
Mtunzi: Hassan S. Kajia
SEHEMU YA KUMI NA NNE
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
Aliamu kurudi akiwa tayari kwa mapambano n kwenda kukutana na kina John na Max ili kupanga mikakati ya kupambana na maadui zao. Walifika ofisini saa mbili asubuhi na kumkuta Antony akiwasubiri nje na gari lake. John alifurahi kumwona pacha wake.
JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈
ENDELEA...
Alijua yuko tayari kupambana.
John aliendelea kuzungumza na Max na Antony juu ya yaliyotokea. Walimweleza Antony kila kitu juu ya mipango yao. Alifanya hivyo ili waweze kuwa tayari katika kuhakikisha wanapata njia ya kukabiliana na maadui zao.
“Safari hii tusiwakawize, najua wapo wengi sana hasa baada ya kuniteka, nilikutana na kundi kubwa. Sasa itabidi tuichukue hii nchi kwa muda watu watatu, tunavamia Mererani tunashambulia migodi afu tutajua tu jengo lao lilipo. Sawa?” Max alisema akiwapa mbinu John na Antony.
“Sawa sawa,” John na Antony waliitikia kuonyesha wako tayari kupambana.
Max alianza kugawa majukumu kwao.
“Antony,” aliita Max.
“Ndio mkuu,” aliitikia Antony huku akimwangalia Mx kwa kuwa tayari kusikia ambacho alikuwa anataka kumwambia.
“Wewe utatumia ile Range Rover nyeusi yenye mitambo mingine ya mawasiliano,” Antony alikabidhiwa Range Rover iliyokamilika mitambo ya kuweza kuwasiliana nao. Gari lake alitakiwa na Max aliache kwani siku zote Max alitumia Range Rover kwani lilikuwa na teknolojia ya mawasiliano iliyokuwa anawajulisha askari wenzake taarifa za aliko na pia wakiwasiliana.
Aliunganisha mawasiliano ya kwenye gari na simu ya John nay a kwake ili popote atakapokuwa waweze kuwasiliana na Antony ambaye ndiye atakayekuwa akilitumia lile gari.
“Nadhani tumemalizana Antony,” Max alimkabidhi antony funguo huku Antony akimwangalia. Alimwona ni mtu aliyejua mbinu nyingi sana katika kupambana na hivyo alijua watashinda tu.
“I think we should start tonight if possible kabla hawajashtukia mipango. Nimeshajua mavazi yao, wale jamaa wanapenda mavazi meusi na miwani meusi, wanatumia gari nyingi zenye rangi ya maziwa na nyingi ni Mini Bus, hivyo Antony utatumia ile Range kuzunguka nayo na kutufahamisha walipo. Ila itakuwa vizuri kama tungejua jengo lao ili tuweze kuwavamia,” John alitoa wazo ambalo Max aliliafiki.
“Kweli John, ni vizuri tukajua wapi wanakotokea ili tujue tunaanzia wapi, nashauri Antony afanye utaratibu kwanza wa kuweza kufika huko kwa kuwafuatilia mpaka watakapoishia,” Max alitoa pendekezo ambalo hata Antony mwenyewe aliafiki na kuona kuwa hilo ndo la msingi zaidi.
Mi nitawafatilia kwanza nikishajua wanaingia wapi nitawashtua then mtanifuata, au sio?” alihoji Antony. Wote walikubali na kuonyesha ishara ya ushindi mapema kwani kila mmoja aliamini mwenzake anaweza kazi.
*****
Saa kumi na mbili jioni, Antony anaondoka na gari kuelekea Mererani. Anawaacha John na Max ambao walikuwa wakimfuata taratibu ili asije akakwama. Mpango wao wa kwenda kulipua mgodi wao kama hatua ya kwanza ya kujua mahali lilipokuwa jingo lile.
Saa mbili na nusu usiku walikuwa wamefika. Hali ilikuwa ni shwari na hivyo, Max alitoka na mabomu mawili ya kutegwa na kwenda moja kwa moja hadi katika uzio. Alitumia mbinu zake kuingia ndani. Alifanikiwa kufika hadi eneo la kuingilia machimboni na kuyatega yale mabomu mawili kisha akaondoka.
Wakiwa kwenye gari wakisogea mbali kidogo la lilipokuwa lango kubwa la kuingilia katika mgodi wa Steve. Max alimwonyesha Antony kifaa cha kulipulia na kubonyeza.
Mlipuko mkubwa ulitokea katika mgodi. Eneo zima likawa halikaliki kwani watu walikimbia ovyo. Dakika chache baadaye Antony alilipua bomu la pili na hivyo kupelekea wasiwasi zaidi uliowafanya baadhi ya wachimbaji kukimbia na kutokomea mbali. Waliamini kwamba wameshinda mpango wao wa kwanza katika kuonyesha kwamba wataweza kuwafikia kiurahisi.
Askari baadhi, walikimbilia gari na kuanza kuondoka wakielekea eneo lilipokuwa jengo lile. Hawakujua kwamba Antony alikuwa akiwafuata nyuma. Aliwafuata hadi alipoona wakiingia. Alishangaa sana kwani hakuona njia bali aliona kichaka. Magari yaliingia kichakani huko. Aliyafuata hadi alipofikia kile kichaka.
Alisimama kwa muda huku akisoma ramani ya magari yalipokuwa yakielekea hadi yalipoishia ambapo aliona lango kubwa likifunguliwa na magari yale kuingia.
Max na John walikuwa wakisubiri mawasiliano na Antony. Waliwasiliana na Antony kujua alipofikia.
“Nimefanikiwa kujua ngome yao ilipo John, inaelekea si rahisi kuingia lakini tukimteka mmoja wao itakuwa rahisi,” alisema Antony ambaye alikuwa njiani kuwafuata wenzake waliokuwa wakimsubiri ndani ya nyumba moja lililoko kule Mererani.
“Utatukuta palepale pa mwanzo tulipokutana,” alisema John wakati akiwasiliana na Antony. “Sawa kwa kuwa nimeshapajua….tusiwaache wale jamaa kwani wataleta maafa makubwa sana, inaelekea ni mtandao mkubwa kiasi cha baadaye kutishia amani ya nchi,” alisema Antony.
“Ni kweli Antony, inabidi tufanye mikakati ya kuwavamia kwa mbinu kali, njoo hapa utatupata,” alisema John.
Antony alifika na kuwaeleza yote waliyoyakuta huko. Waliamua kurudi kwanza mjini kabla hawajarudi tena Mererani kwa ajili ya kushambulia na kufanya lile ambalo walidhamiria kulifanya katika kupambana na uhalifu.
*****
Siku nmbili baadaye John, Antony, Aminata pamoja na Max walikuwa wameshagundua mpango wa Bosi Steve wa kwenda katika mkutano ambao uliwahusisha wafanya biashara wakubwa.
Max alitoa wazo la kwenda huko kuhudhuria ili kujua kitakachoongelewa ikiwa ni pamoja na kumwona Steve na kumtisha. Walikubaliana wafanye hivyo ikiwa ni pamoja na kumteka Steve ili waweze kuwadhibiti na kuwadhoofisha askari wa Mosses Ndula na Mosses mwenyewe.
“Jamani kama tunavyojua leo wanapanga kuingia The Hall City Garden kwa ajili ya mkutano wa wafanyabiashara wakubwa nadhani mpango wetu tutaukamilisha wa kumteka Steve.
Tuanzeni kujipanga namna ya kufanikisha mpango wetu ili tusije tukakose,” Max alisema huku wote wakiwa wanamsikiliza.
“Kweli, inabidi tujipange kabisa ili tusishindwe, tunaweza tukawa tumerahisisha sana kazi. Sasa iweje?” aliuliza Aminata ambaye alikuwa pembeni ya John wakimsikiliza Max.
“Sasa itabidi Antony uwahi ukumbini ili usome mchezo mzima kisha utatusubiri nyuma ya jengo hilo ukiwa tayari umeliweka gari katika mazingira mazuri,” alisema Max.
“Sawa mkuu,” aliitikia Antony huku Max akiendelea kutoa maelezo ya nini kifanyike.
“Mimi na John tutaingia ukumbini alafu Aminata atakuja pale kama mgeni. Wakiwa wanamshangaa pasipo ya sisi kuonekana itakuwa ni njia rahisi ya sisi kumkamata,”
“kweli, ila na mimi nitakuwa makini maana wanajua sehemu nyingi za mikutano huwa tunaingia wote,” alisema Aminata huku akimwangalia Max ambaye alikuwa akitikisa kichwa chake kuonyesha kwamba amekubaliana na mawazo yake.
Antony aliwaacha John na Max na kuondoka kwa ajili ya kufanya maandalizi kwani mkutano wa wafanyabiashara hao ulikuwa uanze majira ya saa kumi na nusu jioni.
Alifika na kuangalia hali ilivyokuwa kasha kuwataarifu wenzake. Wahudumu walikuwa wakipitapita kugawa vinywaji kwa watu ambao walikuwa wakisubiri mkutano kuanza.
“Tumefanikiwa kuingia, Max sasa kazi ni moja tu kuhakikisha Steve anakuwa mikononi mwetu,” alisema John. Waliwasiliana na Antony kuhakikisha kwamba ameshaegesha gari lake nyuma ya ukumbi kwani wana kila sababu ya kufanikisha mpango wao.
Ilikuwa ni zamu ya Bosi Steve kuwasili katika ukumbini ambapo alisindikizwa na Mosses Ndula pamoja na askari wanne waliovalia suti nyeusi na miwani nyeusi kuonyesha kuwa walikuwa makini sana na kazi yao.
Wakati bosi Steve akiingia chumba cha mikutano, Antony aliwasiliana na John, alimjulisha juu ya kuwasili kwa Steve na hivyo John alielekea upande wa mlango wa kutokea wa nyuma ya jengo ili kuhakikisha kuwa unakuwa wazi. Wageni wote walisimama wakati MC akizungumza machache kukaribisha wageni ili mkutano uanze.
Max alikuwa akiangalia nyendo zao huku akimwangalia zaidi Steve ambaye alikuwa mwenye furaha sana. Mhudumu alipitisha glass za wine na Steve aliichukua moja na kuanza kunywa.
Wakati mkutano unaendelea Bosi Steve alitoka na kuelekea maliwatoni. Alimhakikishia Mosses Ndula kuwa atarudi kwani Mosses Ndula alimsihi kuongozana na mlinzi mmoja.
“Usijali ndugu nitarudi mara moja, unakumbuka kabla ya safari ya huku tulikunywa wine nyingine nyumbani kwangu hivyo nahisi haja ndogo, kabla mkutano haujaanza vizuri naona ni bora nikatoe haja ndogo ili niweze kufuatilia, nitatumia dakika tano tu,” alisema Bosi Steve kabla ya kuondoka.
Max alimwona akielekea maliwato. Alihakikisha hamuachi baada ya kuona akiwa mwenyewe bila msindikizaji.
Max mara moja alifika eneo la maliwato kumsubiri Steve aingie. Aliwasiliana na John ili aweze kuzuia watu kuingia eneo hilo na badala yake awashauri watumie maliwato nyingine. Wakati huo hakukuwa na watu wakiingia maliwatoni huko na hivyo ilikuwa ni nafasi nzuri ya Max na John kufanikisha mpango wao.
Haikuchukua muda Bosi Steve aliingia, Max alisubiri hadi amemaliza na kuchomoa bastola yake na kumnyooshea Steve. Bosi Steve alishtuka kusikia sauti ya Max ikimwambia.
“Usijiguse na simama hapo hapo kama ulivyo,” kabla ya kugeuka kumwangalia aliyetoa sauti hiyo alipigwa ngumi na kuzirai. Max aliwasiliana na John kwamba kashamteka hivyo wajitayarishe kuondoka.
Antony alifungua mlango wa gari na kulisogeza mpaka karibu na mlango wa kutokea na hivyo ilimchukua Max dakika mbili kumfikisha Steve ndani ya gari hali ya kuwa amezirai.
Walifika katika nyumba moja kuukuu iliyoko maeneo ya Mianzini wakiwa wameshamteka Bosi Steve. Nyumba hiyo haikuwa inatumiwa na mtu yeyote. Ilikuwa ni saa moja na nusu usiku.
Baada ya Steve kuzinduka John alikuwa amesimama mbele yake. Alishtuka kumwona John.
*****
Ukumbini Mosses Ndula na Askari wake walikuwa wakimtafuta Bosi Steve bila ya mafanikio. Waliamua kutoka na kuelekea nje ya ukumbi wakidhani atakuwa huko kwani hata simu yake haikupatikana. Walizunguka kila mahali nje ya hoteli wakijua labda anavuta sigara sehemu.
“Atakuwa ametekwa, hivyo wasiliana na kikosi cha anga ili kuzunguka na helikopta kujua watekaji,” Mosses Ndula alimwambia mmoja wa askarti wake ili aweze kuwasiliana na askari wa kikosi cha anga waanze kazi ya kumtafuta Bosi Steve mara moja.
MAX mara moja alifika eneo la maliwato kumsubiri Steve aingie. Aliwasiliana na John ili aweze kuzuia watu kuingia eneo hilo na badala yake awashauri watumie maliwato nyingine. Wakati huo hakukuwa na watu wakiingia maliwatoni huko na hivyo ilikuwa ni nafasi nzuri ya Max na John kufanikisha mpango wao.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi