MAUAJI YA KASISI (28)

Zephiline F Ezekiel

SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE
ILIPOISHIA...
Kamanda Amata, hilo jengo unaloliangalia ndio jumba la Don Andreas,” Fr Frank alimwambia Kamanda Amata, “Nimekupa chumba hiki kwa makusudi mazima ili uweze kuliona jumba hilo, sasa sisi tunakuacha ratiba zako utapanga wewe, kama utahitaji msaada kutoka kwetu basi usisite kunijulisha,” Fr Frank akondoka zake.

JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈

ENDELEA...
Kamanda Amata alifunga vifaa vyake ikiwemo camera kubwa moja na darubini yenye nguvu kabisa ambayo inaweza kuona umbali wa kilomita kadhaa pia yenye madini ya kukuwezesha kukuonesha gizani, akaiweka pale dirishani pamoja na kamera ndogo ambayo ingeweza kupata picha nzuri za mnato na mjongeo kupitia darubini hiyo. Alipohakikisha vyote viko sawa, alijaribu kuangalia kwa kupitia darubini ile, aliweza kuona walinzi waliokuwa wakizunguka huku na kule wakiwa na mambwa mwakubwa ya kutisha, ndani ya jumba hilo hakukuwa na chochote kinachoendelea, inaonekana ama watu walikuwa wamelala au walikuwa mahali pengine, lakini yeye alikuwa akifanya majaribio tu, hivyo hakujali kama wapo au la.

§§§§§

BILL VAN GETGAND alikuwa mezani akijaribu kuangalia mtandao huu na ule, alipitia mitandao yote ya mashirika ya ndege zinazoingia na zilizoingia siku tatu nyuma lakini hakuona dalili ya mtu anayemuhisi kufika au kuja. Akafanya mawasiliano na watu wake katika mahoteli lakini haikuonekana kabisa kama kuna mtu kutoka upande anaoufikiria. Bill hata kama alihakikishiwa usalama kuwa hakuna anayemdhania kuwepo nchini humo, bado moyo wake ulihangaika maana alijua wazi kuwa Kamanda Amat anweza kuharibu mambo yote na anaweza kuingia Ujerumani hata kwa kuogelea endapo anabaini kuwa anawindwa.

Usingizi haukua na nafasi kwake siku hiyo, alijaribu kuwapanga vijana wake jinsi anavyoweza ili kuhakikisha anapata habari juu ya ujio anaoutarajia. Bill bila kujua kinachoendelea alifumbua macho na kukuta jua tamu linalopenya katika dirisha lake likimmulika usoni, akajiziba macho kwa kiganja chake cha mkono, hakuelewa saa ngapi alilala ila alijua tu muda ailoamka. Aliketi kitandani alipokumbuka juu ya Kamanda Amata moyo wake ulianza kumuenda mbio na akakosa raha.

Katika maisha ya Bill, maisha yake ya kazi yake ya kijasusi tangu akiwa KGB kule Urusi hakuna siku aliishi kwa hofu kama siku hii ambayo alimuhofia sana Kamanda Amata. Japokuwa alishapambana na majabari katika kazi yake, majitu yenye mbinu na uafanisi mkubwa katika mauaji ya kila aina lakini kwa Kamanda Amata alikuwa anajikuta hana kitu, hasa akifikiria jinsi alivyomuwekea sumu na amepona, kwake aliona Amata anatisha zaidi ya kifo. Alijaribu kutuliza mawazo na alipoona yuko sawa, alitoka katika nyumba yake na kuliendea gari lake aina ya Mercedes Benz na kutokomea mjini. Huku akiwa amejiimarisha kwa kila hali siku hiyo maana alijua lolote linaweza kutokea kwa kuwa alama zake za hatari zilikwishamuonesha hilo. Safari hiyo ilikuwa ni katika moja ya makampuni ya Adreas kama walivyopatana jana yake.

AKIWA ndani ya kanzu nyeusi ya kikasisi huku kichwani akiwa na kofia yake nyeusi aina ya barret, Kamanda Amata alikuwa akitembea tembea katika uwanja wa kanisa hilo kubwa kabisa katika mji huo wa Aachen. Kila aliyemuona alimsalimi kwa lugha ya Kijerumani ambayo alikuwa akiifahamu vema. Alipohakikisha ameyachoka mazingira hayo, akaliendea gari moja jeusi lililokuwa limeegeshwa hapo pembeni kwenye maegesho ya magari.

Akaingia na kuketi nyuma ya usukani, ilikuwa ni Land Rover County short Chassis, aliiwasha na kuitoa taratibu katika maegesho yake, kishs akaliendea geti kubwa na kufuata ujia mrefu uliokuwa ukiiendea barabara kubwa ya kuelekea katikati ya mji, Kamanda Amata aliendesha gari hiyo kwa mwendo wa wastani akielekea njia ile ambayo ilikuwa ikipita katika jumba la bwana Andreas. Njiani gari nyingi zilimpita nay eye akazipita zingine ilimradi kufanya barabara ipendeze. Baada ya mwendo kama wa dakika kumi hivi aliichepuka na kukunja kushoto kisha akaingia kama shimoni na kupita uvunguni mwa hiyo barabara akatoke upande wa pili. ‘AACHEN COMMONWEALTH GRAVE YARD’ (Uwanja wa makaburi ya jumuia ya madola ya Aachen), lilikuwa ni bango kubwa la kijani lililoandikwa kwa maandishi meupe likionesha mshale kuelekea upande wa kushoto, Kamanda Amata akawasha indiketa kueleka upande huo, akapinda na kulielekea geti kubwa upande huo, ambalo lilifunguka lenyewe bila kufunguliwa na mtu.

Akaingiza gari na kushuka, mkononi akiwa na ua moja zuri na kitabu kidogo cha sala. Moja kwa moja akaliendea moja ya makaburi lililokuwa nyuma ya yote, kaburi hilo lilionekana kuwa ni la siku hizi tu kwa uwanja ule ulikuwa umeungana na uwanja wa kuzikia mapadre, akaenda na kulifikia lile kaburi akasimama na kuinua uso wake, mbele yake aliliona jumba kubwa la Don Andreas likiwa limetulia kabisa. Akainama na kuweka lile ua juu ya kaburi hilo, akatulia kimya akiwa amezama katika sala lakini muda wote akiwa analiangalia lile jumba, kwa kutumia miwani yake aliweza kupiga picha kadhaa lile jumba huku akingalia jinsi ulinzi mkali ulivyo, askari waliokaa juu kaabisa ya jengo walionekana kwa uzuri wakiwa na bunduki zao za kawaida tu wakiimarisha doria. Alipohakikisha ameridhika na utafiti wake, aliinuka na kulielekea gari lake, mara akasimama ghafla, baada ya kukuta watu wawili waliosimama katika gari yake mmoja upande huu na mwingine upande ule. Kamanda Amata aliwatazama harakaharaka watu wale waliovaalia suti nyeusi wakiwa na vipara vichwani mwao, kila mmoja alionekana kutafuna jojo ikiwa ni moja ya kupambana na baridi ya mji huo.

Kamanda Amata akaendelea kuifuata gari yake, hakutaka wajue kama ameshtuka kuwaona pale, akafika na kuwasalimu, lakini hakuna aliyejibu, akauendea mlango wa gari yake na kutaka kuufungua, Yule jamaa akamshika mkono kumzuia asiufungue ule mlango, kamanda Amata aligeuka na kumtazama, “Mnataka nini?” aliwauliza kwa lugha ya Kijerumani isiyo na kovu lolote, “Tunakutaka wewe!” mmoja alijibu, wakati huo Yule mwingine alikuwa akizunguka kuja upande ule, alipomfikia Amata akamshika ukosi wa kanzu yake na kumvutia upande ule wa pili alikokuwa wakati huo Yule mwingine alikuwa ameingia katika usukani akisubiri mateka wao apandishwe garini. Kamanda Amata alikuwa mpole kupita maelezo, alipofikisha kwenye mlango wa upande wa pili ndipo alipowaonesha kuwa yeye ni nani, liwiko kilichotua katika kidevu cha yule jamaa kiliangusha jino moja, kabla hajakaa sawa alimpa konde la kwanza na la pili ambayo yalimpeleka chini.

