
Mtunzi: Richard Mwambe
SEHEMU YA TATU
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
Black Cheetah alishtushwa na wito huo kutoka katika lindi la mawazo, akawatazama wanakikundi wenzake ambao yeye aliona wangefaa kwa kazi hiyo lakini sasa walimfanya hata yeye kushikwa na wasiwasi.
JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈
ENDELEA...
“Ok, tunafanya kazi au hatufanyi tuchague moja” aliwapa mtego. Baada ya kutafakari mara mbili mara tatu wote waliamua kuingia kazini kuisaka hiyo monstrance.
Miaka kumi nyuma… Al-hamis kuu 1996
Kanisa la Holy Family lilishehani watu mapaka nje wakifuatilia misa takatifu ya alhamis kuu ambapo yalifanyika maadhimisho ya karamu ya mwisho. Hakukuwa hata na njia ya kupita kuelekea popote kila mtu alipo basi ni hapohapo.
Katika madhabahu makasisi wapatao sita pamoja na baba Askofu walikuwa wakiendesha misa hiyo kubwa ambayo mwisho wake huwa inakuwa na maandamano ya kuhamisha mwili wa Bwana kuupeleka mahali pengine ili waumini wapate kuabudu. Watu waliketi kimya kumsikiliza baba Askofu Njue mara baada ya misa hiyo kuhitimika
“Tuna furaha kuwatangazia kuwa mwaka huu tumepokea Monstarnce maalum kwa maadhimisho ya misa maalum. Monstrance hii ambayo ina historia kubwa katika kanisa ilitengenezwa miaka ya 1878 huko Tanzania katika abasia kubwa ya Wabenedictin iliyopo Peramiho. Na ilitolewa zawadi kwa Baba Mtakatifu Leo XIII na kuhifadhiwa pale Roma. Leo hii imeletwa hapa kwetu kwa ajili ya maadhimisho ya jubilee ya miaka mia moja ya Ukristu hapa Kenya. Na itahifadhiwa hapa mpaka tukio hilo litakapokwisha ndipo tutairudisha Roma” alimaliza maelezo yake na kujongea madhabahuni, akainyanyua juu ile Monstrance kubwa iliyokuwa iking’aa kwa rangi ya dhahabu hasa ilipomulikwa na taa zilizowekwa kwa umaridadi ndani ya kanisa hilo, kengele zililia na kisha maandamano kutoka nje ya kanisa yalifanyika mpaka kwenye kikanisa kingine kidogo, ikahifadhiwa hapo na kuacha watu wakipeana zamu za kufanya ibada usiku huo.
1878
Mahali Fulani huko Tanzania
Vibarua wa wakolono walikuwa wakichimba mashimo makubwa kuingia chini ya milima iliyozunguka eneo hilo, huku wakiwa wamesimamiwa na askari hatari wa kijerumani. Kazi ilikuwa ngumu lakini walifanya hivyo hivyo, walitoa mchanga na kuuchekecha kwenye chekeche maalum na wale wazungu waliondoka na udongo walioutaka na kuingia nao katika chumba maalumu na kuuhifadhi.
Katika milima ile baadaye kulijengwa majengo makubwa na yale mashimo yakawa ndani yake, kila kukicha wazungu wengi walikuwa wakiingia hapo, hawa wakisafiri na hawa wakifika ilimradi shughuli zilikuwa nyingi katika eneo hilo.
Peter Schurmann alikuwa busy kugongagonga chuma kimoja kilichokuwa katika mtindo wa samaki, jasho lilimtoka mwili mzima lakini yeye hakujali aliendelea na kazi yake, na aliporidhika na kile alichokitengeneza alichukua kitu kama uji mzito wa moto na kumwagia ndani yake kisha akauacha upoe kwa muda. Alipokuja kutoa baadae alipata kituchenye umbo la samaki, akaketi na kuanza kukifanyia nakshinaksh. Hakika kazi ya mhunzi yule ilikuwa safi sana chombo kile kilikuwa kiking’aa sana hasa wakati ambapo kinapigwa na mwanga, kishapo akatengeneza mkitako safi kikubwa na kukiunganisha kwa chini ya chombo kile ili kiweze kusimama chenyewe na kweli ilikuwa hivyo, kisha wakakihifadhi katika kanati maalumu. Yake mashimo yaliyopo kule ndani yote yakafukiwa lakini kilibakishwa chumba kimoja ambacho hicho haruhusiwi kuingia mtu yeyote mpaka leo hii. Katika milima iliyozunguka walisimika vitu kama misalaba mikubwa na kuijengea kwa sementi kali sana ambayo si rahisi kuivunja kwa zana za kawaida tulizozizoea. Kile chombo baada ya kukamilika kilihamishwa na kupelekwa kwao.
Chombo kile kilipelekwa huko Italia na kuhifadhiwa kati chumba maalum ndani kabisa ya kanisa la Mtakatifu Petro, Vatican. Chombo hicho kilichojulikana kwa jina la Monstrance kilitolewa mara moja tu kwa mwaka na daima kiliwekwa sehemu maalumu ambayo kila mmoja angeweza kwenda kuadudu huko.
Wiki chache nyuma
Rev. Fr Frederick Gichuru aliketi katika viti vya kupumzikia akisubiri muda wake ufike aingie ndegeni kuelekea Roma kwa kazi maalumu. Watu walikuwa ni wengi uwanjani hapo na kila mmoja wao alikuwa na safari yake, hakuna aliyefuatilia mwenzake anafanya nini au anataka nini.
Tangazo lilisikika kwenye chombo cha kupaaza sauti kuwataka abiria wanaosafiri kwa ndege ya shirika la ndege la uswiss kuingia ndegeni tayari kwa safari. Pembeni ya Fr Gichuru alikaa mtu mmoja mnene aliyeshiba vizuri, inaonekana ndege hiyo yeye aliipanda kutokea Dar es salaam au Kilimanjaro, alimsalimia Fr Gichuru kwa kumpa mkono wake wa kuume.
* * *
Na baada ya ndege hiyo kuwa angani mazungumzo baina yao yalichukua nafasi. Mtu huyu mnene alikuwa akielekea Ujerumani kwa shughuli za kikazi na Fr Gichuru nae alikuwa akielekea Roma kwa shughuli za kikazi vilevile. Ndege ilipotua katika uwanja wa kimataifa wa Geneva, ndipo Fr Gichuru alipogundua kuwa yule mtu mnene mwenye sauti ya kivivu alikuwa akitembea kwa msaada wa fimbo. Waliagana na kila mmoja kuchukua njia yake.
Akiwa kwenye gari iliyokuja kumchukua Fr Gichuru alididimia kwenye kisima kirefu cha mawazo, alijaribu kuyarudisha maongezi yale aliyokuwa akiongea na yule mtu mnene kwenye ndege, ilionekana alikuwa akifahamu vitu vingi labda katika kuzunguka sna nchi mbalimbali za dunia hii, lakini alishtushwa kwa jinsi alivyoizungumzia kwa tuo monstrance ile ambayo Fr Gichuru alikuwa akienda kuifuata ili kuileta Nairobi, Kenya.
Baada ya itifaki zote za kikanisa kukamilika Fr Gichuru alikabidhiwa ile monstrance, aliitazama kwa udadisi na kuigeuzageuza ‘Kile ni chombo cha thamani sana, hata pale kilipo hakuna aneujua uthamani wake’, maneno ya yule bwana yalimrudiarudia kichwani mwake. Aliiweka juu ya kijimeza kidogo na kufanya ishara ya msalaba kisha akaitumbukiza kwenye kisanduku maalumu kwa kazi hiyo tayari kwa safari. Baada ya chakula cha jioni Fr Gichuru alikuwa katika mazungumzo na makasisi mbalimbali katika ukumbi maalum, wakibadilishana mawazo na pia akiwaalika katika adhimisho la jubilee hiyo.
Fr Gustav Macker, alikuwa akizungukazunguka katika bustani ndogo iliyo karibu na lango kuu akiongea na simu bila kuchoka kwa lugha yao ya kijerumani, alionekana mara kama anatoa melekezo Fulani, wakati mwingine kama anajibishana na mtu kwa ukali. Alipomaliza alimuona Fr Gichuru akiwa tayari ameketi ndani ya gari akimngoja kwa safari ya uwanja wa ndege.
“Oh Father, nilikuwa naongea na nyumbani kidogo, tunaweza kwenda?”
“Ndiyo nipo tayari.”
Fr Gustav aliondoa gari na kuelekea uwanja wa ndege, njia nzima hakuna aliyeongea na mwenzake, mara kwa mara Fr Gichuru alikuwa akistuka kila alipokumbuka mzigo alioubeba aliingiwa na giza la hofu.
“Haya Father , mi nakutakia safari njema na Bwana akutangulie” Fr Gustav alimuaga Fr Gichuru, akamkumbati na kumpa mkono kisha yeye akageuza gari na kurudi alikotoka.
Akiwa ndani ya ndege alikuwa akisoma kitabu chake cha riwaya ya ‘Msitu wa Solondo’ kilitungwa huko Tanzania, kilimvutia sana hasa alipojua kuwa kwa nini wazungu hupenda sana kudadisi mambo, alikuwa mara ancheka mwenyewe, mara anakunja uso, mara anajishika moyoni kuonesha mshtuko basi ilimradi riwaya hiyo ilimkamata vilivyo.
Baada ya takribani masaa nane angani, ndege ya shirika la ndege la Uswiss ilikanyaga ardhi ya Nairobi na kujiegesha vyema katika maegesho yake. Watu walishuka mmoja baada ya mwingine na mwisho kabisa Fr Gichuru alishuka akiwa na kijisanduku kile mkononi mwake. Alilakiwa na paroko wake Fr Joe Smith na kumuongoza kuelekea kwenye gari aina ya Land Rover 110 Defender mali ya jimbo kuu la Nairobi. Wakati wanatoka pale uwanja wa ndege na kushika barabara kubwa ya kurudi mjini waliipita gari aina ya Hammer iliyokuwa imeegeshwa na mara tu ile gari iliingia barabarani. Ikiwa nyuma kama gari ya tatu hivi ilikuwa aikiifuatilia ile Land Rover 110.
“Karibu sana Fr Gichuru, safari yako imekuwaje?”
“Safari imekuwa nzuri sana, lakini kuna kitu Fr kinanitia mashaka sana”
“Ooh kitu gani tena Fr?”
Fr Gichuru alimsimulia mazungumzo yote aliyozungumza na yule mtu mnene kule kwenye ndege, juu anavyoijua ile monstrance na jinsio alivyomueleza mara ngapi amewahi kuiona na ni nchi tofauti tofauti na ameahidi kuja Nairobi katika adhimisho hilo la jubilee.
“Ananitia mashaka sana, kwa nini kila inapokwenda na yeye anaenda, ni kipi kinamvutia?” Fr Gichuru alimuuliza Fr Joe
“Inategemea kabisa, lakini labda anapenda kuiona inavyopendeza au ni Mkristo kwelikweli anayedumu sana katika imani”
Walipokaribia katika geti la kanisa ile Hammer iliwapita kwa kasi na kusimama mbele sana. Fr Joe aliichukua monstrance ile na kuihifadhi katika chumba maalumu kilichopo ndani ya nyumba yao.
2
1961
Munichen – Ujerumani
“Ule ni urithi wa ukoo wetu, babu wa baba yangu alisema lazima tufanye juu chini tukauchukue popote utakapokuwepo” mzee wa zaidi ya miaka themanini alikuwa akiongea na mjukuu wake wakiwa shambani juu ya trekta aina ya Massey Furgasson.
“Ha, kumbe eee!” Mjukuu wa miaka saba alikuwa akimsikiliza babu yake kwa makini sana.
“Sasa, wewe mjukuu ndiyo unatakiwa ufanye kazi hiyo, wewe unaonekana mjanja sana”
“Mimi, ah! Naogopa.”
“Usiogope, muda ukifika utajua la kufanya. Ila mjukuu wangu wewe unapenda kufanya nini ukiwa mkubwa?”
“Mimi ningependa kuwa mwanajeshi, nipigane vita.”
“Ha ha ha ha Mjukuu wangu Gustav, vita si jambo jema. Unajua ni kitu gani nilikuwa nafikiria juu yako?”
“Hapana niambie babu”
“Wewe uwe Padre, uongoze kanisa, uchunge kondoo wa Bwana”
“Ha! Nitakuwa nakunywa divai yote” mjukuu alimjibu babu yake na babu mtu alitungua kicheko kadiri ya mawazo ya mjukuu wake.
Miaka michache baadae
Munichen – Ujerumani
Gustav Macker alimaliza masomo yake na kujiunga na seminari kuu ya Mt Augustino iliyopo kati jimbo la Munichen, alikuwa mtii kwa viongozi wake na hata kupendwa na waalimu na walezi wake katika seminari yao. Alimaliza miaka mitano ya falsafa na baada ya kupata stashahada yake alichaguliwa kwenda mji wa Achen hukohuko Ujerumani kuendelea kusoma teolojia kwa miaka mingine mitano, alikuwa ni kijana mpole, mnyenyekevu na mtii kwa kila jambo, daima kila alipoonekana al;ikuwa katika hali ya unyenyekevu wa hali ya juu.
Siku moja alitembelewa na mtu asiyemjua, baada ya mazungumzo marefu sana walifahamiana kuwa kumbe wao ni ndugu, na sasa huyu ambaye angetakiwa kumwita kaka alikuwa ni mtu mkubwa kwatika mji huo wa Achen.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi