SORRY MADAM (35)

0
SEHEMU YA THELATHINI NA TANO
ILIPOISHIA...
“Kipo wapi mkuu tukushuhulikie?”
“Kipo huku juu twendeni mukaking’oe”
Nikaingia jikoni na kujibanza kwenye mlango na wakapita bila kuniona na kuingia chumbani kwa mama na nikatoka na kushuka kwenye ngazi kwa haraka na kutoka nje na kuanza kukumbia na kabla sijafika getini nikaisikia sauti ya baba

NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU

SASA ENDELEA...
“Wewe mpumbavu hapo getini mkamate huyo mshenzi”
Sikusimama na askari wa getini akanipisha na sote kwa pamoja tukatoka getina na tukaingia kwenye taksi na kumuomba dereva aondoke kwa kasi.
“Mbona hujanikamata?”
“Siwezi kufanya hivyo kwa maana mama yako amanisaidia kwenye mengi na nikifanya hivyo nahisi hata mbinguni sinto kanyaga”
“Nashukuru ndugu yangu”

Nikafungua begi langu kutoa noti kumi za dola mia mia na kumpa askari wa getini akanishukuru kupita maelezo kwa muonekano wake tangu azaliwe hakuwahi kushika kiasi cha pesa nilicho mpatia kwa maana anaonekana kuzishangaa
“Eddy kuna gari inatufwatwa kwa nyuma hembu iangalie sio ya baba yako?”
Sheila aliniambia na kunifanya nigeuke na mapigo ya moyo yakanza kunienda mbio baada ya kuiona gari ya baba ikija kwa kasi nyuma yetu na gafla dereva akafunga breki za kistukiza hii ni baada ya basi dogo aina ya DSM kujaribu kilipita lori lenye tela refu na kugongana uso kwa uso na gari ndogo aina ya VOXY iliyokuwa ikija kwa kasi kwenye upande na kusababisha ajali mbaya huku gari hizo zikiziba barabara nzima

Nikafungua begi langu kwa haraka na kutoa noti mojaya dola mia na kumkabithi dereva taksi kisha sisi tukashuka ndani ya gari na kuanza kukimbia rukijichanganya na watu walio anza kukusanyika wakitoa misada kwa majeruhi wa gari mbili hizi.Mimi na Sheila tukapanda bodaboda za pikipiki pasipo baba na watu wake kutuona na kuwaomba boda boda kutupreleka kiwanja cha ndege cha mwalimu Julias Kambarage Nyerere pasipo baba na watu wake kujua ni wapi tulipo elekea.Tukaingia kwenye sehemu ya kutazama ratiba za ndege zilizopo kwa wakati huo na kukuta zimesalia dakika kuni na tano ndege ya shirika la Qatar Airways na nafasi za tiketi zilibakia tatu tu.Tukakata tikakata tiketi mbili na kuwa miongoni mwa abiria wa ndege hii itakayo ondoka ndani ya dakika kumi zijazo.Kwa haraka haraka tukapanda mstari na kuanza kukaguliwa na wakaguzi tulio wakuta kwenye uwanja wa ndege.
“Wewe kijana kaa pembeni”

Askari aliye valia sare zake za kazi huku mwili wake ukiwa umepanda juu na kujazia kwa misuli mizito aliniambia huku akininyooshea mkono wake na kunifanya nianze kupata wasiwasi.Sheila akaruhusiwa kuingia upande wa pili ili kujumuika na abiri wengine wanao iwahi ndege.Nikamkonyeza Sheila asiondoke na anisubiri kwani sikujua ni kitu gani kilicho mfanya askari huyo kuniambia nikae pembeni.Wakaja askari wengine wawili wakiwa na mbwa wakubwa na kusimama karibu yangu huku mbwa wao wakianza kunimusa nusa
“Kijana tunakuomba utufwate tunamazungumzo na wewe”

Askari aliye niambia nisimame pembeni alizungumza huku akiwa amelishika begi langu lenye pesa na vitu vyangu muhimu.Sikuwa na jinsi zaidi ya kuanza kumfwata kwa nyuma askari hadi kwenye moja ya chumba na kuingia naye na kukutana na askari wengine wawili wakiwa wamekaa kwenye moja ya meza moja kubwa na baada ya kumuonamwenzao wakampisha na kuanza kuuanali kwa macho ya dharau kuanzia chini hadi juu na kwaishara wakanionyesha sehemu ya kukaa na nikatii nikiwasubiria waniambie kitu ambacho wanataka kuniambia.Nikashangaa kumuona askar mmoja akilifungua begi langu na baada ya kuziona pesa zangu akaanza kushangilia kisha akavimwaga vitu vyote juu ya meza
“Mbona munamwaga vitu vyangu?”
“Tunakagua tunakuomba uwe mtulivu la sivyo hutotoka mikononi mwetu”

Ikanibidi nikae kimya huku mara kea mara nikiitazama saa ya ukutani na kuona dakika zikikatika taratibu huku zikiwa zimebakia dakika tano tuu ili ndege ifungwe na kuaondoka.Wakaanza kuchagua kitu kimoja baada ya kingine na kuanza kuzisoma baadhi ya karatasi za mama nilizo ziweka kwenye begi na askari mmoja akaanza kuipisha kila karatasi kwa wezake na wakaanza kuisoma taratibu huku wakinitazama usoni
“Hii si nyaraka ya serkali?”
“Ndio inabdidi atueleze vizzuri kuwa hizi karatasi za mikataba amezito wapi”

Askari wakaendelea kubishana wao kwa wao huku wakiendelea kuzitazama karatasia ambazo sikuzisoma na sikujua ni nyaraka gani wanazo zizungumzia.Ikanilazimu kuwaomna ili wanionyeshe karatasi hizo ila wakakataa
“Wewe mikataba ya wizara ya Afya umeitoa wapi?”
“Ehee....”
“Umelisikia vizuri swali langu sina haja ya kulirudia”
“Mikataba hiyo ni ya mama yangu ambeye ni waziri wa hiyo sector”
“Aaaa kumbe nyinyi ndio munaowapelekea wazazi wenu mikataba ili wakasaini ili kuidhulumu serikali yetu si ndio?”
“Sikia mkuu mimi sio kwamba nimeichukua hiyo mikataba kwa ajili a kwenda kumpa mama yangu.....Nyote ninaamini kuwa mujua ya kwamba mama yangu pamoja na viongozi wengine wamekamatwa na sijui kuwa nyinyi muna kazi gani kwa maana hamuonyeshi juhudi zozote katika kuwakomboa viongozi hao”

Nilizungumza kwa hasira huku nikinyanyuka kwenye kiti na kuwafanya askari kuchomoa virungu vyao na kuanza kunisambulia kwa kunipiga sehemu mbali mbali za mwili huku nikimshuhudia mmoja waoa akiingiza pesa zangu kwenye mifuko yake ya suruali na kujikuta nikikasirika na kumsukuma na kuanza kuminyana naye kuzichomoa pesa zangu mifukoni mwake na kuzidi kuwongezea wezake hasira na kuzidi kunipiga virungu na mateke yaliyo tua tumboni na kifuani na kuuufanya mwili wangu kunifanya nianze kutokwa na damu za mdomoni na puani

Gafla mlango ukafunguliwa na akaingia Sheila akiwa ameongozana na waziri mkuu Bi.Maimuna Ramadhani na akaonekana kushanga na kuwafanya askari kuancha kitendo chao cha kunipiga.Nikabaki nikiwa nimejikunyata chini huku damu zikiwa zinaendelea kunimwagika huku mwili mzima ukiwa umetawaliwa na maumivu na uvimbe kwenye sehemu za kichwa chanu.Sheila akapiga magoti hukua akilia kwa uchungu na kutoa kitambaa chake na kuanza kunifuta damu zinazo nitoka
“Hii ndio kazi muliyo agizwa na serikali kuwapiga watu kiasi hichi?”

Swali la wa waziri mkuu likawafanya askari wote kukaa kimya na sikujua waziri mkuu imekuaje akaja katika chumba hichi ila uzuri ni kwamba ni rafiki wa mama na muda mwingi huwa wanashirikina sana katika maswala yao ya kina mama hususani katika uanzilishi wa mambo ya vikoba kwa wanamama wajasiriamali
“Eddy Eddy”
“Mmmmm”

Mdomo wangu haukuweza kufunguka kutokana na kuvimba kwa mdomo ambao pia umejeruhiwa kwa kupiwgwa na askari hawa ambao sasa hivi wamejikausha kama wamemwagiwa maji ya baridi.
“Kwahiyo hamuna majibu ya kutoa”
Nikamnyooshea askari mmoja aliye chukua pesa zangu na kumf anya waziri mkuu kunimtazama huku akiwa haelewi ni nini kinachonifanya nimnyooshee mkono,Nikajitahidi kunyanyuka kwa msaada wa Sheila na akanikalisha kwenye kiti
“Eddy mwanangu pole sana......”

Waziri mkuu akamnong’oneza Sheila na kumfanaya Sheila kutoka ndani ya chumba na baada ya muda akarudi akiwa ameongozaa na mlizi wa waziri mkuu
“Nipe simu”
Mlinzi wa waziri mkuu akatoa simu na kumkabidhi waziri mkuu na akaminya batani na kuiweka simu yake sikioni
“Habari yako kaka”
“Sasa kuna vijana wako wamemjeruhi kijana wangu pasipo kuwa na sababu ya msingi sasa ni hivi ninakuomba uwafute kazi mara moja”
“Asante”

Waziri mkuu akampa mlinzi simu kisha akanisogelea na kunitazama kwa macho ya huruma
“Mwanangu pole sana”
“Asa...n.te”
“Ulikuwa unakwenda wapi?”
“Tulikuwa tunakwenda Iraq mama jana alimpigia simu Eddy na kumuomba amfwate”

Sheila akajibu kwa niamba yangu kwani mdomo wangu ulivimba sana na kunifanya nishindwe kuzungumza vizuri na kumfanya waziri mkuu kuhamaki
“Alisema you Iraq sehemu gani?”
“Hakusema kwani alipokonywa simu na watu walio wateka”
Waziri mkuu akaichukua simu yake na kupiga namba baadhi na kuisikiliazia simu yake na kukifanya chumba kizima kikiwa kimya tukimsikiliza
“Shikamoo muheshimiwa Raisi”
“Mimi nipo salama tu kuna taarifa hapa nimeipata kuwa viongozi wetu wapi Iraq na ndipo walipo shikiliwa mateka”
“Ndio taarifa nimeipata kwa mtoto wa Grace na anadai jana alizungumza na mama yake”
“Sawa mkuu nashukuru kwa ushirikiano wako”

Waziri mkuu akakata simu na kuwatazama askari walio nipiga na kumuagiza mlinzi wake awaandike majina yao pamoja na namba zao za kwenye mashati
“Wa..napes....a zan..gu”
Nilizungumza kwa kujikaza japo ninapata maumivu makali ila ikanilazimu kufanya hivyo na Sheila akasima na kumsogelea askari niliye mnyooshea mkono kwa mara ya kwanza na akanza kumpapasa mifukoni na kuzitoa pesa zangu na kumfanya waziri mkuu kuzidi kupandwa na hasira na kumpiga kibao askari huyo na kumfanya azidi kutetemeka
“Pumbavu...binti watazame na hao wengine”

Sheila akaanza kumpitia askari mmoja baada ya mwengine na kuzitoa wallet zao na kuchomo pesa zote walizo kuwa nazo na nyengine hazikuwa za kwangu ila Sheila akazichukua.Akaingia mkuu wa usimamizi wa uwanja ambaye ni askari mkuu
“Vijana wako hawa kuanzia sasa hivi sitaki kuwaona kazini.SAWA”
“SAWA MKUU”

Tukatoka kwenye chumba huku Sheila akinisaidi katika kutembea na baadhi ya watu wakaanza kutushangaa kila tunapopita.Tukaingia kwenye gari ya waziri mkuu na maja kwa moja wakanipeleka Hospitali ya Muhimbili na madaktari wakanipokea na kuanza kunifanyia huduma huku wakinichoma sindano za kupunguza maumivu.Waziri mkuu akatoa maagizo kwa madaktari nitibiwe katika uangalizi mzuri la sivyo watakiona cha moto kisha yeye akaondoka na kutuacha mimi na Sheila.
Baada ya siku mbili nikapata uwezo wa kuzungumza vizuri kama awali japo kuna sehemu za mwili zina maumivu makali bado.

“Sheila ile simu ilikuwaje wazari mkuu alikuja kwenye chumba tulichopo?”
“Alikuwa kwenye dhiara pale uwanja wa ndee na ndio alikuwa anamaliza kuzunguka kwenye baadhi ya ofisi.Nikamfwata na kumuelezea na kwabati nzur nilivyomuelezea kuhusu wewe akanielewa ndio tukaja mule ndani”
“Aaha nashukuru kwa hilo mke wangu”
“Ila zile tiketi nimezirudisha na nimewaambia kuwa tumepata dharula ila hadi utakapo pona ndio tutakwenda Iraq”
“Sawa ila waziri mkuu hakukupigia siku mbili hizi?”

“Alinipigia na nilimuwambia kuwa unaendelea vizuri na yeye akaniambia zoezi la kuwatafuta viongozi linaendelea vizuri hatuna haja ya sisi kwenda kwa Iraq kwani itaongeza matatizo zaidi”
“Sawa ila ndini ya mwili najisikia maumivu sana”
“Sehemu gani?”
“Hapa kwenye kifua kunaniuma sana nikihema hivi niihisi harufu ya damu”
“Weee ngoja basi nimuite dakari”

Sheila akasimama na kwenda kumuita daktari aliye kabidhiwa kwa kuniangalia kwa ukaribu sana.Sheila akaanza kumuelezea dakatari hali ninayojisikia na kumfa ya daktari kutoa agazo kwa wezake wanifanyie uchunguzi zaidi.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI

KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)