
SEHEMU YA MIA MOJA KUMI NA NNE
ILIPOISHIA...
Sheila akashindwa kustahimili kusimama, akadondoka chini na kutulia akazidi kumchanganya John, aliye livua koti lake kwa kuchanganyikiwa. John amampokonya kipaza sauti mchungaaji
"Wewe mshenzi uloye ziweka hizi video zitoe kabla sinakuua"
NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
John alizungumza huku mishipa ya shingo ikiwa imemsimama, huku jasho jingi likimwagima kama maji.
Video zikabadilika na kuionyesha sura yangu, halisi, huku chini kukiwa na maandishi makubwa R.I.P EDDY, ikaja picha ya Victori, akiwa na John. Huku maandishi yakiandikwa R.I.P VICTORIA.
John akabaki akiwa ameitumbulia macho tv hiyo. Akaifwata Tv na kuinyanyua, akaibamiza chini. Gafla taa zote za kanisani zikazima, huku kagiza kwa mbali kakitanda ndani ya kanisa. Watu wakaanza kuchanganyikiwà mara baada ya moshi mkali, wa mabomo ya machozi kuanza kutapakaa ndani ya kanisa. Nakuzidi kumchanganya John aliye fura kwa hasira kali.
Mirindimo ya risasi, ikaanza kurindima ndani ya kanisa, jambo lililo pelekea watu kulala chini, huku wakipiga mayowe.
"Pretty mbona sielewi?"
Milimuuliza Pretty baada ya kuona hali inazidi kuwa ngumu, Watu walio valia nguo nyeusi wapatao kumi, wakaingia ndani ya kanisa, huku sura zao zikiwa zimezibwa na vinyago, mikononi mwao wakiwa waneshika silaha nzito
"Hata mimi sielewi"
Pretty alinijibu huku akionekana kuto kuelewa ni nini kunacho endelea, kwani si tukio tulilo lipanga kutokea.
Kundi la watu hao, nikawashuhudia wakimnyanyua juu, John aliye legea sikujua wamemfanya kitu gani. Wakambena na Sheila juu na kutoka nao nje yakanisa.
"Twende"
Nilimuambia Pretty huku tukinyanyuka na kutoka nje ya kanisa huku tunakimbia. Tukalikuta gari jeusi, kubwa likiondoka kwa kasi nje yakanisa. Nikakimbia hadi lilipo gari letu, huku Pretty naye akinifwata kwa nyuma. Nikaingia na kuwasha gari. Ikawa ni kazi yangu kulifuluzia gari hilo lililo wabeba Sheila na John ambao wapo kwenye mpango wangu wa kuwaangamiza na sikujua hawa walio vamia na kumteka ni kina nani.
Pretty akabaki kunishanga, kwa jinsi undeshaji wangu ulivyo kama kichaa. Kwani niliyapita magari yaliyo mbele yangu, pasipo kupunguza mwendo kasi wa gari.
"Ohhh Eddy tunafwatwa kwa nyuma"
Kwakupitia kioo cha pembeni, nikaona gari nne za polisi zikitufwata kwa kasi huku zikipiga ving'ora.
"Tulia usiwe na wasiwasi"
Kwa uzoefu wangu, katika kuendesha magari haya ya kampuni ya BMW, ulinisaidia sana kuweza kumudu mwendo kasi wa gari, la maadui lililo wabeba John na Sheila. Polisi hawakukata tamaa kuendelea kutukimbiza kwa nyuma. Nikastukia kuona gari la watu majambazi, wakifungua mlango wa nyuma, wakasimama jamaa wawili wakiwa kwenye mavazi yao yale yale walioyo ingia nayo kanisani, kila mmoja wao akiwa na bunduki zao zinazo toa risasi pamoja na mabomu pale wanapo hitaji kufyatua mabomo hayo.
Mara nyingi bunduki za aina hii wanatumia wanajeshi wakimarekani, hususani wale wanao kwenda kupambana na vikundi vya kigaidi katika nchi za Iraq na nyinginezo zenye vikundi vya kigaidi.
"Eddy......Eddy.......Eddy"
Pretty alizungumza hivyo baada ya kuona watu hao. Umakini wangu wote ukahamia kwao. Wakaanza kupiga risasi zisizo na idadi, kuelekea tulipo sisi. Nilicho kifanya ni kubadilisha njia na kupitia kwenye barabara ya pembeni, ambayo magari yake yanarudi kutoka upande ninao tokea mimi.
Katika siku nilizo jitahidi kuendesha gari, zaidi ya uwezo wangu ni siku ya leo. Mbaya zaidi magari mengi ya upande niliopo yananifwata, kila ninavyo yakwepa ndivyo ajali ya magari mengine yanavyo zidi kubamizana, kutokana na kunikwepa mimi.
"Eddy rudi upande ule"
"Watatuua"
"Kwani ni kina nani?"
"Sijui mimi"
Ptetty akakaa kimya na kuniacha nifanye lile ninalo liweza katika kuyaokoa maisha yetu, kwa maana yapo hatarini kutoweka endapo nitafanya kosa la kugongana na gari lolote. Nikazishubudia gari za polisi jinsi zinavyoshambuliwa na magaidi hao hadi zikapoteza muelekeo.
Nikafanikiwa kulirudisha gari upande ninao paswa kupita, Nilicho kifanya kwa wakati huu, nikuhakikisha ninalipita gari hilo kwa kasi kubwa. Kabla sijachukua uamuzi huo, wakakatiza kulia na kuingia kwenye barabara iliyo nyooka sana. Sikukata tamaa na mimi nikakafanikiwa kukunja huko huko japo gari lilinizidi nguvu, likayumba kidogo, kutokana na kukunja gafla. Nikafanikiwa kuliweka sawa na kuendelea kulifukuzia.
"Wanaelekea kwenye msitu wa Amazon"
Pretty aluzungumza huku akitaza simu yake inayo inyesha ramani ya eneo tulipo.
"Sasa Eddy si tuhairishe kuwafwata"
Pretty alizungumza akionekana kukata tamaa. Sikumjibu chochote zaidi ya kufanya kile kilicho niweka ndani ya gari hili. Nikafanikiwa kulipita gari hili na kuwa mbele yao. Nimejiamini kuwa mbele kutokana na barabara kunyooka tu.
"Unaweza kuendesha kwa mwendi huhuu?"
"Ndio"
"Njoo ukae hapa"
Nikampisha Pretty kwenye siti niliyo kalia kwa utaalamu mkubwa pasipo kupunguza mwendo kasi wa gari, nikarukia siti ya nyuma. Nikalichunguza gari hili vizuri, jinsi linavyo kuja kwa kasi nyuma yetu. Nikafungua mlango wa nyuma
"Eddy unataka kufanya nini!?"
"Nahitaji kwenda juu ya hari hili"
"Umechanganyikiwa wewe?"
"Punguza mwendo"
"Alafu si tutakufa?"
"Nahitaji uwe sawa na hili gari"
"Nini?"
"Fanya hivyo"
Pretty akageuka nakunitazama kwa macho yamshangao.
"Funga mlango"
Nikafanya alivyo hitaji, akafunga breki za gari, kisha akakanyaga breki za gafla huju akilkgeuza kwa mtindo wa kuchora duara, jambo lililo mchanganya dereva wa gari la majambazi hao, Akajitahidi kulikwepa gari letu, linalo endelea kuzunguka huku lilichora duara.
Tukalishuhudia gari hilo likitoks barabarani, na kulivas jiwe kubwa lililopo pembezoni mwa barabara, na kulipelekea gari hilo kubinuka nakuanza kubingiria. Pretty akaluweka sawa gari na kuelekea lilipo gari la majambazi hao. Nikashuka kwenye gari haraka, nikamkuta dereva wao akijitahidi kutoka ndani ya gari hilo. Huku akiwa ameumia vibaya usoni mwake.
Nikaiwahi bunduki yake, nikamtwanga risasi mbili za kichwa. Kwa mwendo wa tahadhari nikazunguka nyuma, kulipo na mlango wa kuingilia ndani. Nikaufungua taratibu, watu wote waliomo ndani nikakyta wakiwa katika hali maututi, Nikamvuta John nje, nikamvuta na sheila nje. Nikarudi ndani ya gari hili lililo lala ubavu, naada ya kubingirika zaidi ya mara kumi mfululizo.
Kila aliye kua na hali mbaya nikamsindikaza kwa ridasi kadhaa. Akabaki mmoja akiwa anatetemeka huku akiniomba nisimuue.
"Nani aliye watuma?"
Nilimuuliza huku, mdomo bunduki nikiuelekezea kichwani mwake.
"Ni...Mad......ame Mery"
Alizungumza huku damu zikimtoka mdomin mwake.
"Yupo wapi?"
"Yu..po......"
Hakuimalizia sentensi yake, akakakata roho. Kuhakikisha amekufa nikamtandika risasi yakichwa. Nikatoka nje ya gari na kumkuta Pretty akiwa amesimama pembeni ya miili John na Sheila.
"Wamekufa au?"
'Wapo hai"
"Sasa si uwaue?"
"Bado ninakazi nao"
Nilizungumza huku nikikagua moja ya bastola niliyo ichomoa kwa majambazi walio waua ndani ya gari.
"Kazi gani?"
"Utaiona"
Tukawabeba na kuwaingiza ndani ya gari, Pretty akaniambia kuna nyumba yake, ipo maemdeo ya karibu ya msitu wa Amazoni. Tukatembea kama kilomita sita hivi, tukafika kwenye ntumba yake iliyopo juu ya mlima. Manzari yake nimazuri sans, na ninyumba iliyo jengwa kwa ustadi vizurii na inagorofa moja kwenda juu.
"Hapa ni kwako kweli?"
"Ndio"
Tumawaingiza ndani, John na Sheila ambao hadi sasa hivi hawajitambui na sura zao zimejaa damu. Nikawajalisha kila mmoja kwenye kiti chake, huku nikiwa nimuwavua nguo na kubakiwa na nguo za ndani. Kila mmoja nikamfunga kwa kamba gumu ya manila.
"Unakwenda kuwafanyaje?"
Pretty aliniuliza baada ya kulimaliza zoezi langu, nililo kuwa nimelifanya.
"Utaona, hadi asubuhi watakuwa wamesha zinduka. Tukatoka ndani ya chumba tulicho waingiza John na Sheila.
"Unahitaji kinywaji?"
"Ndio"
Pretty akafungua, friji na kutoa mzinga wa pombe kali akaja nao kwenye sofa nililo kalia, huku nikitazama taarifa ya habari, kukua nini kunacho endelea katika nchi hii, hususani mwa tukio la leo.
"Hawajatujua"
Pretty alizungumza baada ya kutazama taarifa hiyo kwa muda kidogo.
"Nahisi"
"Hivi umejifunza wapi kuendesha gari?"
"Sijajifunza popote, kikubwa ni kujituma"
Pretty akanitazama usoni mwangu, akapiga fumba moja la pombe kali, kisha akanivutia kwake na kuanza kuninyonya mdomo
"Pretty stop, nina mke"
Nilizungumza huku nikimzuia kuendelea kufanya anacho kifanya
"Mmmm samahani Eddy"
Pretty alizungumza kwa aibu, huku akiyakwepesha macho yake na yangu yasikutane kwa pamoja.
"Usijali"
Hatukulala hadi, kuna pambazuka. Nikawa wa kwanza kuingia kwenye chumba walichopo John na Sheila. Nikawakuta wakiwa wamezinduka, huku wakiwa hawaelewi wamefikaje hapa.
"Henry rafiki yangu asante sana kwa kuja"
John alizungumza baada ya kuniona nikiwa nimesimama mbele yao.
"Pole, jana nikaona harusi imevurugika?"
"Ndio kaka yaani sijui ni mshenzi gani aliye fanya hivi? Tufungue basi kaka"
"Nitawafungua, ila nimemuoji mmoja akadai ni Madam Mery, ndio amewatuma sijui unamjua huyo?"
John akakaa kimya akionekana kumfikiria mtu niliye mtajia
"Ahaaas ndio ninamjus huyu mama ni mshenzi sana, ila nifungue kaka tuondoke nitakuadisia mbele ya safari"
"Usalama hapa upo mzuri tu. Wala usijali ndugu"
"Shem tufungue jamani"
Sheila alizungumza huku akimwagika na machozi.
"Usijali shem, Pretty anaanda vifaa vya kusafisha majeraja yenu"
"Huyo madam, anataka nini kutoka kwako?"
"Anataka mali zake"
Nilimuoji John katika hali ya upole, pasipo kumfanya astuke kwamva mimi ni nani.
"Mali gani?"
John akamtazama, Sheila kisha akanitazama na mimi.
"Kuna jamaa, tulipanga sote wawili tumuangamize tuchukue mali za bana yake sasa, sijamrudishia ndio maana ameamua kuanza vita na mimi. Haki ya Mungu nitamuua huyu mwanamke wee ngoja niwe sawa. Na yeye ndio aliye tuzalilisha kanisani"
"Ahaaaaa, pole sana kaka. Huyo jamaa anaitwa nani?"
"Huyo niliye mchukulia mali?"
"Ndio"
"Ndio kama huyu"
Nilizungumza huku nikiibabadua sura yangu ya bandia, hadi ikatoka yote na kubaki na sura halisi. John na Sheila wakabaki wakiwa wame nitumbulia mimacho. Mwili mzima wa John ukaanza kutetemeka, hadi mkojo ukaanza kulowanisha boxer yake na kutapakaa chini.
"Eddy kuna....."
Pretty alinyamaza baada ya kuingia ndani ya chumba hichi, na kunikuta nikiwa na sura yangu halisi. Pretty akapiga hatua hadi nilipo huku akiwa amebeba sinia kubwa lenye vitu vyenye makali mengi, kama kisu na vifaa vya oparesheni vitumikavyo hospitalini. Huku mkono wake mwengine akiwa ameshika bomu lakutega.
"Pretty...!!!"
Sheila aliita huku akimshangaa, Ptetty aliye simama mbele yao.
"Haya wewe kidume kizima kujikojolea humu ndani ni nini?"
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUTUMIA AKAUNTI YAKO YA FACEBOOK, LIKE UKURASA HUU USIPITWE NA SIMULIZI NA MENGINE HUKO FACEBOOK
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII KAMA MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA
KWA TELEGRAM👇BONYEZA HAPA