Notifications
  • MY DIARY (38)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA NANETULIPOISHIA...Usiku nilishituka usingizini baada ya mbu kuning’aata na kunisumbua sana. Niliwachukia sana hao mbu kwa sababu walinikatisha ndoto yangu ambayo nilikuwa nikiota.Ndoto ilikuwa ikielezea jinsi harusi yangu na Mark itakavyokuwa. Ndoto ilikuwa tamu sana maana ilinipa taswira ya picha halisi ya maisha yangu ya mbeleni.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilishusha neti…
  • MY DIARY (37)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA SABATULIPOISHIA...Hapo alitulia tulii kama mtu aliyeaamia dunia ingine. Kimoyo moyo nikawa najisemeha kama amehamia dunia ingine na kuanza kuwaza ujinga sahuri yake mimi nipo kazini bwana acha nitafute hela. Ndio ni lazima nifanye kazi kwa utaalamu na utundu wa hali ya juu ili waendelee kusimuliana huko mjini ili niendelee kupata hela.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Wewe…
  • MY DIARY (36)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA SITATULIPOISHIA...Sasa wewe fikiria mimi niliyeletewa zawadi sikujua ni zawadi gani lakini yeye tayari alishafungua na kuchungulia na kujua nini kilifungwa huko ndani.Basi nikaendelea kumuhudumia yule mama huku na yeye akiniambia kuwa itabidi nikimmaliza hizo zawadi tusifungue hapo hapo na waniimbie wimbo wa happybirthday.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Tuliendelea na stori mbili…
  • MY DIARY (35)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA TANOTULIPOISHIA...Tatu niliambiwa kuwa ndugu zake na wazazi wake walihusika kwenye mipango hiyo hivyo walibariki kabisa huyo binti kuniacha mimi mumewe wa ndoa na kuamua mtoto wao aolewe upya. Nne ni kwamba huyo mzungu amewaamishia wazazi wake mjini na amewajengea nyumba ya kifahari.Kwa hiyo mimi ninavyowapigiana simu na kuwajulia hali kumbe wenzangu huwa wananichora tu.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (34)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA NANETULIPOISHIA...Hapo nikakumbuka kuwa zile zana zangu za kazi nilikuwa nazo ni vile vifaaa vya kupimia ukimwi ambavyo huwa navitumia kabla ya kukutana na mwanaume yeyote nisiyemfahamu. Nikaamua kumkubalia huku nikiamini kuwa hiyo ndo kinga yangu pekee iliyobaki kama mwanaume huyo atataka kuzini na mimi usiku huo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi tuliondoka na kwenda sehemu…
  • MY DIARY (33)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA TATUTULIPOISHIA...Nilikuwa nachanganya staili za kijamaika na hizi za kwetu, sikuacha pia zile za Nigeria hapo nikapata vitu vyangu vya tofauti kabisa. Basi baada ya kujihakikishia kuwa nipofiti kwa mastahili yangu hayo nilisubiri siku ya shindano ifike nikafanye yangu. Siku ya shindano ilifika na mimi nilikuwa miongoni mwa washiriki walioingia tatu bora.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (32)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA MBILITULIPOISHIA...Lakini kuchepuka kwangu na kuingia mgombani haikumaanisha kuwa sheria ingeniacha hivi hivi.Ilifika mahali ikabidi nizime gari na kutulia tulii kusikilizia nini kitafuata.Tayari nilikuwa nimezungukwa na mapolisi ambao walikuwa wakinifuatilia kwa kutumia pikipiki.Kwa bahati nzuri dereva wa lile gari na yeye alishafika hapo na alishawaambia polisi kuwa mimi naugua ukichaa na nilifufuka kutoka mochwari.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA…
  • MY DIARY (31)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA MOJATULIPOISHIA...“marehemu pia alinieleza kuwa ana miliki duka la vitu vya urembo wa kike ambalo pia Leah analisimamia ila hilo apewe mdogo wake Marry ambaye yupo hapa. Mama mdogo huyo mara baada ya kuyasema hayo alikaa zake chini. Baba mdogo ambaye hakurizika na maelezo hayo alisimama na kusema “kwa hiyo kama marehemu alijua kuwa atakufa hivi karibuni kwani nini hakufuata taratibu za kisheria za kuandika wosia na kurithisha mali.IKIWA UNASOMA…
  • MY DIARY (30)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINITULIPOISHIA...Baada ya hapo Nnilimwomba mama mdogo ajikaze na kuwatarifu ndugu wengine habari hizo za msiba.Tulisaidiana hivyo hivyo maana sio siri kila mmoja alikuwa na uchungu sana kutokana na mazingira ya kifo hicho. Habari zilizidi kusambaa kwa kasi na majirani walianza kukusanyika hapo kwa mama mdogo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Msiba ni msiba tu na ukitaka kujua binadamu…
  • MY DIARY (29)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TISATULIPOISHIA...Hapo sasa nikazidi kuchanganyikiwa ikabidi nimuulize mama huyo alikuwa akifanyia shughuli zake za kujipatia kipato sehemu gani.? Yule dada akanambia kuwa anafanyia soko la ndizi huko Korongoni. Sikuwa na jinsi nilimuomba anipeleke lakini na yeye alisita sita kwa madai kuwa alikuwa na kazi nyingi za kufanya na bado anatakiwa ampeleke mtoto shule.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…

SORRY MADAM (75)

SEHEMU YA SABINI NA TANO
ILIPOISHIA...
Nikiwa nifikiria cha kufanya nikastukia kitu kigumu kikinigusa kichwani mwangu, na kusikia sauti ya mwanaume ikiniamrisha nilale kama nilivyo na nisifanye kitu chochote la sivyo atauchangua ubongo wangu, taa kubwa lenye mwanga mkali likageukia sehemu ya sisi tulipo, juu ya ukuta na kuwafanya Khalid, Dorecy na watu wake kutuona.

NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU

SASA ENDELEA...
Na Khalid akaagiza mtu huyo kunishusha kwenye ukuta.

Nikashusha pumzi taratibu, jamaa akanigusa tena na ndunduki yake kwenye kichwa changu na kuniamrisha kushuka kwenye ukuta, kwa haraka sana nikajigeuza na kuichota miguu yote ya mtu huyo na kumfanya aangukie ndani kama mzigo wa kuni, nikajirusha na kuangukia nje ya sehemu ambayo nimetokea, cha kumsukuru Mungu sijaumia sehemu yoyote ya mwili wangu ambayo itanizuia mimi kukimbia.Nikanyanyuka haraka na kuhakikisha bastola yangu ipo sehemu nilipo iweka nikaikuta ipo.Kelele za ving’ora vya hatari vikanifanya nianze kukimbia kwa kasi zangu zote na kutokomea msituni, kelele za mbwa wengi, nikaanza kuzisikia nyuma yangu, na kadri ninavyo kimbia ndivyo jinsi zilivyo zidi kuja nyuma yangu kwa kasi kubwa.Milio ya bunduki ikazidi kunipa changamoto ya kukimbia kwani watu wa Khalid wapo nyuma yangu, nikajibanza kwenye moja ya mti baada ya kuona risasi zinazidi kuwa nyingi nyuma yangu.Kundi kubwa la walinzi wa Khalid wakazidi kunifwatwa kwa nyuma.
“Mungu bariki”

Nimaneo niliyo yasema kimya kimya moyoni mwangu, kisha nikaanza kujibu mapigo ya risasi niazo rushiwa kwa fujo, nikaendelea kuwafatulia watu wa Khalid na kuwaangamiza kila ambaye nilimfyatulia risasi.
Nikastukia kuona mwanga mkali wa ukinimulika kutoka juu, nikatazama na kukuta ni Helcoptar, nikaanza kusikia sauti kutoka kwenye kipata sauti ikiniomba nijisalimishe la sivyo nitauawa kwani sehemu nzima ya msitu imezingirwa, nikaitoa magazine ya bastola yangu na kukuta imebakiwa na risasi moja tu, na nyuma yangu kundi la watu wasio pungua ishirini, wananifwata kwa kuyata, huku wengine wakiwa awanatokea mbele yangu.Mwanga wa Helcoptar ukaendelea kunimulika kiasi cha kuninyongonyeza kabisa katika kupata matumaini ya kujiokoa.Sikuwa na jinsi zaidi ya kupiga magoti chini, huku miono yangu nikiwa nimeiinyoosha juu.Jamaa wakanizingira na wawili wakanisogelea nakuanza kunipapasa na kunitoa kila kitu nilicho kuwa nacho mfukoni mwangu kisha wakaninyanyua na kunifunga waya mgumu kwenye mikono yangu na safari ya kuelekea ilipo ngome ya Khalid ikaanza.

Ilituchukua mwendo wa dakika zisizo pungua kumi hadi kufika ilipo ngome ya Khalid, nikamuona Dorecy na mume wake wakiwa wamesimama kwenye moja ya ngorofa kubwa lililopo ndani ya ngome, macho yao yote yakiwa kwangu
“Ohooo karibu bwana Eddy”

Muyo ulinistuka sana baada ya kumsikia Khalid akizungumza kiswahili kizuri tu, kwa haraka nikayafikira maneno ya kejeli niliyokuwa ninazungumza na mke wake, nikiamini kwamba Khalid aelewi kitu ambacho ninakizungumza na mke wake.
“Naona umekuja kunitembelea, za masiku bwana Eddy?”
Sikumjibu Khalid zaidi ya kumtazama kwa macho makali katika sehemu ambayo amesimama, pamoja na mke wake
“Mpandisheni huku juu”

Aliwaamuru watu wake na wakaniingiza kwenye moja ya lango kubwa, tukaanza kupandisha ngazi kuelekea ghrorofani, wasiwasi wangu mkubwa ni juu ya mke wangu Phidaya, sijui akiamka asubuhi na kunikuta sipo ndani chumbani, ataamua kufanya maamuzi gani.
“Karibu Eddy, ninafurahi sana kukuona hapa, kwa kipindi hichi kingine.Vipi ulikuwa umekosea njia ya kuja hapa?”

Macho yangu yakagongana na Dorecy aliye valia dera refu, kutokana na ujauzito wake kuwa ni mkubwa.Khalid akazitazama ishara za macho kati yangu na Dorecy kisha akatabasamu.
“Naamini, mke wangu atakuwa na furaha sana kukuona hapa mwanadarasa wake, na munavyo onekana mulikuwa munasoma sana eheee”
“Hee baby, hembu acha maneno yako, mimi huyo Eddy hatukuwa na ushirikiano kwenye masomo”
Dorecy alizungumza kwa sauti nyororo iliyo mbembeleza mumewe, na taratibu akamsogelea mumewe na kuanza kuzichezea nywele za kifua cha mume wake
“Ohh mke wangu, sawa ila vipi, sijaielewa maana ya rafiki yako kuwa hapa?”
“Hata mimi sijui”
“Eddy, ni kwanini upo hapa?”
“Dorecy nipe mali yangu niondoke”
Nlizungumza kwa sauti nzito, na kumfanya Khalid kumgeukia mke wake
“Anakudai?’
“Ahaaa hapana ila sijui kachanganyikiwa huyo”
“Eddy, unamdai nini mke wangu?”

Kwa haraka Dorecy akanikonyeza, pasipo mume wake kumuona, nakuniomba nisizungumze kitu chochote mbele ya mume wake.Nikatabasamua na kumtazama Khalid
“Hapana, ile siku nilipo kutana na nyinyi kule dukani, Dorecy aliniambia kwamba siku moja nije kuwatembelea atanipa mali ya kutosha”
“Ohhh, mke wangu ni mali gani unataka kumpa Eddy?”
“Ni mtaji wa kufungua biashara, siku ile baby si nilikuwambia kwamba kuna bishara ya hoteli nataka kwenda kuifungua Tanzania, so nikaona mtu wa kumuweka awe Eddy kama msimamizi”
“Ahahaaaa hapo nimewaelewa, kwani mulianza kunitisha.Mfungueni”

Khalid aliwaamrisha watu wake wanifungue mikono yangu na wakatii kama bosi wao alivyo agiza, wakanifungua mikono yangu na akawaomba waondoke, Khalid akanikaribisha sebleni kwake, na tukaanza kuzungumza mambo mbalimbali ya maisha, jambo ambalo lilianza kunishangaza kwani Khalid niliye adisiwa na muendesha taksi sio huyu ninaye zungumza naye mbele yangu.
“Bwana Eddy, kunabinti atakuja hapa kukuonyesha chumba cha kulala, mimi ngoja nikapumzike na mke wangu, si unamuona jinsi hali yake ilivyo?”
“Hakuna shida shemeji”

Khalid akanyanyuka na Dorecy na kupandisha ngazi kwenda juu kabisa, macho yangu yakawa na kazi ya kuwachunguza walinzi walio simama kwenye kila kona ya jumba huili kuanzia ndani hadi nje.Akaja dada mmoja aliye valia chupi aina ya bikini na sidiria
“Nifwate”
Alizungumza kwa kingereza, pasipo kuuliza ni wapi ninapo elekea nikanyunyuka na kuanza kumfwata kuelekea sehemu anapo kwenda, tukapita kwenye moja ya kordo ndefu, nyenye wingi wa vyumba kila kona, akafungungua mlango mmojana na sote tukaingia.
“Unapenda nini, whyne, shampen, wicky au juis”

Aliniorodheshea idadi ya vinywaji ambavyo sivitumii kwa wakati huu ambao nipo kwenye ngome ambayo hadi sasa hivi sijajua usalama wangu upo kaika upande gani,kati ya kutoka salama au kutokamu ndani ya ngome hii.
“Sihitaji chochote, asante sana”
“Una hitaji huduma ya mwili wangu”
“Hapana ninashukuru”

Baada ya msichana kumjibu hivyo akajizoa zoa na kutoka ndani ya chumba changu na kuniacha nikiwa ninamawazo sana, nikazima taa za chumba kizima na kuwa giza totoro, nikaanza kuchunguza kuta moja baada ya nyingine, kutazama kama kuta kuwa na kamera zilizo fichwa kwenye kuta za chumba hichi, ambazo mara nyingi baadhi huwa zinachimbiwa ukutani, na zinatoa mwanga mwekundu kila unapo ziona kukiwa na giza.Nikamaliza kukizunguka chumba kizima na sikuona kitu cha aina yoyote, nikaipanga mito mitatu kitandani kama mtu aliye lala na kuifunika kwa shuka.Nikalisogelea dirisha taratibu na kulifungua, ukimya mwingi umetawala nje, kitu kikubwa ninacho kiona ni walinzi wakikatiza katiza kila kona ya ngome hii.

Kitu ambacho kinanifanya nishindwe kushuka kwenye chumba hichi ni kutokana, chumba kipo ghorofani na chini ni mbali sana, mwanga wa jitaa kubwa ukakatiza kwenye dirisha nililo simama na kwa haraka nikajibanza kwenye ukuta ili upite vizuri na walinzi wasione.Ukarudi tena ulipo tokea, kabla sijanyanyuka mlango wa chumbani kwangu ukafunguliwa taratibu na nikamuona Dorecy akiingia huku akiwa amevalia kagauni kakulalia
“Eddy”

Aliniita kwa sauti ya kunong’oneza, huku akielekea kitandani ambapp nimepanga mito vizuri kama mtu aliye lala.Akasimama pembeni ya kitanda changu, niaamini hakuniona kwenye sehemu niliyo simama, akakitazama vizuri mwili wa mito nilio ulaza kisha akakipandisha kigauni chake juu, na kuchomoa kisu kikali alicho kuwa amekificha kwa kukifunga kwenye paja lake kwa mpira kisha kwa haraka akakishusha na kutua kwenye mito jambo lililo nistua sana kuona Dorecy akizidi kuwa katili juu yangu

Dorecy akastuka baada ya kuona kisu kikinyanyuka na mto, ikamlazimu kufunua shuka kwa haraka kwa ajili ya kutazama kama kitandani kwangu kuna mtu, akajikuta akistuka zaidi baada ya kukuta ni mito ndio imejipanga, kwa haraka nikamrukia na kumsukimiza kitandani na kisu chake kikaangukia pembeni, nikakiwahi kukiokota kisu chake, kisha nikamuwahi kulikamata koo lake na kuliminya kwa nguvu zangu zote huku kisu nikiwa nimekinyanyua juu kwa mkono wangu wa kulia
“Unataka kuniua ehee”

Nilizungumza kwa hasira huku nikiendelea kuliminya koo lake na kumfanya atoa mlio wa kukoroma akishiria kukata roho
“E…ddy naa….”
“Hakuna cha kuomba, malaya mkubwa wewe, leo ndio utaijua jina langu la utotoni nilikuwa ninaitwa nani”
Niliendelea kukaba Dorecy koo lake, hadi akaanza kulegea, nikamuachia na kwaharaka nikashuka kitandani na kuivuta miguu yake na akaangukia mgongo kwenye sakafu, nikamnyanyua juu na kumpiga kabali kwa nyuma huku kisu changu nikikiweka kwenye tumbo lake.
“Eddy mpenzi wangu naomba unisamehe nilikuwa ninakutania tuu”

Dorecy alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake.Sikutaka kuzisikiliza porojo zake kwa maana hakuna utani wa kuuana
“Ongoza njia”
“Eheee”
“Ongoza kwenda nje”

Nilizungumza huku nikikikandamiza kidogo kisu kwenye tumbo lake lenye mtoto ndani na kumfanya aanze kutambea huku mwili mzima ukimtetemeka, akafungua mlango, na kukutana na walinzi wawili wenye bunduki wakiwa wamesimama kwenye mlango wa chumba changu, hapo ndipo nikagundua kwamba nilikuwa ninalindwa nje nisitoke.Wakanielekezea bunduki zao, ila mimi nikazidi kumkaba kabali Dorecy huku kisu nikikikandamiza kwenye tumbo lake.

“Waambie washushe bunduki zao la sivyo nakufanyia oparesheni bila ganzi”
Dorecy akawaamuru watu wake waweze kufanya kama nilivyoa mauambia, wakatii kwa haraka, tukaanzaa kutembea kwenye kordo ndefu ya vyumba, huku walinzi wake wakitufwata kwa nyuma, sikuwa na woga wa aina yoyote kutokana bosi wao yupo chini ya mamlaka yangu.Tukafika sebleni na kukutana na walinzi wapata kumi wakiwa na bunduki zao wakitusubiria sisi kutokea kwenye seble hii.
“Eddy, sasa nimeijua rang yako”

Sauti ya Khalid ikanistua, nikamuona akitokea kwenye moja ya chumba huku akiwa amevalia nguo za kulalia na mkononi mwaka akiwa ameshika bastola
“Waamrishe watu wako kutupisha la sivyo ninamuua mke wako”

Nilizungumza kwa sauti kubwa, huku nikiendela kukikandamiza kisu kwenye tumbo la Dorecy ambaye muda wote machozi yanamwagika, kwa ishara Khalid akawaamrisha watu wake kutupisha, tukapita katikati yao huku muda wote nikiwa makini sana, nikiwatazama watu wa Khalid
“Ila Eddy unacheza makida makida kwenye nyaza za umeme”

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI

KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
37 Simulizi Sorry Madam
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni