
Mtunzi: Richard Mwambe
SEHEMU YA KUMI NA TISA
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
“Kamanda Amata karibu sana,” alimkaribisha.
“Asante sana nafurahi kukutana na wewe, sasa kilichonileta hapa ni juu ya mauaji ya kasisi, Fr Gichuru. Ningependa kujua juu yake kwa kifupi ili nijue wapi pa kuanzia,”
JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
ENDELEA...
Amata alianzisha mazungumzo ya kikazi. Fr Joe Smith, alimueleza Amata kila kitu kuanzi asafari yake ya Roma kwenda kuchukua ile monstrance mpaka aliporudi, na mazingira ambayo kifo chake kilitokea, akamueleza pia juu ya kupotea kwa Gichuru kwa takribani masaa 24 na yote yaliyotukia. Kamanda Amata alitulia kitini akisikiliza kwa makini huku akiandika vitu Fulani katika kijitabu chake kidogo.
“Umesema majambazi hao wamechukua Monstrance, unafikiri kuna nini katika chombo hicho?” Amata aliuliza.
“Kwa kweli sijui labda kwa sababu ya malighafi iliyotengenezewa, kwa maana ile monstrance imetengenezwa kwa dhahabu tupu na ni ya gharama sana pia ni ya kihistoria sana katika kanisa,” Fr Joe alieleza.
“Baada ya mauaji ya Kasisi, umesema siku chache baadae mlivamiwa na majambazi ambao sasa ndio walikuja kuichukua hiyo Monstrance, siku ya tukio wewe ulikuwepo?”
“Nilikuwepo, nilijificha huku juu ghorofani, niliangalia mapambano malali sana ya polisi na majambazi, lakini mwisho wa yote ile gari ya majambazi iligonga mti hapo nje na gari nyingine ikaja na kuchuku lile begi kisha wakaondoka, sasa hapo sijaelewa nini kimefanyika,” alijibu kwa ufasaha.
“umesema siku ya mauaji mtawa wa kike Rose alishuhudia na pia umesema siku ya kuibwa hiyo monstrance mtawa huyohuyo alishuhudia, je huoni kuwa kuna uhusiano kati ya matuklio haya? Nikimaanisha kuwa Rose anahusika moja kwa moja, na yeye anaweza kutufungua masikio katika hili,” Amata alimshtua kidogo Fr Joe na kumuacha akiwa na bumbuwazi, aliporudiwa na fahamu alijibu.
“Hapana, ni bahati tu labda niseme, mtawa Rose yeye anahudumu huko kanisani ndiyo maana haya yote yamemkuta huko, lakini kuhusika yeye sina uhakika na hilo,” Fr Joe alijibu kwa upole.
“Naweza kumuona Sr Rose?” Kamanda Amata aliuliza, na bila kuchelewa alivuta simu yake na kupiga kwa masista, akongea maneno machache na kukata simu ile.
“Kamanda Amata, tunahitaji kupata hii Monstrance, Vatican haitatuelewa kabisa, mimi naumia sana,” Fr Joe aliongea huku akitoa machozi.
“Usijali father, itapatikana tu endapo mtanipa ushirikiano wa karibu,” Kamanda Amata alipokuwa akisema hayo mara mlango ukafunguliwa na mtawa Rose aliingia ndani ya ofisi ile na kuwakuwa watu hao wawili pamoja na Fr Joe, akakribishwa kiti na kuketi upande ule wa Fr Joe, akatulia na kutazamana na Amata.
“Ahusiki tangu machoni pake,” Kamanda Amata alitamka hayo, kawa kuwa alitazamana macho na mtawa yule na kuyasoma kitaalamu na kugundua kuwa hana hatia, kwani mwenye hatia usomeka tangun machoni na katika pua zake.
“Pole sana Sr Rose kwa mikasa iliyokukumba, tupo hapa katika kuona ni jinsi gani ambayo itatusaidia ili kupatikana kwa ile monstrance, nikuulize swali moja ulipopelekwa polisi kwa mahojiano ulihojiwa na askari gani, unaweza kumjua kwa jina?” Kamanda Amata aliuliza kitu ambacho hakuna kati yao aliwaza.
“Anaitwa Sargean Maria,” Rose alijibu.
“Ok, asante, nilitaka kujua hilo tu, sasa kuanzia sasa hutakiwi kumueleza mtu yoyote habari hii isipokuwa mimi tu kama nikihitaji,” Amata alisistiza, “Fr Joe, mimi nimekuja kufanya kazi hii kwa siri sana , hakuna anyejua uwepo wangu hapa Nairobi, naomba usimueleze mtu yoyote juu ya uwepo wangu hapa kwako na Nairobi kwa ujumla, mimi nitawasiliana na wewe kwa jinsi ninayoijua mimi tu, sawa father?”
“Sawa, usijali Kamanda,” Fr Joe alijibu.
“lakini kabla sijaondoka, naweza kutembelea chumba cha marehemu? Nahitaji kujua kama naweza kupata chochote cha kunisaidia katika kazi yangu,” Amata aliomba, Fr Joe akamchukua na kumpeleka katika chumba hicho kidogo chenye kitanda cha futi tatu na nusu, kilikuwa chumba cha kimasikini hasa, meza moja ya mbao ilibeba vitabu vichache na kitabu kimoja cha kumbukumbu, ukutani palikuwa na kanzu zilizoning’inizwa, bila shaka zilikuwa za marehemu, Kamanda Amata akavuta hatua fupi mpaka pale mezani na kunyanyua kile kijitabu cha kumbukumbu, akafungua kurasa moja baada ya nyingine, kijitabu hicho kikamvutia sana, akamtazama Fr Joe akaona yuko mbali kimawazo, akakitia katika mfuko wa ndani wa koti lake, kisha wakarudi mpaka pale ofisini na kauagana, akamchukua Kahaba Rose na kuondoka akiahidi kurudi tena muda wowote.
Dakika chache baadae kahaba Rose na Kamanda Amata walikuwa tayari barabarani kuelekea mjini, mbele kidogo baada ya kuvuka eneo la St Paul kuelekea Westland hakuna aliyekuwa akiongea na mwenzake katika gari, Kamanda Amata alipinda kushoto na kuingiza gari katika maegesho ya supermarket ya Nakumatt.
“Nawataka watu wawili kwanza,” alimueleza kahaba Rose
“Nani na nani na wa nini?” Rose aliuliza
“Utawapata wapi? Kwa vyovyote kila mmoja yuko mafichoni mwake saa hii,” Rose alieleza
“Mimi najua pa kuwapata na wewe unajua jinsi ya kuwapata,” Kamanda aliongea kwa kujiamini kama ilivyo kawaida yake, “Ok mpango utakuwa hivi, wewe utarudi nyumbani kwako, kwa kuwa wale jamaa wanakutafuta wakuue mimi nitakuwa pale ili niwashughulikie na wanipe ramani ya wapi Bill alipo.”
Kahaba Rose hakuwa na la kupinga hoja hiyo alitikisa kichwa juu chini kuashiria kuwa ameelewa vyema mpango mkakati huo jinsi ulivyo. Rose aliinua mkono wake wenye saa na kuitazama.
“Vipi, Saa ngapi?” Amata aliuliza.
“Saa nane kasoro,” Rose alijibu huku akishusha mkono wake.
“Ok, twende tupate chakula cha mchana kisha tuanze shughuli yetu,” kamanda alieleza huku akifungua mlango wa gari kushuka nje, naye Rose akafanya vivyo hivyo. Kati ya viti vingi vilivyo mbele yao wawili hawa walichagua viwili vilivyowafaa na kuketi kabla hawajaagiza juice wakati wakisubiri chakula cha mchana.
Kamanda Amata alijitahidi kutupa jicho huku na kule kuchunguza lolote ambalo linaweza kumsaidia katika sakata lake hilo lakini hakuna kitu, ila mara kadhaa alitabasamu kwa kumuona kijana mmoja teja jinsi alivyokuwa akirandaranda kwa mwendo wa madaha katika maeneo huyo bila kuchoka kuomba pesa ndogondogo kwa wateja wa eneo hilo, ilikuwa kero kwa kiasi Fulani kwa waliopo eneo hilo kila askari walipokuwa wakimtoa yeye alirudi kwa njia nyingine.
“Vipi mbona unamshangaa huyo teja?” Rose aliuliza
“Ah huwa napenda wanavyotembea,” Amata alijibu.
“Kweli hauna kazi.” Rose alimkebehi Amata
“Hata hii ya kumwangalia ni kazi pia,” Amata alijibu huku akitoa tabasamu lake la nadra mbele za watu. Wakiwa katika mazungumzo na Kahaba Rose mara Yule teja akaja mpaka pale katika meza waliyoketi Amata na Rose, huku udenda ukimtoka. Rose alijaribu kumfukuza na kuita askari wa ulinzi, lakini Kamanda Amata alizuia Yule kijana asiondolewe pale.
“Muacheni, ni mgeni wangu huyu, mpeni juice tafadhali na biskuti kadhaa,” Kamanda Amata aliamuru na amri ikatekelezwa haraka. Kamanda Amata alitazamana uso kwa uso na kijana Yule ‘teja’ macho yao yaligongana na kuangaliana kwa kina, Yule kijana alikuwa akipepesa macho kwa mtindo wa ajabu sana, harakaharaka, akaifumba na kufumbua kwa mitindo tofauti, akigeuzageuza mboni zake kwa hali ya kupendeza, naye Amata alikuwa akimfanyia vivyo hivyo kwa kupeana muda, pembeni Rose alikuwa akifa kwa kucheke alipokuwa akiangalia wawili hao walipokuwa katika huo mchezo wa ajabu, mchezo wa macho. Baada ya kumaliza juice yake Yule kijana alinyanyuka akatoa ishara ya kuishukuru, Amata akampa shilingi mia ya Kenya na kumruhusu aende.
“Mh, duniani kuna mambo” Rose alisema, Amata akageuka kumtazama Rose, “Kwa nini wasema hivo?” Amata aliuliza.
“Si kama hivi, kijana Yule madawa yamemuharibu kabisa, ona sasa hata wazazi wake wamepata hasara ya kulea,” Rose alilalama.
“Usiseme hivo, hawa ni watu wa kuwapenda tu, katika kupenda usibague maana leo kesho hujui ni katika mazingira gani utahitaji msaada wa nani.” Kamanda alimueleza Rose kwa upole.
“Ok, sasa amekaa hapa anachekacheka tu na ndio mlikuwa mnafanya nini na macho?” Rose aliuliza.
“Aaah hawa huwa hawapendi kuongea wao ni kuchekacheka tu kama ulivyoona na kuchezesha macho vile ni jambo wanalolipenda sana,” Amata alieleza. Alitupa jicho nje ya wigo wa supermarket ile na kumuona Yule teja akipotelea mitaani.
§§§§§
“Vipi afande mbona una mawazo mengi sana?” afande Otholong’ong’o alimtupia swali Sargeant Maria aliyekuwa amesawajika uso kwa mawazo na macho yake yakiwa yametopea kwa uchovu, aliinua uso na kumwangalia askari huyu kijana ambaye katika mapambano yao na majambazi aliumizwa mguu kwa risasi, sasa alikuwa amerudi nyumbani baada ya matibabu kukamilika. Alikuwa nyumbani kwake maeneo ya Kasarani kwa mapumziko akiuguza jeraha lake.
“Nimepambana na kazi nyingi za upelelezi lakini hii inanitoa jasho afande,” Marina alieleza, “Kwa nini? Mbona kama imeisha maana wale wawili wamekufa bado huyo Mellina, na kumpata sio tabu, unafikiri atakuwa amekimbia?” Otho aliuliza.
“Kukimbia sidhani., lakini hata hivyo pia anweza kuwa hayuko nchini, hali akijua kuwa swahiba zake wameuawa,” Marina alieleza.
“Kazi ndogo afande, anzisha msako wa kwenye mabasi yote ya abiria, treni na hata ndege ili kumbaini kama bado yupo ao kakimbia, sambaza na picha zake kwenye maeneo husika,” Otho aliongea, huku akijaribu kuinuka pale kitini.
“Otho! Ni point ambayo sikuwaza kichwani yangu, umenipa wazo, sasa lazima nimtie mkononi,” Maria alieleza lakini sauti kavu ya Otho ilimpa tena swali ambalo lilimrudisha Maria katika lindi la mawazo, “Na baada ya kumpata Mellina, nini kitafuata? Na hicho chombo kilichoibwa kanisani tutyakipataje?” lilikuwa swali gumu lililoulizwa na Otho. Maria alitulia kimya huku akichezea simu yake, akikosa jibu la moja kwa moja la kumpa Otho aliyeonekana akilisubiri kwa hamu sana, “Tumpate kwanza Mellina, yeye ndiye atatupatia picha nzima ya nini kilitokea na nani anahusika katika hilo, kishapo tutajua hicho chombo kipo wapi na jinsi ya kukipata, lakini Otho, kesi hii ina mambo ya ajabu mengi sana” Maria alimsimulia Otho juu ya Yule kichaa na maneno tata aliyomueleza na pia jinsi alivyomtoweka kimiujiza. Otho alimsikiliza bosi wake mpaka alipomalizia mkasa huo.
“Ila majamazi sio watu aisee, kinachonichanganya wakati wa mapambano yetu, kuna gari nyingine ilikuja na kumchukua cheetah na hilo begi kisha wakaondoka zao,
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi