
SEHEMU YA THELATHINI NA NNE
ILIPOISHIA...
Kuepusha shari nikatoka kwenye kituo cha polisi na kuingia ndani ya gari na kumsubiria Sheila ambaye baada ya robo saa akatoka na kuingia ndani ya gari
“Wamesemaje?”
“Wametaka tuwalipe gharama za matibabu pamoja na gharama za vitu vilivyo haribika kwenye hoteli.Kumbe yule mzee ndio mmiliki wa hoteli na yule mwanaye alikuwa kama msimamizi pale”
NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
“Na wanataka kiasi gani cha pesa”
“Milioni moja na nusu”
“Waache upuuzi wao tuondoke watapewa na babu zao”
“Eddy”
“Tuondoke zetu wasilete uhuni yeye si amesema sisi hatuwezi kumlipa basi achana nao”
“Edd achana kuwa mbishi mume wangu wameniomba nije kujadiliana na wewe ili tujue tunawalipa nini?”
“Ahaa basi majadiliano yetu mimi na wewe ni kwamba hakuna swala la kuwalipa cha msingi tuondoke zetu kwanza ninahitaji tufike Dar leo hii kabla ya saa nne usiku na sasa hivi ni saa kumi na mbili jioni”
“Eddy nakuomba tuwalipe mume wangu tuepushane na shari dhidi yao kwani watu wenyewe wanaonekana hivi hivi ni washirikina”
“Funga mkanda wewe unaogopa wachawi?”
“Ehhhee”
“Na waturoge basi kama niwacawi kweli”
Nikawasha gari na kuondoka eneo la kituo cha polisi nakuendela na safari huku gari nikiizidisha mwendo na kumfanya Sheila kuwa na wasiwasi na mwendo ninao tembea nao kwani ninatembea na zaidi ya spidi 220 ambacho ni kiwango cha juu na gari za kawaida za Tanzania mwisho wa spidi yake ni 180.
“Eddy punguza mwendo basi”
“Ninaharaka mke wangu”
“Jamani baba angu haraka ya wapi wakati tunaekelekea nyumbani”
“Nataka niwahi kufika ili nipange safari ninahitaji kwenda Iraq”
“Eddy nimesikia vibaya au.....Unataka kwenda wapi?”
“Iraq ndipo mama alipo kamatwa na hapa ninataka kwenda kutoa taarifa kwenye wizara ya mama wajue wananisaidiaje”
“Mume wangu nitabaki na nini?”
“Si nitarudi kwani ninakwenda kufa huko na hapa breki ya kwanza ni nyumbani kwetu”
“Sawa mume wangu”
Tukafanikiwa kufika Dar es Salaam saa tano na robo usiku na moja kwa moja tukafikizia nyumbani na kupiga honi na akatoka askari huku akiwa ameishika bunduki yake kwa umakini na kuniomba nishuke kwenye gari kwani ninahisi hakujua kama ni mimi
“Eddy habari yako”
“Salama vipi kaka”
“Safi tuu nifungulie geti niingie”
“Siwezi kufanya hivyo kwani bosi ameniambia nisimruhusu mtu yoyote kuingia ndani”
“Bosi gani na wewe si unajua kuwa hapa ni kwetu sasa kwanini usiniruhusu?”
“Baba yako ndio amesema nisiruhusu mtu yoyote kuingia ndani kwani anawageni humo ndani”
“Amerudi lini?”
“Anasiku nne tangu arudi hapa”
“Na ha wageni ndio wamefungua mziki huo kwa sauti ya juu hivyo?”
“Ndio”
Nikashuka ndani ya gari kufungua geti dogo na kuingia ndani huku Sheila akinifwata kwanyuma kwa hatua za haraka,Nikaufungua mlango na kukuta wasichana nane wakiwa wamevalia chupi huku wawili wakiw uchi kabisa wakikatika mauono mbele ya baba ambaye anaonekana amelewa huku akipiga kelele za kufurahia
“BABA....BABA”
Baba akastuka na kuchukua rimoti ya redio na kuizima kisha akanyanyuka huku akiwa anayumba yumba na mkononi kwake akiwa ameshika chupa ya whyne na akaanza kupiga hatua za taratibbu kunifwata kwenye sehemu niliyo simama
“Baba ni nini unacho kifanya ina maana wewe hujui kitu kilicho mpata mama na unakula raha na hawa machangudoa zako?”
Nilizungumza kwa uchungu huku machozi yakianza kunilenga lenga
“Wee koma kwanza ni nani aliye kupa ruhusa ya kuingia humu ndani kwangu?”
“Kwahiyo kwenye nyumba hii mimi sina ruhusa ya kuingia?”
Nikastukia kibao kikali kikitua kwenye shavu langu na kunifanya niyumbe na Sheila akanisaidia kisimama wima nisianguke chini
“Huna mamlaka ya kuzungumza mbele yangu na kuanzia leo hii mama zako ni wale pale wanao cheza mbela yangu na mama yako kwanza hajui mapenzi kitandani.....Ni mzito hajui kukatika anakaa kama boga lililo ozeana”
Maneno ya baba yakazidi kunipandisha hasira na mbaya zaidi wasichana alio kuwa nao wakaanza kucheka kwa dharau huku wakinizomea na kuongea maneno ya kejeli.Baba akanitazama kwa macho yaliyo jaa pombe nyingi na kumfwata Sheila na akatazama kwa muda na kumfanya Sheila kuanza kutetemeka na gafla akamshika ziwa na kunifanya nishindwe kuvumilia.Nikamsukuma baba na akanguka chini na akanipiga teka la kustukiza na lililonifanya nianguke kama mzigo kisha akasimama na kuanza kuruka ruka kama wapiganaji wa kick boxre na kunifanyia kidole chake akiniomba ninyanyuke ili tupigane
“Eddy usifanye”
Sheila akanishika mkono na kuninyanyua na kunivuta kwa nyuma huku akinizuia nisipigane na baba
“Eddy twende zetu nyumbani”
“Wewe malaya unataka kumpeleka wapi mwanangu”
“Mimi sio mwanao na ninawapa hawa Malaya zako dakika mbili watoke humu ndani la sivyo nitawaua”
“Ohhh Eddy hii ni nyumba yangu na kuhusu mama yako hawezi kurudi ndani ya hii nyumba tena kwani tayari AMESHAKUFA”
Moyo ukaanza kuniuma baada ya kusikia mama kuwa amekufa,Sheila akanishika kiuno na tukafungua mlango na kutoka nje huku machozi yakinimwagika na chuki zidi ya baba ikazidi kunipanda kiasi kwamba nilatamani kurudi na kupiga naye ila Sheila akazidi kunionya nisifanye kitu cha namna hii
“KUANZIA LEO HII MAMA ZAKO NI WALE PALE WANAO CHEZA MBELA YANGU NA MAMA YAKO KWANZA HAJUI MAPENZI KITANDANI.....NI MZITO HAJUI KUKATIKA ANAKAA KAMA BOGA LILILO OZENA”
Maneno ya baba ya baba yakezidi kujirudia kichwani mwangu na kuzidi kunichanganya na kuanza kupanga mipango ya kumuua baba pale nitakapo pata nafasi,Sheila akaniingiza kwenya gari na akaingia upande wa dereva na tukaondoka katika eneno la nyumbani.Ndani ya dakika ishirini tukafika nyumbabi kwake na tukashuka kwenye gari akanifungulia mlango ni nakapitiliza mojakwa moja hadi ndani kwake na kujitupa kitandani na kumuacha akifunga miliango,Sikutegemea ata siku moja baba yangu atakuja kinidhalilisha mbele za watu mbaya zaidi ananizalilisha kuhusia na mama yangu kipenzi.Sheila hakunisesha chochote zaidi ya kuvua nguo zake na kupanda kitandani na kukaa pembeni na akaanza kunivua nguo moja baada ya nyingine na kubakiwa na boxr.Kutokana na hasira na kuchoka usingizi mzito ukanipitia na kulala fofo
***
“Eddy baby kumepambazuka amka ukanywe chai”
“Saa ngapi sasa hivi?”
“Saa tatu”
Sheila akaninyanyua kitandani na kunivalisha ndala na kuniingiza bafuni na kila kitu anachonifanyia Sheila sikuwahi kusanyiwa na mwanameke wa aina yoyote na taratibu nikajikuta upendo ukijijenga ndani ya moyo wangu na kujiapia kuto kumuacha Sheila.Nikamaliza kuoga na kwenda moja kwa moja mezani na tukaanza kunywa chai kwa pamoja huku akiendelea kunifariji
“Sheila yale ndio maisha ambayo nilikuwa nikukuambia kuhusiana na baba yangu.....Na sijui ni kwanini anamfanyia mama vile na kitu kingine ambacho kinaniumiza roho ni jinsi baba alivyotembea na mfanyakazi wa ndani na kumpa mimba tena juu ya kitanda wanacholala na mama”
“Mmmm pole mume wangu ila hapa ninahisi kuna kitu tu kinachoendelea kwenye hili swala zima la kutekwa kwa mama na ninavyo kumbuka baba yako alisema kuwa mama amefariki.......Ina maana anajua mama kuwa ametekwa”
Nikakaa kimya na kunyanyuka kwenye kiti na kuingia ndani na kuvaa nguo kwa haraka na huku Sheila akinitazama
“Baby unakwenda wapi?”
“Nakwenda kutoa taari juu ya sehemu aliyopo mama kama jana alibvyo niambia kwenye simu”
“Unaonaje tukaenda sisi wenyewe Iraq kwa maana hapa ninahisia mbaya kuhusiana na lilicho yokea kwa mama mkwe”
“Ila ngoja kwanza niende nikazungumze nao”
“Eddy nisikilize mimi ninakuomba twende pasipo kuzungumza na mtu wa aina yoyote kwa maana hili swala lina mikono ya watu wazito na si bure”
Wazo la Sheila nikalikubali na akaanza kuvaa nguo zake na kuchakua hati zake za kusafiria na ikatulazimu kwenda nyumbani kuchukua hati yangu ya kusafiria kwa maana nisingeweza kwenda sehemu yoyote pasipo hati hiyo.Tukakodi taksi hadi nyumbani kwetu nikamuomba dereva kusimamisha gari mbali kidogo na ilipo nyumba yetu na nikashuka na kutembea hatua chache hadi nyumbani na kugonga geti na akatoka askari
“Eddy umerudi tena mdogo wangu”
“Huyu pimbi yupo humo ndani?”
“Ametoka muda huu ameondoka na wale wadada wa jana usiku”
“Powa naningia ndani dakika kadhaa tuu nitatoka”
“Fanya fasta asije akakukuta”
Nikaingia ndani na moja kwa moja nikaingia ndani kwa mama na kufugua kwenye droo yake aliyo tengenezwa kwa chuma na kujengewa ukutani na nikaingiza namba za siri na ikafunguka na kukuta vitu maalumu ambavyo ni vya siri sana pamoja na pesa ya kutosha,Nikachukua hati yangu ya kusafiria pamoja na pesa zote zipatazo dola za kimarekani laki moja na nusu ni sawa na milioni 24 za Kitanzania na kuziweka kwenye begi la mgongoni na kabla sijakifunga ndipo nikaona katatasi zilizo ambatanishwa kwa pamoja zipatazo tano huku zikiwa na maandishi makubwa na nikaanza kuzisoma haraka haraka na kukuta ni maelezo ya mama
“MIMI GRACE J.MAPUNDA NINAANDIKA NIKIWA NA AKILI ZANGU TIMAMU PASIPO KUSHAURIWA NA MTU WA AINA YOYOTE.MALI ZOTE AMBAZO NINAZIMILIKI NI ZA MWANAGU EDDY GODWIN PALE ITAKAPOTOKEA NIMEFARIKI YEYE NDIO ATAKUWA MSIMAMIZI NA MMILIKI MKUU WA MALI ZOTE AMBAZO NI
1.NYUMBA NINAYOISHI YENYE DHAMANI YA SHILINGI BILIONI 1.5 ZA KITANZANIA PAMOJA NA NYUMBA ZANGU TANO ZA KIFAHARI ZINAZOPATIKANA ARUSHA ZIPO MBILI,MWANZA MOJA NA TANGA MOJA”
2.MADUKA NANE.HOTEL MBILI ZILIZOPO AFRIKA KUSINI NA VITEGA UCHUMI VILIVYOPO UINGEREZA NA MAREKANI IKIWEMO HISA ASILIMI 35 ZILIZOPO KWENYE KAMPUNI YA UTENGENEZAJI WA MAGARI NCHINI MAREKANI”
3.GARI 8 ZA KIFAHARI”
Sikutaka kuzisoma aina za magari ambayo mama ameyaorodhesha kwa maana ninayafahamu yote na kuachana na mambo mengi ambayo mama ameyaandika na nikajikuta nikistushwa na maneno yaliyopo karatasi ya mwisho
“MUME WANGU ASIHUSISHWE KWENYE CHOCHOTE KILICHO ANDIKWA KWENYE HUU WOSIA WANGU KWA MAANA HAJAHUSIKA KATIKA KUPANDA NILIVYO NAVYO NA SI BABA HALISI WA EDDY”
Nikahisi nguvu zikiniishia na swala zima la nani ni baba yangu liakaanza kunijia kichwani na nikazitoa karatasi zote zilizopo ndani ya kisanduku maalumu cha mama na nikafungua droo zake na kutoa cheni na pete zake za dhahabu na vitu vyenye dhamani na kuviingiza ndani ya begi na kabla sijatoka ndani kwake nikakumbuka kubeba albamu yenye picha zake na zangu kisha nikaridhika nafsini mwangu na kuufungua mlango na kutoka kabla sijashuka kwenye ngazi nikasikia mlango ukifunguliwa na nikaisikia sauti ya baba ikizungumza na watu wa wili nikachangulia nikawaona watu wawili wakiwa wamevalia nguo za jeshi huku wakiwa wameshika nyundo na sururu mikononi mwao
“Nimeshindwa kufungua kijidro kilichopo ukutani na huyu mwanamke amebadilisha namba za siri”
“Kipo wapi mkuu tukushuhulikie?”
“Kipo huku juu twendeni mukaking’oe”
Nikaingia jikoni na kujibanza kwenye mlango na wakapita bila kuniona na kuingia chumbani kwa mama na nikatoka na kushuka kwenye ngazi kwa haraka na kutoka nje na kuanza kukumbia na kabla sijafika getini nikaisikia sauti ya baba
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com