
Mtunzi: Richard Mwambe
SEHEMU YA KUMI NA SITA
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
“Kuna kazi nyingine anafanya huko mjini,” alipojibu hayo mara simu yake ya mkononi ikaita kutoka katika mfuko wa jeans, Amata akainyakuwa na kusoma jina lililopo hapo juu ‘Moriyo’, “Moriyo ndo nani?” Amata aliuliza tena.
“Ni mwenzangu yuko hapo chini ananisubiri, tumeambiwa tupeleke haraka hilo begi,”
JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
ENDELEA...
Kamanda Amata hakupenda kupoteza muda, alimuwekea ile bastola katika sikio lake la kuume, “Usiniue kaka, nina watoto mimi watalelewa na nani?” alilia kwa uchungu.
“Ungekuwa na watoto unaowajali, ungefanya kazi za kishetani kama hizi, sikuui lakini lazima uwe mlemavu ili siku zote za maisha yako umkumbuke Kamanda Amata,” alipotamka jina hilo, akamuona Yule jamaa akishituka na kuguna kama aliyekutana na jinamizi.
“Umesema we nani?” aliliza hata akawa amesahau kama ana jeraha baya la risasi katika goti lake, “Amata, Kamanda Amata, na siyo mzimu ni mimi mwenyewe halisi, namtaka huyo Wambugu na mwenzake Bill,” Yule jamaa bado aliduwaa akimkodolea macho Amata, “WE umeshakufa kaka,” Yule jamaa aliongea kwa unyonge.
“Ni sawa, na sasa nimefufuka kutoa wafu kama nilivyosema,” kabla hajaendelea na lolote, Kamanda Amata alimshuhudia Yule jamaa akitapatapa akirusha miguu huku na kule, alipomtazama vizuri, aligundua tundu la risasi kifuani mwake, risasi imepigwa wakati gani, kitendawili. Alichosikia yeye ni mvumo hafifu wa kitu kama nyigu kumbe tayari chuma hicho kilishatumwa kutoa uhai wa mtu. Amata alitazama huku na kule bado ukimya ulitawala, mara akasikia nyayo za mtu zikitembea harakaharaka kwenye korido, akatoka haraka na kuufungua mlango , akashuhudia mtu akiishia kwenye lifti ya jingo hilo, haraka akakimbia na kuziwahi ngazi za kushukia chini na kuteremka nazo. Kamanda Amata alfika chini na kushsudia Yule mtu akiwahi kuingia katika gari Fulani, lakini kabla hajaisjia garini, tayari shabaha isiyo na chembe ya uongo kutoka katika mikono makini ya Kamanda Amata, Tanzania Secret Agency ilikuwa imeshafumua ubongo wa kiumbe huyo na kumfanya alalie kiti cha dereva bila uhai huku miguu ake bado ikiwa nje ya gari hiyo, kazi imeanza. Hakumjali marehemu wa ndani wala nje, aliichukua ile simu aliyokuwa ameichukua kwa Yule jamaa wa kule ndani na kuifungua, haikuwa na namba hata moja, akenda kwenye meseji pale mwili ulimsisimka hata nywele alihisi zina simama baada ya kukutana na ujumbe uliondikwa,
‘Hakikisha kahaba Rose anauawa kabla ya jua la asubuhi, kisha nitakupa kazi ingine,’
‘Kahaba Rose,’ Kamanda Amata alilirudia jina hilo akilini mwake mara kwa mara, akiwa amesimama kwenye kiambaza cha ukuta aliendelea kusukuti juu ya kahaba huyo kamanahusika na lolote katika sakata hili, lakini muunganiko wa matukio haukuwa sawa kwake, alimfikiria Yule mwanamke aliyepewa kumstarehesha kama ndiye lakini haikuwa hivyo, nwuisho alimua la kuamua, kumsaka kahaba ni kazi ndogo sana, aliweka bastola yake mfukoni na kuiendea simu iliyokuwa jirani, ‘simu ya jamii’ akukwanyua mkono kutoka katika kikalio chake na kubofya namba yenye tarakimu tatu na kusikiliza upande wa pili.
“Yes hallo tukusaidie nini?” ilikuwa ni sauti ya polisi wa kikenya, ambayo ilitaka kumfanya Amata kucheka lakini hakufanya hivyo.
“Intercontinental hotel, kuna mauaji yametokea na pia kwenye maegesho ya gari ya hoteli iyo hiyo pia kuna mauaji mengine yametokea,” kisha akakta simu, halafu akacheka kutokana nay eye kuiga lafudhi ile ya kikenya. Alitoka eneo lile na kubana sehemu nyingine, muda kidogo alishuhudia gari mbili za polisi waliofika eneo hilo na kuivamia hoteli hiyo, alipoona hilo kwake limewezekana, akabaki na kazi yingine ngumu ya kumpata kahaba Rose na vipi awe ahusiki na hili, lilikuwa swali linguine, akasonya na kuingia mtaani akiacha hekaheka za wale askari zikiendelea.
˜˜˜
Jua change la Nairobi lilianza kuikwea anga tulivu la jiji hilo, watu huku na huko walikuwa wakiwahi makazini, wengien kwenye matatu na wengine kwa miuu yao wenyewe, ilimradi tu ilionekana asubuhi tulivu.
Lakini hali haikuwa hivo katika kanisa kuu la Familia takatifu, wakiwa bado hawajaondokewa na majonzi ya kifo cha Fr Gichuru, asubuhi hii wanaamka na kupotelewa na monstrance ambayo ililetwa kutoka Vaticna, maalumu kwa ajili ya maadhimisho ya jubilee ya miaka mia moja ya ukristu nchini hapo. ‘Kwa nini wameichukua?’ lilikuwa ni swaligumu kidogo kwa maana hakuna aliyejua lolote juu yachombo hicho zaidi ya yeye anayekitafuta.
“Tutaieleza nini Vatican?” sauti ya masikitiko ilimtoka mhashamu askofu Njue iliyotoka kwa tabu kidogo kutokana na uzee uliokuwa ukipiga hodi kwa kasi ya ajabu iliwafikia makasisi wachache waliokuwa wameketi pamoja nae katika meza yake kubwa anayoitumia kwa mikutano na wasaidizi wake hao, wakiwa katika hali ya ukimya hakuna aliyekuwa na jibu sahihi juu ya swali hilo lililoulizwa na baba Askofu.
Habari ya kuibiwa kwa Monstrance hiyo ilitapakaa kama upepo wa pwani, kila mtu alisema lile ambalo kwake lilikuwa ni sahihi. Mapigano ya polisi na majambazi usiku uliotangulia lilikuwa gumzo linginem kukutwa kwa mwili wa Cheetah katika ghetto ilikuwa ndiyo habari ya kuvutia zaidi kwani jmbazi hilo sugu limetingisha sehemu mbalimbali lakini hakuna watu walioweza kumtia mbaroni, kila mtu hakuna aliyejua, jambazi huyo amekufaje, wengine walionekana kufurahia kifo hicho lakini wengine walisikitika ‘kwa nini hawakumkamata hai’ basi ilimradi ni mazungumzo mchanganyiko. Hakuna aliyezungumzia mauaji ya kasisi ambayo ni wiki moja tu imepita bali kila mtu alikuwa anavytiwa na vifo vya majambazi hao wawili na kuibiwa kile chombo kitakatifu. Magazeti hayakuwa mbali kupamba kurasa za mbele kwa picha na habari moto moto.
Ni sergeant Maria tu aliyesimama katika uwanja wa kanisa hilo akiwa hana furaha sana, akiwa na askari wawili wenye furaha, walionekana wakizungumza jambo Fulani na paroko wa kanisa hilo Fr Joh Smith, wakipeana maelekezo ya hapa na pale, wakitazama hiki na kile, baada ya mazungumzo marefu waliagana na kuahidi kurudi tena kwa uchunguzi wa kina.
“Afande,” mmoja wale askari aliita, Sargeant Maria akageuka kumtazama kwa jicho lake kali, “Inaonekana hauna furaha, nini tatizo zaidi?”
“Furaha yangu ingekuwa kubwa kama Cheetah, angepatikana na roho yake, lakini haikuwa hivyo, kwa desturi ya majambazi lazima wamegeukana katika malipo,” Sargeant Mari alijibu huku akijiingiza kwenye gari ake.
“Itakuwa Mellina kamgeuka Cheetah, hilo linawezekana? Maana aliyebaki hai ni yeye tu na hapa amekimbia,” Yule askari aliongeza maswali, Sargeant Maria Litulia kwa muda kisha akainua uso wake na kumwangalia kija huyu, “Umenipa wazo jipya, Mellina anaweza asiwe aliyemuua Cheetah, uko sawa, sasa nani? Wambugu au Bill!! Kazi bado ngumu, twendeni kituoni,” aliamuru huku akiwa anatoa kalamu na kijitabu chake akaandika mambo Fulani Fulani humo.
Sergeant Maria akiwa tayari akili yaje imekaa vyema alimuru vijana wake waanze msako kumsaka Mellina popote atakapopatikana na aletwe akiwa hai ili aeleze kisha chote kabisa na sababu ya wao kufanya hayo yote. Jeshi la polisi likajipanga kuhakikisha ile monstrance inapatikana na Mellina anatiwa nguvuni wakati huohuo idara kubwa za usalamaa zimejipanga kumtia nguvu Bill Van Vetgand, wakiwa hata hawana habari ya ujambazi huo wakiuona kwao ni matukio ya kipolisi ya kila siku, wakiwa hawajui kuwa kuna muungano mkubwa katika hayo yote mawili, wao walikaza jicho lao kwa jasusi Bill pekee, wakiwa wamemtega kila upande kwa kila mtindo lakini walishangaa Bill hakuonekana mjini kote, ametoweka. Hali hii iliwafanya kuchanganyikiwa zaidi, atatowekeaje wakati njia zote za kutokea nje ya Nairobi zimefungwa na wanausalama? Hii iliwapa moyo FBI na vyombo vinine kuwa mtu huyu hatari bado yupo Nairobi, hivyo waliongeza msako tuli, msako usiyo na fujo.
Siku hiyo asubuhi, kikao kifupi cha maafisa wa polisi kilikuwa kikiendelea katika ofisi ya mkuu wa polisi mkoa wa kati, Inspekta Saitoti.
“Sargeant Maria, nahitaji hizo tafutishi haraka, Mellina kama nilivyokuagiza, namhitaji hapa, hiyo Monstrance lazima ipatikane kwa udi na uvumba, pia nahitaji uchunguzi wa kina juu ya mauaji pale hotelini ili tujue kama vina uhusiano au la,” Saitoti alizungumza kwa ukali huku akiirekebisha kofis yake kichwani mwake.
“Sawa afande, opereshen inaendelea na kikosi kipo kazini, ripoti itakuja jioni afande,” Maria alijibu kiaskari.
“Nakuaminia sana, piga kazi,” alimalizia Saitoti.
Sargeant Maria alitoka ofisini akionekana kusawajika uso wake kwa mawazo lukuki, akapita kaunta na kuzunguka nyuma ya kituo hicho ambapo kuna mgahawa mdogo na kuketi ndani yake, kisha akaagiza sturungi (Sturungi ni chai ya rangi) ili imchangamshe kidogo. Akiwa katika meza hiyo pamoja na maafande wengine, mara kijana mmoja mchafu sana aliingia kwenye mgahawa huo na kuketi mbele ya sergeant Maria, wakatazamana macho, maria akakunja sura yake kuonesha hakuridhika kwa kijana huyo kuketi hapo.
“Afande, nna njaa, ninunulie japo chai kisha nitakutatulia tatizo lako linalokuumiza kichwa,” yule kijana akajieleza, Maria alimwangalia tena na tena.
“Niambie kwanza!” Maria alidai lakini yule kijana akawa kimya akimtazama afande huyo wa kike aliyeshupaa kwa misuli kama mwanaume…
Sergeant Maria akamuagizia chai Yule kijana na kumpatia, naye akaanza kunywa kwa fujo bila kujali kama chai hiyo ni ya moto, alionekana hasa ana njaa kali asubuhi hiyo. Maria alitazama saa yake na kuona tayari asubuhi imepamba moto anahitaji kwenda katika majukumu mengine.
“Naona una haraka ya kuondoka, subiri kwanza,” Yule kijana akamueleza Maria, naye akavuta subira, akatulia kitini na kuanza kusoma gazeti la Daily Nation. Yule kijana alipomaliza kunywa ile chai akamshukuru sana sergeant Maria aliyekuwa ameketi mbele yake.
“Afande, usione mi nimevaa hivi labda ukafikiri ni kichaa au mvuta bangi, hapana, nina akili na ni mzima kabisa, hii ni moja tu ya miondoko ya mji mkubwa kama huu” akameza mate na kuendelea na hab ari yake ambayo sergeant Maria aliona kama anapotezewa muda, “Najua unaona kama nakupotezea muda, lakini kazi unayoenda kuifanya mimi ndio nitakupa msaada mkubwa sana, sikia, hiyo kesi unayoifuatilia ya Mauaji ya kasisi ni kesi pan asana kuliko wewe na wenzako mnavyoichukulia, ninyi mnatazama mauaji ya Fr Gichuru, na kumsaka muuaji na monstrance iliyopotea, lakini hali sivyo ilivyo, kwa uwezo wenu nyie lazima mtaishia katikati kwani katika kesi hiyo kuna mkono wa kimataifa, mkono nambao pambano lake lazima liwe la kimataifa vilevile,”
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi