
Mtunzi: Richard Mwambe
SEHEMU YA THELATHINI NA TANO
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
kwa mbele akaona kuna pacha ya bomba hilo ikiungana na bomba linguine ambalo nalo lilikuwa likileta maji kuunga na hili nkisha kuelekea yanakokwenda, Frank alipoifikia ile pacha akasikia kelele ya mtu anayekimbia katika maji, akatul.ia kusibri aone mtu huyo ni nani.
§§§§§
KAMANDA Amata alipoona kuwa lile lango la kwenda chini alikoingia Bill limejifunga,
JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈
ENDELEA...
akachoka ghafla, akatazama huku na kule, alichokiona akajua tu ni switchi ya mlango huo, akaelekea pale ukutani hakuwa na akaminya namba ya siri ambayo kuna jinsi unavyoipanga inaweza kufungua kila aina ya mlango, akaingiza tarakimu hizo kumi na mbili na alama Fulani kwa mpangilio maalumu, akabonyeza ok, akadaiwa kuweka alama ya kidole gumba, akajua tu lazima ni kidole cha Andreas kinachohatajika, alimtazama akiwa pale chini amelala hana uhai.
“Ndiyo shida ya dhukuma, ukidhulumu utadhulumiwa” akaongea mwenyewe huku akiuendea ule mwili, akachukua kipande cha kioo kizito kilichovunjika hapo, akakata kidole gumba cha Andreas na kwenda kukipachika pale kwenye ile sense, taa ya kijani ikawaka, ule mlango ukafunguka, haraka akauendea, alipotazama mezani akagundua kuwa Bill ameisahau ile fimbo yake Amata akaitazama na kuichukua, alipoigeuza geuza akagundua kuwa haikuwa fimbo ya kawaida, akaingia nnayo na ule mlango ukajifunga, alimweza kumuona Bill kwa mbali akiendelea kwenda, “Billlllllll…..” aliita, lakini Bill hakusimama. Baada ya kumfuata kama dakika moja na nusu hivi, akamuona Bill akisimama na kugeuka alikotoka, akiwa na begi lake mkononi. Bill hakuwa na ujanja, alikuwa katikati, huku Frank Edson FBI huku Kamanda Amata TSA.
“Bill, huna ujanja, mwisho wako umefika,” ilikuwa sauti ya Fr Frank. Amata aliiskia akajua kuwa ni Frank anaye ongea lakini bado alikuwa hajamuona kutokezea. Bill alibaki pale katikati akihema. Mara Frank akatokezea na kugongana macho na Kamanda Amata. “Kamanda Amata, niachie Bill niondoke naye, asante sana kwa kazi kubwa uliyoifanya ya kunirahisishia kumpata Bill Van Getgand, asante sana, huyu inabidi afike hai pale Washington,” Fr Frank alimwambia Kamanda Amata.
“Sikia Frank, unajua kuwa ulikwishakufa wewe? Kwa nini husemi asante kwa kukurudishia uhai wako? Sasa sikiliza Bill utamchukua akiwa hai wala usijali cha muhimu ni kutafuta njia nya kutoka humu ndani, na njia hiyo lazima yeye Bill atuoneshe,” Kamanda Amata akamwambia Frank, Frank akamsogelea Bill na kumnyang’anya lile begi, Bill hakuwa na ubishi, Frank akamrushia begi Amata, nae akalidaka. “Haya, njia ya kutoka humu ndani iko wapi?” akamuuliza Bill, alipoona ukimya wake unazidi, akaamua kutumia nguvu, alimshika Bill kwenye ukosei wa shati na kumbamiza kwenye kingo za bomba hilo mara kadhaa, Bill alikuwa akitokwa na damu nyingi katika paji lake la uso.
“Frank! Mbona huna huruma wakati wewe ni mchungaji wa kanisa?” Kamanda aliuliza, “Kwa taarifa yako, ukimfanya hivyo hatofika hai Washington, nifuate njia ipo huku,” akaongeza, kisha akatangulia na Frank akamfuata na Bill akiwa katikati mikono akiwa ameshika kichwani. Walikwenda mpaka kwenye ule mlango, akaufungua na wakatoka wote, wakaingia kwenye chumba kile cha siri, kisha wakaelekea katika lile sebule kubwa, Frank alishangaa kulikuta lile jitu lililomtia adabu likiwa marehemu, Frank moyoni mwake alikiri kuwa Kamanda ni kiboko kama amelizimisha jitu hatari kama lile. Jumba la Andreas lilikuwa kimya ni polisi tu waliokuja kutoka mjini walikuwa huku na kule wakifanya upekuzi wa hapa na pale.
“Weka mikono juu!” ilikuwa sauti ya polisi mmoja wa kike akimuamuru kamanda Amata. Amata akanyanyua mikono juu ile fimbo aliyoichukua pale mezani ikaanguka chini, na Yule poilisi akamuamuru mwenza aichukue. Mara Bill akatokea na nyuma akiwamo Fr Frank Edson.
“Frank Edson FBI,” akaonesha na kitambulisho, wale polisi wakaja kumchukua Bill na kumtia pingu. “Na huyu?” waliuliza juu ya Kamanda Amata, “Muacheni aende zake, ni mwenzetu kutoka shirika la upelelezi Tanzania,” Yule askari akamwita na kumuongoza kuelekea kwenye gari ya polisi. Nje ya jumba la Andreas kulitanda gari za polisi zikiwaka vimulimuli vilivyong’aza eneo lote hilo, Kamanda Amata akatazama saa yake, ilikuwa ni saa kumi na mbili alfajiri. Polisi walikuwa wakikusanya miili na kufanya upekuzi wa hali ya juu katika jumba hilo ambalo siku na miaka yote waliliona ni jumba la mtu mwema.
Mlio wa Helkopta ulisikika ukikaribia eneo hilo, Frank akamtazama Amata, “Kamanda, Bill anaondoka moja kwa moja USA, uje muagane tafadhali,” Fran alimwambia Amata kwa nyodo. Kamanda Amata akavuta hatua na kufika pale aliposimama Bill huku nyuma yake akiwa ameshikwa na polisi wawili wa kijerumani na Frank alikuwa alikuwa nyuma yao.
Bill na Amata wakawa uso kwa uso, “Bill nilikwambia siku yetu inakuja, na ndiyo leo, nitautwaa uhai wako kwan kisasi cha Fr Gichuru, Kahaba Rose na wengine wote uliowapotezea maisha yao pa sin a hatia. Nakuapia, hautakanyaga gereza la Guantanamo wala wapi sijui,” kamanda Amata aliongea kwa sauti ya chini ni Bill aliyekuwa akisikia na wale polisi wawili, Frank alikuwa akiongea na redio aliyopewa na mmoja makamanda waliokuja na kikosi hicho.
Bill alimtazama Kamanda Amata, akamtemea mate usoni, Kamanda Amata akamkazia macho Bill, “Sintoyafuta mate haya mpaka nihakikishe umekufa na haupo katika dunia hii, kifo chako ulikinunua mwenyewe kwa gharama kubwa sana,” Bill aliposikia maneno hayo aliikumbuka ile fimbo yake na akaitazama ikiwa nikononi mwa Amata, kisha Kamanda akageuka na kuondoka kueleka upande ambao gari za polisi zilegeshwa, waandishi wa habari kama kawaida yao, walichukua picha huku na huku na kutafuta majibu ya maswali yao. Dakika chache helkopta kubwa likakanyaga ardhi yenye nyasi safi na kutulia tuli, wanajeshi wane waliovalia sare ya jeshi yenye nembo ya bendera ya Marekani walishuka na kumchukua Bill tayari kuondoka nae, itifaki za kuondoka na mtuhumiwa huyo zilifanywa haraka sana na pande mbili za mataifa hayo rafiki. Kamanda Amata alikuwa kasimama upande wa pili wa gari moja ya bpolisi akiwa kaegemeza tumbo lake kwenye ubavu wa gari hiyo, begi lake kalitupia ndani ya gari na ile fimbo ya Bill kaiweka juu ya gari, akiangalia kila kinachoendelea.
Aliishika ile fimbo na kuwa kama mtu anayeichunguza pale juu ya gari, bahati ilioje alipogundua kuwa ile haikuwa fimbo bali ni silaha mbaya sana yenye risasi za mtindo wa msumari, silaha ya Kirusi iliyotumiwa sana na wanazi wa KGB ambamo Bill alikuwa mmoja wao nyakati hizo, aliitazama haraka na kuikuta bado nina risasi tatu, akaiweka vizuri juu ya gari na kulenga shabaha, hakuna aliyemwangalia wala kugundua hila yake. Mguu wa Bill ulikuwa ukikanyaga ngazi ya helkopta hiyo huku akisukumiwa ndani na wale wanajeshi, Fr Frank alikuwa akifuata nyuma, lo, mara walishuhudia Bill akijishika kifua, mara kichwa, akalegea na kuanguka chini, tafrani ikazuka, walipomwangalia tayari alikuwa marehemu, lakini hakuonekana tundu lolote la risasi.
Kamanda Amata aliingia kwenye gari mara tu baada ya kumaliza azma yake, alikuwa akisubiri Bill akanyage japo ngazi ya helkopta hiyo, naye palepale akafyatua bunduki hiyo ya siri, bunduki ya kijasusi, akamtoa uhai Bill Van Getgand.
Fr Frank Edson akawaacha wale wanajeshi wakimhudumia Bill ambaye alikuwa tayari marehemu, akamjia Kamanda pale aliposimama, na kamanda akatoka pale alipo kumuendea Frank, akampa mkono, lakini Frank hakuupokea mkono huo.
“Kamanda Amata, umefanya nini sasa?” Frank aliuliza.
“tatizo nini, wewe ulimtaka akiwa hai sivyo, si umemshika akiwa hai, na mimi nilishakwambia serikali ya Dodoma inataka roho yake tu basi. Asante sana Frank, umeifanya kazi yangu kuimaliza kwa wepesi kuliko nilivyofikiria,” kisha Kamanda Amata akageuka na kuingia kwenye gari iliyokuwa imekwishawashwa tayari, Frank alibaki kumtazama hakuwa na la kufanya, aliitazama ile gari ikitoka getini na kutokomea mjini huku na zingine zikiendelea kutoka moja baada ya nyingine.
DAR ES SALAAM
Saa 09:30 usiku
SIMU YA kitandani mwa Madam S iliunguruma kwa fujo usiku huo, alishtuka na kukunja sura kama kawaida yake kwani alikuwa hapendi sana kukatishwa usingizi. Aliinyakua simu hiyo na kuiweka sikioni.
“Madam S!” ilikuwa suti ya Chiba.
“Ee Chiba, niambie, mbona usiku sana,” Madam S aliuliza.
“Fungua, televisheni yako, Deustche Welle,” akamwambia na ile simu ikakatika. Madam S akaiwahi rimoti haraka na kuwasha luninga yake kubwa iliyofungwa ukutani katika chumba chake cha kulala. Habari ya dharula aliyoikuta kwenye kioo hicho ilimfurahisha kuliko habari zote alizowahi kuzisikia. Ilikuwa ni habari ya moja kwa moja iliyobebwa na maadishi ‘Breaking News’ ilikuwa ikieleza juu ya kukamatwa kwa jasusi lililoisumbua dunia, lakini hata hivyo ikasemekana limejiua kabla halijapakiwa katika helkopta tayari kupelekwa Marekani. Habari hiyo ilikuwa ikisifia shirika la nkipelelezi la Marekani kwa kufanikiwa kulinasa jasusi hilo. Akiwa katika kutazama habari hiyo, fax yake ya mezani karibu na kitanda ikaanza kutoa mlio kama wa mdudu, kijikaratsi chepesi kilikuwa kikitoka na maadishi. Akaiendea na kuisoma fax hiyo.
“…kazi uliyonituma nimeimaliza, Bill Van Getgand amekshaisalimisha roho yake... TSA 1” Madam S alijua kuwa ujumbe huo umetoka kwa Kamanda Amata, akatabasamu, akazima luninga yake na kurudi kitandani.
HATIMA
KAMANDA Amata alikuwa kwenye kititanda cha wagonjwa katika kliniki binafsi ndani ya mji huo wa Aachen, akigangwa majeraha na maumivu mengine. Huku akijisomea magazeti nya siku hiyo akipata habari za tukio lililotukia usiku wa siku hiyo na kusoma habari nyingi za kweli na za uongo.
“Kamanda, Sindano!” alishtuliwa na sauti laini ya kike, kamanda Amata akamwangalia Yule muuguzi wa kizungu aliyekuwa na chano yake yenye kila kitu kwa ajili ya tiba hiyo. Kiukweli pamoja na ujasiri wote, kamanda Amata kwenye swala la sindano alisalimu amri, aliogopa sana kitu hicho tangu utoto. Alitamani kulia alivumilia mpaka shughuli hiyo ilipokamilika.
“Asante dada mzuri, hata sikujua kama umenichoma sindano,”Amata alimchokoza muuguzi. “Kwa nini?” Yule muuguzi akauliza. “Kwa jinsi ulivyo na mikono laini, na upendo unaomfanya mgonjwa asihisi hata kama anapasuliwa nini kuchomwa sindano!” Amata aliongea kwa lugha ya uchokozi, “Hallo,” Kamanda aliita tena wakati Yule muuguzi alipokuwa akitoka mle chumbani, “Nini? Unahitaji sindano nyingine?” akauliza huku akirudishia mlango na kurudi kwa Amata, Kamanda Amata akampa ishara ya kuwa asogee amwambie kitu, Yule muuguzi akasoge kumsikiliza, Kamanda akamshika kwa mikono yake kichwani pande za masikio, akamvutia kwake, hakukuwa na ubishi, akambusu na ndimi zao zikabadilishana mawazo.
Baada ya dakika kama mbili za mchezo huo ambao uliwafanya wote wasahau majukumu na magonjwa yao, akamtoa na kumtazama usoni. Yule mwanadada alikuwa akihema kwa nguvu, pepo limechukua nafasi, akajichomoa kutoka kwenye mikono ya Kamanda, akavua viatu na kumpandia kitandani, shughuli mpya ikaamka, Kamanda Amata alipogundua kuwa pazia la dirisha liko wazi, akshika kimnyororo kidogo cha kazi hiyo na kukivuta, pazia likarudi mahala pake na kuwaficha wawili hao kati ulimwengu wa peke yao.
MWISHO
Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi