SEHEMU YA THELATHINI NA TATU
ILIPOISHIA...
Madam Rukia alibadilisha mada baada ya mume wake kufika katika eneo tulilopo na sikuwa na haja ya kujiuliza ni kwanini amebadilisha mada nikajua moja kwa moja ahitaji mumu wake atambue kuwa mimi nilikuwa naye poriniNIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
“Hivi wamesemaje kuhusiana na swala zima la shule kuendelea?”
“Wamesema watatoa tangazo kwenye vyomba vya habari pele shule itakapo funguliwa ila kwa sasa wameunda tume ya madai yaliyopelekea shule kufungwa ambayo itachunguza kila kitu na wanafunzi walio kamatwa na polisi wapo wengine wanahojiwa”
“Sasa hiyo tume watatumia muda gani kuchunguza hayo madai yato kwa maana siku zinakwenda mbele na masomo ndio hivyo yamesimama?”
“Mimi wala sielewi ila kidato cha sita na cha nne wamesambazwa kwenye shule za jirani ili kuendelea na masomo hadi pale majengo yatakapo fanyiwa ukarabati nao ndio watarudi”
“Ahaaa....”
“Wewe sasa hivi unakwenda wapi Dar au kwa Marry?”
“Huyo Merry mimi wala sihiaji kumsikia kwa maana mume wake amenizingu sana majuzi”
“Wee amekuonea wapi?”
“Si nilikwenda kumcheki hospitalini sasa nikawakuta wana mazungumzo yao basi mimi ikanibidi niwaache niondoke zao basi jamaa akanifwata na kuanza kunipiga vibao mbele za watu na mimi nikampiga basi mambo yakaharibika pale hospitali nikaamua kumpotezea”
“Ndio ukaumia hivyo?”
“Hapa nilipata ajali ya gari ndio maana nikafungwa huu mbadeji”
“Pole mwaya ila yule mume wa Marry anajisikia sana”
“Kwani anafanya kazi gani?”
“Ni muwekezaji kwenye madini anasimamia kampuni ya baba yake kwenye kuchimba madini”
“Tena nimekumbuka kuna kitu nahitaji unisaidie?”
“Kitu gani?”
“Si unamjua yule mdogo wa mke wa mwalimu Nyange”
“Yupi?”
“Tuye mrefu refu kiasi na nimweupe”
“Ahaaa unamzungumzia Manka”
“Ehee huyo huyo”
“Mmmm yule mtoto wa watu anamatatizo sana kwani ni juzi juzi aliungua na maji ya moto usoni”
“Kwa nini?”
“Akili yake si imemruka yaani zinaingia na kutoka.Kuna kipindi akili yake inakuwa sawa na kuna kipindi akili yake inapote hii nikutokana na ajali iliyo mpata”
Nikaanza kujisikia vibaya moyoni mwangu kwa maana Manka ni dada yangu japo nimefanya naye mapenzi pasipo kujua ila bado ni dada yangu
“Hivi kwenye ajali ndugu zake walisalimika?”
“Yaaa dada yake alipona na shemeji yake siku ya ajali wao walibaki Dar na kutokana na gari yao kujaa watu”
“Mmmm.......nasikia alikuwa na ujauzito?”
“Ulitoka chezea ajali wewe ila mbona unaniuliza maswali mengi ambayo ni vigumu kwa mtu kama wewe kutambua hayo mambo?”
“Kawaida tuu”
Madam Rukia akaondoka na mume wake wakaniacha nikilisimamaia gari langu lioshwe na mafundi wasaidizi wa mume wa madam Rukia.Wakamaliza kulisafisha gari langu nikawalipa pesa na kuingia kwenye ofisi waliyo ingia Madam Rukia na mumewe
“Jamani mimi ndio ninaondoka zangu hivi”
“Bwaba mdogo karibu sana”
“Asante na pesa ya matengenezo nimewalipa vijana wako”
“Hakuna shida nakukaribisha tena na tena”
“Asante madam mimi ngoja niamshe popo”
“Eddy unakiswahili cha kihuni kuamsha popo ndio nini?”
“Maana yake ni kuondoka”
“Ahaa sasa hembu nianchie namba yako ya simu endapo kutatokea lolote nitakujulisha”
“Sawa”
Nikamuandikia Madam Rukia namba yangu ya simu kwenye simu yake kisha na mimi nikajibipu na nikaisave namba yake nikaanachana nao na kurudi zangu hospitakini nikamkuta Sheila akimaliza kuagana na manesi wake ambao alishaanza kuwazoena kama dada zake na kuwafanya baadhi ya manesi kumwagikwa na machozi haswa nesi aliyekuwa akimuhudumia Sheila kwa karibu sana na ndio alikuwa akiitoa simu yake kwa ajili ya mawasiliano.Tukaondoka hospitalini na kurudi katika hoteli tuliyo fikizia na kuchukua mizigo yetu ambayo tulikuta imehifadhiwa kwenye sehemu malumu hii ni baada ya muda wetu wa vyumba tulivyo lipia ulikwisha.Safari ikaanza taratibu huku nikiendesha gari kwa umakini mkubwa kuepuka ajali zisizo na ulazima
“Eddy nakupenda sana mume wangu”
“Nakupenda pia mke wangu”
“Yaani natamani hata tuishi pamoja kabisa”
“Usijali mke wangu tutaishi pamoja”
Tukaendelea na safari huku ukimya ukiwa umetawala ndani ya gari,Sheila akaweka vizuri siti yake aliyo kalia na kuanza kulala na kuniacha mimi nikiendelea kuendesha gari hadi tunafika Mombo mida ya saa tisa alasiri nikamuamsha Sheila na tukaingia kwenye hoteli ambayo ninapenda kuingia kwa kupata chakula nikiwa kwenye safari kati ya Dar na Arusha.Simu yangu ikaingia meseji na namba ngeni ambayo si yatanzania huku ujumbe wake ukiwa ni mfupi sana na kunistua kidogo
‘NIPIGIE’
Nikabaki nikiwa nimeutazama kwa muda huku nikiwa na maswali kichwani ni nani aliye nitumia ujumbe wa namna hiyo.Nikaingia kwenye akaunti yangu ya simu na kununua muda wa kutosha wa maongezi kisha nikaipiga namba ya simu
“Eddy mwangu hujambo”
Nikaisikia sauti ya mama na nikajikuta nikisimama kwa haraka na kuelekea kwenye vyoo kuzungumza na simu ambayo kwangu ni muhimu sana
“Sijambo mama shikamoo”
“Marahaba mwanangu sina muda wa kupoteza ila ninakuomba uje nchini Iraq tupo kizuizini na hap.....”
Nikasikia mama akitoa kelele za kupigwa na watu ambao wanazungumza kiarabu ambacho sikuwa ninakielewa na baada ya muda kidogo simu ikakata na kujikuta nikianza kupandwa na hasira huku jasho likinimwagika.Nikatoka na kwabahi mbaya kwenye mlango wa kuingilia chooni nikagongana na jamaa anaye onekana ni sharobaro na kuifanya simu yake ya gharama aliyokuwa anaichezea kuanguka chini na kupasuka kioo,Nikataka kuondoka jamaa akanishika mkono na kunivuta nirudi sehemu aliyo simama
“Wewe fala umeangusha simu yangu hata kuniomba msamaha unaondoka ondoka”
“Fala mwenyewe kwanza niachie mkono wangu kati ya simu hako kakopo kako ndio unakaita ni simu”
“Kwa hiyo mimi unaniita fala si ndio”
Jamaa alizungumza kwa hasira kiasi kwamba akanishika tisheti yangu kifuani na kuanza kuikinja huku akinivuta kiasi kwamba akazidi kunipandisha hasira.Nikaitoa mikono yake kwa nguvu kifuani kwangu na kumsukuma jamaa na akarudi nyuma kidogo na kuanza kunirushia ngumi ambazo zilinipata kifuani.Nikajirusha na bega langu kilampiga tumboni kwake kama wanavyofanya wacheza miyereka na nikamsukuma na sote tukajikuta tukiangukia mlango wa choo hadi ukavunjika.Nikanyanyuka haraka na kamkaba jamaa shingoni kwa muda na kuwafanya watu walio liona tukio kuja kutuamua
“Eddy mume wangu ni nini unacho kifanya”
Sheila alizunumza huku akinishika mkono akisaidiana na watu wanao amua ugomvi kuniondoa katika sehemu ya tukio
“Wewe boya tuu kamlale mama yako ambaye ni Malaya”
Jamaa alinitukana tusi lililoamsha hasira zangu upya na kujikuta nikiwazidi nguvu watu walio nishika na kwenda kumvaa jamaa na safari hii nikaanza kumshindilia ngumi za hasira kiasi kwamba jamaa akapasuka sehemu ya jicho lake na uso wake kujaa damu idadi ya watu ikazidi kuongezeka na kunitoa katika sehemu ya ugomvi na kuniingiza kwenye moja ya chumba kinachotumika kama ofisi ya eneo hili la hoteli.
“Eddy mume wangu punguza hasira nakuomba tafadhali nipo chini ya miguu yako.Nakuomba baby”
Sheila akazidi kuendelea katika kunituliza kiasi kwamba nikabaki nimekaa kimya huku mwili ukiwa unanitetemeka kwa hasira huku meno yangu nikiwa nimeyakaza kwa kuyang’ata kwa uchungu na hasira kwani katika maisha yangu kitu ambacho kinanichukiza ni mtu kumsema mama yangu vibaya
“Eddy wangu nakuomba uachene na wapumbavu mume wangu wasikupotezee muda wako...Ehhee tulia mume wangu sawa”
Sheila alizungumza huku akinikumbatia na kuanza kunifuta machozi yanayonitoka kwa hasira,wakaingia askari wawili na wakasimama mbele yetu huku wakijishauri kitu cha kuniuliza na mmoja wao nikamkumbuka haraka ni miongoni mwa askari walio nikamata siku Manka na familia yake walipo pata ajali na wakanipeleka kituo cha polisi mimi na dereva wa mama
“Kaka zangu niwasaidie nini?”
“Ahaa tulikuja kumchukua jamaa akatoe maelezo kituoni kwa tukio zima lililo tokea”
“SIENDI KOKOTE NA OLE WAKE MTU ANIGUSE NINAKUFA NAYE”
Askri wakakaa kimya huku wakinitazama na kumfanya Sheila awakonyeze kwa ishara ya kuniacha hadi hasira zipungue.Askari wakatoka na kuniacha na ndani ya lisaa hali yangu ikarudi kama awali hii ni baada ya Sheila kunibembeleza kwa kila aina ya maneno mazuri ya kuvutia.Tukatoka ndani ya chumba tulichopo huku Sheila akinipigisha stori za kunifurahisha na kunifanya nicheke,Nikakutana na askari waliokuja kunikamata wakanifwata kiustaarabu na kuniomba niongozane nao hadi kwenye kituo chao na sikufanya ubishi.Tukaingia kwenye gari letu na kuongozana nao huku na wao wakiwa kwenye gari lao na haikichukua muda tukafika kwenye kituo cha polisi
Nikakutana na baadhi ya wazee wapatao wanne wakiwa mamevalia mashati ya kijani sura zao zikiwa zimejikunja baada ya sisi kuingia na pembeni yao akiwa amekaa kijana niliye pigana naye na sura yake ikiwa na maplasta huku ikiwa imevilia damu.Wakaanza kuzungumza lugha ya kipare ambacho ninakielewa viruzi kwani walianza kumuuliza kijana wao ni nani aliye mpiga na akawajana kwa kuninyooshea kidole kuwa mimi ndio nilio mpiga hadi akaumia sura nzima
“Mimi ni diwani kwani umepiga mwanangu”
Mzee mmoja mwenye kitambi cha wastani alizungumza kwa hasira na kabla sijamjiu Sheila akanifinya mkononi na kunifanya nimtazame bila ya kumjibu chochote kwani nilipanga kupa tusi ambalo asinge nisahamu maishani mwake
“Mzee wangu ninakuomba umsamehe mume wangu kwani ni hasira tuu ndizo zilipelekea ugomvi kati yake na huyo mwenzake”
“Wewe koma mwanamke Malaya mkubwa usiye na haya wewe unaweza ukamuita huyu kapupwe wako mume ehee kwanza sijazungumza na wewe”
Mzee akazidi kuzungumza kwa hasira kiasi kwamba nikajikuta na mimi hasira zikaanza kunipanda taratibu na Sheila akanishika kifuni ili jazba ishuke na sikuelewa ni kwanini askari wamekaa kimya mzee akiwa anazungumza
“Sawa mzee wangu ila ninakomba mumsamehe na kama kuna gharama zozote tupo tayari kuwalipa”
“Wewe mwanamke huwezi kunilipa mimi....Uliza hapa mjini mzima wananijua mim ni nani?’
“Mzee wangu naona ustaarabu umekushinda...Sijaja hapa kusikiliza kuwa wewe ni nani au unakazi gani.....Na nyinyi mumekuja kunichukua kule ili nije nikutane na wazee kama hawa wasio na aki.....”
Sheila akaniziba mdomo ili nisimalizie nilichokuwa nikikizungumza kwani kingeamsha ugomvi upya
“Mzee wangu tukauomba utusamehe kwa yaliyo jitokeza sema kama kuna kiasi chochote chapaesa ninaweza kukulipa”
Kuepusha shari nikatoka kwenye kituo cha polisi na kuingia ndani ya gari na kumsubiria Sheila ambaye baada ya robo saa akatoka na kuingia ndani ya gari
“Wamesemaje?”
“Wametaka tuwalipe gharama za matibabu pamoja na gharama za vitu vilivyo haribika kwenye hoteli.Kumbe yule mzee ndio mmiliki wa hoteli na yule mwanaye alikuwa kama msimamizi pale”
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com