Wewe simamemi hapohapo,” nilisema kwa sauti kubwa.
Sikujua niliupata wapi ujasiri wangu, saut ile ambayo niliitumia kusema maneno hayo ilikuwa na utisho mkubwa na kuwafanya wale vijana kuogopa, hivyo kuanza kukimbia na ule mfuko huku wakimwacha mzee huyo akiwa chini akilia.
Nikamsogelea, mzee huyo alikuwa ni wa Kihindi, ilikuwa ni lazima niyaokoe maisha yake. Niliogopa kwani sikutaka kujiaminisha kwamba wale watu waliondoka moja kwa moja, niliamini kwamba wanaweza kurudi tena kumalizia kazi yao.
Mzee yule alikuwa akilia kwa maumivu makali, alipoteza damu nyingi, pale chini alipokuwa hakuwa na msaada mwingine zaidi yangu. Roho yangu iliniuma sana kiasi cha kusema kwamba ni lazima nimsaidie kwa nguvu zote.
“Nisaidieee....nakufaaaa....nakufaaaa....” aliniambia mzee huyo huku akilia.
Nikambeba na kumpeleka pembeni, nilipofika kwenye kibaraza kimoja, nikalishika shati lake kwa lengo la kulichana ili nimfunge kwenye kidonda kilichokuwa kimesababishwa na risasi.
Wakati nimemvua shati hilo na kulichana, nikasikia kitu kimetokea kwenye mfuko wa shati na kuanguka. Sikujua ni nini, nilikichukua harakaharaka na kukiweka kwenye mfuko wangu wa suruali na kuendelea kumfunga.
Baada kama ya dakika ishirini ndipo walinzi wenzangu wakafika hapo ambapo tukambeba na kumpeleka katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
“Nyie ni akina nani?” alituuliza nesi mmoja huku akiniangalia hasa mimi ambaye nguo zangu zilikuwa na damu nyingi.
“Wasamaria wema dada!”
“Mmemuokota wapi huyu?”
“Sisi ni walinzi, tulisikia milio ya risasi, kuna watu wakataka kumuua, tukamsaidia!”
“Sawa. Muacheni, njooni asubuhi tena mkiwa mmetoa taarifa kituo cha polisi,” alituambia na sisi kuondoka.
Tuliondoka huku tukisimuliana kile kilichotokea, kila mmoja alinishangaa, nilionekana kuwa mtu wa ajabu sana, iliwezekanaje niende kumsaidia yule mzee na wakati nilisikia milio ya risasi?
Sikuwa na jibu la kuwapa zaidi ya kuwaambia kwamba mimi mwenyewe nilishangaa. Tulilinda siku hiyo kwa kujificha sana, nakumbuka tulikuwa kama wanne hivi.
Ilipofika asubuhi, nikaondoka na kuelekea kwenye kichumba changu nilichopewa kwa ajili ya kukaa huko na kujilaza kitandani, siku hiyo nilichoka kupita kawaida.
Wakati nikiwa nimevua suruali na kubaki na boksa ndipo nikakumbua kuhusu kile kitu nilichokiokota na kukiweka mfukoni.
Haraka sana nikaichukua surualia yangu, nilipokitoa kitu hicho, nilipigwa na mshangao baada ya macho yangu kugongana na almasi iliyokuwa na ukubwa kama mfuniko wa kisoda.
“Hii nini? Almasi au kipande cha chupa?” nilijiuliza na kukiangalia vizuri, ni baada ya sekunde kadhaa nikapata jibu kwamba kile kilikuwa ni kipande cha almasi, mapigo yangu ya moyo yakaanza kudunda kwa nguvu, sikuamini kile nilichokuwa nikikiona. Hii ilimaanisha umasikini ndiyo basi tena ama nini? Kila nilichojiuliza, nikakosa jibu.
Nilishtuka sana, nilijiona kama mtu ambaye alikuwa kwenye mlango wa kuelekea kwenye mafanikio makubwa. Ile ilikuwa ni dhahabu, kipande kikubwa kabisa ambacho kama ningekiuza basi ningepata pesa nyingi mno na kuwa tajiri mkubwa.
Hii ilimaanisha kwamba ningechukua msichana yeyote ninayemtaka na kulala naye, ningenunua simu kubwa zaidi, kujenga nyumba ya kifahari na kukunua gari moja matata kabisa.
Nilifurahi lakini sikutakiwa kuwa na pupa, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kutaka kumfahamu zaidi yule mzee, nilimfanyia utu, hii haikumaanisha kwamba nilitakiwa niachache naye kisa tu nimepata almasi.
Siku hiyo mchana nikaondoka na kuelekea hospitalini kumuona mzee huyo. Nilipofika hapo, nikakutana na manesi ambao walinipeleka mpaka kwenye chumba alichokuwa ambapo huko nikakutana na familia yake iliyokuwa na majonzi mno.
Kulikuwa na mwanamke mmoja mtu mzima ambaye nahisi ndiye alikuwa mke wake, mabinti wawili wazuri wa umri wangu lakini pia kulikuwa na kijana mwingine.
Nesi akanitambulisha kwao kwamba mimi ndiye niliyemuokoa kutoka kwa wauaji na kumchukua kumpeleka hospitalini hapo. Walifurahi na kunishukuru kwani mimi ndiye niliokoa maisha yake.
Niliwahadithia kilichokuwa kimetokea, walinisikiliza na kunishangaa, haikuwa rahisi kwa binadamu wa kawaida kwenda kumuokoa mtu kwa watu waliokuwa na bastola na wakati hakukuwa na kitu mkononi.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa urafiki wangu na familia hii, tuliendelea kuwa karibu na kukutana hospitalini hapo kuzungumza huku upande mwingine wa moyo wangu nikiwa na hamu ya kufahamu kuhusu yule mzee.
“Mimi naitwa Nurat,” aliniambia msichana mmoja miongoni mwa wale watoto wa mzee yule.
“Ulijitambulisha mule ndani!” nilimwambia huku nikicheka.
“Najua! Ila ninahitaji kukufahamu zaidi!”
“Naitwa Edward Francis! Nipo singo, sijaoa, sina demu, mpenzi wala mke,” nilimwambia huku nikitabasamu, akaanza kucheka.
Huyu Nurat ambaye nilikuwa nazungumza naye alikuwa msichana mrembo mno, alikuwa na nywele ndefu, sura nyembamba na macho ya goroli. Kwa kumwangalia tu ilikuwa ni rahisi kusema kwamba alikuwa Mwarabu halisi na hata Kiswahili chake alichokuwa akiongea kilikuwa ni kile Kiswarabu kabisa.
Nilimpenda kutoka moyoni, tangu nizaliwe sikuwahi kufanya mapenzi na Mwarabu, siyo hivyo tu, hata kushika kiuno chake sikuwahi kufanya hivyo.
Nilikuwa na hamu kubwa, nilitamani kumwambia kwamba nilimpenda na hivyo nilihitaji penzi kutoka kwake. Kwa jinsi alivyokuwa akiongea, lipsi zilivyokuwa zikicheza, kifua saa sita nilipagawa kupita kawaida.
Kila nilipomwangalia, moyo wangu uliniambia ‘Edward! Unasubiri nini?’. Sikutakiwa kuwa na presha kwa sababu watoto wazuri kama hawa unatakiwa kuwafuata kwa mahesabu makali sana.
Naweza kusema kwamba huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kuzoeana na Nurat. Kila siku tulikuwa tukionana na yeye ndiye aliyejaribu kuyabadilisha maisha yangu baada ya kufika katika chumba kidogo nilichokuwa nikiishi.
Alininunulia kitanda cha chuma, chumba kikapigwa rangi na kunipa kiasi cha shilingi milioni moja kwa ajili ya matumizi yangu mengine.
Kumbuka mpaka kipindi hicho sikuwa nimeiuza ile almasi kwa sababu sikujua soko lipo wapi na sikuwa na mtu wa kumwamini hata kidogo.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi