
Mtunzi: Richard Mwambe
SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
kwa mara ya kwanza Maria alitabasamu kwa bashasha, akainuka na kumfuata Inspekta Saitoti ofisini kwake.
“Ndiyo afande,” Saitoti aliitikia hata kama hakuitwa, baada ya kupokea saluti ya utii. Maria akampa taarifa hiyo tamu ambayo ilimfanya ashibe hata kama hajala.
JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈
ENDELEA...
Mara moja inspekta Saitoti akaamuru gari ya plisi kutoka kuelekea Kisumu kumleta huyo anayeitwa Mellina. Safari ikaanza, Sargeant maria akiwa katika cabin ya gari na askari kadhaa wakiwa nyuma, mwendo wa kasi wa gari hiyo ulifanya kila aliye barabarani kupisha.
Upande mwingine, jeshi la polisi mkoa wa Kisumu lilikuwa katika masikitiko makubwa kwa kupoteza askari wao wawili katika tukio hilo. Haikuwa kazi rahisi kukubali lililotokea lakini bado hali ilikuwa hivyo ilivyo.
Baada ya masaa kadhaa gari ya polisi kutoka Nairobi iliingia katika uwanja wa Hospitali ya Avenue pale Kisumu. Sergeant Maria alikuwa wa kwanza kushuka na hakuuliza chochote moja kwa moja aliingia ndani ya hospitali hiyo na kuelekea katika wodi aliyoambiwa huku nyuma akifuatiwa na vijana wake waliovalia kishari kabisa na bunduki zao mgongoni. Mellina alikuwa hoi, drip ya maji ikiwa inaendelea kuingia mwilini mwake, Maria alisimama mbela ya kitanda hicho na kwa jicho la hasira huku akiuma meno alimtazama Mellina.
“Ulifikiri utafika wapi wewe kiumbe?” Sergeant Maria alimuuliza Mellina. Mellina alimsonya Maria, na Maria aktabasamau na kuendelea kumwambia, “Huu ni mkono wa dola, haukimbiliki, haya nimekuja kukuchukua na dhambi zako utaenda kutubu Nairobi, ila lazima kitanzi kiitafune shingo yako, mwanaharamu wewe!” kisha Maria akaondoka na Mellina akabebwa katika kitanda maalum, akawekwa ndani ya gari la wagonjwa, kasha safari ikaanza kurudi Nairobi chini ya ulinzi mkali.
§§§§§
Ndani ya Dagoreti corner super pub, Kamanda Amata aliketi karibu kabisa na kaunta wakati Ndege alibana kule kunako mlango wa kuiingilia wateja wote. Mbinu hiyo ilitegwa mahsus kuwakamata wale waliomuua Rose Kahaba, Amata na Ndege walijiua wazi kuwa katika sakata hilo nguvu ya watu wawili ingetosha ilimradi tua mnajipanga kitaalamu. Kamanda Amata alitembea taratibu kuelekea mbele kabisa ya pub ile, akavuta kiti na kuketi. Mhudumu alipokuja alimkuita Amata amekwishaketi.
“Nikusaidiwe nini kaka?” Mhudumu huyu mwenye lafudhi ya Kimombasa alimuuliza Kamnada Amata pale alipoketi.
“Nipe Tusker light,” Amata alijibu, alipokwisha letewa alimsubiri yule aliyemhitaji katika pub hiyo. Melchior Ndege aliketi meza ya mlangoni kabidsa akisubiri aone kile kitakachoendelea kwa kamanda na hao wageni wake.
Ndege aliiona Toyota Spacio moja ikiegeshwa mbele tu ya pub hiyo , akaikazia macho sana na kuwaangalia watu wanaoshuka kuingia ndani ya pub hiyo. Vijana wawili mashababi, wakateremka na kuongeza mambo machache kasha wakaingia ndani na kuelekea moja kwa moja sehemu walioelekezwa, Kamanda Amata akawapa ishara aliyowaambia, wakamfuata na kuketi pembeni yake. Mhudumu wa puba hiyo akaja, vikaagizwa vinywaji na nyama choma za kufa mtu.
“Niambieni kazi ilikuwaje?” Amata alianzisha mazungumzo
“Ah boss, kazi ilikuwa easy tu, tulimkuta anaoga tukammalizia huko huko!” mmoja alijjibu
“Hamkupata upinzani wowote?” kamanda aliendelea
“Hatukupata boss, ila boss mwanamke mzuri kama Yule kwa nini ulitutuma tukatishe maisha yake kinyama vile?” mwingine aliuliza swali lisilo na tija. Kamanda Amata alimtazama kwa jicho kali.
“We unaijua kazi yako?” alamwuliza. “Ndiyo,” naye akajibu
“Yule mwanamke mzuri kwa sura lakini si mzuri kwa roho, kama mlimuua bila kumbaka basi mmekosa utamu alionao,” Amata aliposema hayo wote wakacheka.
“Ilo muhimu boss,” Yule wa kwanza akasema. “Dah! Aisee nyi mna dhambi kweli yaani mmembaka hivihivi halafu ndo mkamuua, au kwa sababu alikuwa anaoga mkamtamani?” kamanda Amata alizidi kuwafurahisha wale vijana.
“Sasa Boss, si hatutaki kukaa sana si unajua Nairobi imechafuka sasa hivi,” jamaa alimwambia Amata.
“Usijali, nataka mnipeleke mlipomfukia Yule Malaya, malipo yenu nayafanya sasa hivi kama ifuatavyo,” Kamanda Amata akavuta briefcase yake ndogo na kuifungua, akavuta bulungutu moja la pesa na kumpa kila mmoja la kwake, “Sina haja ya kuhesabu kwani najua kazi mloifanya ni kubwa,” aliwaambia. Vinywaji vilizidi kuteketea kati yao, na walipomaliza.
Walijipanga kuondoka. Melchior Ndege, alikuwa kwenye meza moja karibu kabisa na mlango wa kutokea nje, alimuona Kamanda Amata akinyanyuka na wale vijana, alijua wapi wanaelekeakea kwani mazungumzo yao yote alikuwa akiyasikia kupitia earphone zake ndogo alizopachika sikioni zikiongozwa na kinasa sauti ambacho Kamanda Amata alikipachika kama moja ya kifungo cha shati, haikuwa rahisi kwa mtu wa kawaida kugundua hilo mara moja. Akawatazama walipokuwa wakija taratibu huku wakiongea akawaruhusu wapiti pale alipoketi na kuilekea ile Toyota Spacio.
Mara simu ya mmoja wapo ikaita, akaitoa mfukoni na kuitazama kiooni, private number, akaipokea na kuongeza na mtu wa upande wa pili.
“Yeah, nimewapa kazi mbona hamnijulishi kinachoendelea?” sauti ya mtu wa upande wa pili iliuliza.
“We ni nani, na kazi gani ulitupatia?” Yule kijana akauliza. Kamanda Amata alishajua nini kinaendelea katika majibizano hayo, akajiandaa kwa litakalofuata, huku Ndege akiwa bado ameketi kataika kiti kilekile alikuwa akiangalia nini kitaendelea.
Baada ya kuongeza na ile simu, akashusha mkono wake na kumgeukia Amata, akiwa mekunja sura kama mtu aliekula pilipili pa si kutarajia, alifyatua ngumi kumuelekea Amata, lakini akamkosa kwa kuwa Amata aliepa kwa ustadi sana.
“Nini kijana mbona unarusha ngumi bila taarifa?” Amata aliuliza.
“Bastard! Unajifanya wewe ndo ulotupa kazi kumbe sio?” alilalama Yule jambazi.
“Kama si mimi kwa nini nimewalipa? Basi twendeni kwa huyo anayesema yeye ndo kawapa kazi, mtakuja kukamatwa na polisi bure,” Amata aliwaambia, wale jamaa wakabaki wamrchanganyikiwa hawajui lipi la kufanya, nani boss nani tajiri, wakatazamana, “Samahani Boss” mwingine aliyekuiwa kasimama pembeni akajibu. Kisha wakaingia kwenye gari pamoja na Amata, safari ikaanza.
Baada ya kukata mitaa kadhaa wakaliacha jiji la Nairobi na kuchukua barabara ya kuelekea Kisumu mpaka njia panda ya Kinangop, wakapita Soko mjinga na kusonga mbele kama kilomita tano hivi, wakachepuka na kuingia kushoto barabara ya vumbi mwendo mfupi wakasimama, “Aisee, mmemzika mbali hivi?” Amata aliuliza, “Ah boss, umesahau kama ulituagiza tumlete huku,” akajibu mmoja wao.
“Ah, nshasahau aisee,!” Amata alijibu baada ya kujigundua kuwa amejisahau. Wakafika eneo lile walilomfukia Rose, Amata alinyamaza kimya mara wakasikia majani yakitaikisika na mtu mmoja akaibuka kama ninja.
“Hapo hapo mlipo, mikono juu,” Yule mtu aliamuru. Hawakuwa na ujanja walikubaliana na hilo wote wakaweka mikono yao juu.
“Tunawatafuita sana wauaji kama ninyi, fukua hapo!” aliamuru Yule mtu, kamanda Amata akiwa mikono yake iko hewani alijua wazi kila kinachoendelea, akatulia kimya, wale vijana wakaonekana jinsi wanavyotetemeka. Mara taa za gari zikamulika upande ule zikimaanisha kuna gari ambayo ilikuwa inakuja pale walipo. Polisi watatu waliteremka wakiwa na pingu mkononi mwao, wakawafunga wote pamoja na Kamanda Amata, kasha wakawapakia katika Land cruiser yao wakawapakia, Yule aliyewakamata kwanza akavua soksi aliyoivaa kichwani na kuruhusu sura yake kuonekana, Melchior Ndege alikuwa kasimama mbele yao.
“Fukua hapa,” Ndege akawaamuru vijana waliokuja na gari ya polisi, wakafanya hivyo na kuukuta mwili wa mwanamke kwenye mfuko mkubwa wa plastiki, ‘Ukatili gani huu,’ Ndege alijiuliza kichwani mwake.
§§§§§
Wambugu, alibaki kujiuliza maswali mengi, vijana aliowapa kazi walikuwa hawajarudi kumpa taarifa, alipowapigia akagundua wazi kuwa hakuna uelewano kati yao. Aliendelea kuketi pale kitandani akijiuliza la kufanya, tayari alikwishajua kuwa kuna mchezo umechezwa kati yake na vijana wake. Akinuka na kulisogelea dirisha, moyo wake haukuwa na amani hata kidogo, aliona siku zinavyozidi kwenda ndivyo hali inavyozidi kuwa mbaya, alihaha, sasa alibaini wazi kuwa Bill alikuwa msaliti mbaya kuliko msaliti wa kawaida. Akachukua rimoti na kuwasha tv, habari ya saa mbili usiku ilikuwa ipo katikati lakini alibaki mdomo wazi kwa habari aliyokuwa anaiona mbele yake, habari ya kukamatwa kwa jamabazi sugu la kike lililowasumbua polisi kwa miaka mingi, Mellina.
Wambugu hakuamini anachokiona mbele yake, ‘Mellina katika mkono wa dola’ alijiwazia akiwa kasimama huku kajishika kiuno, ‘bass hapa usalama hakuna tena usalama,’ akazidi kugubikwa na mawazo. Wambugu akaamua kutoroka maana alijuwa wazi kuwa endapo Mellina atabanwa vya kutosha lazima atataja, alifunga kibegi chake harakaharaka akaweka kila anachoona kinafaa katika kibegi chake akakiweka mgongoni, bastola yake akaipachika kiunoni na ikafunikwa kwa jacket alilokuwa amelivaa, akauacha mlango na kutoka nje ya gesti hiyo a,liyopanga na kutokomea mtaani.
Gari moja nyeupe ilisimama kando mwa gest hiyo, kijana mmoja shababi, akashuka na kuiendea kaunta ya nyumba hiyo, “Mwenyeji wangu yuko chumba namba saba,” alimwambia Yule mhudumu pale kaunta.
“Chumba namba saba leo hakina mtu, tayari ame-check out,” Yule dada alijibu.
“Amecheck out? Lini?” Kamanda Amata akauliza.
“Yaani hata masaa mawili hayajaisha,” Yule dada akamueleza, Amata alipita kwenye korido mpaka katika kile chumba na kumkuta mtu wa usafi akifanya kazi yake. Akarudi kaunta, hana la kusema, akarudi kwenye gari. “Vipi?” Ndege akamuuliza.
“Jamaa kaondoka, hayupo hapa, tena wanasema kuwa ni kama masaa mawili yaliyopita” Amata na Ndege walikuwa hawana la kufanya.
“Ningempata huyu mshenzi leo, ndo angenipa uelekeo wa Bill yuko wapi!” Kamanda Amata alimwambia Ndege.
“Usikate tamaa braza, tutampata ndani ya masaa ishirini na nne, mimi ndiyo ninayoijua Nairobi na Kenya yangu,” Ndege alijibu huku akigeuza gari na kutrudi mjini.
“MADAM S, Kamanda Amata yupo Nairobi, kwa habari tulizozipata kutoka kwa watu wetu huko,” Chiba alimwambia Madam. Madam S alitikisa kichwa kutokana na kujua hilo kwa kuwa tangu muda mrefu alihisi kwa vyovyote atakuwa huko.
“Vizuri sana Chiba, sasa mpelekee taarifa mwambie namhitaji haraka sana ofisini.” Madam S alitoa amri.
Ilikuwa ni usiku ambao Madam S alibanwa na kazi nyingi, akikumbuka kikao chake cha machana na watu wengine wa idara ya usalama wa taifa alihisi jambo jipya hasa kutokana na kutoroka kwa Amata hospitali na kwenda kusikojulikana.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi