
Mtunzi: Richard Mwambe
SEHEMU YA TANO
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
“Fr, ni nini, nieleze nikusaidie” Fr Joe aliinuka kitini na kulmuendea Fr Gichuru huku akimueleza maneno hayo, alitoa kitambaa chake na kumfuta machozi. Fr Gichuru aliinuka kitini pamoja na Fr Joe wakatoka nje kwenye kabustani kadogo na kutembeatembea wakiwa na rozali zao mikononi.
JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
ENDELEA...
“Fr Joe! Nililala kama kawaida mara baada ya masifu ya jioni, katikati ya usiku huo niliota nipo Roma makao makuu ya kanisa, nipo juu kabisa ya mnara wa jengo hilo, niliangalia chini palikuwa parefu sana, isingekuwa rahisi hata kuruka, sikuwa na msaada, nililia na machozi yangu yalikuwa ni machozi ya damu, yalitirirka na kulowesha kanzu yangu nyeupe lakini hayakufika chini bali yote yalituama kifuani upande wa moyo wangu. Nilimuona Malaika kasimama mbele yangu mkononi kashika kikombe, akanisogelea akanipa kikombe hicho ambacho ndani yake kulikuwa na divai nyekundu lakini cha kushangaza mlikuwa na risasi ndani yake, akanambia
‘Kunywa’, nikasita akanambia kuwa ‘yakupasa unywe’, nilikiangalia kikombe kile, mwsho nilikitwaa na kunywa, nilipomaliza tu nilihisi kizunguzungu na kuanguka kutoka juu ya mnara ule kuelekea chini, lakini kabla sijafika chini nilishtuka kutoka usingizini.
Mara moja niliitafakari ile ndoto lakini sikupata maana yake, nikapiga magoti kusali, wakati nasali niakaanza kusikia kelele za mlango wa Sakristia ukifunguliwa, kelele zile zilikuwa kubwa mno hata kuyasumbua masikio yangu, nilinyanyuka na kuitwaa kanzu yangu kisha nikaja chumbani kwako nikakukuta umelala, nikakuacha na kwenda kungalia nini kinachotukia huko, lo! Fr Frederick alijishika kifuani na kukumbuka ahadi yake na yule jambazi ‘ibaki kuwa siri yetu’…”
“Oh Bill, aaaah, uuuuh” sauti ya kimahaba iliyoashiria kuwa viumbe hao wapo kwenye ulimwengu mwingine zilitawala chumba kimojawapo katika hotel kubwa inayojulikana kama Plazza Hotel iliyopo katikati ya jiji la Nairobi.
Bill, mtu mnene alikuwa kitandani akipewa raha na msichana wa Kikikuyu kutoka North Kinangop, binti huyo alihakikisha anampagawisha mzee huyo mpaka ammalize kabisa, na hivyo ndivyo ilivyokuwa, Bill alikuwa nyang’anyang’a kwa penzi alilopewa na msichana huyo aliyembeba usiku uliopita katika mtaa wa Koinange hapo hapo Nairobi kwa dau la kulipana dola za kimarekani, alimfurahia jinsi alivyomkatia kiuno kwa mitindo ya ajabu hata akafanywa kusahau adhma ya kumtaka msichana huyo kimapenzi.
Rosemary Wangui alihakikisha anamkamua Bill mtu mnene mpaka tone la mwisho akiwa na lengo moja tu la kuchota madola yake yaliyojaa katika mkoba maalumu wa ngozi.
Penzi la uongo na muda mfupi liliendelea katika kitanda cha hotel hiyo, hakuna aliyekiogopa kifo, baada ya kuona hawafaidi utamu wa maumbile yao ndipo walipokubaliana kutokutumia kinga ili kutiana hasara roho, hapo sasa ndipo mtu mnene alipoahidi donge nono kwa shughuli aliyopewa na msichana huyo aliahidi kufanya lolote kwa jinsi alivyopagawisha na mtu mnene, Bill.
“Rose, you are so sweet baby!” Bill alitamka maneno hayo huku akijifunga taulo kuelekea maliwato.
“Same to you my cock” Rose alimsindikiza Bill kwa macho wakati akielekea maliwatoni huku moyo wake ukimuenda mbio kwa kuuona ule mkoba wa Bill ulioshiba manoti. Dakika chache baadae Bill alitoka maliwato na kuketi juu ya kitanda na kuruhusu minyama ya mwili wake kutikisika kwa jinsi alivyojitupa hapo.
“Rose!” Bill aliita
“Yes, Sir!” Rose aliitika kwa adabu ya uongo.
“Unauona ule mkoba wenye pesa?” Bill alimtupia swali Rose
“Yeah nauona, vipi?”
“Nitakupa ule mkoba kama ulivyo, na pesa yake ndani” Bill alizungumza hayo na kumwangalia Rose usoni, Rose hakuamini anayoyasikia kutoka mtu mnene, tabasamu pana lilichanua usoni mwa mrembo huyu, tabasamu la kuuaga umasikini, tabasamu la utajiri wa dharula.
“Sijaelewa darling” Rose alisema kuonesha kuwa hajaelewa aliloambiwa.
“Nini hujaelewa? Kwenye ule mkoba kuna dola za kimarekani nyingi tu, nahitaji kukupa wewe pamoja na mkoba wake kama ulivyo”. Rose alibaki kimya, kisha akafungua kinywa chake na kumwambia mtu mnene “Asante,” akamkumbatia na kukutanisha ndimi zao ambazo zilichukua muda kidogo kila moja kuonja ladha ya nyingine. Kisha Bill akamtoa Rose kinywani mwake.
“Sikia, hakuna ujira usiyo na kazi kwanza” Bill aliongea, akainua glass yake ya pombe ya kirusia ‘Pushkin’ akapiga funda moja na kumtupia jicho Rose aliyejilaza kitandani na kuegamia upande wa mbele wa kitanda hicho kwa kutumia mto wa kulalia.
“Nakusikiliza” Rose alimwambia Bill mtu mnene.
“Unamjua huyu?” Bill alimuuliza Rose na kumpa picha ndogo iliyoonekana kwenye kioo cha simu yake kubwa, Rose aliipokea na kuiangalia kwa makini sana kisha akatikisa kichwa kuashiria ameifahamu.
“Mmh! Namfahamu, kafanyaje?”
“Namtaka huyu mtu nizungumze nae kirefu, na wewe nataka unifanikishie hilo”
Rose alibaki midomo wazi, alimwangalia Bill mtu mnene hakummaliza
“Kivipi?” akauliza
“Nataka ufanye kila hila ya kike, umlete mahali halafu vijana wangu watawateka wote wawili ila wewe watakuacha nay eye tutamchukua kwa kuwa tuna shida naye” Bill alimueleza kinagaubaga, Rose alionesha woga sana katika hilo, alijifikiria kwa kina, pesa anazitamani, kulitekeleza hilo ni vigumu, ugomvi mkubwa kati ya nafsi yeke ulizuka haikuwa rahisi kwake kuuamua, alinyanyuaka kutoka pale kitandani alipokaa na kuvuta hatua chache kuelekea maliwato alipita mbele ya Bill akiwa mtupu kama alivyozaliwa, Bill alibaki hoi na kushuhudia jogoo lake likiinua taulo kuashiria network imerudi.
3
Sajent Maria na koplo Othorong’ong’o walibaki kutazamana hawakuwa na jibu sahihi juu ya mauaji yale, waliperuzi kwa pamoja faili lile walilokabidhiwa na Inspekta Simon Saitoti
“Kwa maelezo ya Fr Joe, yule paroko, nafikiri tuifanyie kazi hiyo taarifa tuliyopewa” koplo Othorong’ong’o alimueleza sajent Maria aliyekuwa ameketi kwenye benchi huku akiwa na redio call yake mkononi.
“Uko sahihi, lakini haya maelezo yangekuwa timilifu sana kama tungeonana na marehemu lakini haikuwa hivyo” sajenti Maria alionesha ugumu wa kazi ulipo.
“Sajenti, hivi tukifanya uchunguzi kwenye mitaa ya vibaka kama Kawangware kule hatuwezi kupata habari yoyote ya huyu Cheetah, ili tupate kwa kuanzia?” koplo Othorong’ong’o aliuliza.
“Unafikiri Cheetah kwa hadhi yake atakuwa anjificha kule ambako kila mara tunaenda kwa msako, kule wamejaa wahamiaji haramu koplo” sajenti Maria alimjibu koplo Othorong’ong’o, kisha kimya kifupi kikatawala.
“Nafikiri litakuwa jambo la busara sana tukijaribu njia hiyo, ila twende kiraia zaidi ili tuchangamane nao kisha tuweze kupata habari yoyote inayoweza kutuanzishia game hii.” Walikubaliana kuingia mtaa huo jioni ya siku hiyo kujichanganya ili kupata lolote la kuanzia katika kesi hiyo iliyoonekana kuwatoa kijasho kidogo.’
Walikubaliana kukutana baada ya muda kidogo wa mapumziko ambapo kila mmoja wao aliutumia kwa jinsi anavyojua yeye.
‘A Catholic priest murdered after returning from Rome’.
Kilikuwa ni kichwa cha habari kilichosomeka juu kabisa katika ukurasa wa mbele wa gazeti la Daily Nation la siku hiyo, mwandishi wa gazeti hilo alieleza kwa kina habari hiyo aliyoifanyia uchunguzi wa kutosha na wa kuridhisha. Sajenti Maria alilishusha gazeti lile lililokuwa limeuficha uso wake na kulitua magotini pake na kuruhusu wazo moja lipite kidogo kisha akaendelea tena kuisoma habari ile iliyomsisimua sana kama riwaya tamu za Richard Mwambe, alipojiridhisha na habari hiyo aliandika vitu fulani katika kijitabu chake cha kumbukumbu kisha akalifunga na kuingia ofisini kwake ambako alimkuta koplo Otho’ amesinzia kitini, akamshtua na kumueleza juu ya gazeti lile kwa jinsi lilivyoandika kwa kina juu ya habari.
“Sajenti, turudi kwa Fr Joe kwa mahojiano kidogo ili tujue kwa undani juu ya safari yake ya Roma na kama kulikuwa na uadui wowote na mtu,”
“Positive, koplo” Maria alijibu na mara moja wakaelekea katika kanisa kuu la Familia takatifu kwa kazi hiyo.
* * *
“Marehemu Fr Gichuru hakuwa na mazoea ya kuhifadhi kumbukumbu sehemu? Ama kwa maandishi au njia yoyote ile?” lilikuwa ni swali kutoka kwa koplo Otho’
“Yeah, alikuwa anaandika sana, daima alikuwa na diary yake” Fr Joe alijibu hukua akinyanyuka na kuingia kwenye chumba cha marehemu Fr Gichuru, kisha akarudi na diary ndogo mkononi mwake na kuiweka mezani, sajenti Maria aliichukua mikononi mwake
“Fr, samahani kwa kukusumbua mara kwa mara lakini nafikiri ndani ya diary hii tunaweza kupata chochote kitakachotusaidia, kama unaturuhusu tuondoke nayo ili kuendelea na upelelezi”
“Oh ninyi mpo kazini, usijali mama, nenda nayo ukimaliza kazi nayo uirejeshe kwa kumbukumbu hapa” Fr Joe aliwakabidhi ile diary na kuagana nao, akawasindikiza mpaka getini, walipokuwa wanaagana pale getini, mwanamke mmoja mnene lakini aliyeonekana ana mwili wa mazoezi akiwa kavalia sketi nyeusi, iliyobeba blauzi nyeupe na juu yake ikafunikwa na kijikoti cheusi, aliingia getini na kuwapita sajenti Maria na koplo Otho’ wakati wakiagana na Fr Joe. Jicho la sajenti Maria halikuondoka kwa yule dada aliyekuwa akitembea kwa mwendo wa wastani akielekea kanisani kulikokuwa kukiendelea na maombolezo. Baada ya maagano yale, sajenti Maria alirudi garini pamoja na koplo Otho’
“Koplo, umemuona yule dada aliyetupita pale?” Maria aliuliza
“Nimemuona, halafu sura yake si ngeni kichwani mwangu” koplo Otho’ alijibu na kuongezea. Sajenti Maria alitulia kwa nukta kadhaa, akavuta kijidroo cha dashboard ya gari na kutoa kamera ndogo ambayo unaivaa kama saa mkononi, akateremka garini.
“Nakuja koplo, Linda mkia wangu tafadhali” Maria alitamka hayo huku akiurudishia mlango wa gari ile na kurudi kule kanisani kwa kutumia njia ile aliyopita yule dada wakati huo akiivaa ile camera mkononi mwake. Ilikuwa ni hatua chache tu alimuona yule dada akiwa katikati ya watu akijipenyeza ili kupata eneo zuri la kumuezesha kujua kinachojir katika kanisa hilo ambalo lilijawa na waumini waliokuwa wakiomboleza kwa nyimbo na zaburi. Sajent Maria aliendelea kumuangalia kwa makini, alimuona akitoa simu yake na kuandika kitu kama ujumbe mfupi kisha kuirudisha kotini, na muda huohuo alijipenyeza tena kuelekea upande mwingine ndipo alipogongana kikumbo na sajenti Maria ambaye kwa uzoefu wake wa kazi ya kipolisi alikuwa tayari amekwisha mpekua kwa kumgusagusa.
“Dada, we vipi? Mbona unagonga watu ovyo, huoni njia?” yule dada aliuliza
“Samahani nilikuwa nasoma saa hata sikukuona, samahani sana”
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi