MAUAJI YA KASISI (2)

Zephiline F Ezekiel

SEHEMU YA PILI
ILIPOISHIA...
sista Rose akafanya hivyo na Fr Gichuru akamuwekea mikono kichwani kumbariki, mara mwanga wa taa za gari ukawamulika kutoka getini, hakuna liyejua ni gari ya nani, Fr Gichuru akamuacha Sr Rose aendelee na shughuli yake yeye akaliendea geti…

JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈

ENDELEA...
Sista Rose alikuwa kajibanza kwenye ua kubwa lililo karibu kabisa na mlango wa kuingilia sakristia, akiangalia kinachoendelea, baada ya mabishano mafupi kati ya Fr Giochuru na wale jamaa waliokuja na ile gari mara alishuhudia kasisi yule akianguka chini kwa kishindo na sauti ya kike iliamuru wengine kupanda garini na kuondoka kwa kasi. Sista Rose alibaki akitetemeka huku machozi yakimwagika na si kumbubujika, alishindwa afanye nini, awaamshe wenzake au aende kumsaidia Fr Gichuru, alikuwa njia panda hakujua afanye nini. Gari ile ilipoondoka alirudi nyumbani kwao akilia na kuwapa taarifa wenzake ambao wote waliamka na kwenda kuona tukio hilo kisha kupiga simu polisi na kwa paroko ambaye alikuwa ameenda kigangoni kwa misa ya alfajiri…

“Poleni kwa msiba huo mzito” sajenti Maria alitoa pole akiwa na macho makavu kabisa, “Labda sista niambie, unaweza kukumbuka aina ya gari walilokuja nalo?”

“Kwa kweli ni shida kulikumbuka kwa kuwa kulikuwa na giza na mi nilikuwa mbali kidogo” sista alijibu.

“Kipi cha pekee unachokumbuka katika tukio hilo?”

“Sauti ya mwanamke iliyokuwa ikimhimiza mwenzake kumaliza kazi, nilisikia wakitamka jina ‘Black Cheetah’” alimaliza na kutungua kilio.

“Ok waweza kwenda tutakapokuhitaji tutakupa taarifa.

* * *

Black Cheetah, jambazi sugu linalotafutwa na polisi ukanda wote wa Africa Mashariki, linajikuta katika sakata jipya, sakata la mauaji ya kasisi. Kila mtu aliamini kuwa jambazi hilo si bure tu bali linatumia hata nguvu za giza kwa jinsi linavyoweza kuwatoroka polisi katika mazingira ya kutatanisha hata wenyewe kushindwa kujielewa inakuwakuwaje. Hakuna aliyekuwa halijui jina hili, si mtoto wala mtu mzima, jina la Black Cheetah halikuisha midomoni mwao.

Sajenti Maria alishtushwa kusikia jina hilo likitajwa na sista Rose kuwa aliisikia sauti ya kike ikilitamka katika tukio hilo. Alitafakari akaona kibarua hicho si cha kitoto ni kucheza na mtu au watu waliokomaa kwenye taaluma.

Black Cheetahm, kama anavyojiita ni kijana mtukutu, mkakamavu, muasi aliyetoroka katika kundi lao la M23 huko mashariki mwa Congo, aliyetokea kuwa jambazi sugu na tishio katika ukanda wote wa Afrika ya mashariki, alikuwa akikodiwa na matajiri wakubwa kutekeleza mauaji au wizi wa kutumia silaha. Mara kadhaa ameshahusishwa na wizi wa benki uliotokea Dar es salaam Tanzania miaka michache iliyopita, mlipuko wa bomu uliotokea Kampala wakati watu wakiangalia mpira na matukio mengi yaliyotukia huko Kenya ambayo hata hatuwezi kuyaainisha hapa, kwa ujumla alikuwa gaidi.

Mwezi mmoja uliopita


Gari aina ya Hammer nyeusi ilisogea taratibu katika maegesho ya hoteli ya Ngong Hills, watu watatu, wanaume, wakashuka wakiwa ndani ya suti nyeusi zilizotanguliwa na shati nyeupe, mmoja kati yao mwenye mwili mnene alikuwa akitembea kwa msaada wa fimbo maalum, taratibu waliingia hotelini hapo na moja kwa moja wakaelekea sehemu ya chakula na kuchukua meza yenye viti vine na kuketi, kiti kimoja kilibaki wazi wakaagiza vyakula na vinywaji na kuanza maongezi yao. Maongezi yaliendelea na baada ya muda kidogo kijana mmoja aliingia mahali pale akiwa kavalia koti kubwa la bluu nyeusi akiwa na kofia kubwa aina ya pama, kwa hatua za maringo aliijongea meza hiyo, kila mtu alimuangalia kwa mwendo wake hususan camera za usalama. Alifika katika meza ile na kuvuta kiti kimoja kilichobaki kikimsubiri yeye, akaketi na kuiweka bilauri yake vizuri kabla ya kuimiminia kinywaji kilichokuwa hapo.

“Yes, Cheetah…” yule bwana anaetembea kwa msaada wa fimbo alimkaribisha

“Nimeitika wito wako, bwana Bill” Cheetah alijibu.

“Vizuri, hawa ni wadau wenzangu ambao sote tumekuita ili tukupe kazi maalum” aliendelea

“Nawasikiliza”

“Kuna kazi ndogo tunataka utufanyie” alizungumza bwana Wambugu, akajikohoza na kuendelea “Tunataka kitu kinachoitwa Monstrance, kimehifadhiwa katika kanisa kuu la Familia Takatifu hapa Nairobi, of course ni kazi ndogo tu”

“Hakuna kazi ndogo kama itahitaji kumwaga damu, hasa damu ya watu wasio na hatia” Cheetah alimjibu Wambugu

“No! hatumwagi damu, ni kujua ilipo na kuichukua basi”

“Unafikiri tutaipata kwa urahisi kama unavyofikiria? Maana ingekuwa ivyo basi hata wewe ungeenda pale na kuichukua, lakini kama umeniita mimi maana ni kwamba hiyo si kazi ndogo kwa vyovyote lazima vyuma vitaongea” Cheetah alimaliza kauli yake na kuinua bilauri iliyojaa kilevi na kujimiminia kinywani mwake baada ya kulishuighulikia pande la nyama lililokuwa ndani ya sahani hiyo.

“Hilo nalo neno bwana Cheetah. By the way wewe utajua la kufanya, sisi tunachotaka ni Monstrance basi” alimaliza bwana Wambugu.

“Ok, tusipoteze muda, mimi nitaunda kikosi kazi kitakachoweza kufanikisha kazi hiyo, lakini mjue kule ni kanisani, wale makasisi wana mazindiko yao, hivyo lazima mnipatie fedha iliyotakata”

“Ha ha ha ha ha hilo usitie shaka bwanaaa bwana Cheetah” cheko la kivivu lilimtoka yule bwana anyetembea kwa fimbo, kisha akainua simu yake na kubofya namba kadhaa, punde tu vijana wawili waliingia pamwe na briefcase ndogo mkononi, ikawekwa mezani, kwa ishara ya mkono ya mkono yule bwana alimuomba Wambugu kuifungua, baada ya kuzungusha vijinamba Fulani mara yenyewe ilifyatuka kuashiria kuwa kilichopo kiljaa ndani yake kwa kukandamizwa hasa. Naam manoti yenye sura za Moi na Kenyatta yalipangwa na kubanwa katika mabandali kibao, Black Cheetah macho yalimtoka pima.

“Ukifanikisha kazi basi hata briefcase hii ni mali yako” yule bwana alizungumza kivivu.

Black Cheetah alitikisa kichwa juu chini juu chini kuashiria amekubaliana nao. Kwa kuanzia alipewa mabandali kadhaa katika mfuko wa plastiki. Waliagana wane hao na Cheetah akaondoka zake akiwaacha wao wakiendelea kutumbua mavyakula yaliyojaa mezani hapo.

Katika maegesho ya magari, Cheetah aliisogelea gari yake na kusimama kidogo kisha akaangalia uku na huku, hakuona yeyote wala chochote cha kushuku, akaingia na kukaa nyuma ya usukani, milango ikafungwa na vyoo vyote vikabaki juu. Aliufungu ule mfuko wa karatasi na kuhesabu burungutu zile, si haba takribani laki mbili za Kenya, alikenua kwa furaha na kulazimisha tabasamu ambalo halikuendani na uso wake khasilan. Alitia gia na kuyaacha maegesho, baada ya kulivuka geti moja kwa moja aliningia barabara ya Ngong na kurudi katikati ya jiji la Nairobi.

“Hivi unafikiri tutafanikiwa kuipata?”Wambugu alimwuliza yule bwana anyetembelea fimbo

“Ha ha ha ha Wambugu unanichekesha sana, kazi iko kwa Cheetah lazima atararua mpaka tuipate, na tukishaitia mkononi yule Don kule Ujerumani atatukatisha kwa pesa nyingi, si ya kitoto” aliongea kwa sauti yake ya kivivu huku mdomoni akitafuna vyakula aina aina.

