SORRY MADAM (45)

0
SEHEMU YA AROBAINI NA TANO
ILIPOISHIA...
“HAAA HUYU MAMA NAYE YUOPO.....KWELI MUNGU HAPENDI DHAMBI KUNA SIKU BWANA ALIKUWA NA DEREVA WAKE SASA KWA BAHATI MBAYA NIKAMCHOMEKEA KWA MBELE ILE BARABARA YA KUINGILIA K.C.M.C NILIKUWA NAMUWAHISHA MGONJWA HOSPITALINI.AHAAAA ALIKWENDA KUNILAZA POLISI HADI SIKU ANAONDOKA ARUSHA NDIO WAKANIACHIA...... TENA HAO WATEKAJI KAMA WANAJUA WAMFANYE WA KWANZA KUFA KWA MAANA YULE MAMA ROHO MBAYA SANA”

NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU

SASA ENDELEA...
Baba akanisogelea na kunishika bega na kuniomba ninyanyuke kisha akaniweka vizuri shati langu na kuniomba twende nje.Akaanza kunitembeza kwenye eneo la jumba lake la kifahari na kwaharaka haraka utajiri wa baba ni mara tano ya utaji alio nao mama.Ila moyoni mwangu sikuweza kuiruhusu chuki iliyopo kati ya wazazi wangu kunitawala moyoni mwangu ila chuki yangu kwa sasa ilibaki kwa baba mkubwa ambaye amemtekana mama akisaidia na Emmy mwanamke aliye jitambulisha kama daktari

Baba akanionyesha chumba changu kikubwa ambacho nitakitumia kwa kulala na nikikubwa sana na kina vitu vingi sana vya kuvutia japo kwa mama ni tajiri ila baba amezidi kuwa na utajiri mkubwa.Muda wa usiku wageni ambao ni rafiki wa baba wakaanza kukusanyika kwa ajili ya sherehe na kabla ya sherehe kuanza nikawa nipo kwenye chumba maalumu huku nikiwa na mwana mitindo ambaye amenitengenezea suti nzuri inayo endana na mimi na kazi hii ameifanya ndani ya msaa machache jambo ambalo limenishangaza na hapa nikagundua kuwa wezetu wenye nchi zilizo piga hatua wamechangamka sana kwenye utendaji wao wa kazi
“Unajionaje kijana?”

Mwanmitindo aliniuliza baada yakuivaa suti aliyo nitengenezea huku nikiwa nimesimama mbele ya kioo nikiwa nimependeza kiasi kwamba hata mimi kimoyo moyo nikaanza kujisifia kabla sijasifiwa
“Imenikaa vizuri?”
“Hakuna sehemu ambayo inakupa shida kwenye kutembea au imekubana sehemu?”
“Sina kila sehemu imekaa sawa”
“Hembu tembea hadi pale mbele”

Nikapiga hataa kama sita kisha akaniomba nigeuke na kurudi sehemu niliyo simama awali na hadi ninafika nikasikia makofi yakipigwa na nikageuka na kukutana na mama mke wa baba kwa sasa akiingia kwa mwendo wa madaha hadi sehemu niliyo simama
“Unaonekena ni kijana mzuri..mtanashati eheee?”
Sikumjibu kitu cha aina yoyote zaidi ya kumtazama jinsi anavyo niangalia kuanzia chini hadi juu kwa macho ya dharau
“Josh ninakuomba utoke na tunataka tuzungumze”

Mwanamitindo akatoka na kutuacha tukiwa tumetazamana na mke wa baba na baada ya mlango kufungwa sura yake ikabadilika na ikakusanya mikunjo migi ya hasira.
“Huwezi kuichukua nafasi ya mwangu mbele ya baba yako,sijui amekuokota amekununua,amekuiba ila nitahakikisha hapati chochote kwenye uridhi huu wa baba yako”
Mke wa baba alizungumza huku sura yake akiwa ameikunja na meno yake akiwa ameyang’ata kwa hasira

“Sikiliza wewe mwanamke hunijui sikujui sasa kama unaitaji kunijua utanijua kwa herufi kubwa sawa?”
“Hahaa sina haja ya kukujua omba omba kama wewe usiye na wazazi na nikawaida yenu vijana masikini kama nyinyi hapa Afrika kusini kuwaparamia watu wenye fedha zao na kuwaona ni kama wazazi wenu sasa kama umtumwa na huyo mama yako Malaya aliye shindwa kukulea basi kamwambie nafasi imkwisha”
Nikamtazama kwa hasira mke wa baba kiasi kwamba mwili mzima ukaanza kunitetemeka,
“Na kingine nitahakikisha humalizi wiki utakuwa umeondoka ndani ya hii nyumba”
“Etiii ehee....?”
“Na hakuna cha Etii ehee mbwa wewe uliye kosa pa kula”

Nikajikuta nikiunyanyu mkono wangu wa kulia kwa kasi ya ajabu nikaupeleka kwenye shavu la mke wa baba na kabla haumfikia mlango ukafunguliwa na nikamuona baba akiingia na nikaushusha chini kwa haraka na kumstukia mke wa baba akiangua kiliao huku akilishika shavu lake akidai nimepiga kitendo kilicho zidi kunipandisha hasira
“Mume wangu umeamua kuniletea mwanao aje kuniadhiu mimi....Si ndio?”
Mke wa baba alizungumza kwa sauti ya kufoka na kumuona baba akiwa amenywea na taratibu akaanza kupiga hatau za kumfwata mke wake
“Pole mke wangu.....Eddy mwangu mona upo hivyo?”
“Yaani mbele yangu unamuita huyo ngedere wako mwanao....?”
“Mke wangu huyo sio ngedere ni mwangangu”
“Wewe vipi kati ya watoto huyo unaweza kusema ni mtoto hembu muangalie anaonekana hivi hivi ni mama yake ni mbwa koko”

Maneno machafu ya mke wa baba yakanizidi kunikasirisha hadi nikashindwa kuizuia hasira yangu na kwaharaka nikamchomoa mikononi mwa baba ambaye anaonekana kuwa anamdekeza mwanamke wake.Nikamvuta karibu ya sura yangu huku nikiwa nimelishika sehemu ya kifuani kwake kwenye gauni lake alilo livaa na nikamuona anayafumba macho yake kwa kuongopa
“Nitakuua”
Nilizungumza kwa hasira na kumsukumia sehemu aliyoo baba na akamdaka mke wake na wote wakajikuta wakianguka chini kisha mke wake akasimama haraka
“Niue sasa kama unaweza”

Nikapiga hataa za haraka hadi sehemu aliyo simama na nikamtisha kama ninampiga kofi akaikuja mikono yake akiuficha uso wake na kwakutuma mguu wangu wa kulia nikipiga teke miguu yake yote miwili na kumrusha juu kidogo kimo cha mbuzi na akaanguka chini kama mzigo na kuendelea kulia,nikapiga goti kwa haraka na kuishika shingo yake na kwa haraka na kumsogelea karibu
“Usidhubutu siku hata moja kumuambia mama yangu ni Malaya na usinifananishe na mnyamwa wa aina yoyote na kama unataka kunifananisha nifananishe na shetani”
“Eddy mwanangu ninakuomba utulize jazba msamehe bure tuu”

Nikaisikia sauti ya baba ikizungumza kwa upole na unyenyekevu na nikamuachia na kusimama na kumaacha akikohoa kohoa
“Baba kumbe haya ndio maisha unayo ishi na huyu mwanamke asiye na adamu....anakazi ya kukupelekesha kama boya.Wewe ni mwanaume unatakiwa kumtawala mwanamke na si mwanamke kukutawala wewe”
“Mwanangu usizungumze hivyo”
Baba alizungumza huku akiinama na kutaka kumpa mke wake mkono ili amnyanyue na kwa haraka nikaiwahi mikono yao na kuichanisha
“Muache anyanyuke mwenyewe na tuone sasa kama atashindwa kunyanyuka”

Nikamsogeza baba mbali na mke wake ambaye akanyanyuka taratibu huku sura yake ikiwa imejaa machozi na aibu na akawa ananitazama kwa macho wiziwizi na akaanza kupiga hatua za haraka kuelekea mlango ulipo na kabla hajaufikia nikamuita kwa sauti ya ukali na akasimama na nikamfwata hadi sehemu alipo simama
“Kinacho kuliza ni nini?”
“Mmmm hakuna kitu”
“Futa machozi”

Mke wa baba akaanza kufuta mchozi kwa kutumia gauni leke kisha akabaki akinitazama ninavyo hisi hakuamini kama mimi ninaweza kufanya nilicho mfanyia mbele ya mume wake
“Nenda kajiandae na kwenye sherehe ninakuhitaji nikuone na nitakaa na wewe”
“Sawa”
Mke wa baba akatoka na kuufunga mlango kwa nguvu na kunifanya nianze kucheka na baba naye akanifwatia kwa kucheka

“Baba hivi huyu mke wako unaishi naye vipi?”
“Wee acha tuu mwanangu,Afadhali umekuja na wewe kwa maana huyu mwanamke ananipelekesha sana yaani hadi ikifikia kipindi nikirudi nyumbani tuu furaha yote inanipotea”
“Sasa kwanini na wewe baba unakuwa hivyo?”
“Yaani hata mimi mwenye sielewi ni kwa nini yaani akizungumza yeye huwa mimi sina la kubisha kwake”
“Kwani umeomtoa wapi?”
“Ahaa naye ana historia yeke ndefu tuu nitakusimulia siku nyingine...sasa hivi twende kwenye sherehe nahisi imesha anza na wanatusubiria sisi”
“Sawa baba”

Tukatoka na baba chumbani na kukuta mwana mitindo mlangoni na baada ya kuniona anakisimamisha na kuanza kuiziweka nguo zangu vizuri kisha akatoa viatu vinavyoendana na suti niliyo ivaa ambayo ni ya rangi ya bluu na nikavua viatu nilivyo vivaa na kuvaa alivyo nipa kisha tukaelekea sehemu yenye bustani iliyo pambwa vizuri na kukutana na watu wachache ila wamevali vizuri.Tukakaa sehemu ambayo tumeandaliwa na muongoza sherehe akaendelea na kazi yake,Macho yangu yakawa na kazi ya kutafuta ni wapi alipo mke wa baba na nikamuaga baba ninaelekea msalani(chooni) na akamuomba mlinzi wake mmoja kunifikisha msalani

Nikapita kwenye moja ya kordo na kumuona mke wa baba akiwa amekumbatiana na jamaa mmoja huku wakiwa wananyonyana midomo yao,mlinzi naye akashuhudia tukio hilo na nikataka kwenda ila jamaa akanizuia na kuitoa simu yake mfukoni na kupiga picha kadhaa na tukaendelea na safari yetu huku moyoni mwangu nikizidi kupata maumivu nikijiuliza ni kwanini baba anaishi na mwanamke wa namna hii

Nikamaliza haya zangu na tukarudi kwenye bustani na hatukuwaoa kwenye eneo walilo kuwepo,Nikamkuta mke wa bab akiwa amekaa pembeni ya baba huku akicheka akimtazama mchakeshaji anaye endelea kufanya yake.Nikajikausha huku mara kwa mara nikimtazama kwa macho makali na nikazidi kuumia pale anavyo mbusu busu baba machavuni na mdomoni akijifanya kama anampenda sana baba

Wakati wa kutambulishwa ukawadia na baba akanitambulisha kama mimi ndio mridhi wake wa pekee kitendo kilicho mchukiza mke wake japo kila nilipo mtazama akatabasamu akiashiria kuwa anafuaha moyoni mwake.Sherehe ikaisha huku moyoni mwangu nikitamani kumuambia baba juu ya tukio alilo lifanya mkewe ila nikaona hatomfanya kitiu chochote.Nikaelekea chumbani kwangu na nikaoga na kupanda kitandani na mawazo ya wapi alipo mama yakanza kunitawala kichani kwangu
Nikanyanyuka na kuisogelea meza iliyo na kumputer aina ya HP,nikaiwasha na kwabahati nzuri nikakuta imeunganishwa na hudumu ya internet.Nikaingia kwenye mtandao unao husiana na taarifa za serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,Nikaanza kutafuta tafuta habari itakayo husiana na mama na nikakutana na habari ya iliyo andikwa kwa maandishi makubwa ikisema
“WAZIRI WA AFYA ATOROSHWA HOSPITALINI HUKO AFRIKA KUSINI ALIPOKUWA AMELEZWA”

Nikaanchana nayo kwani ni habari iliyo tolewa mwezi na nusu ulio pita na nikakutana na taarifa nyingine inayo husiana na mama
{“BI GRACE INASADIKIKA AMETEKWA NA KUNDI LA KIGAIDI LA AL-SHABABI”}
Mapigo ya moyo yakaanza kuniende mbio na nikaifungua taaribu hiyo na kuanza kuisoma huku mwili mzima ukinitetemeka hadi nijajikuta ninacho kisoma sikilewi.

{“Mume wa Bi Magreti bwana Godwin amabeye ni mkuu wa jeshi kikosi maalumu amedai kuwa mke wake ametekwa na magaidi hao ambao wanahitaji kiasi cha dola za kimarekani milioni 50 kutoka kwenye serikali ya Tanzania ili kumuachia huru waziri huyo”}
{”Raisi aishutumu serilakali ya Afrika kuwa hawapo makini katika swala la ulinzi viongozi wanao toka nchi mbalimbali wanao lazwa kwa ajili ya matibabu katika hospitali zao”}

Nikajikuta nikijikuna kichwa kiasi kwamba nikahisi nywele nitazitoa kwa kuzivuta.Moyo kwa moja nilajua kuwa mama hajatekwa na kundi hilo la magaidi kama inavyo semekana na moja kwa moja atakuwa ni baba ambaye kwa sasa anajifanya kuwa watekaji ni kundi la Al-shababi.

Nikaendelea kutafuta habari nyingine na kukutana na habari nyingine ikesema
{“HIZI NDIZO PICHA ZINAZO MUONYESHA WAZIRI BI MAGRET AKIWA MIKONONI MWA MAGAIDI WALIO TOA SIKU KUMI NA TANO KWA SETIKALI YA TANZANIA”}

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI

KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)