MAUAJI YA KASISI (25)

Zephiline F Ezekiel

SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO
ILIPOISHIA...
Alipofika tu pale hospitali alikutana na Bwana Shikuku, kila mmoja alimkumbuka mwenzie, waksalimiana kwa bashasha kwa kuwa ni miaka mingi hawajaonana. Baada ya hapo wote wawili wakaelekea ndani ya hospitali hiyo kumuona Ndege aliyekuwa amelala usingizi.

JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈

ENDELEA...
“Kwa nini usimrudishe Nairobi kwa matibabu?” Madam S akauliza.

“Amesema hatotoka hapa mpaka amuone Kamanda Amata,” Shikuku alijibu.

“Ok, wameivana hawa. Ulikuwa unajua kama AmaTa yuko hapa?” madam S aliuliza tena.

“Ndio kwanza nafahamu sasa kuwa yuko hapa siku nzote sikuwa najua,” Shikuku alidanganya, wakati Ndege alishamwambia kuwa kamanda Amata yupo Nairobi kwa shughuli hiyo ila si kiofisi.

Madam S alitulia kimya akitafakari jambo Fulani, alionekana wazi kukosa raha usiku huo, aliitazama saa yake ilikuwa tayari ni saa kumi alfajiri.

§§§§§

Kamanda Amata alikunja kona kali kuingia ile barabara ambayo ile pikipiki iliingia, alipoenda kama mwendo wa mita mia hivi hakuiona ile pikipiki wala dalili zake, akajua kwa vyovyote huyu jamaa atakuwa mitaa, akasimamisha gari na kushuka bastola yake mkononi, akawa anashangaa akitafuta huku na kule akizungukazunguka kwa hadhari kubwa sana, alipokuwa tayari kukata tama alisikia mnguruno wa pikipiki kwenye vichaka, akawahi na kuiona ikitokomea porini, akainu bastola yake na kufyatua risasi ya kwanza haikua na shabaha ila ya pili alipiga tairi na kulitoa upepo, ile pikipiki ikaanguka, na Wambugu akawa chini, Kamanda Amata akafika eneo lile na kumkuta Wambugu amekwishasimama na amejiandaa kwa mapigano, Kamanda Amata alitaka kufyatua risasi lakini akakuta zimemuishia, aliirusha ile bastola kumpiga nayo Wambugu, Wambugu aliruka hewani kama ninja na kuipiga tik tak ile bastola ikapotelea kwenye vichaka, wakati huo tayari Amata alifika pale kabla hajajiweka sawa, mguu wa nguvu ulimshukia Amata begani, akayumba upande na Wambugu akasimama kwa mguu mmoja kisha akaushusha ule mwingine taratibu kwa madaha,

“Siku zote mnajua kuwa kila mtu ni bwege, kama ulikuwa hujui basi mimi ni Sempai,” Wambugu alijisifu huku akisimama katika pozi la kungfu, Kamanda Amata akaona hapo ndo penyewe, “Huwa sijibishani na wahalifu kabla sijawafundisha adabu,” Kamanda Amata alizungumza kwa gadhabu, akaruka hewani kiufundi na kuimshia mapigo makali Wambugu, lakini mapigo yote aliyapangua vizuri sana, kisha akaanza yeye kupeleka mashambulizi ya mikono kwa Kamanda Amata, ambaye naye alikuwa akiyapangua kiufundi sana mpaka Wambugu akamaliza mapigo yote, Kamanda Amata alipomuona sasa hana ujanja mwingine ndipo alipombadilishia staili kutoka kungfu kwenda kick boxing.

Teke la kwanza lilitua mbavuni kabla hajakaa sawa lapili likatu shingoni kisha zikafuata ngumi mfululiozo kama ishirini na tano zilizomuacha Wambugu hoi akigalagala, “Nyanyuka juu Sempai, upambane na mwanaume wa shoka, hayo mapigo niliyokupa niliagizwa na Melchior Ndege sasa naanza ya kwangu,” Kamanda Amata alipomaliza maneno hayo, alijivuta kwa hatua ndefu amgfikie Wambugu, lo, Wambugu akamzidi ujanja, alijirusha kutoka pale alipolala akasimama kisha akajibinua na miguu yake yote miwili ikatua tumboni mwa Amata na kumfanya ateme damu, hasira za Amata zikawaka ghafla, aligeuka nyuma kwa kasi na kumchota ngwala Wambugu lakini jamaa akaruka na ule mguu ukapita chini kisha Wambugu akashusha pigo moja la karate lililotua sawia kwenya shingo ya Amata na kumpeleka chini mzima mzima. Kamanda Amata alitambaa kama motto, damu zikimvuja puani na mdomoni, akaona wazi asipofanya makeke anaweza akazimishwa na watu wasiione maiti yake.

“Ha ha ha ha Tanzania Secret Agency namba 1 ndio wewe!!? Unatambaa kama motto, nyanyuka upambane na jabali la chuma linalotisha kama kifo, Kenya yote wananijua na hapa kila goti linapigwa,” Wambugu akasema hayo kwa kujitamba akijipigapiga kifuani. Maneno hayo yalimuuma sana Amata, akanyanyuka kwa kasi na kugeuka akitazamana na Wambugu ambaye mkononi mwake alikuwa ameokota gongo, akaliinu na kumpiga nalo Kamanda lakini Kamanda akalidaka kwa mkono mmoja, akatazamana na macho mabaya ya Wambugu.

Taswira za mauaji ya kikatili ya kahaba Rose ikamjia na kumtia hasira, taswira ya Ndege akiungua moto ikamjia na kumuongezea hasira, kauli ya kushushwa cheo ikamaliza kila kitu akilini mwake.

Kamanda Amata akiwa kalishika lile gongo kwa mkono mmoja alinyanyua mguu wake na kulikanyaga kwa juu akalivunja kwa mtindo huo kisha akabaki na kipande, kwa hasira na visasi akamchoma nacho Wambugu tumboni, yowe la uchungu lilimtoka akaanguka chini, Amata akamuendea palepale alipo na kumvua kibegi chake kisha akakivaa yeye mgongoni, akamnyang’anya simu yake na kuitia mfukoni kisha akamkamata ukosi wa jacket lake na kumburuza mpaka kwenye kibarabara, akampigiza sura yake chini kwa nguvu, “Bill yuko wapi?” akamuuliza kabla hajajibu akampigiza tena kwa nguvu na kuvunja mfupa wa pua. “Sasa ukiniua ndio ntasema?” Wambugu alijibu kwa uchungu. “Nambie haraka, Bill yuko wapi?” Kamanda aliuliza kwa kelele maana hasira ilikuwa bado imetawala kichwa chake. Wambugu alinyanyua uso wake na kutema mabonge ya damu,

“Kuna binadamu ambao hamtakiwi kuzaliwa kabisa, kama wewe na Bill, nakuuliza mara ya mwisho kabla sijakutenganisha na roho yako, Bill yuko wapi?” Kamanda aliendelea kuhoji,

“Mi si si si sssjui,” Wambugu alijibu kwa tabu sana. Kamanda Amata akamburuza mpaka aliposimamisha gari na kumuinua akamsimamisha wima akimuegemezea katika bodi la gari. “Wambugu! Nakuua,” Amata alimwambia,

“Niue braza, kwa maana ukiniacha hai nitateseka sana na mkono wa sheria,” Wambugu akajibu.

“Niambie Bill yuko wapi?” akauliza tena,

“Braza utanitesa utaniua lakini mimi sijui Bill yuko wapi alishatoroka hapa muda mrefu,” kamanda Amata alishikwa na hasira akampiga kichwa kimoja maridadi na kumuachia akianguka chini kama mzigo.

Mara taa za gari mbili zikawamulika kutoka barabara kuu, na zile gari zikaja mpaka pale, walikuwa ni polisi, wakateremka haraka na kumuweka Kamanda Amata chini ya ulinzi. Kamanda Amata akanyosha mikono juu, wale polisi wakaja na kumtia pingu, nyuma yao akaja mtu mnene kiasi aliyeonekana kuwa na sura ya kikatili isiyo na chembe ya huruma, akamuendea Kamanda Amata, akamtazama usoni, juu mpaka chini,

“Hey, askari!” akaita,

“Mfungue pingu Kamanda, mpe na begi lake,” wale askari wakafanya hivyo, kamanda Amata akapokea lile begin a kulitupia mgongoni.

“Mzima au amekufa?” Yule bwana akamuuliza Kamanda. “Mzima huyo hawezi kufa kirahisi,” Amata akajibu. Yule bwana akatoa amri ya kupakiwa Wambugu garini kisha yeye na Kamanda Amata wakaingia katika gari ndogo ya polisi na kurudi mjini.

“Kamanda Amata, umetusaidia kazi moja ngumu sana ambayo jeshi la polisi la Kenya na vyombo vingine vya usalama imetusumbua kwa miaka takribani kumi kumpata huyu mtu, asante sana kijana” akamshukuru Kamanda na safari ikaendelea mpaka kituo cha polisi cha Embu.

Madam S na Mashaka walikuwa hapo kituoni pia wakimsubiri Kamanda Amata, walimuona alipokuwa akishuka katika ile gari na waziwazi alikuwa ameumia sana kwa jinsi alivyokuwa akitembea, wakakutana uso kwa uso na Amata, wakatazamana. “Madam, kijana wako huyo wapo, sisi hatuna deni nae!” alisema Yule bwana mwenye mwili mnene, kisha akapita kwenda ndani ya kituo hicho, ijapokuwa ilikuwa alfajiri lakini watu walijazana kutaka kuhakikisha kama kweli jambazi sugu Wambugu limekamatwa, jambazi lililowanyima usingizi Wakenya wengi kwa miaka mingi.

Kamanda Amata, Madam S na Mashaka waliingia kwenye gari yao na kuondopka eneo lile, moja kwa moja mpaka hospitali ya Agha Khan ili kwanza apate huduma ya kwanza. Ndani ya nusu saa alikuwa tayari amefanyiwa check up ya nguvu na kutibiwa palipohusika, Mashaka akamuendea Amata katika chumba alichokuwapo kisha akamkabidhi begi jeusi mpano wa briefcase, alkipofungua ndani akakuta suti mpya, saa ya kisasa kwa kazi yake na bastola ndogo.

“Umerudi katika hali yako Kamanda,” Madam S alimwambia walipokutana mara tu Kamanda alipotoka kule ndani, “Yeah, lakini bado kitu kimoja,” kamanda alisema, “Nini?”

“Nataka kumuona Ndege,” akajibu. Wote watatu wakaingia wodini alikolazwa Ndege na kumkuta tayari amewekwa katika kitanda cha magurudumu, amefungwa mikanda sawia na chupa ya majiiliyowekwa baada ya ile ya damu ikiendelea kwenda, “Melchior Ndege,” Kamanda alimwita huku akwa amemuinamia pale kitandani, “Amekufa au amekimbia?” Ndege aliuliza kwa shauku, “Hali yake ilivyo hawezi kuiona jioni, yuko katika mikono ya polisi,” Amata alimwambia Ndege ambaye alionekana wazi kuifurahia habari hiyo. “Asante Kamanda,” Ndege alishukuru, “Asante na wewe” Kamanda akamalizia.

§§§§§

Kama kuna habari iliyomfurahisha Sargeant Maria, basi ni hii ya kupatikana kwa Wambugu, kwa sababu baada ya kumbana sana Mellina kwa kipigo na mateso makali alitaja washirika wote akiwamo Wambugu. Sargeant Maria na wenzake waliishiwa nguvu kusikia kuwa Wambugu anahusika na mauaji ya Kasisi, swali lilikuwa, tutampataje? Lakini ghafla alfajiri hiyo wanaambiwa kuwa Wambugu kapatikana huko Embu karibu na msitu wa Njukiri baada ya vyombo vya usalama kupambana nae vilivyo, baada ya kutaka kujua zaidi ndipo Sargeant Maria aliposikia juu ya Kamanda Amata ambaye yeye siku zote alijua ni mtu wa kwenye riwaya tu, hakujua kuwa ni burudani ya waandishi kuandika visa vyake kila amalizapo kimoja na kuanza kingine. Ulikuwa ni ushindi mkubwa, mkubwa sana, Maria alijiuliza, Mellina tumemkamata, Cheetah, kauawa, Wambui kauawa, Wambugu ndio huyu hapa, sasa ile Mostrance ambayo ndicho chanzi cha kazi nzima haijapatikana, bado kuna kazi mbele.

8

SIKU MOJA BAADAE - DAR ES SALAAM

KAMANDA AMATA na Madam S walikuwa wakitembea kwenye korido ya jengo la ukumbi wa jiji, wakiwa wanatoka kupata kahawa katika kamgahawa kadogo ndani ya ukumbi huo, walikuwa wakizungumza mawili matatu, wakibadilishana mawazo ya hili na lile.

“Sasa Kamanda, kama uliovyoambiwa, umeshuswa cheo na umebadilishiwa idara, idara gani mi na wewe hatujui, lakini nataka uniambie jambo moja tu, baada ya kumkamata Wambugu, umepata chochote juu ya jasusi Bill Van Getgand?” Madam S akauliza. Wakasimama na kugeukiana, “Yeah, Bill yupo German, alishaondoka kitambo sana, na habari hizi nimezifanyia uchunguzi wa kina sana kutoka katika tafutishi zangu kupitia simu na maelezo ya Wambugu,” Kamanda Amata akajibu.

“Ok, Una akili sana Kamanda, siwezi kupata mtu kama wewe tena katika ofisi yangu. Sikiliza, baadae nitakupigia simu tuonane.” Baada ya mazungumzo machache kati yao waliagana na kuondoka kila mtu na hamsini zake.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi

Chapisha Maoni