
Mtunzi: Richard Mwambe
SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
“Usijali, maadam tumepata tunachotaka basi,” Don Andreas akamtia nguvu kwa maneno hayo.
“Hii mali yetu kaka, aliwekeza baba wa babu yetu, alikuwa na makusudi mazima juu yake,” Andreas aliendelea kuongea huku akiigeuzageuza ile monstrance mikononi mwake,
JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
ENDELEA...
“Pure Gold!” alitamka maneno hayo huku akiibusu. Akairudisha katika begi lake na kuketi tena kochini. “Ndio Bwana Bill, kazi yangu mi na wewe imekwisha, au kuna linguine la kuniambia? Maana malipo yako tayari yapo benki haijapungua hata senti moja nyekundu,” Andreas alimwambia Bill. Tabasamu pana likamjia Bill usoni, likachanua kama ua la yugiyugi, akainua glass yake na kugonga cheers na Andreas, wakati glass hizo zikagongana simu ya Bill ikaita kwa fujo katika mfuko wake wa shati, akaitoa na kukutana na ujumbe mfupi wa maandishi,
“…Wambugu amekufa mikononi mwa polisi, kazi ya Kamanda Amata,”
Meseji hiyo ilimshtua sana Bill. “Vipi? Mbona unashtuka?” Andreas akauliza. Bill akashusha glass yake na kuiweka mezani. “Mmoja wa vijana wangu ambaye nilimpanga wa mwisho kufa, ameuawa,” Bill alijibu.
“Sasa wewe kinakushtua nyingi, si ndio amekufa!” Andreas akamwambia.
“Tatizo sio kufa, ila nani kamuua” Bill akamwambia Andreas.
Andreas akatikisa kichwa kuashiria kuwa amemuelewa Bill, “Ok, nani amemuua?” akauliza.
“Amekufa mikononi mwa polisi, na ni kazi ya Kamanda Amata, Jasusi la kiafrika kutoka Tanzania, TSA,” Bill akajibu.
“Unasema! Africa kuna majasusi? Tangu lini? Tena Tanzania?” Andreas alionekana kushangazwa na taarifa hiyo.
“Don Andreas, hata kama ASfrica hakuna majasusi, lakini huyu Amata ni zaidi ya Jasusi,” Bill alieleza huku mikono yake ikiwa kiunoni.
“Acha uwoga wewe, wao wapo Africa wewe upo Ulaya, waache wauane tu, hiyo ndiyo sera yetu mataifa makubwa, tunawachonganisha wanauana sisi tunakula maisha,” Andreas akajibu huku akijimiminia kinywaji chake kama kawaida lakini Bill hali haikuwa sawa kama mwanzo, Lijitupa kochini na kuweka mikono yake huku na huko kisha akashusha pumzi ya kina.
“Andreas, ili tuwe na amani katika hili lazima Amata auawe kwa njia yoyote ile,” Bill aliongea kwa jazba.
“Kama wewe umesema kuwa ni mtu hatari basi fanya kazi ili asiharibu mambo yetu, nakuaminia wewe ni jasusi wa KGB hata kama uliwasaliti na kuwakimbia,” Andreas alimwambia Bill huku akimpigapiga mgongoni.
Bill Van Getgand aliingiwa ganzi mwili mzima baada ya kusikia Wambugu kafia katika mikono ya polisi na ni kazi ya Kamanda Amata, hiyo ilikuwa ni salamu tu ambayo alijikuta anashindwa kuijibu. Alikumbuka sumu kali aliyompatia akijua kwa vyovyote asingeamka kwa muda mfupi kama ule, japokuwa hakusikia habari za kifo chake redioni, bado Bill aliamini kabisa kuwa Kamanda Amata mpaka dakika hiyo ni marehemu. Ukimya uliendelea akitafakari jinsi gani swahiba wake Wambugu atakuwa ametoa siri za mpango wao na labda hatari kubwa itakuwa ikiwanyemelea.
Bia iligoma kupita kooni, akili yake bado ilikuwa inazunguka huku na huko akifikiri la kuifanya, alipopata jibu akainua glass yake na kujitupia kinywaji kama kawaida, huku laptop yake ndogo ikiwa mezani tayari kwa kazi Fulani. Aliifungua na kutaka kuingia mtandaoni, Bill nalikuwa na uwezo wa kuingia mtandao wowote anaoutaka kwa kutumia nywila za bandia ambazo huzibuni kiufundi sana yeye mwenyewe na kufungua faili au mtandao wowote anaoutaka ili kujipatia taarifa kwa ajili ya mambo yake ya kijasusi, aliingiza nyila zake ili kuifungua kompyuta hiyo, ilipofunguka kioo chote kilikuwa cha blue, “Shiit!!!” akang’aka, akajaribu tena, hali ilikuwa ileile, akabaki mdomo wazi, kijasho chembamba kikamtiririka kutoka kwapani mpaka maeneo ya kiuno, Bill alihangaika kutumia njia zake zote lakini hakufanikiwa.
Ilikuwa ni kazi ya kijana Frank Masai aliyekuwa akishirikiana na Chiba katika kuunda kirusi kibaya kabisa maalumu kwa kuiua kompyuta ya Bill kusudi asiweze kuingia katika mtandao wa siri za usalama wa Taifa la Tanzania, walifanikiwa, Bill Van Getgand alibaki teee, hana la kufanya, “Wameniweza,” akajisemea kwa sauti ya chini. Bill alikurupuka kitini na kumuaga Andreas kuwa atarudi jioni ya siku ya hiyo, alitoka nje ya hekalu hilo la kifahari na kuingia kwenye gari yake aina ya Jaguar na kuondoka zake. Akiwa na mawazo mengi kichwani alielekea moja kwa moja katika hotel aliyofikia ili akajaribu mbinu nyingine kupata taarifa za watu mbalimbali na mienendo yao kwa siku hiyo.
Saa 10:30 jioni
QATAR AIRWAYS ilikanyaga ardhi ya Ujerumani jioni hiyo ikiwa tayari imemaliza safari yake iliyoanzia Doha na kupita miji kadhaa kabla ya kufika Berlin. Katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Schonefeld, watu walikuwa wengi wakija kuwapokea na kuwalaki ndugu zao waliokuwa wakitoka pande mbalimbali za dunia kuja ama kusalimia jamaa au ndio wanarudi nyumbani, ilimradi tu maisha ya binadamu ni ya kuhamahama. Miongoni mwa waliokuja kupokea ndugu zao alionekana mtu mmoja mwenye ndevu nyingi, aliyevaa vazi la kikasisi lililomkaa sawia, kanzu ndefu nyeusi na kofia kubwa ya rangi hiyo hiyo, alisimama karibu na nguzo Fulani akiwa hana papara ya lolote, alionekana kumfahamu vyema Yule anayekuja kumpokea na si vinginevyo.
Baada ya Kamanda Amata kukamilisha itifaki za uhamiaji ambapo aliingia Ujerumani kama mwandishi wa habari, aliiweka kamera yake vizuri kifuani mwake, kizibao cha khaki kilichomkaa vyema na jeans yake nyeusi, vilimuonesha wazi kuwa ni mwanahabari halisi, usoni mwake aliipachika miwani safi nyeusi, miwani ambayo inaweza kuvuta vitu vya mbele pindi unapojitikisa kichwa kichwa chako, miwani hiyo ina uwezo wa kukuonesha vitu vya nyuma yako kwa kutumia vioo vidogo vilivyowekwa kwenye miimo yake, ina uwezo wa kurekodi picha mjongeo na sauti kwa wakati mmoja. Mkononi mwake alivaa saa kubwa ya kisasa ‘Casio’ yenye uwezo wa kutuma na kupokea fax fupi, inayoweza kukata chuma chenye ugumu wowote kwa kutumia miali mikali ya laser CO2 iliyowekwa ndani yake, kiatu chake cha mpira kisichoathirika kwa mafuta yoyote wala kuungua kwa moto kirahisi kilikuwa mguuni mwake.
Taratibu alitoka katika mlango wa kutokea wasafiri, akiangaza huku na huko na kwa kufanya hivyo miwani yake iliweza kumsogezea watu wote karibu na kuweza kuwachambua kwa harakaharaka, kwa mbali alimuona Yule kasisi aliyekuwa kwenye kiti cha chuma akiwa anasubiri mgeni wake, Kamanda Amata akasita kidogo, mara mkono wake ukafinywa na kitu kama sindano ndogo sana, akainua saa yake na kuiangalia, ilikuwa ikiwaka taa ndogo sana nykundu katikati ya mishale yake, akabofya kitu Fulani na ikaonesha maandishi katika kioo, ‘A priest’ yaani ikimaanisha Kasisi. Hakusita alimuendea kasisi huyo na wakakutana uso kwa uso kila mmoja akimwangalia mwenzake kwa umakini wa hali ya juu.
“Karibu Berlin,” Yule Kasisi alimkaribisha Kamanda wakakumbatiana kusalimiana kisha lile sanduku lake likachukuliwa na Yule Kasisi nay eye akafuata kwa nyuma, muda wote alikuwa akitembea huku akitazama kila amuonaye kuona kama kuna hatari yoyote. Moja kwa moja wakaiendea gari moja ya kisasa sana VolksWagen (VW) modeli mpya wakaingia na kuketi ndani yake.
