SORRY MADAM (32)

0
SEHEMU YA THELATHINI NA MBILI
ILIPOISHIA...
Nikanyanyuka kitandani na kufungua dirisha na kuchungulia kwa chini nikiangalia watu wanao ingia na kutoka ndani ya hospitalini hii.Mawazo ya ajabu yakaanza kunitawala akilini mwangu na gafla nikamuona mama kwa chini akiwa amekaa pembeni ya jeneza huku akiwa amevalia nguo yeupe huku puani akiwa na pamba na akaanza kuniita huku akilia kwa uchungu kiasi kwamba nikaanza kuchanganyikiwa

NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU

SASA ENDELEA...
Kwa nyuma yake akatokea mtu mwenye nyundo kubwa na kuinyanyua juu na kuanza kumshindilia nyondo za kichwani na kusababisha damu kuruka na mtu huyo akaanza kucheka huku akuninyooshea kidole.Kwa hasira nikapanda kwenye dirishana kabala sijajirusha nikastukia nikishikwa kwa nyuma na kuaza kuvuta na madaktari wawili wa kiume

“Eddy mume wangu nini unataka kufanya....Kwa nini unataka kujiua,Eddy nakupenda tena nakupenda sana mume wangu kwa nini jamami?”
Sheila alizungumza huku akilia kiasi kwamba akataka kushuka kitandani ila madaktari wakamzuia
“Mama yangu amekufa”
“Eddy mama hajafa”
“Mama yangu amekua mimi nitaishi na nini.....Hadi sasa hivi simjui nani na baba yangu halisi”
“Eddy mama hajafa nakuomba usimpe shetani mawazo kama hayo yakatawala kichwani kwako”
“Sheila nimemuona mama pele chini yupo kwenye jenezaa na kuna mtu amempiga hadi amekufa”
“Baby sio mama.....Dokta namuomba mumlete hapa”

Madaktari wakanikalisha kwenye kitanda na Sheile hakujali kama anajeraha kifuni kwake,akanivuta na kunikumbatia kwa nguvu huku sote tukiendelea kulia
“Mama amekufa”
“Eddy acha kuzungumza hivyo nakuomba tafandali”
“Sheila”
“Mmmm”
“Unanipenda?”
“Eddy nakupenda tena sana”
“Nakuomba nife”
“Eddy ni nini unacho kizungumza?”
“Sheila mama yangu ameshakufa sina dhamani tena duniani...Mama yangu ndio rafiki yangu wa karibu.....Sheila mimi sina upendo wa baba si...”

Sheila akanivuta na kuanza kuninyonya mdomo kwa nguvu kunizuia nisiendelee kuzungumza,Madaktari wakatoka ndani ya chumba na kutuacha tukiendelea na kitendo ambacho kilianza kuusisimua mwili wangu.Sheila akauchukua mkono wangu na kuushikisha kwenye chuchu yake ya kushoto na nikaanza kuiminya taratibu ila nikajikuta nikimuachia Sheila
“Sheila unaumwa sitaki tufanye sasa hivi”
“Eddy....”
“Hapana unaumwa”
“Ok mume wangu asante kwa kunijali.....Alafu baby ukilia unakuwa kama yale makatuni ya Tom na Jerryjea yakilia”

Nikajikuta nikitabasamu na kumfanya Sheila na yeye kutabasamu huku akiishika shika pua yangu na kuanza kuiminya minya kiasi kwamba furaja yangu ikaanza kunirejea taratibu
“Na wewe ukilia unakuwa kama wale katuni wa powefull girl machozi yao yanaruka kama maji haswa yule Babon akilia machozi yanaruka hayo kama bomba lililo pasuka”
“Jamani baby kwa hiyo machozi yangu yanaruka kama maji ya bomba lililo pasuka?”
“Ndio unatisha kama nini?”
“Hata wewe ukilia unatisha unakuwa kama yale mazombi ya wrong turn...Kuna ile sijui ni part one kuna kazombi kamoja kaliuliwa wacha baba mtu aanze kulia sasa yule ndio unafanana nye”

Nikazidi kucheka huku na kujikuta nikisahau tukio lililo tokea katika dakika chache zilizo pita
“Basi na wewe unakuwa kama yule kale kasichana kwenye wrong turn kalicho mfumania jamaa yake akiwachungulia jamaa wakifanya mapenzi....Uliona jinsi kalivyokuwa kanalia kwa hasira”
“Mmmmmm haya baby wewe ndio umeshindi....Mume wangu unapenda nikuzalie mtoto wa kike au wa kiume”
“Nataka wa kike ili mtu akija kumchumbia kitangulizi cha mahari nataka mabasi saba”
“Hahaa mume wanagu hayo mabasi saba jamani mtu wa watu atayatolea wapi au ndio hivyo unataka ujipatie mtaji kupitia mtoto wako?”

“Ndio na atakuwa mzuri kama wewe mama yao”
“Mmmmm mimi nataka wachukue lipsi zako na macho yako?”
“Sawa itakuwa ni vizuri pia.....Eddy nikuambie kitu?”
“Niambie”
“Mungu akipenda nahitaji unioe kwa ndoa ya kanisani”
“Nikimaliza kusoma tuu nafunga ndoa na wewe”
“Kwelu mume wangu?”
“Kweli kwani nahitaji kuyaanza maisha mapema”

“Kweli mume wagu...Alafu nilikuwa nimesahau,Vipi shuleni kwenu hali inaendeleaje?”
“Mmmm hata mimi sijui inaendeleaje alafu sina namba ya simu ya mtu wa shule nikamuuliza”
“Mume wangu ninahitaji usome na mimi baada ya kukuzalia tu mtoto nitarudi shule kusoma kwa maana nahitaji familia yetu iwe ya wasomi zaidi hata ukimuhimiza mtoto asome kweli awe anasoma kweli.....Sio mama unamumbia mtoto nenda shule wakati wewe mwenyewe shule hukuipenda”
“Kweli mke wangu ila vipi umeshakula?”
“Baby nilionja onja kwani muda ule nilipopiga simu na ikapokelewa na mwanamke ndio muda ambao nilikuwa ninakula chakula na baada ya simu ile hamu ya kula yote ikapotea”
“Ngoja nikanunue chispi tuje tule...Tena nimekubuka nikakununulie na simu kabisa sipendi hivi unavyo azima azima simu za watu”

“Sawa baby ila nakuomba usichelewe na kama unakwenda tumia gari usipande kwenye hizo ndubwasha zinazo endeshwa na wavuta bangi na ukapata ajali bure”
“Sawa baby...ila kwa mbali ninaanza kuhisi kichwa kinaniuma”
“Pole baby nenda ukanywe dawa kwanza ndio uende huko unaotaka kwenda”
“Hapa dawa nitazipatia wapi?”
“Mume wangu hospitali nzima ukose dawa za kunywa.....Sikia nenda kwenye ofisi iliyopo pale chini ya ngazi kuna masister utawakuta waombe na watakusaidia”
“Sawa baby”

Nikambusu Sheila mdomoni na kufungua mlango na kutoka na moja kwa moja nikashuka hadi kwenye chumba alicho nielekeza Sheila.Nikagonga mlango mara tatu na suti ya kike iliyopo ndani ya chumba hicho ikaniruhusu niingie.Nikafungua mlango na kuwakuta manesi watatu wakiwa wameshika mashavu yao huku wakionekana wanyongea na macho yao wameyaelekezea kwenye kioo cha Tv iliyopo ndani ya chumba hicho.Na mimi ikanibidi ninagalie wanacho kitazama na kukuta mipigo ya moyo yakiende kwa kasi baada ya kuiona ndege kubwa ikiwa imeanguka huku inawaka moto na kutoa moshi mwingi na mweusi huku kikosi cha zima moto ambacho sikujua ni cha nchi gani wakijitahidi kuzima moto kwa kutumia magari yao maalumu ya kuzimia moto huku baadhi ya miili inayoonekana kuwa imefariki ikitolewa ndani ya ndege hiyo

“Karibu kaka yangu tukusaidie nini?”
Nesi mmoja aliniuliza swali ila sikumjibu nikabaki nikiitazama taarifa inayorushwa kupitia kituo cha televishion ya SKY NEWS kinachopatikana nchini uingereza.Mapigo ya moyo yakazidi kunienda mbio kana kwamba nimekimbia umbali mrefu pasipo kupumzika.Nikayasoma maandishi makubwa yaliopo ubavuni mwa ndege hiyo na kukuta yameandikwa Emirates kiasi kwamba nikajikuta nikishusha pumzi taratibu na manesi wote wakabaki wakinitazama

“Kaka kaka”
“Naam”
“Mbona unashangaa?”
“Ninatazama hiyo taarifa ya habari”
“Inasikitisha sana kwa maana watu wote waliopo kwenye hiyo ndege wamefariki”
“Imekuwaje hiyo ndege ikaanguka?”
“Ilianguaka kipindi inapaa imesababishwa na hali ya hewa kutokuwa nzuri”
“Imeangukia nchi gani?”
“Imeangukia Tailand”

Kidogo nafsi yangu ikapata unafuu na tabasanu likarudi usoni mwangu taratabu kwani nilidhani itakuwa ni ndege ambayo amepanda mama.Nikawaomba dawa za kutuliza maumivu ya kichwa wakanipatia pamoja na maji nikazinywa na kuwashukuru na kuondoka na kuwaacha wakiendelea na shughuli zao.Nikaenda kwenye maduka ya simu ambayo hayakuwa mbali sana na hopsitali na kununua simu kwa ajili ya Sheila na kupitia kwenye sehemu wanapouza chipisi.Nikanunua chips za kutosha na kurudi hospitali na kumkuta Sheila akizungumza na madaktari
“Hali yako inazidi kuridhisha na baada ya siku kadhaa tunaweza kukupa ruhusa ya kutoka hospitali”
“Kwani hamuwezi kunipata hata leo?”
“Kwa leo ni vigumu inabidi umalizie dozi yako ya vidonge na sindano za kukausha kidonda na baada ya hapo tutakuwa huru katika kukuruhusu.”

Tukakaa hospitalini siku mbili huku nikiendelea kumuuguza Sheila na ndani ya siku mbili sikuweza kupata taarifa yoyote kuhusiana na Mama juu ya kupatikana kwa ndege yao ambayo imetekwa na watu wasio julikana.Sheila akaruhusiwa kutoka hospitalini na akapewa vidonge ambavyo endapo atajisikia maumivu ameze.Nikapepeleka gari gereji kufanyiwa ukarabati wa vitu vidogo vidogo na kumuacha Sheila akijiandaa kwa ajili ya safari ya kurudi Dar es Salaam
“Kaka hii gari umeinunua wapi?”
“Kwa nini?”
“Nina mwaka wa 21 tangu nianze kutengeneza magari ila sijawahi kuiona gari ya dizain hii kwa maana mmmm imekusanya mambo mengi”
“Ahaaa hizi gari mbona zipo ukihitaji unazipata tuu”
“Aise ila hii gari si chini ya milioni mia na kitu”
“Imezidi zaidi ya hapo”

Niliendelea kuzungumza na fundi mkuu wa gareji ambayo nimeileta gari yangu,Nikastukia nikiguswa bega kwa nyuma nikageuka na kukutana na sura ya Madam Rukia na kunifanya nistuke kiasi kwamba mapigo ya moyo yakaaza kunienda mbio
“Mbona unastuka Eddy?”
“Ha.....pana nimeshangaa tu kukuona hapa”
“Wife(mke) unajuananaye huyo kijana?”
Fundi gereji aliuliza swali na kujikuta nikizidi kupata kigugumizi chakuzumza kiasi kwamba nikaabaki nimekaa kimya
“Ndio ni mwanafunzi wangu wa kidato cha tano,huyo ndio chanzo cha shele yetu kufungiwa”
“Kaka sura yako inaonyesha mpole kumbe ni mkorofi kiasi hicho?”
“Hapana mambo ya kawaida”

Nilizungumza huku nikibabaika kwani kila nikimtazama Madam Rukia ninakumbuka tukio lililotokea porini na jinsi nilivyo fanya naye mapenzi kwenye kichaka isitoshe nikakumbuka niliusikia mlio wa bunduki na kujua ni lazima atakuwa ameuawa na mkuu wa shule
“Ehee lete story Edy ile siku ilikuwaje?”
Madam Rukia aliniuliza swali baada ya mume wake kuondoka na kuingia kwenye moja ya chumba na kuanza kuzungumza na wafanyakazi wake.Nikamuadisia Madam Rukia kuanzia tulipo achana hadi nikafika hopsitalini na yeye akaanza kuniadisia tangu tulipo achana

“Mimi ile siku bwana nilikutana na vijana ambao ni wanakijiji cha karibu kwenye ule msitu wenyewe walikuwa wanakwenda kuwinda.....Sasa pale ulipo niacha mkuu wa shule na wezake si wakawa wananifwata basi wale vijana wakatanda ile sehemu tuliyopo na kuanza kuwashambulia waalimu na kuwatoa mbio za kufa mtu basi ikawa ndio pona pona yangu”
“Mbona nilisikia mlio wa bunduki alipigwa nani?”

“Ahh mkuu wa shule si alikuwa anajifanya kidume anapiga bastola juu hewani ili kuwatisha wale vijana......Wee alipigwa gongo moja la pua hata sijui ile bastola aliitupia wapi nilisikia akitoa ukulele wa uwii na kuanza kukimbia....sasa na ile miguu yake yenye matege ya kaekejea upande mmoja ungekuwepo ungecheka”
“Mmmm sasa ulirudije mjini?”
“Wale vijana wakaniazimisha simu na nikampigia my husband(mume wangu) nikamuelekeza nilipo akaja kunichukua na tukarudi mjini pamoja”
“Ulimuambia jamaa kuhusiana na jinsi ulivyo fika porini?”
“Ndio ila nilimuambia kuna majambazi ndio waliniteke...Ehee Madam Merry anaendelea vizuri amefanyiwa upasuaji na kizazi chake kimerekebishwa vizuri ila sasa hivi yupo powa”

Madam Rukia alibadilisha mada baada ya mume wake kufika katika eneo tulilopo na sikuwa na haja ya kujiuliza ni kwanini amebadilisha mada nikajua moja kwa moja ahitaji mumu wake atambue kuwa mimi nilikuwa naye porini

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI

KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)