Mtunzi: Global Publisher
SEHEMU YA KUMI NA TATU
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
akaondoka zake bila kuaga mtu.
Wakati anaondoka, mama Shua alikuwa uani. Alijua mumewe angeenda kuoga lakini alipoona kimya, akaingiwa na wasiwasi, akaenda chumbani na kukuta kiasi cha pesa juu ya meza,
JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈
ENDELEA...
lakini baba Shua hakuwepo…
“Khaa! Huyu kaenda wapi tena?” alijiuliza. Alimwamsha Shua na kumuuliza lakini alionekana hajui lolote maana alikuwa usingizini.
Aliingiwa na wasiwasi kwamba, huenda ameamua yeye ndiyo ahame kwenye nyumba hiyo na kumwacha yeye na Musa wake, lakini alipofungua kabati la nguo hakuona mabadiliko. Wingi wa nguo ulikuwa uleule na haikuwa rahisi kubaini kwamba, mumewe ametoka na begi lenye nguo chache.
Hata alipokwenda kwenye sehemu ya viatu alibaini kuwa, ni pea moja tu haipo kwa tafsiri rahisi ni kwamba ndivyo alivyovaa…
“Mh! Mimi sijui sasa,” alijisemea moyoni kama vile aliisikia sauti kichwani ikimuuliza.
Alitoka nje na kukuta na Musa naye akiwa ametoka ili akaoge…
“Mambo?” Musa alisalimia.
“Poa tu,” mama Shua alijibu kwa mkato sana huku akichukua tahadhari kwa lolote endapo mumewe angetokea na kuhisi vibaya.
Akili haikumpa mama Shua, akaamua kumpigia simu baba Shua lengo ni kutaka kujua aliko lakini simu yake iliita kwa muda mrefu sana bila kupokelewa.
Je, nini kitaendelea hapo? Usikose kusoma kwenye Gazeti la Ijumaa, siku ya Ijumaa.
Baba Shua aliiona simu hiyo ya mkewe lakini hakuona sababu ya kuipokea…
“Kwanza niipokee ili iweje? Najua anataka kujua kuhusu nilipo, halafu akishajua ili iwe nini? Mbona mimi sitaki kujua mambo yake?” alisema moyoni baba Shua na ili kupangua simu ya mkewe, alimpiga mabusu Maua mpaka wakajikuta wakiangukia kwenye kochi kubwa……puu..!
Ukimya ulitawala, kilichosikika ni miguno ya mmmmm…mmmm, Maua alikuwa akihema kwa nguvu kama aliyetoka kufukuzwa…
“Mmmm…mmmm…”
“Ngoja nikafunge mlango,” alisema Maua, baba Shua akamwachia kwa muda.
Maua alifunga mlango haraka na kumrejea baba Shua pale kwenye kochi kubwa. Ukimya ukaendelea kutawala lakini mihemko ya hapa na pale ilisikika kiasi kwamba, kama chumbani kungekuwa na mtu mzima anafuatilia, lazima angetoka kuungana na wawili hao…
“Benny,” aliita Maua kwa sauti iliyotoka kwa chini sana…
“Yes Maua,” Benny naye aliitika kwa kufuata biti ya kuita ya Maua…
“Si utachelewa kazini wewe?”
“Hata kama…usijali Maua.”
Maua kusikia hivyo, akamshika mkono wa kulia baba Shua na kusimama naye, wakaenda chumbani, wakajifungia na kupanda kitandani..!
Figisufigisu ilitawala kitandani, Maua alikuwa akionesha umahiri kwenye uwanja kwa mkakati wa kumrejesha baba Shua kwenye himaya yake. Muda mwingi wa mchezo alimtaka asahau machungu ya kwa mkewe, kwani yeye yupo kwa ajili yake.
***
Baada ya nusu saa, Maua alikuwa amemshika mkono baba Shua, wakawa wanatoka nje. Mkononi Maua alishika funguo za gari…
“Sasa baby si uende na gari…au utakuwa umesahau kuendesha?” alisema Maua…
“Nisahau kuendesha gari sweet..! Haitawezekana hata siku moja.”
Baba Shua alipokea funguo, akazama kwenye gari na kuondoka…
“Kishakwisha huyu…safari hii hachomoki! Ndiyo atajua mapenzi ya kweli yalikuwa wapi kati yangu na yule malaya wake wa nyumbani,” aliwaza Maua akiwa anarudi ndani.
Yeye ni mfanyabiashara wa kuuza nguo za kike na vipodozi toka nchini Thailand na shughuli zake ni popote. Wakati mwingine wateja wake hufika hadi nyumbani. Tena wengi ni wale wanaonunua kwake kwa jumla na kwenda kuuza rejareja madukani mwao.
Kuna siku Maua anaweza kushinda nyumbani na kujikuta akiingiza milioni mpaka kumi.
***
Mama Shua akili ilimlala kabisa. Hakuamini kama baba Shua anaweza kumchunia kiasi kile…
“Ana maana gani sasa kukaa kimya kiasi hiki? Mimi nifikirieje? Kama ameona mimi na yeye basi, si aseme tu kuliko kuwekana roho juu namna hii,” alisema moyoni mama Shua lakini sauti nyingine ilimjibu…
“Kwanza shukuru Mungu wewe…angekuwa mwanaume mwingine angekuua hata kwa kukuchinja! Wewe umeona wapi mume au mke anamwona mwenzake akiingia chumbani kwa mtu mwingine ili kusaliti halafu anavumilia tu?”
Mama Shua aliamua kuvaa, akaondoka. Lakini si kwenda kazini kwake, bali kwa baba Shua akajue nini kilimsibu.
Akiwa ameshatoka, mbele alimwona Musa akiingia kwenye gari lake, mama Shua akasimama mahali ili kumpa nafasi Musa ya kupotea kwanza mbele ya macho yake ndipo na yeye aendelee na safari yake.
Mama Shua anafika nje ya ofisi ya mume wake, baba Shua naye anawasili kwa gari la Maua.
Aliegesha gari mahali, akashuka na kutembea kwa mwendo wa pole kuelekea ndani. Mama Shua hakuweza kuvumilia na alijuwa kwa tabia ya mume wake ya siku mbili zile, angeweza kumpita bila kumsemesha, akasimama njiani kwenda ndani…
“Baba Shua nataka tuongee kidogo,” alisema mama Shua kwa sauti ya chini sana…
“Mimi na wewe tutaongea nini sasa? Na tangu lini mahali pa kuongelea pamekuwa hapa ofisini?” alijibu baba Shua akiwa anaendelea kutembea kiasi kwamba, baadhi ya wafanyakazi walipoiona picha hiyo walishangaa kwani wanawajua wawili hao kwamba ni mke na mume.
Mama Shua hakutaka makuu, akaamua kugeuza kuondoka huku moyoni akiwa na faraja kwani alishajua mumewe amefika kazini lakini alikuwa na maswali kibao…
“Hili gari ni la nani? Halafu kama jipya! Kalitoa wapi? Au huko alikokwenda? Maana kwa muda aliotokea nyumbani isingekuwa rahisi ndiyo awe anafika kazini muda huu, lazima alipitia mahali…
“Atakuwa amelinunua au kalikopa? Lakini lilishaanza kutembea,” aliwaza moyoni mama Shua akitokomea kabisa eneo hilo.
Alifika nyumbani akiwa amechoka sana kiakili na mwili. Aliwaza namna ya kuwasiliana na mama yake na kumweleza matatizo yake lakini moyo ulisita. Alijua ataamsha hasira za mama huyo.
Alimwangalia mtoto wake, Shua. Akamhurumia sana huku akitingisha kichwa.
***
Saa sita mchana, Musa alimtumia meseji mama Shua…
“Upo?”
Mama Shua alipoisoma meseji hiyo alisonya kwa nguvu kiasi kwamba, kama nyumba ya tatu kulikuwa na mtu muda huo angesikia…
“Huyu kijana mjinga sana. Yaani anadhani mimi niko poa? Kwani ye hajaona yaliyotokea?” alijiuliza moyoni mama Shua.
Musa alipoona meseji haijajibiwa, aliamua kupiga. Simu yake iliita mpaka ikakatika…
“Khaa! Huyu mbona hapokei simu?” alijiuliza Musa, akapiga tena. Safari hii, mama Shua aliamua kupokea huku uso ameukunja vibaya sana…
“Haloo…”
“Baby, mbona hupokei simu yangu jamani? Unajua nimekuandalia zawadi gani lakini?”
Uso wa mama Shua ulianza kukunjuka kwa mbali sana…
“Ah! Samahani sana jamani baby, nilikuwa mbali na simu…enhe! Zawadi gani hiyo my darling?”
“Ni ‘sapraizi’…”
“Jamani baby wa mimi si uniambie tu…”
“Tukikutana nitakuonesha achilia mbali kukwambia…”
“Da! Lini sasa tutakutana..?”
“Wewe tu…”
“Basi iwe leo jioni…”
“Wapi?”
“Panga wewe ila isiwe kule kwa siku zote maana kuna mzee mmoja wa kijijini ni mnoko vibaya sana…”
“Nyumbani kwako lakini kukoje?”
“Wapi?” “Kwa wewe na mume wako…hajamaindi ile ishu?”
“Wee hayo yaache Musa bwana…nitakwambia kitu siku nyingine lakini… ila hali si nzuri kivile.”
Walizungumza, wakapanga kukutana maeneo mengine jioni ya siku hiyo ambapo mama Shua angetokea nyumbani na si kazini kwani hakwenda kazini.
***
Maua, muda mwingi aliutumia kuchati na baba Shua kwa kumtumia meseji mbalimbali za mahaba na kumpa pole kwa kazi. Pia kumsifia kwamba yeye ni mchapakazi hodari.
Ilipofika mchana wa saa saba, Maua alimtumia meseji baba Shua ya kumuulizia kuhusu chakula…
“Baby lanchi.”
Kwa baba Shua lilikuwa jambo geni na jipya pia. Hakuwahi kuwaza kwamba, Maua anaweza kurejesha mapenzi ya dhati kiasi hicho. Alijisikia furaha moyoni, ilimsaidia pia kumsahau mama Shua na tabia zake.
***
Saa kumi na moja, baba Shua alikuwa ndani ya gari akielekea Kinondoni kwa rafiki yake anayeitwa Jome.
Alipofika kwa Jome, akashtuka sana Jome…
“Ee bwana vipi?” aliuliza Jome.
“Poa, vipi kwani?” “Mbona nimemwona shem mahali…”
“Wapi?”
“Pale Hoteli ya Bwawani One…”
“Na nani?”
“Ah! Sina hakika lakini wewe ni mwanaume utakuwa unajua namaanisha nini!”
“We niambie tu, umemwona na nani?”
“Na dogo mmoja hivi…”
“Namjua…” “Ah! Kwa hiyo unajua kila kitu kuhusu shemeji?”
“Najua.”
“He! Ee bwana…kwani kuna nini?”
“Kaka…mama Shua si yule tena…mama Shua kadanganyika na huyo dogo uliyemwona naye…nilitaka kuchukua hatua kali, lakini nimeona nimwache yeye na maisha hayo na mimi niwe na maisha mengine, naamini itanisaidia…”
“Da! Kwani yule dogo unamjua?”
“Nini kumjua Jome, naishi naye nyumba moja. Nikienda chooni napita mlangoni kwake.”
“We Benny…kweli?”
“Kweli Jome…”
“Ah! Ina maana nafuu na Maua?”
“Ndiyo niko naye sasa…”
“Ha! Kweli kaka?” “Kweli Jome.”
Basi, baada ya hapo walizungumza mambo mengi mpaka ikafika hatua wakaagana. Jome alimsindikiza baba Shua nje mpaka kwenye gari…
“Ha! Benny, una usafiri mara hii?”
“Wa Maua…”
“Heee! Maua huyuhuyu Maua shemeji yangu wa kitambo?”
“Huyohuyo bwana…amekuja kwa kasi sana.”
“Safi sana…safi sana…sasa Maua ndiye mke,” alisema Jome…
“Kaka ni kweli. Nimekwenda hadi kwake. Kaniingiza ndani kasema hakuna mwanaume aliyewahi kuingia. kanitambulisha mpaka kwa majirani zake kwamba mimi ndiye mchumba wake nilikuwa nje ya nchi kimasomo.”
Hapo, baba Shua na Jome walisimama nje kwenye gari wakizungumza…
“Inaelekea wapi sasa?” aliuliza Jome…
“Home kwanza, halafu Kimara kurudisha gari la Maua…”
“Nipe lifti, niache hapo mbele tu,” alisema Jome, wakaingia garini wote.
Baba Shua alipita barabara ileile yenye Hoteli ya Bwawani One, akaliona gari la Musa…
***
“Yaani baby nimeshukuru sana kwa zawadi. Bonge la gauni, kama ulinipima vile,” alisema mama Shua akimwambia Musa huku wakiwa wamekaa kwenye baa ya Hoteli ya Bwawani One wakinywa juisi kwanza kabla ya kuzama chumbani kwa ajili ya majomboz…
***
“Jome ndiyo hoteli hii ulipomwona mama Shua?” aliuliza baba Shua…
“Hapahapa…tena wale pale wamekaa. Hebu ingia na sisi tukakae tuone,” alishauri Jome, baba Shua akaingiza gari kwenye maegesho ya hoteli hiyo na kupaki sanjari na gari la Musa, wakashuka wote.
Walikwenda kukaa nyuma ya meza waliyokaa mama Shua na Musa na walipokaa, Musa aliwaona kwa sababu aliwafesi, mama Shua aliwapa mgongo…
“Mama Shua tumekwisha…mume wako na jamaa mwingine wamekaa nyuma yako,” alisema Musa kwa sauti ya chini huku akiangalia sakafuni kwa aibu kubwa…
“Wewe Musa…unasema kweli?” aliuliza mama Shua…
“Mungu vile! Halafu inaonekana wamejua wewe upo hapa. Na mbaya zaidi walipokaa, huwezi kukimbia wala kufanya lolote zaidi ya kuonekana."
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi
