CHUZI NDIO HILO, HAKUNA KUONJA (12)

Zephiline F Ezekiel

SEHEMU YA KUMI NA MBILI
ILIPOISHIA...
Ndani ya saa moja, Maua alimkaribisha baba Shua chumbani…

“Njoo upaone mahali anapolala ubavu wako,” alisema Maua.

JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈

ENDELEA...
Baba Shua akiwa ameshakunywa wine glasi mbili, hivyo amechangamka kidogo, alimfuata Maua kwa nyuma hadi chumbani…

“Da! Chumba kama cha waziri wa fedha,” alitania baba Shua, Maua akacheka.

Ni kweli kilikuwa chumba kizuri, kilichosheheni kila kinachohitajika kwa ajili ya chumba.

Kitanda cha kisasa kilichozibwa na godoro kubwa, kabati kubwa la nguo, redio yenye kutumia CD sita na kiyoyozi cha ndani kwa ndani, vyote hivyo vilikifanya chumba hicho kuvutia zaidi.

Baba Shua alifikia kujitupa na kunesanesa kidogo huku akimsifia Maua kwa kujitahidi kutengeneza maisha yake vizuri…

“Da! Umejitahidi sana baby wangu…hongera sana…”

“Asante sweet, lakini siku zile tukiwa bado wote uliweza kunipa njia ya namna ya kutumia fedha. Kwa hiyo kwa kutumia maelekezo yako nikawa nimejifunza jinsi ya kubana matumizi,” alisema Maua huku akiachia tabasamu laini na kumwangalia baba Shua.

Walizungumza mengi chumbani, mwishowe walijikuta wamejitupa wote kitandani. Walichezacheza wakiwa kwenye nguo, baadaye Maua alitoka kitandani na kwenda kufunga mlango kwa funguo…

“Kwarakacha…kwarakacha…kwacha!” Msichana wa kazi aligunia moyoni. Kwake lilikuwa tukio geni sana kumwona bosi wake akiingia chumbani kwake na mwanaume. Hajawahi kuona!Simu ya baba Shua iliita, akaitupia macho na kuona jina la mke wake, akaipuuza…

“Baby mbona hupokei simu?” Maua alimuuliza

 “Ah! Si yule malaya anapiga…”

“Ungepokea sasa…unajua anataka kukwambia nini?”

“Achana naye,” alisema baba Shua akianza kukunja sura.

Maua baada ya kauli hiyo, hakutaka kupoteza muda, akapanda kitandani na kuanza kumvua nguo baba Shua huku tayari akiwa na mihemko ya kimahabamahaba…

“Baby,” aliita Maua kwa sauti yenye kuashiria kubembeleza mwana…

“Niambie Maua…”

“Nikupe dawa ya kumwacha mke wako?” aliuliza Maua kwa sauti iliyotoka nje kwa kupitia tundu za pua…

“Kama ipi Maua?”

“We sema uko tayari au hauko tayari?”

“Niko tayari…kwa mambo anayonifanyia? Aisee niko tayari…hivi hapa ninavyojua mimi kwa sababu ameshatekwa na huyo Musa wake hataweza kurudi kwenye reli ninayoitaka mimi kama mume.”

“Da! Aisee pole sana. Basi mimi nitakupa…lakini nikwambie mapema, hiyo dawa si ya mitishamba wala vidonge vya hospitali.”

“Ni dawa gani sasa jamani Maua mpenzi wangu, hebu niambie kidogo basi…”

“Wala usiwe na wasiwasi Benny kwani wewe si unahisi mkeo anakusaliti?”

“Maua si kwamba nahisi, ni kweli ananisaliti. Nimekwambia anaingia chumbani kwa mpangaji mwenzangu nikiwa namwona kwa macho yangu halafu unasema nahisi, maana yake nini? Halafu yule kijana tangu anahamia pale siku ya kwanza nilimuazia vibaya kwamba atakuwa ananisaliti na mke wangu, sijui kwa nini niliwaza hivyo?!”

“Huenda ni akili yako ilijiongeza tu. Wapo watu wameumbwa hivyo. Wanajiongeza wenyewe hivyo huwa hawahitaji kuongezwa.”

“Oke, sawa…sasa niambie hiyo dawa ni ipi?”

“Nitakwambia, we tuendelee kuwa pamoja tu,” alisema Maua huku akimshika mikono baba Shua na kuanza kumnyooshanyoosha. Pia akahamia sehemu mbalimbali za mwili na kumkandakanda huku akimpongeza kwa maneno ya mahaba…

“Benny…”

“Niambie Maua…”

“Unajua namshangaa sana huyo mke wako…”

“Kwa nini? Japokuwa hata mimi mwenyewe namshangaa…”

“Yaani mwanaume mzuri kama wewe anakutenda hivi?! anajua thamani ya mwanaume kweli? Tatizo binadamu wengi wanapenda kupata lakini hawawezi kutumia…

“Utakuta watu wanapishana kwenye maofisi kutafuta kazi lakini wakishapata hawatendi. Mimi huwa naamini watu wengi wanatafuta ajira na siyo kazi…”

“Una maanisha nini Maua kwa huo mfano wako?” aliuliza baba Shua…

“Namaanisha kwamba, siku hizi wanawake wengi wanatafuta kuolewa lakini si ndoa…”

“Ha! Maua, kuolewa na ndoa si jambo moja mpenzi wangu?”

“Hapana Benny! Kuolewa ni mwanamke kumpata mwanaume wa kuishi naye akahesabiwa yeye ni mke wa fulani. Ndoa ni zile taratibu zilizopo. Yaani uvumilivu, uaminifu na tendo lenyewe.

“Sasa kama mke anaingia kwenye chumba cha mwanaume ndani ya nyumba moja hiyohiyo, huyo anaijua ndoa kweli? Si alitafuta kuolewa tu!”

Benny alimwelewa vizuri Maua kiasi kwamba alimkisi kama ishara kwamba, amemkubali. Maua naye akambusu Benny, kisha wakazama kwenye tukio lingine la denda! Kwa dakika kadhaa hakuna aliyekuwa akiongea.

Kila mmoja aliguswa na hisia za mapenzi yao miaka miwili nyuma ambapo walikuwa moto.

Kutokana na hali hiyo, walifika mahali kila mmoja alifanya anachotaka kwa vitendo bila kutoa sauti.

Mfano, Maua alipotaka Benny ageuke alimshika na kumgeuza, Benny akajua na kuendelea kujigeuza mwenyewe.

Benny naye alipotaka Maua alale chali, alimshika akaashiria kumlaza, Maua akalala mwenyewe huku akiyakaza macho kwa mwelekeo wa mwanaume huyo kama anayeuliza ‘kuna lingine?’

Hali iliendelea hadi wakafika mahali wakajikuta tayari wapo uwanjani na mechi imeanza.

Siku hiyo, Maua alitumia ufundi wake wote kuhakikisha anakidhi hitaji la mapenzi kwa Benny. Ilifika mahali hata Benny mwenyewe alishangaa kuona mambo makubwa kwa Maua. Akajiuliza amepatia wapi uzoefu huo?

Kingine alichokifanya Maua siku hiyo ni kwenda sambamba na Benny huku akiendelea kumsifia kwa mambo mbalimbali, akikumbushia hata madogo tu aliyoyafanya Benny zamani kuhusu yeye.

Ukichanganya na sauti aliyokuwa akiitumia sasa, weee! Benny namaanisha baba Shua, alisahau kabisa kama alifunga ndoa na sasa ana mtoto mmoja wa kike anaitwa Shua.

Kichwani alianza kumsahau ghafla mama Shua. Ile hali ya kuumia moyo kwa sababu ya usaliti wake ilianza kumtoka na kujiona kama kawaida. Akili yake ya wivu ilianza kuhamia kwa demu wake huyo…

“Maua,” aliita huku mikiki ya mpira ikiwa inaendelea…

“Abee…”

“Unajua nikija kukuona na mwingine nitakasirika..?”

“Ukiniona na mwingine au na mwanaume mwingine? Maana unaweza kuniona nikiwa na shoga yangu Hadija, pia utakasirika sweet?” aliuliza Maua.

Hapo ni baada ya mechi yao kufika mwisho na sasa walikuwa wamepumzika huku wakihema kwa kasi ya shughuli pevu…

Baba Shua alirudi akamkuta mama Shua sebuleni akiwa katika hali ya kutojua nini kinaendelea. Aliingia chumbani bila kusalimia, akapanda kitandani kulala maana alishaoga nyumbani kwa Maua na kupakwa mafuta ya losheni na pafyumu juu.

Kitendo cha baba Shua kumpita kama hamuoni kilimuumiza akili mama Shua, akahisi kama kuna la ziada ya pale…

“Afadhali hata angenisalimia lakini kunipita kasi bila salamu maana yake nini sasa?” alijiuliza mama Shua.

Alijishauri kuhusu kumfuata au kutomfuata mumewe, chumbani lakini mwisho wa yote aliona itakuwa ujinga kumfuata…

“Yaani kumtenda kote kule halafu nimfuate? Je, akinipiga nitasema amenionea? Pengine karudi bado na hasira, kaepusha mabaya kwa kwenda chumbani halafu eti nimfuate, si itakuwa naendekeza ushetani!”

***

Kule chumbani akiwa tayari kitandani, baba Shua naye aliwaza yake kwamba, endapo mama Shua atamuibukia chumbani salama yake afikie kulala. Lakini akisema amuulize kwa nini hajamsalimia, atavaa na kuondoka zake kurudi kwa Maua…

“Tena kwanza ngoja nimpigie simu Maua, aliniambia nikifika nimjulishe,” alisema moyoni baba Shua, akashika simu yake na kumwendea hewani Maua lakini wakati huohuo, mama Shua naye akaingia kwa lengo la kupanda kitandani kulala…

“Ee mambo vipi? Umelala nini..? Bado..? Oke…mimi ndiyo nipo kitandani muda huu…nilisema nitakupigia nikiwa nimejilegeza kitandani…usijali…aaa! Wewee…wewee! Mmmh! Acha bwana…teh…the! Haya poa…na wewe pia…aaaa bwana acha mambo yako wewe…oke oke.”

Mama Shua alifuatilia sana mazungumzo hayo ili kujua mumewe anaongea na nani kwenye simu. Kwa mbali alihisi anaongea na mwanamke, lakini pia akahisi ni mwanaume, hasa kwenye vile vipengele vya ‘acha bwana…oke oke poa.’

Baba Shua naye akawa anamuwaza Maua na maneno yake ya kwenye simu…

“Mh! Maua bwana…ei nibusu…hivi anavyoamini ningembusu kweli? Ingewezekana wapi kwanza? Ye anajua mke wangu atakuwepo sasa ningembusu vipi? hata kama kweli tumerudisha majeshi nyuma lakini si kwa kiasi cha kuleta ubaya. Mbaya aachwe na ubaya wake.”

Usiku wa siku hiyo ulikuwa mrefu kwa wote wawili lakini kila mmoja alikuwa akiwaza yake.

Mama Shua yeye aliwaza maisha yatakavyokuwa baada ya kutoka kwa baba Shua kutokana na hali ilivyokuwa wakati baba Shua yeye alikuwa akiwaza maisha yake na Maua…

“Siamini kama atanitenda kama mama Shua…kwanza Maua hata tulipokuwa klozdi enzi zile sikuwahi kumuwazia kwamba ananisaliti. Naamini si msaliti,” aliwaza baba Shua.

***

Kwake Maua mambo yalikuwa vilevile kama baba Shua. Muda mwingi alimuwaza mama Shua na uovu wake kwa mumewe hasa akizingatia kwamba, ndiye aliyevunja uhusiano wake na baba Shua…

“Mshenzi sana yule mwanamke. Yaani aliingilia penzi langu kumbe hawezi chochote. Haya sasa…ndoa imemshinda sijui atasemaje!”

***

Baba Shua alilala usingizi mzito siku hiyo, tena akikoroma jambo lililomshangaza sana mkewe mama Shua kwani alitarajia kuwa, kutokana na mambo yaliyotokea, angelala kimang’amumang’amu.

“Mh! Yaani baba Shua pamoja na mambo yote yaliyotokea, bado analala usingizi kweli? Ina maana kitendo changu hakijamkera? Mbona mi mwenyewe nimekereka?” alijiuliza mama Shua bila kupata majibu. Mpaka kunakucha, mama Shua hakuwa amelala usingizi unaoeleweka.

***

Kulikucha, mama Shua alitoka kitandani, akaenda uani kufanya kazi za usafi huku akiwa ametenga maji ya kuoga kwa ajili ya mumewe baba Shua.

Lakini baba Shua akiwa kitandani hajatoka bado lakini alishaamka, akaanza kuchati na Maua…

“Mambo baby, ndiyo naamka mimi,” alituma ujumbe huo baba Shua…

“Ooh! Thanx God kwa ajili ya wewe! Mimi nimeshaamka. Ila natamani sana kama ungekuja kuoga kwangu kabla ya kwenda kazini…”

“Da! Nguo sasa ndiyo tatizo mama…”

“Nguo! Si utabeba za kuvaa baada ya kuoga.”

Baba Shua aliamini ni ushauri mzuri hasa akizingatia kwamba, hana mawasiliano pale kwake zaidi ya msichana wa kazi na binti yake Shua.

Alitoka kitandani, akachukua begi dogo la mgongoni, akaingiza suruali moja, singilendi moja na shati moja, viatu na soksi alivaa kabisa, akaondoka zake bila kuaga mtu.

Wakati anaondoka, mama Shua alikuwa uani. Alijua mumewe angeenda kuoga lakini alipoona kimya, akaingiwa na wasiwasi, akaenda chumbani na kukuta kiasi cha pesa juu ya meza,

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi

Chapisha Maoni