“Naitwa Fr Frank, raia wa Austria, nafanya kazi katika kanisa kuu la Achen,” alijitambulisha Yule Kasisi, Kamanda Amata akatikisa kichwa kuashiri kuwa ameelewa alichoambiwa.
“Yeah, kamanda Amata,” kisha wakacheka pamoja na kugonganisha viganja vya mikono yao. Kwa jinsi walivyokuwa wakipanga waliona haitakuwa vyema Kamanda asishukie moja kwa moja Aachen, ila ashukie Berlin kisha aende Aachen kwa usafiri wa gari, hii ilikuwa ni mbinu ya kuwapoteza malengo kama wapo wanaomsubiri. Mazungumzo yaliendelea kati ya wawili hao huku wakijaribu kupanga mkakati wa kumaliza kazi yao.
“Kilichonileta Fr Frank, sio Bill tu, ila nahitaji kuipata ile Monstrance pia,” Kamanda Amata alimwambia yule Kasisi.
“Unajua, Bill baada ya kumchunguza sana, nimegundua kuwa anafanya kazi na tajiri mmoja anaitwa Andreas Schurmann au ‘Don’ kama wengi walivyozoea kumwita, na mimi tangu nimekuja hapa najua kwa vyovyote vile monstrance ile ipo kwake,” Fr Frank alimueleza Kamanda Amata, “Andreas anafanya nini zaidi?” Kamanda kauliza.
“Yeye ni mfanyabiashara mkubwa, ana viwanda na mahoteli makubwa, nyumba tu anayoishi inaizidi ikulu ya Ujerumani,” Fr Frank alimjibu Kamanda.
“Safi nahitaji kuiona nyumba yake na ikiwezekana pia kujua baadhi ya makampuni yake ili nijue nafanya nini,” kamanda Amata alieleza. “Ila ni kibarua kigumu sana Kamanda, “Yule jamaa ana ulinzi kama Rais wa nchi” Fr Frank aliendelea kumueleza Kamanda hali halisi ya kitu alichokuja kukifuata. Kamanda Amata alijaribu kuangalia uzito na kubwa wa kazi yenyewe.
Masaa matano yaliwatosha kufika mji wa Achen ulio kilomita 538.8 kutoka Berlin, kamanda Amata alitulia tuli kama maji ya mtungini, akiwa amechoka na safari kwa namna moja au nyingine. Saa tatu usiku, walifika katika kanisa kuu la Aachen ‘Aachener Dom’ kama linavyoitwa. “Utakaa hapa na sisi, pana usalama zaidi kuliko hotelini, katika mahotel, huku kwenye nchi zetu, huwa wanatoa siri za wageni wanaofika kwa watu wa usalama na wengine kwa wenye nia mbaya. Usijali Kamanda, hapa pako sawa na hii oda tumepewa kutoka kwa watu wako wa ubalozi,” Fr Frank akiwa katika kusema hayo alikuwa tayari akiegesha gari katika maegesho ya ndani ya jengo kubwa kabisa lililojengwa kiustadi nyuma ya kanisa hilo. Hakuwa na la kusema, zaidi ya kufuata kila anachoambiwa.
Mhudumu aliyepokea mizigo ya Amata alimkaribisha katika chumba maalum kilichokuwa ghorofa ya tatu upande wa kaskazini wa kanisa hilo kubwa. Alikikagua kwa jinsi anavyojua yeye lakini hakuona chochote kilichowekwa kwa nia mbaya kwa ajili yake, aliliendea dirisha dogo lililokuwa hapo, akavuta pazia na kuangalia nje huku akiwa amezima taa ya ndani, hakuna kitu alichokiona zaidi ya jengo kubwa umbali kama wa kilomita moja hivi, likipendezeshwa kwa taa nyingi na nzuri. Akiwa bado akiliangalia jengo hilo mlango ukafunguliwa na Fr Frank akaingia, sasa akiwa katika mavazi ya kawaida kabisa, lakini cha kushangaza hakuwa na ndevu tena, “Kamanda Amata, hilo jengo unaloliangalia ndio jumba la Don Andreas,” Fr Frank alimwambia Kamanda Amata, “Nimekupa chumba hiki kwa makusudi mazima ili uweze kuliona jumba hilo, sasa sisi tunakuacha ratiba zako utapanga wewe, kama utahitaji msaada kutoka kwetu basi usisite kunijulisha,” Fr Frank akondoka zake.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi