SEHEMU YA THELATHINI
ILIPOISHIA...
Nikastuka baada ya kuwaona watu wawili wenye miili mikubwa wakiwa wamevalia makoti meusi na makofia yaliyo yaficha sura zao na kubaki macho wa kishuka kwenye gari ya polisi huku wakiwa na bubduki mikononi wakizielekezea kwangu.NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
Nikairudisha gari nyuma kwa kasi ya ajabu na kuwafanya jamaa kuanza kunishambuli kwa risasi.
‘HALO BWANA EDDY GODWIN GARI YAKO IMEPATA ULINZI BINAFSI’
Sauti ya kike ilisikika kupitia spika zilizopo kwenye gari ambalo kwangu kila kinacho fanyika ninaona ni kipya na sauti hii si ngeni kwangu
‘CHAGUA SILAHA’
Kioo kidogo kilianza kunionyesha aina za bunduki zilizopo ndani ya gari kwa kigugumizi nikajikuta nikijiminyia kwenye silaha ambayo wala sikujua itajitokeza wapi,Gafla gari yangu ikasimama na haikurudi nyuma na nikaanza kusikia mtetemeko ndani ya gari na kuona vitu vyenye moto na vinavyokwenda kwa kasi kali vikitoka sehemu ya mbele ya gari na vikielekea lilipo gari la polisi na kulifanya lirushwe juu na kulipuka huku jamaa wanao nirushia risasi wakianguka chini
“UPO SALAMA BWANA EDDY GODWIN UNAWEZA KUENDELEA NA SAFARI YAKO.ASANTE”
Gari ikarudi katika hali yake ya kawaida na taratibu nikaanza kukanyaga mafuta na kufika katika sehemu ambayo wameangukia watu ambao sikujua lengo lao ni nini hadi wanisambule kwa risasi.Nikawachungulia kupitia kwenye kioo nikagundua wamefariki kwani miili yao ilijaa matobo mengi yaliyo tokana vichuma vya bomu zilizo toka kwenye gari huku damu nyingi zikivuja kwenye miili yao,Nikashuka huku nikitetemeka na kuanza kumfunua mmoja baada ya mwengine na kujikuta kumbukumbu zangu zikirudi hadi siku niliyo kamatwa pamoja na derava wetu na kuingizwa katika maabusu ya kituo cha polisi Lushoto na kulikuwa na majaamaa yenye misuli mikubwa na katika mazungumzo yetu walisema wao ni majambazi sugu wanashuhulika na utekaji wa magari.Sura mbili za majamaa wale ndizo zilizo lala chini,Sikutaka ushahidi nikaingia haraka ndani ya gari na kuondoka katika eneo hili.Baada ya lisaa nikawa nimefika mjini na muda ulio timu sasa ni saa kumi na nusu usiku.Nikafika hospitalini na kulisimamisha gari katika maengesho ya magari nikatoa simu yangu mfukoni na kuakuta missed call nyingi za Sheila.Nikafumba macho yangu na kusali kwa kumshukuru Mungu kunisaidia kutoka katika majanga yaliyo nikuta ila nafsi na moyo wangu vikajikuta vikiniuma kutokana na kifo cha madam Rukia
Nikashuka ndani ya gari na kwenda moja kwa moja katika chuma alicholazwa Sheila ila sikumkuta na nikatoa simu na kumpigia akapokea nesi
“Mgonjwa wangu yupo wapi?”
“Tumemuhamisha chumba panda huku gorofani ukunje kushoto chumba namba 16 ndipo alipo mgonjwa wako”
“Sawa”
Nikafanya kama alivyonielekeza nesi na kuingia katika chumba namba 16 na kumkuta Sheila akiwa hana raha na baada ya kuniona akataka kushuka kitandani kuja kunikumbatia ila sindano ya dripu ilimzuia,Nikamfwata na kumkumbatia na sote tukajikuta tukitokwa na machozi ya furaha
“Mume wangu pole”
“Asante mke wangu”
“Mimi kidogo hali yangu inaendele vizuri zile sindano walizo nichoma kidogo kidonda kimeanza kukauka kwa haraka”
“Nijambo la kumshukuru Mungu”
Nikaanza kumuadisia Sheila yaliyo nikuta ila sikumuadisia juu ya Madam Rukia kwani ninajua nilicho kitenda hakikustahili kwa mimi kumfanyia
“Sasa huyo uliye mgonga anaendeleaje?”
“Sijajua ila asubuhi itanibidi nikamfwatilie niweze kujua ni nani?”
“Utampatia wapi?”
“Nitauliza uliza na itanibidi niweze kuwa na pesa ya kumsaidia kama nitamuona na hapa sina hata pesa?”
“Kwani ni kiasi gani cha pesa kitatosha?”
“Sijajua ila niwe na pesa ya kutosha”
“Basi nitakupa kadi ya benki ukachukue pesa ya kutosha”
“Sawa mke wangu”
Tukaendelea kuzungumza mazungumzo ya kawaida hadi asubuhi nichukua kadi moja ya Sheila na akaniambia namba zake za siri kisha nikaondoka.Sikutaka nitumie gari kuhofia watu wa eneo nililo gonga mtu jana kuweza kulijua.Nikatembea kwa miguu hadi benki na nikabaki ninashangaa baada ya kukuta salio la akaunti ya Sheila milioni miambili na themanini 280.00.
“Huyu mwanamke kumbe anapesa kiasi hichi?”
Nikachagua huduma ya kutoa pesa nikaanza kutoa kiasi kidogo dogo hadi ikatimu milioni moja na nusu.Nikaingia kwenye duka kubwa la nguo na kununua nguo nyingine mpya pamoja na viatu.Nikanunua begi la mgongoni na kuziweka nguo nilizo zivua pamoja na viatu kisha nikatoka nje na kuingia kwenye kihoteli kidogo nikaagizia chakula kifungua kinya na kuanza kuka taratibu huku kichwa changu kikisongwa na mawazo.Nikamaliza na kutoka kwenye mgahawa huo na moja kwa moja nikaeleka kwenye vituo vya kukodisha taksi nikaingia kwenye taksi moja na kumuomba dereva anifikishe kweye hosptali ya mkoa.Tukafika na nikamuomba derava taksi anisubiri
“Lakini kaka itabidi pesa iongezeke”
“Haina shinda”
“Niachie japo advance ili nipate moyo wa kukusubiria”
Nikatoa elfu ishirini na kumpa kisha nikaelekea kweye ofisi ya daktari wajana na kukuta foleni kubwa ya watu wakiwa wanasubiri kuingia ndani ya ofisi hiyo.Nikawasalimia wakaitikia baadhi huku wengine wakionekana wapo kwenye maumivu makali ya magonjwa yao
“Samahani dada akitoka huyo mtu humo ndani unaweza ukanifanyia msaada niingie nikaonane na daktari mara moja?”
“Mmm kaka yangu ni bora uakapanga foleni tuu kwani mimi nimekuja tangu saa kumi na mbili asubuhi na foleni ilikuwa kubwa kama nini?”
“Dada mimi sio kama ninaumwa ila ninaingia mara moja kumuona huyo daktari tuu”
“Nimesema panga foleni mbona wewe kaka sio muelewa”
Watu waliopo nyuma ya dada wakaanza kulalamila wengine wakitaka niingie wengine wakikataa nisipishwe na dada huyo.
“Jamani samaani kama nitakuwa nimewaudhi kwa ombi langu”
“Ndio umetuudhi wewe utoke zako huko nyuma ulete kwato zako huku mbele,Unadhani na nina atakubaliana na ujinga kama huo kama vipi wewe ondoka”
Jamaa mmoja alizungumza kwa hasira kiasi kwamba watu wa karibu yake wakaanza kumtuliza hasira.Nikamuangalia kwa macho ya hasira kisha nikapiga hatua na kuufungua mlango wa daktari na kuingia bila dokta na kuwaacha watu wakilalamika.Daktari alipo niona akastuka na akanitazama kwa mshangao
“Mgonjwa wangu yupo wapi?”
“Kijana huo sio utaratibu wa kazi kama uliwakuta wezako kwenye foleni inabidi ukae kwenye foleni”
“Dokta hilo sio jibu nataka nijui mgojwa wangu yupo wapi?”
“Nakuomba uwe mpole kijana.Mgonjwa wako yu....yuu”
“Yuuu yuuu nini sema yupo wapi.....?”
Kwa haraka haraka nikaanza kuhisi kuna kitu ambacho daktari ananificha kwani kwa jinsi anavyo zungumza ananipa wasiwasi
“Yupo kwenye wodi ya wazazi”
“Twende ukanionyeshe”
Daktari akajishauri kisha akamuomba mgojwa wake niliye mkuta amsubiri anarudi ndani ya muda mchache.Tukatoka nje na kuwafanya wagonjwa wanao lalamika kukaa kimya huku wakitutumbulia mimacho ya mshangao.Tukaelekea kwenye moja ya wodi na kumkuta Madam Mery akiwa amelala kwenye moja ya kitanda huku pembeni yake akiwepo jamaa ambaye nilimuona kwenye picha za harusi yao kwa na moja kwa moja nikajua ndio mume wake.Madam Mery baada ya kuniona akastuka huku kwa ishara akiniomba nisisogee kwenye kitanda chake.
“Mgojwa wako yule pale”
Dokta aliniambia baada ya kuniona nimesimama
“Pesa iliyo baki ni kiasi gani?”
“Imeshalipwa na yule jamaa pale kwenye kitanda”
“Powa nakushukuru dokta”
“Na wewe pia nakushukuru”
Dokta akaondoka na kuniacha nikiwa nimesimama huku macho yangu yakimtazama Madam Mery hadi jamaa yake anakaanza kuhisi kitu.Jamaa akapiga hatua za kunifwa na kabla hajanifikia nikageuka na kuondoka kwa hataua za haraka na kutoka katika wodi na kumfanya jamaa kuongeza mwendo na kuja kunishika bega
“Kaka vipi?”
Jamaa alinisalimia huku akinitazama machoni
“Salama tuu vipi?”
“Mbona umemtazama mke wnagu na ukaondoka baada ya mimi kukutazama?”
“Kwani tatizo lako ni nini?”
“Nahitaji kujua kama wewe unamjua mke wangu au humjui?”
“Simjui”
“Sasa kwanini umtazame?”
“Wee jamaa vipi kumtizima mke wanko ni kosa?”
“Ndio ni kosa sipendi mke wangu atazamwe...Na ukirudia kumtazama nitakutoa duniani”
Jamaa alizungumza huku akilifunua koti la suti yake na kunionyesha bastola aliyo ichomeka kiunoni mwake.Sikutaka ugomvi naye nikageuka na kuanza kupiga hatua za kuondoka kabla sijafika mbali na sehemu niliyo kuwa nimesimama nikastukia nikivutwa tisheti na nikageuka na kumkuta mume wa Madam Mery akinitazama kwa hasira
“Mimi ninakusemesha alafu wewe unaondoaka ina maana umenidharau si ndio?”
Jamaa alizungumza kwa hasira na sauti ya juu na macho yangu nikayapeleka hadi kwenye kioo cha TV(Luninga) iliyopo eneo la mapumzikio ya wagonjwa na kuitazama taarifa ya habari inayorusha na shirika la utangazaji nchini Uingereza shirila la BBC inayozungumzia kupotea kwa ndege ya shirika la KLM iliyokuwa ikitokea nchini Tanzania na inavyosemekana ina viongozi wa juu wa serikali wa nchi ya Tanzania na moja kwa moja nikatambau mama yangu ni miongoni mwa viongozi hao na mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio
Gafla nikastukia kibao kikali kikitua shavuni mwangu kikitokea kwa jaamaa na kunifanya niyumbe na kumgonga nesi mmoja anaye saidiana na mwenzake katika kusukukuma kitanda cha matairi na juu yake kuna mgonjwa ambaye sikuamini macho yangu kwani ni Manka ndiye aliyelazwa juu ya kitanda hicho kuku sura yake ikajaa michubuko na amewekewa kifaa maalumu cha kuhemea huku macho yake akiwa ameyafumba na hali yake inaonekana sio nzuri
“Kaka kuwa makini?”
Nesi alizungumza huku akijiweka vizuri na nikabaki nimeduwaa huku nikiwaangalia wanavyokisukuma kitanda wakielekea kwenye moja ya chumba ambacho kina maandishi mekundu makubwa juu ya malango ambayo yameandikwa ICU huku chini kukiwa na maandishi yaliyo andikwa CHUMBA CHA WAGONJWA MAHUTUTI.
Jamaa akanishika tisheti na kunigeuza huku akirusha ngumi ambayo kabla haijanifikia nikaidaka na kumuangalia kwa macho ya kumshangaa na kuzifanya kumbukumba za tukio lake na langu linalo endelea katika sehemu hii kurudi
“Oyaa brother vipi wewe?”
“Sio vipi stozi zako nimezipata na utajuta kunijua”
Jamaa alizungumza huku akilivua koki lake la suti kwa dhumuni la kupigana na mimi,Akiwa anakamilisha kazi yake ya kulivua koti lake la suti nikampiga ngumi ya pua na kumfanya atoa ukulele mkali huku akiwa ameinama na kuishika pua yake,Watu na waauguzi walipo kwenye eneo hili wakanza kujisogeza kwa haraka huku wengine wakiomba ugomvi usiendelee,
“Wewe dogo lazima nikutafute tuu sehemu yoyote na nilazima nikuue”
Jamaa alizungumza huku akishikwa na baadhi ya watu,sikutaka kumjibu kitu cha aina yoyote zaidi ya kuelekea kwenye chumba ambacho nilimuona Manka akiingizwa kabla sijakifikia madaktari wawili wakanizuia
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com