MAUAJI YA KASISI (21)

Zephiline F Ezekiel

SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA
ILIPOISHIA...
“Wewe unamtaka Bill? Lakini kuna kesi nyingine hapa inaungana nay a Bill. Kiasi kwamba lazima na hiyo uifanyie kazi ili upate picha kamili,” ndege alimwambia Kamanda.

JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈

ENDELEA...
“Yeah, ya mauaji ya kasisi?” Kamanda aliuliza kupata uhakika.

“Ndiyo hiyo, kwa sababu inaonekana Bill anahusika kwa namna moja au nyingine,”

“Nimeshaanza kuifatilia ila nataka nimfahamu mtu anayeitwa sergeant Maria kwa kuwa yeye nasikia ndio kashika hiyo kesi,” Kamanda alimuelezea Ndege.

“Usijali, kumpata Maria si kazi ngumu,” Ndege akajibu huku akiizungusha gari kwenye mzunguko wa Dagoreti corner, mtaa wa kwanza, wa pili, nyumba ya tano, Ndege alipita kama hataki kusimama mahali hapo na mbele alikunja kona na kuegesha gari karibu na duka noja kubwa la bidhaa mbalimbali, wakateremka, kwanza Ndege akaingia dukani na kununua jojo mbili wakagawana na kutembea taratibu wakiielekea nyumba ya Rose, walipofika mlangoni wakashangaa mlango uko wazi, Ndege akachomoa bastola yake na Kamanda akafanya vivyo hivyo, kisha kwa mwendo wa kunyata wakapita na kuingia ndani, chumba kwa chumba huyu upande huu na huyu upande ule, wakafika chumba cha maraehemu, kamanda alipotupa jicho kitandani hakuna ule mwili, akatazama huku na kule baadae kidogo Ndege akaungana nae, wote wakabaki hawana la kusema, mwili umeenda wapi hakuna jibu.

“Ndege, nilinde tafadhali,” kamanda Amata alimwambia Ndege na kuirudisha bastola yake kiunoni mwake kisha akakijongea kitanda kile alichokuwa amelazwa marehemu, akatazama kwa makini ni mashuka yaleyale tu, alipokuwa anatoka, akaona kikaratasi kidogo chini karibu na kitanda, akakiokota, namba ya simu, akakitia mfukoni, mara wakasikia mlango ukifunguliwa na watu wakibishana, Kamanda na Ndege, wakajificha.

“Mi nina uhakika ni humu humu maana pale si uliinama!” sauti moja ilimwambia mwingine

“Hapa mi sina uhakika unajua,” ingine iliijibu ile ya kwanza

“Tutakuwa tumecheza blanda kweli yaani, sasa tajiri tutampataje? Maana kasema yeye tumpate kwa simu na ye atatulipa kwa simu, hataki tuonane kwa sura.” Ile sauti ya kwanza ilisema.

“Dah huu utata sasa, any way ngoja tuone, fasta basi wasije kutukuta,”

Wale watu wakaingia ndani na kuelekea chumba kile kilichokuwa na ule mwili, wakapekua hapa na pale hawakuona kitu, kasha wakarudi mpaka chooni ambako walianzia kazia ile. Kamanda Amata aliyekuwa katika ficho lake akapata wazo haraka, akatoa peni yake na kijikaratasi kingine kasha akaandika namba yake ya simu anayotumia pale Kenya akachana katika mtindo uleule na kukitupa chini kwenye korido kasha akajificha tena.

“Ah, we, hiki huku,” mmoja wa wale jamaa akakiona na kuikiokota kasha wote wakatoka nje na kuchukua gari yao wakatokome. Ndege na Kamanda wakatoka mafichoni mwao, “Dah, Kamanda kwa nini ulinizuia nisiwashambulie wale jamaa? Tungepata majibu ya maswali yetu,” Ndege alimlaumu Amata.

“Hapana, tunayemtaka sana ni Bill, na Bill mtu mwingine anayejua siri yake kama si Mellina basi ni Wambugu, unajua walikuwa wanatafuta nini?” Kamanda aliuliza

“Sikuwaelewa,” Ndege alijibu. Kamanda Amata akatoa kijikaratasi na kumuonesha, namba ya simu.

“Sasa mbona walisema wamekipata? Sielewi hapo!” Ndege alibaki njia panda.

“Sikia ndege, ukisikia TSA namba 1, ndio mimi, nacheza na akli yako nakutangulia sekunde kadhaa mbele ndiyo maana ya Intelijensia, mi niliokota hii karatasi kabla yao, baadae nikaandika nyingine nikaweka namba zangu ndiyo ile walioiokota wao,” Kamanda Amata akamueleza Ndege.

“Dah! We mkali kaka, sasa inakuwaje?” Ndege aliuliza

“Tutafute sehemu tukae tusubiri watatupigia kasha tunawanasa na watatuambia tajiri wao yuko wapi,” Amata alijibu.

“Lakini tufanye kitu Fulani, twende kwenye shirika la simu hii, tukaombe information zote za namba hii, miito iliyofanya kwa sauti na ujumbe ili tumtafute mtu huyu yuko wapi nan i nani,” Ndege alitoa ushauri, Amata akatikisa kichwa nan a kumpigapiga mgongoni kuashiria kuwa wazo zuri alilotoa.

Wakatoka ndani ya nyumba ile na kuzunguka kule walikoacha gari yao, kwa haraka sana Kamanda Amata aliona ile gari yao haina upepo tairi moja, walipoikabia Kamanda Amata akamshika mkono Ndege na kupita naye wakaiacha ile gari yao pale na kuchukua tax kisha wakaondoka, wakamwambia dreva akawaache barabara ya Waiyaki maeneo ya Westland, wakamlipa nao wakaongoza kuelekea pale makao makuu ya kampuni ya simu ya Kenyatta Telecom, wakafika na kujitambulisha kasha wakapata kuonana na mhusika, mtu wa ICT, baada ya kujitambulisha na kusema shida yao, Yule kijana akafanya kazi hiyo kwa haraka na kuwakabidhi CD moja yenye kila kitu.

“Hii ni MP3 ina audio, data na sms zote,” aliwaeleza. Kamanda Amata na Ndege walitazamana na kumshukuru wakimuachia shilingi za Kenya 5000 wakaondoka zao.

Ndani ya ofisi ya Ndege pale katika jengo la KICC, kamanda Amata na Ndege walikuwa wawili tu ofisini humo wakiwa wameiweka CD ile katika chombo maalum na kuchambua simu zote zilizotoka na kuingia, meseji zote walisoma mpaka wakachoka, lakini hawakukata tamaa, simu a mapenzi ziliwafanya wacheke sana, meseji za nguoni zilizowaacha midomo wazi, wakiwa wamekata tama kabisa kuona kwamba katika namba ile hakuna wanachokiitaji, ndipo walipoona simu moja iliyowashtua, sauti ya mtu mwenye lafudhi ya kizungu, wakajua kwa vyovyote ataku Bill, walisikiliza ujumbe ule mpaka mwisho wakatazamana, haukua mbaya wala haukuwa mzuri, bali ulimtaka mwenye namba ile ajifiche na asionekane nje kwa usalama wake kwani kwa kufanya hivyo atahatarisha maisha yake. Waliinakili ile namba waliyoiona kwenye vitabu vya kumbukumbu vya kila mmoja kisha wakaamua kuondoka zao. Wakiwa njiani simu ya Amata ikaita na kawaida simu hiyo ilikuwa ikipigwa na Rose tu, akainyanyua akitabasamu, akabadilisha sauti na kuongea Kiswahili cha Kenya.

“Sasa mkubwa, kazi imekamilika,” sauti ya upande wa pili ikasema.

“Oh vizuri sana sana sana, sasa kwa kazi mliyofanya, nimeona pia tuonane niwapongeze kidogo, kama mpo radhi tuonane mahali pa utulivu,” Kamanda Amata alisema. Kimya kidogo kikatawala kati yao, “Sawa Boss, tukuone wapi?” ile sauti ikauliza.

“Tuonane Dagoreti Corner the super pub saa mbili kamili usiku.”

“Sawa boss,” ile sauti ilijibu. Ndegeakamtazama Kamanda Amata wakati akikata ile simu.

“Bingo!” Ndege akatamka, akainua mkono na kutazama saa yake, saa kumi na mbili jioni.

§§§§§

Basi la Eldoreti, lililokuwa likitoka Nairobi kuelekea kampala Uganda lilifika eneo la Kisumu, askari wa usalama barabarani katika kituo cha ukaguzi usiku huo wakalisimamisha. Mlango ukafunguliwa na mmoja wao akaingia na kuwatazama abiria, wengine walilala na wengine walikuwa wakiangalia filamu ya Kinigeria iliyokuwa ikiendelea ndani ya basi hilo.

“Haya wote weka vipande yenu juu, tunataka kagua,” askari Yule aliyetangulia aliwaambia abiri, waliolala wakaamka na kila mmoja akatoa kitambulisho chake na kunyoosha juu, ukaguzi ukaanza.

Karibu kabisa na mlango pale mbele alikuwapo mwanamke aliyevaa baibui jeusi na kuruhusu macho tu kuonekana. Askari aliyekuwa aikagua, akaichukua passport yake, Jamila Babiker, ilikuwa ni jina lililondikwa juu ya hati ile, Yule askari aliitazama kwa makini na kuigeuzageuza, akamtazama na Yule mwanamke kwa vizuri, kasha akashuka na ile hati mpaka kwenye ofisi yao ndogo iliyopo hapo, aikiwa na mwenzake waliendelea kuikagua na walipoona hawaridhiki katika hilo, wakamshusha Yule mwanamke na kumleta katika kile kiofisi.

“Mamaa, hii hati yako mbona inatutia wasiwasi?” askari mmoja aliuliza

“Kwa nini wasema hivo na kila siku natumia hiyo hiyo?” alijibu Yule mwanamke.

“Ok, una uhakika na hilo? Sema ukweli kama ni feki tuelewane hapahapa tukuache uende,” askari mwingine alidakia.

Wazo hilo likamfanya Yule mwanamke ababaike kujibu. “Hapana hiyo ni halali kabisa, ni hati yangu ninayotumia kila niendako. Yule askari akavuta simu yake na kupiga simu mahali Fulani, baada ya muda kidogo akatuka zile namba za ile hati ambayo alikuwa nayo pale mkononi mwake. Baada ya muda kidogo ile simu iliita tena na Yule askari akainyanyua, Yule mwanamke akajua sasa mambo yanaharibika maana anajua wazi alichokifanya katika ile hati. Baada ya Yule askari kumaliza kuongea na simu, akamtazama Yule mwanamke.

“Unatufanya sisi wajinga sio?” Yule askari akamuuliza. Yule mwanamke akawa amejishika kiuno mkono wa kushoto na ule wa kulia ameuingiza kwenye mfuko wa lile baibui lake.

“Wamesema ya nani kama si yangu?” aliuliza kwa jeuri.

“Hii ni hati ya Elizabeth Wangari Joseph” Yule askari alijibu huku akiinuka na pingu mkononi, askari wa nyuma yake alikuwa akija kumkamata kwa nyuma, Yule mwanamke kwa wepesi wa ajabu, alipiga teke la nyuma ambalo lilitua sawia katika tumbo la Yule askari wa nyuma na kumsukuma mpaka kwenye lile basi akajibamiza mgongo na kuanguka chini, wakati huo Yule mwanamke akutoa mkono wake wa kulia ukiwa na bastola moja kwa moja akafyatua na kumpiga Yule askari wa mbele kifuani, akarushwa na kujibamiza kwenye ukuta wa ile ofisi, Yule mwanamke akageuka nyuma kwa kasi na bastola mkononi, risasi ya pili ilitua kichwani kwa Yule askari aliyeangukia kwenye basi.

“Leo mtamjua Mellina, nyau nyinyi,” alitamka Yule mwanamke.

“Mikono juu weka silaha chini!” askari mwingine aliyekuwa upande wa pili wa basi. Mellina alijiangusha chini na kuviringika kupita uvunguni mwa basi akatokea upande wa pili, aliposimama na kutazama nyuma alipaishwa juu kwa risasi ya askari aliyekuwa ndani ya gari, alilenga shabaha hiyo ya haraka kupitia dirisha la basi, Mellina alianguka chini na kutoa yowe la maumivu, aligalagala damu ikimmwagika kutoka katika bega lake la kulia, walea skari wakamfiki na kumtia pingu huku jeraha lake bado likivuja damu.

“Mfunge kitambaa kwenye jeraha, asije akatufia njiani,” askari mmoja alipiga kelele, wakamfunga vyema, na kumchukua mzobemzobe wakisaidiwa na wananchi waliokuwa kwenye basi, wale wenye moyo mgumu, maana kelele zilitawala eneo hilo.

Mellina hakuwa na ujanja, hakika, mbio za sakafuni huishia ukingoni.

Taarifa hiyo ya kupendeza ilimfikia Sargeant Maria, tangu sakata hilo lianze, kwa mara ya kwanza Maria alitabasamu kwa bashasha, akainuka na kumfuata Inspekta Saitoti ofisini kwake.

“Ndiyo afande,” Saitoti aliitikia hata kama hakuitwa, baada ya kupokea saluti ya utii. Maria akampa taarifa hiyo tamu ambayo ilimfanya ashibe hata kama hajala.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi

Chapisha Maoni