
Mtunzi: Hassan S. Kajia
SEHEMU YA KUMI NA TATU
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
“Nadhani itakuwa ni wao maana wana kisa na sisi. Antony tutampata wapi wakati huu?” anatakiwa kuwa na sisi kwani kipindi kile alikuja tukafanikisha.”
“Kwani alirudi Nairobi?”
“Ndiyo, na sasa itabidi aje tena,” John alisema huku akichukua kikombe cha chai na kubwia kidogo.
JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈
ENDELEA...
John aliendelea kusema.
“Sikuwahi fikiria kutekwa kirahisi namna ile, inaelekea wale jamaa walilifanya mipango yao siku nyingi kuhakikisha kwamba wanatuangamiza, ila walipata wapi picha yangu? Au ya Antony ile?” John aliuliza swali ambalo hakuna aliyejua jibu lake.
“Unajua ni nini John? Max alianza kumwambia John. Mi nadhani hao jamaa watakuwa wameweka makachero wa kutufuatilia pamoja na kuifuatilia serikali ni nini wanafanya pamoja na wewe, si unajua mzee wako alikuwa karibu sana na serikali,” John alitikisa kichwa kuonyesha kwamba amekubaliana na jambo ambalo Max alikuwa amelizungumza.
“Na tena hao hao makachero ndio watakuwa wamewapa hiyo picha yako, inawezekana pia picha yangu watakuwa nayo. Kwani hawajakuonyesha picha za watu wanaowatafuta?” wote walibaki kimya kutafakari nini cha kufanya juu ya watu hao. Vikombe vya chai vilinyanyuliwa na kila mmoja alikunywa kidogo na kurudisha.
Hiyo ni katika kufikiria cha kufanya.
“Ebwana kaka kwani watu hao waliwapeleka wapi?” aliuliza Max ambaye bado alikuwa anashauku ya kujua kwamba kina John walipelekwa wapi..
“Dah! Kaka sehemu tuliyoingizwa hata siijui, ila inaonekana ni bonge la jumba alilomiliki yule mkubwa wao ila sijui ipo pande zipi. Inabidi kaka tufanye mpango wa kujua wapi hilo jumba lilipo ili tuweze pia kufanikisha kazi yetu. Mikakati tutaipanga wenyewe, tumtafute Antony kabla ya kuijulisha serikali juu ya mkasa huu kwani serikali imetupa kazi hivyo haipaswi kuonyesha kama tumeshindwa, nna uhakika hii kazi ni ndogo sana,” alimaliza John huku akitikisa kichwa kuonyesha kazi anayoenda kuifanya ni ndogo sana.
“Shemeji ilikuwaje ukaweza kuwatoroka hao jamaa pamoja na wifi yangu?” Michelle ambaye alikuwa na hamu ya kujua stori nzima aliona kwamba hajaridhika na hicho kidogo alichosema John na hivyo alihoji zaidi ili kupewa uhondo zaidi.
“Shemeji, hiyo ilikuwa ni sehemu ya kazi yangu, hata wifi yako hakuamini kitu kilichotokea, sikuwa tayari kupoteza maisha yangu mikononi mwa wale washenzi hivyo ilikuwa ni lazima nitumie mbinu nizijuazo hadi tukapona. Wifi yako alikuwa kashakataa tamaa lakini kilio chake nilikisikiia na hivyo ilinibidi nichukue hatua na kuwafundisha adabu washenzi wale,” John alikuwa anaongea huku akimwangalia Michelle ambaye alikuwa akisikiliza kwa makini na kwa huruma kwa kile kilichotokea.
“Ni wapumbavu sana kwani niliwalaghai wanifungue kamba ili niweze kuagana na mke wangu, hawakujua kwamba ile ilikuwa mbinu mojawapo ambayo hawajawahi kukutana nayo milele hadi mauti yao yalivyowafika siku hiyo. Nilipambana na mmoja nikahakikisha namnyang’aya silaha kisha nikaiwahi na kuwafyatulia risasi wale wawili waliobaki. Hivyo tukapata nafasi ya kuondoka eneo hilo. Nilichukua silaha zao zote na kutoweka nazo.
John alimaliza huku wote wakicheka kwa furaha ya kuwa pamoja baada ya kipindi kifupi cha kutekwa kwa John na Aminata.
“Dah! Poleni sana, kaka umeonyesha jinsi ulivyokomaa na mafunzo tuliyopewa kipindi kile, unakumbuka watu arubaini waliondolewa kwa ajili ya kushindwa zoezi lile jepesi tuu la kumsoma adui amekaaje. Watu kama hao wangekuwa wameshakufa siku nyingi. Ila kaka hongera sana,” Max alimsifia John huku wote wakicheka kwa furaha.
Alimwona John ni mwenye kupokea mafunzo na kuyaelewa haraka kwani hata Aminata alipomfundisha pamoja na Antony walichukua muda mrefu mpaka kumaliza mafunzo. Hata Aminata alishangaa kuona wakielewa mafunzo haraka. Alijua ni kwa sababu ya haraka yao ya kutaka kulipiza kisasi cha mauaji ya baba yao kuchuku mgodi wao.
“Shemu, sasa nimeambiwa nisiende, unadhani wawili mtaweza?” Aminata aliuliza huku akinyanyua kikombe cha chai na kunywa. John alisimama na kukaa karibu na Max. alipatwa na aibu baada ya Aminata kusem vile. Hali hiyo ilimfanya Aminata aelewe kwamba anataka kumwambia kuhusu kubaki kwake wasiende pamoja. John alitaka kuongea jambo na Max huku Aminata akimwangalia kwa jinsi alivyokuwa akimsogeleahuku Max akiwa tayari kumsikiliza John.
“Max nadhani sasa tumtafute Antony ili tufanye mipango,” John alimsihi Max kuonesha kuwa alikuwa na shauku ya kupambana na adui zao.
“Ni kweli, na mbona tumeshalizungumzia hilo, Max alisema huku akimwangalia Aminata na kuhisi kwamba kulikuwa kuna jambo linaloendelea baina ya John na Aminata.
“Nitampigia simu aje, nadhani mipango tutaifanyia nyumbani kwangu kesho jioni,” John alisema huku akijaribu kumsisitiza Max kwamba ana nia ya kuwasiliana na Antony ilia je.
“Kwani Antony alisema hatakuja mwanzo?”
“Hapana,” alijibu John.
“Basi mpigie simu ili tuanze hii ishu mara moja,” Max alisema huku John akijitayarisha kumwambia jambo ambalo alijua ni lazima angebembeleza ili Max amwelewe.
“Aminata nataka akae na shemu ili sisi tuende, najua ni kazi yake lakini kwa sasa naomba akae kwanza pembeni tuende mi na wewe,” John ambaye alikuwa amekaa karibu zaidi na Max alimwambia kwa sauti ya chini.
“Kwa nini tusiende naye, unajua anajua mbinu nyingi sana, tuwe naye bana,” Max alimsihi John.
“Hapana, nimemwambia kuwa tunaye mtoto na likitokea baya atatukosa wote. Nimeonelea yeye abaki afu tuende mimi na wewe na Antony.”
“Mi sijajua, kwani yeye alisemaje?”
“Alikataa kabisa, naomba umshauri basi.”
“Mi kukushauri ntakushauri twende naye kwani najua Aminata ni komandoo, anaweza kupambana na matukio mengi ameweza kwa nini hili ashindwe na tena tuko wengi, labda Michelle ndo siwezi nikamwambia aende maana hajui lolote, ila Aminata mi naomba tuwe naye. Kumbuka ni mwalimu wako na anajua zaidi haya mambo.”
“Dah, ila kama ni hivyo tutamwelekeza tulipokwama atusaidie.” John alionekana kutokufurahia kwenda pamoja na mke wake, Aminata. Alitafuta njia yoyote itakayomfanya asiende ili awe karibu na mtoto wao.
“Sawa kama atakuja tu kama msaada. Mi nadhani wawili tukiongezeka na Antony tutaweza.”
“Basi watabaki hapa kwako.”
Max alikuwa anaishi maeneo ya Kijenge. Aliishi pamoja na Mishelle japo hawakuwa wamefunga ndoa.
Kwa kuhofia maisha yao kwa kipindi walichokuwa wakiugulia maumivu waliyoypata baada ya kuwekwa nguvuni na Mosses, John na Aminata ilibidi washinde na kulala nyumbani kwa John mpaka kwa kipindi hicho. Habari za kutekwa kwao zilienea sehemu nyingi. Waandishi wa habari na viongozi walifika na kuwatakia hali.
Waliwaeleza ya kwamba hawakujua walipopelekwa wala nani aliyefanya unyama ule. Hivyo hawakutaka polisi wafuatilie ili wao wakamilishe lengo lao baada ya kubaini kwamba baadhi ya viongozi walikuwa wakiwasaidia Steve na Mosses katika harakati zao za kufanya uhalifu kwa masilahi yao na viongozi.
Ni katika kikao ambacho kilikuwa kikizungumzia masuala ya ulinzi na amani nchini. Maofisa usalama wote walikuwepo wakiwemo Max, John na Aminata. John na Aminata walishangaa kuwaona Steve na Mosses ambao hawakuwa wahusika. Max ambaye alikuwa hajawajua alielezwa na John na Aminata.
Yaliyoongelewa huko yalikuwa ni yale yale ya askari kulinda raia na mali zao. Hawakusikia lolote kuhusu uhalifu unaoendelea. Walihisi jamaa wameshaongea na waziri wa ulinzi ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika kikao hicho na ambaye ndiye aliyesisitiza ulinzi wa askari kwa raia.
“Bado… hajaongea kitu kabisa… sijasikia akizungumzia lolote kuhusu uhalifu mkubwa unaoendelea kuumiza watu. Na wahalifu wenyewe wapo hapa hapa na wao wanasikiliza,” Aminata aliwaka akiwaambia John na Max ambao walikuwa wamesimama wakimsikiliza waziri wa Ulinzi.
“Huyu mtu aliteuliwa na rais kimakosa, hafai kuwepo….., dawa za kulevya zimepitishwa mara ngapi hapa… ulinzi upi kwa raia wakati raia na mali zao wanalia hawajui pa kukimbilia. Leo anasisitiza badala ya kuwakamata hao wanaojifanya wajuaji alafu ndio rafiki zake,” Max alisema huku akiitikiwa na Hancy kwa kutikisa kichwa chake.
Hawakuendelea tena kukaa pale. Max na John walianza kutoka nje. Aminata alikuwa akiangaliana sana na Mosses ambaye alikuwa ameshikilia glasi ya wine akiwa amesimama pembeni ya Steve. Alishtuka sana baada ya kugundua yule alikuwa ni Aminata na hivyo aliita walinzi wake na kusimama nao karibu.furaha yote ilimwondoka akawa hajui la kufanya. Hakumweleza Steve hadi pale waliporudi katika jumba lake ndipo alipomsmulia kisa kizima.
“Sasa kwa nini wakusumbue hivyo, tuwatafuteni na tuhakikishe tunawapoteza, alisema Steve kwa kufoka. Tukio ambalo liliendeshwa wiki moja baadaye kwa kuwateka John na Aminata wakati wakiwa njiani kuelekea kwa Aminata kupumzika.
*****
Ni baada ya kula chakula cha jioni ndipo Max akalikumbuka gari la Aminata ambalo baada ya kutekwa liliachwa palepale barabarani. Habari zilipomfikia Max aliamua kufuatilia na kulipata gari lile na kulipeleka kituo cha polisi kwa ajili ya usalama.
“Shemeji sidhani hata kama unalikumbuka gari lako?” Max
alichokoza Aminata ambaye alisahau kabisa kuhusu gari lake walilolitumia kabla ya kutekwa.
“Sidhani kama nilishawahi kulifikiria tangu tutekwe, kikubwa kilikuwa ni juu ya maisha yetu na nashukuru tupo hai,” Aminata alimjibu kuonyesha kuwa hakujali sana anasa zaidi ya uhai wake. Huku akicheka aliomba aelezwe kuhusu gari lake.
“Gari lako shemeji nililikuta Barabara ya Barakuda nikalipeleka polisi kwa usalama zaidi. Nilikuwa njiani kuja kwako kuangalia kama John alikuwa huko baada ya simu yake kuwa haipatikani. Ukilihitaji tutaongozana kwenda kulitoa huko,” alimaliza Max.
Baada ya maongezi yao ya muda mrefu Max aliwakaribisha wageni wake John na Aminata katika chumba cha kulala na yeye na Michelle wakaongozana kwenda kulala.
*****
Asubuhi ya siku inayofuata John na Max walielekea ofisini kwa Max tayari kukutana na Antony ambaye alikuwa amesharudi nchini akitokea nchini Kenya ambako alikuwa amerudi kwa ajili ya biashara zake. Safari hii hakuwa zaidi akijihusisha na biashara bali alikuwa anatafuta zana za kufanyia kazi. Kazi moja tu ambayo baada ya kuambiwa na John kwamba Mosses alikuwa hai na kwamba walitekwa sasa alijua ni lazima wammalize.
Aliamu kurudi akiwa tayari kwa mapambano n kwenda kukutana na kina John na Max ili kupanga mikakati ya kupambana na maadui zao. Walifika ofisini saa mbili asubuhi na kumkuta Antony akiwasubiri nje na gari lake. John alifurahi kumwona pacha wake.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi