SORRY MADAM (38)

Zephiline F Ezekiel
SEHEMU YA THELATHINI NA NANE
ILIPOISHIA...
Nilizungumza na Sheila akanielezea kisa kizima na alidai kuwa ameonewa kwa maana tangu siku ambayo wewe ulipelekwa katika chumba cha kufanyiwa oparsheni ndio siku ya yeye alipo kamatwa na polisi kwanza akashikiliwa kwa kosa la kutaka kumuua mkuu wa jeshi ila kutoka na ushaidi kutoka kwa manesi na madaktari ukamsaidia sana Sheila kuishinda kesi ya kumjerehi baba yako ambaye alitaka kukuua hadharani”

NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU

SASA ENDELEA...
“Ina maana baba yangu yupo hai?”
“Ndio yupo hai na nimiongoni mwa watu walio nipa vitishi endapo nitaendelea kulifwatilia hili swala.......”
“Mama yangu je yupo hai?”
“Mama nilipata habari kuwa amelazwa nchini Afrika kusini kwani alipata ugonjwa wa mstuko wa moyo na hadi sasa hivi sijajua anaendeleaje”

Nikashusha pumzi nyingi huku nikijaribau kusubiria ni nini kilitokea katika maisha yangu ila sikupata pichaya aina yoyote
“Ishu ilikuwa hivi.......Alitengenezwa mtu anaye fanana na Sheila na kwakupitia picha rada zilizopo hospitali alionekana akitoka kwenye chumba ulichokuwa umelazwa huku akiwa ameshika sindano mkononi na kwamadai ya madaktari wakasema kuwa msichana huyo ndio amehusika kwa kukuchoma sindano ya sumu iliyo pelekea maisha yako kuwa mwisho”
“Ngoja kwanza unataka kuniambia kuwa Sheila yeye hakuuhusika na chochote?”
“Ndio Sheila hajausika na kiyu cha aina yoyote juu ya kukuchoma sindaono kwa maana kipindi tukio la wewe kuchomwa sindano linatokea Sheila alikuwa mikononi mwa polisi na hadi sasa hivi ninavyo zungumza Sheila ndio huyo siku zake zina hesabika”
“Huyo daktari aliye dhibisha kuwa nimechomwa sindano ya sumu ni yupi huyo?”
“Ngoja nikuonyeshe”

John akatoa simu yake na kuwela upende wa video na nikamuona daktari wa familia akiwa anazungumza kwa masikitiko makubwa na mbele ya waandishi wa habari na kunifanya nibaki mdomo wazi
“Sasa huyu mzee ndio mbaya wenu katika hii familia?”
“Kwa nini?”
“Yeye ndio chanzo kikubwa cha baba yako na mama yako katika kugombana?”
“Wewe umejuaje?”
“Mimi nilimuhoji siku akiwa amelewa sana kwa maana huyu mzee ni mjomba wangu na akanieleza vitu vingi sana juu ya familia yako”

“Vitu gani?”
“Kwanza yeye ndie aliye muambia baba yako kuwa wewe sio mtoto wake wa kumzaa na kitu kikubwa kilicho msababisha baba yako kuchukua uamuzi wa kutaka kumuua mama yako pamoja na wewe ili kuweza kuzirisi mali zote ambazo mama yako anazo”
“Mmmm sasa mimi mbona ninafanana sana na baba yangu?”
“Ndio kutokana baba yako ana pacha wake ambaye ni doto na yeye ndio baba yako wa damu na wao wanafanana sana kiasi kwamba ni vigumu sana kwa mtu kuweza kutambua kuwa wewe baba yako si huyo mkuu wa jeshi”

Ni habari mpya katika maisha yangu kwani mama yangu hakuweza kuniambia siku hata moja kuwa baba yangu ni pacha wa baba yangu wa sasa ambaye amejenga chuki kubwa juu yangu na mama yangu,Nikajikuta machozi yakianza kunimwagika
“Kaka jikaze usilie ila huo ni ukweli ambao mimi ninakuambia na huyu daktari mimi ni mtu wangu wa karibu ukiachilia kuwa ni mjomba wangu ila ni zaidi ya hapo kwani vitu vyake vingi huniambia kiasi kwamba vingine siwezi kuvizungumza hapa........Ila ninakuomba sasa hivi tukajaribu kuyaokoa maisha Sheila ambeye niliapa kumsaidi Sheila hadi mwisho wa maisha yake tana kuna hii sauti niliirekodi kipindi anazungumza kwa uchungu na mimi”

‘NI KWELI SIJAMUUA EDDY WANGU MIMI NINAMPENDA SANA NA YEYE NDIO MWANAUME WA NDOTO ZANGU.....MIMI NIPO RADHI KUFA KWA AJILI YA MUME WANGU EDDY NIKAONANE NAYE PEPONI KWA MUNGU.....JOHN NAKUOMBA USIJISUMBUE SANA KWA AJILI YANGU KWANI MIMI HUU NDIO MWISHO WA MAISHA YANGU”

“HAPANA SHEILA USILIE MIMI NIPO TAYARI KUKUSAIDIA KUUVUMBUA UKWELI JUU YA HILI KWANI SIAMINI KAMA WEWE NDIO MUUAJI”
“HAPANA JOHN WEWE NIACHE TU NIKAFUNGWE SINA JINSI YA KUFANYA NA HUU NDIO MWISHO WA MAISHA YANGU BAI JOHN”

John akazima simu yake baada ya kuniona ninazidi kutokwa na mahozi mengi na akaniomba nikaze twende tupate msaada wa mwana sheria wa serikali.Tukasimama na John na kutoka nje ya duka huku sura yangu nikiwa nimeiinamisha chini ili watu wasiyaone machozi yangu,Tuakapanda kwenye pikipiki yake na moja kwa moja tukaelekea kwenye mahakama ya Kisutu na John akanipeleka kwenye ofisi za mwanasheria wa serikali aliye simamamia kesi ya kuhukumiwa kwa Sheila na kitendo cha kuingia kwenye ofisi yake kikamfanya mwana sheria huyu kustuka kiasi kwamba akanyanyuka na kubaki akinitazama

“Mkuu samahani kwa kukuingilia ofisini kwako pasipo kuwa na taarifa maalumu ila kama unavyo one mbele yako nimekuja na Eddy ambaye inasadikika ni mfu”
Mwanaheria wa serikali akabaki amesimama pasipo kujibu kitu cha aina yoyote na kubaki akibabaika pasipo kujibu kitu cha iana yoyote
“Mkuu tunahitaji msaada wako wa hali na mali”
“Ehhee umesema amefufuka?”
“Hilo mimi sijui atasema mwenyewe kwamba amefufuka ila kidhibitisho ni kwamba Eddy mwenyewe huyu hapa na hajafa kama mulivyo mdhania ila ninakuomba uweze kutusaidi kuhairisha mauaji ya Sheila”
“Dooo watakuwa wanakaribia kumua kwani zimebaki dakika 45 tu kabla hajanyongwa”

Mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio kiasi kwamba nikajikuta nikanza kuzunguka zunguka ndani ya ofisi ya mwanasheria wa serikali na kuwaacha John na mwanasheria wa serikali wakizungumza
“Tunakuomba sana uweze kutausaidi kama tunaweza kwenda kumuona”
“Ahaa sasa hiyo ni ngumu kwa maana amesha kabidhiwa kwa askari maalamu wana shuhulika na hilo swala kwa hiyo mimi siwezi kwenda”
“Nipo chini ya miguu yako kiongozi ninakuomba twende au tuambie tu niwapi alipo”
“Kwa hilo mimi siwezi kuzungumza chochote juu ya hilo”

John akapia maoti huku sura yeke ikiwa ina mwagikwa na machozi na ila mwasheria akaanza kutingisha kichwa cheke akishiria hataki kukubaliana na kile anacho obwa na John.Kwa hasira nikapiga hatua hadi sehemu aliyo simama mwanasheria wa serikali na kumvuta tai yake na kumsogeza karibu na sura yangu iliyo jaa ndavu nyingi na nikamuangalia jocho kali kiasi kwamba akabaki akiwa ananitazama kiwoga
“UNAKWENDA AU HUENDI?”
“Mmmmm”

Nikaishika shingo ya mwanasheria mkuu na kuinamisha kwenye meza yake kwa hasira na kwa haraka nikachukua peni iliyopo kwenye meza na kuishusha kwa kasi hadi kwenye shabu lake na kuanza kuigandamiza kwa kwa nguvu huku mwili mzima ukiwa unanitetemeka kwa hasira
“Nakwenda nakwenda......”
Mwanasheria mkuu alizungumza huku akitoa ukelele wa kulia,nikamnyanyua na kumuamrisha kutangulia mbele huku nikiwa ninamfwata nyumba huku nikiwa karibu yake sana endapo atajaribu kukimbia tu ningemfanya kitu ambacho asinge kisahau kwenye maisha yeke.Kila tulipo pita watu walinishangaa na hatua chache kabla mwanasheria wa serikali hatujafika kwenye maegecho ya magari akachomoka kwa kasi akikimbia kitendo kilichonifanya na mimi kukimbia kwa kasi zaidi yake na uzuri wenyewe yeye ni mnene na anakitambi likubwa

Kwa nguvu zungu zote nikarusha teke lililo mpiga kwenye miguu yake kwa nyuma na kumfanya aanguke kama mzigo wa kuni na akaangukia pua kitendo kiliho shuhudiwa na watu wengi ikiwemo askari walio anza kukimbia wakija kwenye eneo tulilopo huku bunduki zao zikiwa mikononi mwao huku wakinimrisha nisifanye kitu cha iana yoyote na John akabaki akiwa haamini kitu alicho kiona

Nikamnyanyua mwanasheria wa serikali na kumuamrisha kuelekea lilipo gari lake na askari walio kuwa wakinifwata wakajikuta wakisimama huku wakionekana kunishangaa.Ila mmoja wao akanifwata akiwa na bunduki yake na kumbukumbu zikanikumbusha kuwa ni askari wa getini ambaye mara ya mwisho alinisaidia katika kotoroka mikononi mwa baba
“Eddy vipi tena?”
“Safi”
Nilizungumza huku nikumuongoza mwanasheria hadi kwenye gari lake nikamuomba funguo yake kilazima na akaitoa kabla sijaingia kwenye gari nikastukia nikiguswa bega na nikageuka nikakutana na sura ya askari wa getini

“Kaka Eddy huyo mkuu ana nini?”
“Si unamkumbuka yule binti niliye kuwa naye siku ile tulivyo kuwa tunatoroka home?”
“Ndio si amehukumiwa kifuno cha maisha tayari?”
“Ndio ila kwa kosa la kuonewa sasa ndio huyu fala ninamuomba anipeleke alipo anakazi ya kunizingua hapa”
“Ahaa mimi ninapajua tunaweza kwenda pamoja”

Tukaingia ndani ya gari na kumkabidhi askari wetu wa getini funguo ya gari na safari ikaanza.Kitu ambacho ninakishukuru kutoka kwa askari wetu wa getini ni kuwa mtu muelewa japo ni askari wa jeshi la polisi ila mama alipendekaza kuwa askari wa kuilinda nyumba yetu kutokana na upole na hekima aliyo nayo ni tofauti na maaskari wengine ambao wana dharau kiasi kwamba mtu unashindwa kuwadhamini katika maisha
“Kaka Eddy unajua hata mimi niliamini kuwa umefariki dunia?”
“Sijakufa ndugu yangu ila wee acha tuu”
“Basi unajua habari za kifo chako zilinistua kiasi kwamba nikawa nipo njia panda kwa maana yule binti kwa muonekano anaonekana anakupenda kiasi kwamba hasikii la mtu juu yako sasa sikuelewa nilipo ambiwa kuwa amesababisha kifo chako”
“Najua zote ni mbinu za mzee ila zitafikia mwisho”
“JAMANI NINAOMBA MUNISIKILIZE”

Mwanasheria wa serikali alizungumza na kutufanya sote tukae kimya na kumsikila kitu anacho taka kutuambia
“Jamani ukweli ni kwamba Sheila hajanyongwa japo mahakama ilitoa hukumu ya namna hiyo”
Sote tukajikuta tukiguna kila mmoja kwa mtindo anao ujua yeye mwenyewe kiasi kwamba tukabaki tukimsikilizia kitua atakacho kizungumza
“Ukweli ni kwamba Mr Godwin alitokea kumpenda yule binti na akahitaji tuweze kumhukumu hivyo ila yeye amepanga safari ya kwenda naye kuishi visiwa vya Komoro na hapa ninavyo zungumza amenitumia meseji akidai yupo uwanja wa ndege kwa ajili ya safari ya kuelekea visiwa vya Comoro”

Nikajihisi nguvu za mwili zikiniiishia kiasi kwamba nikabaki nikiwa kimya nisijue nini cha kufanya na hasira kali dhidi ya baba yangu ikanipanda na kujikuta nikinyang’ata meno yangu kiasi kwamba sauti ya msuguano wake ikasikika kwa kila mtu.
“Muheshimiwa amekuambia kuwa anaondoka na ndege ya saa ngapi?”
“Ngoja niwaonyeshe meseji aliyo nitumia”

Mwanasheria akatoa meseji aliyo tumiwa na baba na kuanza kumuonyesha John ambaye nikamshuhudia akishusha pumzi nyingi kiasi kwamba akionekana kuchoka na kile alicho kisoma na kabla hajamuonyesha askari wetu wa getini nikampokonya simu na kuisoma meseji iliyopo kwenye simu yake

{MR KILONGO MIMI NIPO NIPO UWANJA WA NDEGE NINAELEKEA VISIWA VYA COMORO KULA RAHA NA HUYU MTOTO,JANA NIMEMUONJA NI MTAMU SANA.ILE PESA NIMEKUINGIZIA KWENYE AKAUNTI YAKO ASANTE KWA KAZI NZURI ULIYO IFANYA NA HAKIKISHA UNAMALIZIA JUHUDI ZA KUZIBINAFSISHA MALI ZA MKE WANGU NITAKUPA ROBO YA UTAJIRI WANGU}

Nikabaki nikiwa ninatetemeka kwa hasira kiasi kwamba nikajihisi michuruziko ikinitoka puani kwangu na matone baadhi yakadondoka kwenye mapaja juu ya nguo za wauguzi nilizo zivaa na kugundua kuwa ni damu ndio zimenitoka puani na sikujua zimesababishwa na nini kwani ndio mara yangu ya kwanza kutokwa na damu za puani.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI

KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger

Chapisha Maoni