“Don!” Wambugu alishangaa

“Yeah, Don, anaitwa Don Fredrick Schurmann, ni tajiri sana katika mji wa Achen, yeye ndiye anayetaka hiyo Monstrance, amesema tukiifikisha mikononi mwake tutapata pesa nyingi sana, ha ha ha ha !” alimaliza kwa kucheka na kunyanyua bilauri yake iliyojaa mnvinyo wa Sant Raphael.

* * *

Katika bar kubwa ya Dagoreti Corner super pub, watu walijaa sana wakiburudika kwa vinywaji, nyama choma huku muziki laini wa The Mushroom ukisikika kutoka katika spika kubwa zilizozunguka eneo hilo. Hakuna aliyefikiria kesho kila mmoja alijiachia kwa starehe zake alizoziona kuwa zinamfaa, ilimradi siku ilipita katika mtindo huo. Katika kona moja ya pub hiyo watu watatu waliketi katika mtindo wa mzunguko mmoja wao alikuwa mwanamke walionekana kana kwamba wana mazungumzo mazito sana, hivyo hakuna mtu ambaye alisogelea eneo lile zaidi ya mhudumu wa pub hiyo, naye alikuja tu kuleta alichoagizwa na kuondoka zake.

“Ndiyo vijana, kuna kazi ya kuifanya haraka iwezekanavyo” Cheetah alianzisha mazungumzo.

“Tunakusikia mkuu” sauti pekee ya kike iliiitikia kauli hiyo.

“Tunatakiwa kuchukua mzigo pale Holy Family Basilica

“Mapesa mangapi tukachukue?” aliuliza kijana mwingine aliyeketi hapo.

“Siyo pesa Bwana Gichui, kuna kitu kinaitwa Monstrance, mnakijua?” Cheetah aliwauliza na wote wakatazamana.

“Monstrance!?” Mellina Wanjiku alishtuka na kujishika kifua kwa mshangao.

“Unashtuka nini, unaijua?” Cheetah aliuliza, na yeye alionekana kushtuka kidogo na kuanza kujiuliza kama kapokea mbuzi kwenye gunia safari hii.

“Naijua Monstrance, ni chombo kitakatifu sana, kukishika kwa hila inaweza kuwa matatizo kwetu” Mellina alijibu kwa upole sana, akatulia kidogo kisha akaendelea “Pamoja na ujambazi ninaoufanya sikuwa kufikiri kuligeukia kanisa, kuna nini kwenye Monstrance hiyo?” aliuliza Mellina

“Ah vile vitu vya wakatoliki huwa vinatengenezwa kwa dhahabu tu, itakuwa ndiyo wanayoitaka” alijibu Gichui.

Black Cheetah alijikuta kwenye mtihani mgumu, kama kuna vitu aliviogopa ni miujiza ya Kimungu ambayo mara nyingi aliisoma kati vitabu vitakatifu, mtihani mkubwa! Alijiona amefanya ujinga kutokuuliza nini kilichomo katika monstrance hiyo, je kama wakizikuta nyingi ni ipi ya kuichukua, utata!

“Cheetah!” aliita Mellina.

Black Cheetah alishtushwa na wito huo kutoka katika lindi la mawazo, akawatazama wanakikundi wenzake ambao yeye aliona wangefaa kwa kazi hiyo lakini sasa walimfanya hata yeye kushikwa na wasiwasi.

“Ok, tunafanya kazi au hatufanyi tuchague moja” aliwapa mtego. Baada ya kutafakari mara mbili mara tatu wote waliamua kuingia kazini kuisaka hiyo monstrance.

(monstrance ni chombo maalum kinachotumika kwa wakristo hasa dhehebu la katoliki katika ibada za Ekaristi Takatifu kama alhamis kuu na siku ya Ekarist, hutengenezwa ama kwa dhahabu au upakwa rangi ya dhahabu)

“Ah vile vitu vya wakatoliki huwa vinatengenezwa kwa dhahabu tu, itakuwa ndiyo wanayoitaka” alijibu Gichui.

Black Cheetah alijikuta kwenye mtihani mgumu, kama kuna vitu aliviogopa ni miujiza ya Kimungu ambayo mara nyingi aliisoma kati vitabu vitakatifu, mtihani mkubwa! Alijiona amefanya ujinga kutokuuliza nini kilichomo katika monstrance hiyo, je kama wakizikuta nyingi ni ipi ya kuichukua, utata!

“Cheetah!” aliita Mellina.

Black Cheetah alishtushwa na wito huo kutoka katika lindi la mawazo, akawatazama wanakikundi wenzake ambao yeye aliona wangefaa kwa kazi hiyo lakini sasa walimfanya hata yeye kushikwa na wasiwasi.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi

Chapisha Maoni