Yule wa ndani akaona mwenzake anazidiwa, akachomoa bastola aanze mashsmbulizi, akachelewa, Kamanda Amata hakuwepo mahali pale, alikuwa ametoweka kama mzuka, akiwa katika kushangaa hilo aliguswa mgongoni na Kamanda ambaye alikuwa nyuma yake upande ambao hakutarajia, alipogeuka alikutana na konde moja lililoshiba kisawasawa ambalo lilimpotezea mtandao kwa sekunde kadhaa, alivutwa chini na Amata na kupewa kichapo cha mbwa mwizi ambacho kilimuacha hoi, akamshika mkono wake huku akimshikisha bastola ileile akamgeukia yule mwingine aliyekuwa akijivutavua pale chini, kwa kupitia uvungu wa gari, alivyatua risasi moja ilifumua vyema goti lake kisha akamgeuzia huyu aliyekuwa naye na kumfanya kitu kilekile. “Mpeni ujumbe Bill, mwambieni kifo chake kimekuja mlangoni mwake,” Kamanda Amata aliwaambia kwa lugha ya Kijerumani na kuingia kwenya gari yake na kutokomea. Yule mwenye bastola akaona asipoteze nafasi, akacheza na bastola yake kulenga tairi la gari ya Amata lakini alishangaa vyuma vikigongana tu, alipotazama ile bastola haiukua na magazine, alibaki kuduwaa maana hakujua ni wakati gani imeondolewa.

Kamanda Amata aliendesha gari kwa kasi sana mara hii kuelekea misheni alikofikia, aliingia getini na kukuta misa ya maazishi ikiendelea, akaegesha gari na kuteremka harakaharaka, akauendea mlango mkubwa na kupanda kuelekea katika chumba chake, akafika na kujifungia chumbani, akaenda katika ule mtambo wake alioufunga pale dirishani na kuanza kuchunguza nyumba ile, hakujua ni jinsi gani wamejua kama yupo katika mji huo au wameotea kwa kuwa yeye ni mweusi. ‘Mara hii sipotezi nafasi,’ alijiwazia, akchungulia vyema kupitia ile darubini yake, akaangalia vizuri jumba lile tena kwa dirisha moja baada ya jingine, alipofika dirisha la ghorofa ya pili ndipo aliweka tuo kuangalia kinachoendelea. Hakuweza kusikia lakini aliweza kuona matendo ya watu wawili waliokuwa wakibishana kitu, alijaribu kuziangalia sura zao lakini hakufanikiwa kuzipata, akageuza darubini yake na kuangalia upande mwingine wa jengo lile.

Gari moja nyeusi aina ya BMW ya kisasa kabisa ilikuwa ikiegeshwa polepole kabisa mbele ya jumba lile huku ikifuatwa na gari nyingine mbili za mtindo ule. Mtu mmoja mnene, aliyevalia nadhifu kabisa alishuka ngazi akifuatwa na wanadada wawili na vijana wengine wawili waliokuwa kwenye suti nadhifu. Kamanda Amata aliendelea kuwachunguza na kuwaona wakiwa kamili na vyombo vya mawasiliano masikioni mwao, wote wakaingia katika magari na kisha ule msafara ukaondoka, na kuchukua barabara kuu kuelkea upande wa pili wa mji. Kamanda Amata akashusha pumzi, lengo lake yeye ajue kama Bill huwa anapatikana katika jumba lile au la. Alichomoa memorycard kutoka katika ile darubini akaipachika katika kompyuta yake kisha akatuma zile picha kwa Chiba Tanzania, acheki kama zina lolote. ‘Nimuueje Bill?’ alijiuliza, ‘Uso kwa uso au nimdungue kwa mbali?’ bado alikuwa akishindana na nafsi yake katika kuamua juu ya hilo, ‘Kumdungua ni kumuogopa, nitapambana nae,’ alikata shauri.

§§§§§

BILL hakuamini anchosikia kutoka kwa mmoja wafuasi wake, kuwa Kamanda Amata yupo Aachen na tayari ameshawajeruhi vibaya walinzi wa nje wa Andreas waliokuwa wakimfuatilia kule makaburini. “Nani aliwaambia yule mtu anafuatwa namna hiyo mliyofanya nyie?” Bill aliwauliza wale vibaraka wake. Baada ya kumaliza mazungumzo yake na watu wake, hakuna kilichokuja akilini mwake zaidi ya kukimbia mji huo na kujificha sehemu nyingine, ‘Lakini nitaonekana nimemuogopa, nitapambana nae hapahapa. Bill alitoka mchana huo na kuelekea mjini ambako baada ya pitapita zake akaingia katika kanisa kuu la mji huo, akiwa sasa medhamiria na ameamua kumsaka Amata kwa njia yoyote ile.

Alikuta watoto wakicheza cheza katika ngazi za kanisa hilo, mara mbele yake gari oja ilikuwa ikija pale aliposimama, Bill akaisimamisha, alikuwa ni Fr Frank, akitoka kwenda mjini kutafuta mahitaji, Bill aliiendea ile gari na kufungua mlango akaingia na kuketi kiti cha pembeni bastola mkononi,

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi

Chapisha Maoni