JAMANI DADA MARTHA... LOOO! (8)

Zephiline F Ezekiel
JAMANI DADA MARTHA... LOOO! (8)
Jina: JAMANI DADA MARTHA... LOOO! Mtunzi: 2jiachie SEHEMU YA NANE ILIPOISHIA... Roi alikaribishwa chumbani kwa Martha kwa mabusu mfululizo huku akipewa pole kwa kazi za mchana kutwa halafu akaambiwa… JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media ? IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI 👉 GUSA HAPA KU-INSTALL 👈 ENDELEA... “Baby, nilikumbuka kwamba kule nyumbani kwako baada ya kufunga, funguo uliiweka kulekule au ulikuja nayo?” aliuliza Martha… “Iko kwenye gari.” “Nilipenda kwenda kufanya usafi baby, labda kesho sasa.” “Kesho sawa, utakwenda. Saa ngapi?” “Jioni, kwenye saa kumi hivi.” *** Usiku wa siku hiyo, Martha alihisi kitu tofauti kwa Roi. Licha ya kumshikashika ili achaji lakini alionekana hana habari na kwanza alikuwa mbali… “Sweet, mbona kama upo mbali kimawazo?” aliuliza Martha… “Hapana, kuchoka tu na shughuli.” “Mmh! Baby jamani! Sasa ukichoka hivyo mimi nitapataje haki yangu?” “Kesho bwana,” alisema Roi akilala baada ya kutoka kuoga. *** Saa kumi na mbili, Martha alimka na kuamza kumshikashika…