SORRY MADAM (46)

0
SEHEMU YA AROBAINI NA SITA
ILIPOISHIA...
Nikaendelea kutafuta habari nyingine na kukutana na habari nyingine ikesema
{“HIZI NDIZO PICHA ZINAZO MUONYESHA WAZIRI BI MAGRET AKIWA MIKONONI MWA MAGAIDI WALIO TOA SIKU KUMI NA TANO KWA SETIKALI YA TANZANIA”}

NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU

SASA ENDELEA...
Nikaanza kutazama picha moja baada ya nyengine na kumuona jinsi mama alivyo fungwa kitambaa cheusi machoni mwake huku kichwani mwake akiwa amewekewa mitutu kama sita ya bunduki aina ya SMG.Machozi yakaanza kunimwagika baada ya kuiona picha nyingine ya mama akiwa amechorwa maandishi ya kiarabu yenye rangi nyekundu kwenye kifufua chake huku mkono mmoja wa mtu ulio valia gloves nyeusi ukimshika kwenye sehemu ya chini ya kidevu chake huku akimminya mashavu yake kwa nguvu

Nikajikuta mkono wangu ukielekea kwenye kitufe cha kuzimia computer na kurudi kitandani huku machozi yakinimwagika na hasira ikawa imenikaba kifuani mwangu hadi nikahisi kifua changu kinaweza kunipasuka.Sikupata usingizi hadi asubuhi na kitu cha kwanza nikamsubiria baba ili nimpe taaria hiyo.
Baba akanikuta nimekaa sebleni nikiwa nimeshika tama na baada ya salamu nikamuomba nizungumze naye na akakubali na akakaa pembeni yangu na nikanza kumsimulia kuanzai A hadi Z kwa hali aliyo kuwa nayo mama

“Sasa hapo tutafanyaje mwanangu?”
“Una hizo milioni 50?”
“Mmmm hicho ni kiasi kikuwa cha pesa japo ninacho ila ngoja kwanza tujua hiyo hali itakwenda vipi?”
“Basi inanibidi nirudi Tanzania leo?”
“Kwa leo mwangu siwezi kukuruhusu kurudi Tanzania ila ngoja nitwapa hiyo kazi wafanya kazi wangu hiyo kazi”
“Wataiweza kweli?”
“Ndio ila sio hawa una waona hapa kuna wengine nitawapa”
“Lini utawapa?”
“Leo ngoja tupate kifungua kinywa kisha tutakwenda kwa hao watu wangu na sipendi waje hapa kwani wanatafutwa sana kwa matukio wanayo yafanya inanibidi tuwafwate”
“Sawa”

Tukapata kifungua kinywa kisha nika tukajiandaa kwa ajili ya kwenda alipo ndiambia baba na tukatumia gari jengine ambao linaendesha na yule mlinzi wake wa jana sukiku,Ndani ya gari sote tukawa kimya huku akili yangu ikiwa inamuwazia mama yangu.Tukafika kwenye gorofa moja na baba akashuka
“Eddy nisubirini nikaongee na kiongozi mmoja hapa wa jeshi kisha tutawafwata hao watu”
“Sawa baba ila nina ombi”
“Ombi gani mwanangu?”
“Baba ninaomba pesa ya kununua simu kwa ajili ya mawasiliano”
“Sawa”

Baba akatoa kikadi cha banki na akaniandika namba zake za siri kwenye kikaratasi na kumuomba dereva wake anipeleke kwanye ATM za banki na kish yeye akaingia kweye ndani ya gorofa na sisi tukaondoka.
“Kaka hivi simu za gharama huku nitazipata wapi?”
“Maduka yapo mengi tuu utakapo hitaji wewe nitakupeleka”
“Maduka yanatumia pesa aina ya dola au Rand”
“Inategemea na duka lenyewe linatumia pesa ya aiana gani ila ninakushauri ukatoa dola ya marekani”
“Sawa utanirushia zile picha za jana”
“Sawa”

Tukafika kwenye gorofa ambalo lina mashine za kutolea pesa(ATM) na tukashuka ndani ya gari na jamaa akabaki njea na mimi nikaingia ndani.Nikachukua kiasi cha pesa ya kunitosha hata kwa matumizi mengine kisha nikatoka nje na kumkuta jamaa akiminyana na dada aliye na nywele zilizo changuka huku dada huyo akiwa amenipa mgongo na mavazi yake yakiwa yamechafuka na kuchanika chanika sana.Mwili wake umejaa ukurutu na amepauka sana huku ukiwa umedhohofika sana japo anaonekana kuwa na nguvu nyingi na kwaharaka haraka nikatambua kuwa dada huyu ni kichaa
“Eddy nenda kwenye gari ninakuja sasa hiv....khaaa”

Jamaa alipiga kelele baada ya dada huyo kumng’ata kwanye mkono kisha akanigeukia na mimi na kujikuta nikibaki nikiwa nimesimama huku nikiwa nimemshangaa kichaa huyu kwani ni Sheila mpenzi wangu ambaye mara ya mwisho kumuona ni siku niliyo gongwa na gari.Nikiwa nimesimama Sheila akamuachia jamaa na kunirukia mimi na sote tukaanaguka chini huku nikijitahidi kumshika kichwa chake anacho taka kuning’ata kwa meno yake yaliyo machafu huku akidondosha udenda mwingi na akinguruma kama mbwa mkali mwenye njaa kali

Mlinzi akamuwahi Sheila na kumnyanyua juaa na lipindi tukio linatokea askari waliweza kuliona na wakamkamata Sheila na kabla hawajaondoka naye nikawazuia
“Jamani samahani kaka zangu ninamuhitaji huyo binti”
“Huyu ni mwenda wazimu na ametoroka katika hospitali ya vichaa na karibia wiki sasa tunamtafuta”
“Sawa nimewaelewa sijui tunaweza tukaongozana hadi sehemu ilipo hiyo hospitali?”
“Kwani wewe unamfahamu huyu binti?”
“Hapana ila ninahitaji kuweza kuyafahamu maendeleo yake”

Askari wakanitazama kisha wakaniruhusu kama kuongozana nao,tukaingia kwenye gari letu na kuongozana na askari hadi kwenye hospitali ambayo ni yawatu walio pungukiwa na akili.Sheila akakabidhiwa kwa madaktari na polisi wakanionyesha sehemu ambayo ninaweza kupata kawimu za maendeleo ya Sheila,
“Samahani dada yangu”
Nilimuuliza nesi mmoja niliye mkuta kwenye dirisha la kuudumia wateka wanao hitaji huduma kwenye hospitali hii
“Bila samahani”
“Kuna mgonjwa ameletwa dakika tano zilizo pita na ninaomba kuweza kujua takwimu zake za nyuma”
“Ahaaa juyo dada aliyeletwa hapa akiwa hajitambui na kadris siku zilivyo zidi kwenda alikuwa msumbufu anapiga wezake hadi kunasiku alimuua mwenzake mmoja kwa kumpiga kwa chupa kichwani”

Nikajikuta nikiwa nimeuacha mdomo wangu wazi kwa mshangao kwa maana sikutegemea kusikia taarifa kama hiyo
“Labda tatizo leke kubwa haswa ni nin?”
“Mmmm kwa mimi siwezi kujibu labda ngoja nikukutanishe na daktari ambaye alikuwa akimuhudumia tangu siku ya kwanza alipo kuja”
Akanyanyua mkonga wake wa simu na kuzungumza na mtu aliyo upande wa pili wa simu kisha akaniomba niweze kuingia ndani kwenye ofisi ambayo ipo upande wangu wa kushoto na ikanilazimu kumuacha nje dereva,Nikamkuta daktari wa kiume mwenye umri mkubwa kiasi na akaniruhusu nikae pembeni kwenye kiti

“Nikusaidie nini kijana?”
“Kuna mgonjwa ambaye ameletwa muda mchache ulio pita na sijui ninaweza kupata taarifa yake ya nyuma?”
“Wagonjwa walio letwa muda mcha ulio pita ni wengi labda wewe unamzungumzia yupi kati ya hawa?”
Daktari akawasha Tv yake kwa kutumi rimoti na nikaziona picha za Sheila akiwa ameshikwa na askari

“Huyo picha namba tano”
Nilimuonyesha daktari kwa kutumi kidole na akaizima Tv yake na kunigeukia huku akisaidiwa na kiti chake chenye uwezo wa kuzunguka
“Huyo hapa sisi tunamuita Vaiper Lady”
“Kwa nini?”
“Kwanza nimkali na ninamfananisha na hao nyoka ambao wanasifa ya kung’ata sana,Pili hatulitambui jina lake halisi ni nani”
“Sawa ila tatizo lake ni nini?”
“Huyu binti amedhirika sana kiakili hii ni kutokana na mambo magumu ambayo ameweza kupitia huku nyuma.Pia ubongo wake umetingishika kiasi kwamba imemfanya akili zake kufyatuka”
“Akili yake imetingishika?”

“Ndio ina maana aliweza kupigwa kwa kitu kizito kichwani ambacho kiliipelekea akili yake kucheza kidogo na jambo kubwa la kumshukuru Mungu ni kwamba mishipa ya damu haikuweza kupasuka kichwani mwake”
“Anaweza akapona?”
“Mmmm sidhani kwa maana sisi tumejaribu kutumia ujuzi wetu mwingi ila tumeshindwa ila kitu kibaya zaidi huwa hapendi kuona jinsia ya kiume na alashawahi kufanya tukio la mauaji kwa….”
“Hili nilisha ambiwa……Sasa dokta imi ninahitaji kukaa naye kwa ukaribu sana ili niweze kumtuliza”
“Wewe kijana unahitaji kufa au…..kwa maana hataki kuona jinsia yoyote ya kiume”
“Mimi nitaweza dokta na Mungu akibariki kesho nitakuja kwa kazi hiyo”
“Mmmm kwa kweli si……”

Nikachomo noti mbili za dola mimi kwenye mfuko wa suruali na kumuwekea daktari mezani na akanyamaza
“Kaka utahitaji kiwango kingine zaidi ya hicho nitakupatia”
Daktaria akanyamaza kimya na kushindwa kuzungumza kwa aibu na nikanyanyuka na kumuacha akiwa ananishangaa.Hali ya furaha ikanitoweka kabisa na hata ndani ya gari nikawa kimya huku nikimuwazia Sheila na sikusema kuwa ninamfahamu Sheila hii ni kuepuka maswali mengi yasiyo na msingi kwangu.Tukaingia kwenye moja ya duka la simu na kununua simu aina ya Blackbery.Tukarudi kwenye jengo ambalo baba aliingia na kumkuta akiwa anatusubiri

“Mbona mumechelewa?”
“Ahaa kuna sehemu sehemu nilipitia”
“Hiyo simu umesha nunua?”
“Ndio baba”
“Sasa turudi nyumbai kwa maana lile swala nimesha likabidhi kwa wahusikana wameniahidi ndani ya siku mbili watanipa jibu”
“Kweli baba?”
“Ndio wewe kuwa na amani na kama utataka kuendelea kutazama tazama mji nipige simu nyumbani nije kuchukuliwa na gari nyingine?”
“Hapana kwanza nimechoka ninahitaji kupumzika kidogo alafu ninaomba namba yako baba”
“Sawa”

Baba akanipatia namba yake ya simu na kutokana sikuwa na line ikamlazimu kunipa laini yake moja ya simu ambayo haitumii sana.Tukarudi nyumbai huku msongamano wa mawazo ukiwa umenitawala na moja kwa moja nikagundua baba wa zamani mzee Godwin ndio chanzo cha Sheila kuwa katika hali kama hii.Sikuweza kupata suingiza kabina na kila nilipo jaribu kuivuta amani kutawala usoni mwangu nikajikutani kishindwa kabisa na sura yangu ikawa imetawaliwa na mikunjo ya hasira.Nikiwa nemekaa kwenye moja ya masofa ya kupumzikia yaliyopo kwenye bustani yenye maua mengo mazuri na kuna kijibwawa kidogo chenye maji masafi na upepo mwingi nikamuoana mke wa baba akiwa na yule jamaa wa jana usiku wakiwa kwenye moja ya kijijumba kilicho kwa vioo na ndani yake kukiwa na maua mengi yanayo uteshwa kwa masaada wa mwanga wa jua

Wakanza kushikana shikana na mwisho wa siku wakanza kupeana mambo ya chumbani bila kujali kama wanaweza wakaonekana na mtu.Nilicho kifanya ni kurekodi tukio zima mwanzo hadi mwisho hadi wanamaliza na jamaa akawa wa kwanza kutoka na baada ya dakika kama kumi mke wa baba naye akatoka huku akijifanya kunusa nusa kipande cha ua alicho toka nacho na kwabahati mbaya macho yetu yakakutana na akanipandisha na kunishu kiasi kwamba akaanza kunikera
“Mama ninakuomba”

Akatembea kwa mwendo wa madaha huku mdomo wake akiwa ameubenua kiasi kwamba nikaanza kujiuliza sijui kipigo cha jana amekisaha
“Unasemaje?”
“Hivi baba yangu ni nani kwako?”
“Khaa wewe unamuona ni nani?”
“Jibu nililo kuuliza”
“Ni mume wangu”
“Una uhakika na unacho kizungumza?”
“Ndio kwa maana hata pete hii hapa ninayo”
“Unajua siku zote kwenye maisha usipende kumfanyia mwenzako kile usicho penda kufanyiwa”
“Una maana gani?”
“Utaijua wewe nenda zako”

Akaniandisha kuanzi chini hadi kitendo ambacho maishani mwangu sipendi mwanamke anifanyie akaachia msunyo mkali uliao nifanya ninyanyuke kwa haraka na kumfwata kwa hasira na akaanza kukimbia ila kutonaka na uwezo wangu wa kukimbia nikamdaka katika mlango wa kuingilia sebleni na kukutana na baba akiwa anatoka ndani

“Huyu mwanao ni mwenda wazimu nini?’
Sikumjibu kitu cha aina yoyote zaidi ya kumfwata na nilipo sikia swala la uwenda wazimu na mimi nikajichetua sana na ili nionekane ni mwenda wazimu kweli.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI

KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)