SORRY MADAM (73)

0
SEHEMU YA SABINI NA TATU
ILIPOISHIA...
PHIDAYA AKANIRUSHIA KWA NYUMA BASTOLA YAKE, NIKAUCHUKUA MKANDA WA SITI WA SITI YA NYUMA NA KUANZA KUUVUTA NIKIJARIBU KUUKATA ILA NIKASHINDWA.NIKAMTAZAMA
“EDDY UNATAKA KUFANYAJE?”
“NATAKA KUKATA HUU MKANDA NIUFUNGE MGUU WANGU UNAVUTA SANA”

NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU

SASA ENDELEA...
PHIDAYA AKAFUNGUA KWENYE KISANDUKU KILICHOPO PEMBENI YA SITI YA DEREVA, NA KUANZA KUTOA VITUVITU, VILIVYOMO NDANI YA KISANDUKU, AKABAHATIKA KUPATA MKASI NA KUNIKABITHI.NIKAUCHUKUA MKASI NA KUUKATA MKANDA WA SITI NA KUUFUNGA MGUU WANGU ULIO VUNJIKA, MAENEO YA MAPAJANI, HADI NILIPO HAKIKISHA KWAMBA NIMEUNGUZA MISULI KUVUTA, NIKAJILAZA VIZURI KWENYE SITI NA KUTOA MAGAZINE YA BASTOLA NA KUKUTA IKIWA NA RISASI ZA KUTOSHA.NIKAITAZAMA GARI INAYO TUFWATILIA, NIKASHUHUDIA JINSI INAVYO KUJA KWA KASI,

AKACHOMOKA JAA MAA MMOJA KWENYE KIOO CHA GARI LAO HUKU AKIWA NA BUNDUKI AKIJIANDAA KUFYATU RISASI NYINGINE KWENYE GARI LATEU.NIKAANZA KUHESABU MOJA HADI TATU KIMOYO MOYO HUKU BASTOLA NIKIWA NIMEISHIKA KWA UMAKINI MKONONI MWANGU, NIKABANA UMZI KWA NGUVU, KISHA NIKAFYATUA RISASI TATU MFULULIZO KUELEKEA ALIPO JAAMA, KWA BAHATI NZURI RISASI ZOTE LILIATA KIFUANI NA KUSABABISHA KUNING’INIA TU

NIKAFYARUA RISASI NYINGINE MBILI KWENYE KIOO CHA DEREVA NA KULISABABISHA GARI LAO KUYUMBA, JAMBO LILILO PELEKEA GARI KUANZA KUSHUKA CHINI KWENYE KORONGO LILILO EMBEZONI MWA BARABRA, NA KUANZA KUBINGIRIA KWENDA CHINI.PHDAYA AKAZIDI KUONGEZA MWENDO WA GARI TUKIKATIZA KWENYE MILIMA, SIKUJUA NI WAPI TUNAPO ELEKEA ILA IKANILAZIMU KUWA MTULIVU

“UPO FRESHI EDDY?”
“NDIO NIPO POWA, TUNAELEKEA WAPI?”
“HUKU TUNAPO ELEKEA NI KWENYE SHAMBA LANGU, LA PAMBA”
“AHAA SAWA”
NDANI YA DAKIKA AROBAINI NA TANO TUKAWA TUMEFANIKIWA KUFIKA KWENYE SHAMBA LAKE, LENYE MITI MINGI YA PAMBA, TUKAINGIA NDANI YA SHAMBA HADI TUKAKUTA NYUMBA MOJA NZURI IKIWA KATIKATI YA SHAMBA NA IMEZUNGUKWA NA PAMBA NYINGI

“KARIBU”
PHIDAYA ALIZUNGUMZA HUKU AKISIMAMISHA GARI LAKE, AKAFUNGUA MLANGO NA KUSHUKA, AKAFUNGUA MLANGO WA SITI YA NYUMA AMBAPO NIPO, KISHA AKANISAIDIA KUSHUKA NDANI YA GARI, AKAENDELEA KUNISAIDIA KUTEMBEA HADI NDANI YA NYUMBA YAKE, NDOGO ILA IMETENGENEZWA KWA USTADI WA HALI YA JUU, AKAWASHA TAA NA TARATIBU AKANIKALISHA KWENYE MOJA YA SOFA KUBWA LILILOPO NDANI YA NYUMBA YAKE

“POLE SANA EDDY”
“NASHUKURU, HAPA UNAISHI NA NANI?”
“HUWA NINAISHI PEKE YANGU, MUDA WA MAPUMZIKO, KAMA LIKIZO na huwa ninanunua vyakula vinavyoweza kudumu hata kwa miezi sita pasipo kuharibika na kama unavyo ona, umbali kutoka huku hadi mjini”
“Ahaaa sawa”

Phidaya akaingia kwenye moja ya chumba kisha akarudi akiwa amebadilisha nguzo alizo kuwa amezivaa na kukaa kwenye moja ya sofa ambalo lipo karibu na sofa nililo jilaza
“Eddy kuna kitu nahitaji kukuuliza”
“Uliza kama huto jali”
“Wewe haswa ni nani?”
“Kivipi?”
“Nahitaji kujua ukweli kuhusu wewe, juu ya maisha yako na kazi zako”

Phidaya alizungumza huku akinitazama machoni, kwa umakini.Nikaanza kumuelezea Phidaya juu ya maisha yangu ya nyuma, kuhusiana na machafuko yanayo endelea kwenye familia yangu, japo kuna baadhi ya vitu sikuviweka wazi kwake, kama swala la kumuua Derick kikatili sana.
“Pole sana Eddy”
“Asante”
Sikuona haja ya kuendelea kukaa na sura bandia, ikanilazimu kuvua sura bandia nilivyo pandikizwa juu ya sura yangu japo inasababisha maumivu mengi, ila nilijikaza, na ikawa ndio mara ya kwanza kwa Phidaya kuiona sura yangu halisi
***
Hali ya mguu wangu kuendelea kuimarika huku vidonge vya kurudisha kumbukumbu anavyo nipa Phidaya vikaanza kufanya kazi, na taratibu kumbukumbu zangu zikaanza kurudi moja hadi nyingi, hali iliyoa anza kuleta matumaini kati yangu na Phidaya ambaye anaendelea kunipatia matibabu kila kukicha, kwa dawa na mazoezi ambayo Phidaya, ananipatia nikajikuta mguu ukianza kupona, hadi nikaanza kuacha kutembele gongo lililo kuwa likinisaidia kutembelea.Baada ya miezi minne nikawa nimepona kabisa hata maumivu ambayo nilikuwa nikiyapata yakawa yamekwisha kabisa
Katika kipindi ambacho tumeishi kwenye hili shamba la pamba, haikutokea hata siku moja mimi na Phidaya tukazungumzia swala zima la mahusiano ya kimapenzi, kwani heshima niliyo jijengea kwa Phidaya ni kama, dada na kaka

“Eddy hivi, una mchumba?”
“Hapana”
“Unamipango gani kwa sasa”
“Nahitaji kurudi, Tanzania kujua kama mama yangu yupo hai au lah”
“Nitakusaidia katika hilo pia”

Phidaya alizungumza huku akinitazama kwa macho malegevu, yaliyo jaa hisia kali za kimapenzi, akanisogelea sehemu nilipo simama na kunikumbatia kwa nguvu.Ikachukua kama dakika tano, Phidaya akiwa amenikumbatia mwilini mwangu.Phidaya akaanza uchokozi wa kama mwanamke akiwa anahitaji kitu muhimu kutoka kwa mwanaume.Kutokana na uzoefu wangu wa kuwajua wanawake, haikunia shida sana ikanilazimu na mimi kuanza kuonyesha makeke yangu ya mikono yangu kupita sehemu mbali mbali za mwili wa Phidaya, na taratibu tukajikuta tukizama kwenye dimbwi kuwa la mapenzi, na kadri ya jinsi tulivyozidi kupeana raha, ndivyo jinsi, hisia kali za upendo zilivyo zidi kukua kati yetu

Siku ya pili tukakubaliana kwenda mjini kufanya baadhi ya manunuzi ya vitu vya kuweka ndani, ikiwemo chakula kwani kinakaribia kuisha.Alfajiri na mapema tukaingia kwenye taksi ambayo tulikuja nayo kipindi tunatoroka kutoka mjini.Phidaya akawa ni dereva wa kuendesha hadi tukafika mjini, tukapitia benki ambapo Phidaya alichukua kiasi kikubwa cha kutosha kwa manunuzi tulio yapanga kisha, tukaingia kwenye maduka ya nguo, na akaninunulia nguo mpya

“Kuna duka flani la kike ninahitaji nikanunue nguo”
Phidaya alizungumza huku akiendelea kunichagulia nguo ambazo alihisi kwamba zitaupendezesha mwili wangu
“Lipo wapi?”
“Upande wa pili wa barabara, ili kufidia muda wewe chagua nguo utakazo ona zinatosha, nikuachie pesa, na utanikuta kwenye hilo duku”
“Nitalijuaje?”
“Ukivuka tu barabara upande wa kulia kwako, utakuta duka lina masanamu mengi yamevalishwa nguo za kike”
“Ahaaa powa”

Phidaya akaniachia kiasi cha kutosha na kuvuka upande wa pili wa barabara, mimi nikachagua nguo zangu kisha nikaelekea kwenye duka alipo Phidaya, nikamkuta akiwa anachagua nguo,
“Eddy hii inanifaa?”
“Ndio inakufaa”

Tukiwa tunaendelea kuchagua nguo akaingia mwanayume mmoja akiwa amebeba mkoba wa kike, akasimama akitizama tizama baadhi ya nguo, akatoa simu yake ambayo inaita nakuzugumza na simu, kisha akaikata na akasimama akitazama nje.Baada ya muda akaingia mdada aliye jitanda baibui lililo funika hadi macho yake huku tumbo lake kidogo likiwa ni kubwa akionekana ni mjamzito, dada huyo akavua baibui lake ndipo macho yangu yakamshuhudia Dorecy akiwa amesimama kiuvivu, huku mimba aliyo nayo ikionekana kumpelekesha sana, na kwabahati mbaya hakuniona mimi nilipo
Nikamtazama kwa makini jinsi anavyo zungumza na mume wake, hadi Phidaya akanigusa bega

“Mbona unamtazama sana yule dada wa watu?”
“Ninamfahamu”
“Unamfahamu?”
“Ndio”
“Ni nani?”
“Anaitwa Dorecy”
Tulizungumza kwa sauti ya chini huku, tukimtazama Dorecy akichagua chagua nguo na mume wake
“Huyu ndio yule msichana, aliye nipiga na kuondoka na kiasi kikubwa cha madini yangu”
“Ahaaa”
“Ngoja kwanza, nisubiri hapa”

Nilizungumza huku nikizunguka upande wa pili alipo Dorecy na mumuwe, nikajibanza kwenye moja ya kabati lenye nguo, simu ya mume wa Dorecy ikaita na kumlazimu kutoka nje kuzungumza na simu hiyo.Nikapiga hatu za umakini, hadi sehemu alipo simama Dorecy na kumgusa kwa nyuma.Akageuka, na kujikuta akinitazama kwa macho yaliyo jaa mshangao mkubwa kwani hakutarajia kuniona nikiwa katika eneo hili.Nikamvuta hadi kwenye sehemu ambayo si rahisi kwa watu kutuona, hii ni kutokana na wingi wa nguo zilizo pangwa

“Eddy..nisamehe”
“Sikia sina haja ya kuombwa msamaha, ninacho kihitaji ni madini yangu, la sivyo nitalitumbua tumbua hili jitumbo lako kama sikujui”
Nilizungumza kwa sauti nzito iliyo jaa hasira pamoja na msisitizo mkali, mwili mzima wa Dorecy ukawa na kazi ya kutetemeka mithili ya mtu aliyepo kwenye baridi kali sana
“Yaaa, yaapo kulee”

Nikatazama juu kuchunguza kama kuna kamera yoyote ya ulinzi, ila sikuona, nikamtndika Dorecy kofi moja la kumuweka sawa
“Nimekuambia nahitaji madini yangu sawa?”
“Ndio, yapo kwa kule kule kwangu”
“Nitayapataje?”
“Eeheee?”

Nikaona Dorecy anababaika sana na kunipotezea muda, nikamtandika kibao cha pili ambacho nikizoto kuliko hata cha mara ya kwanza, hadi kuna dada mmoja akachungulia, nikajifanya nikimkumbatia Dorecy kama mpenzi wangu, dada aliye chungulia akaachia tabasamu na mimi, nikatabasamu kinafki ili airudishe sura yake alipo itoa.Alipo irudisha nikamuachia Dorecy na kumkuta sura yake imejaa machozi mengi

“Usijidai unalia kinafki, sasa leo nitakuzalilisha mbele ya mume wako”
“Hapana Eddy usifanye hivyo, mume wangu ni mtu mwenye pesa sana, atakudhuru wewe”
“Haaa na anidhuru kwahiyo pesa zake ndio unadhani kwamba ninaziogopa, si ndio”
Nilizungumza kwa hasira huku nikiwa nimeshika kiganja cha mkono wa kuliwa wa Dorecy na kukiminya kwa nguvu zangu zote.Dorecy akaanza kutoa kilio cha maumivu, simu yake aliyo ishika mkono wakushoto ikaita na kuona jina mume wake

“Pokea sasa”
Nilimuamrisha huku nikimuachia mkono, kabla ya kupokea nikamuona mume wake akija nyuma ya Dorecy
“Mumeo huyo hapo, ole wako uropoke”
Dorecy akajifuta machozi haraka, hadi mume wake anafika sehemu tuliyopo, sura yake imejaa uchangamfu wa gafla, wakazungumza kiarabu ambacho sikukielewa, nikashangaa mume wake akinipa mkono huku akiwa na tabasamu

“Eddy huyu ni mume wangu, anaitwa Khalid, nimemuambi kwamba tumesoma wote”
Nikatingisha kichwa, nikilipokea tabasamu la mume wake, tukaachiana mikono, kitu ambacho mume wake alikifanya na kuzidi kuniboa ni kumkumbatia Dorecy kwa nyuma na kuanza kumchezea chezea tumbo lake huku akizungumza maneno nisiyo yaelewa, Dorecy akanitazama machoni, na kugundua nilivyo kasirika
“Anasema, kwamba mtoto nitakaye mzaa atamleta Tanzania”
Dorecy alitafsiri maneno aliyo yazungumza mume wake
“Muambie hatutaki watoto kama wake, na utazaa Zombi kama sijakusoa”

Mume wa Dorecy akatabasamu baada ya Dorecy kumtafsiria nilicho kizungumza, na nina uhakika kwamba Dorecy alicho kizungumza sicho nilicho muambia
“Nataka, madini yangu, la sivyo nitakufanyia oparesheni bila ganzi ya hilo jitumbo lako”
Nilizungumza na kuachia tabasamu pana, kumfanya mume wa Dorecy kuto kuelewa kitu ninacho kimaanisha, nikawapa mikono na kuondoka zangu kurudi sehemuu nilipo muacha Phidaya

“Eddy umemaliza?”
“Ndio, ila kuna kazi nahitaji kuifanya peke yangu”
“Kazi gani?”
“Tutazungumza”
Phidaya akawa amesha maliza kununia alichokuwa anahitaji kukinunua, tukatoka nje na kuingia ndani ya gari

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI

KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)