
SEHEMU YA TISINI NA SITA
ILIPOISHIA...
Mama alumuambia fereva wake, akawasiliana na wezake waliopo kwenye gari moja ya mbele na nyingine gari moja lililopo nyuma yetu. Msafara ukabadilika kama alivyo sema mama, tukafika serena Hotel, nakupokelewa na wahudumu. Tukatafuta sehemu iliyo tulia na kaa mimi na mama, hata mlizi wake, wa kike aliamua kukaa mbali kidogo na ilipo meza yetu, asisikie tunacho kizungumza.NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
"Heee una lipi la kuzungumza?"
"Mama, ninaamini kwamba nilisha wahi kukukosea mimi kama mwanao wa pekee."
"Ila uliweza kunisamehee, kwani mtoto kwa mama, hua akui. Kama tunavyo sema sisi waswahili"
"Ndio mwanangu, nalitambua hilo"
"MÃ ma, kunakitu ninahitaji nikuombe?"
"Omba tu mwanangu, usipo niomba wewe ni nani atakaye niomba mwengine"
Nikashusha pumzi tataribu, huku nikitazama chini, kwani hata ujasiri wa kumtazama mama, machoni ulinipotea gafla.
"Mama...."
"Mmmm"
Nikajikuta nikishusha pumzii kwa nguvu. Kila nilicho taka kukizungumza kikanipotea gafla kichwani mwanfu, nikajikuta nikibaki.
"Zungumza mbona umekaa kimya?"
"Nilitaka kukuambia kua...."
"Kua nina kupenda sana mama yangu. Upendo wangu sijawahi kuweka bayana kwako. Mama yangu wewe ni mfano mzurikwenye maisha yangu
Hakuna mama kama wewe"
Maneno yangu, yakapelekea hadi mama kulengwa lengwa na machozi.
"Nakupenda pia mwanangu, nipo tayari kuupoteza utajiri wañgu, ila si wewe mwanangu"
"Japo wamama wengi, hawapendi kuwaomba misamaha watoto wao, ila kwangu nitofauti."
"Eddy mwanangi, ninakuomba unisamehe"
"Nikusamehe kwa kipi mama?"
Mama akajifuta machozi kwa kitambaa, chake. Akavichukua viganja vyangu, na kuvikutanisha kwa pamoja.
"Najua matatizo yote, yaliyo kupata chanzo ni mimi. Niliamua kuzaa na mdogo wa Gidwin kwa ajili ya....."
"No mama, hlo nilisha kusamehe, siku nyingi. Haikuwa kisa lako kufanya vile, pia nashukuru kwakuzaa na baba yangu, ila si godwin"
Mama akakaa kimya, hakutarajia kama nitazungumza kitu kama hicho. Kabla hatujazumgumza, simu yangu ikaita, nikaitoa mfukoni na kukuta Sheila ndio anaye piga.
"Mume"
"Mmm"
"Mumefikia wapi?"
"Tupi Serena"
"Na nani upo?"
"Kwani nyumbani, nilitoka na nani?"
”Mama"
"Sasa inakuaje, unauliza kwamba nipo na nani?"
"Samahani mume wangu, kama nimefanya kosa"
"Poa"
"Piga picha unitumie whatsapp, nimekumis mume wangu"
"Poa"
"Jamani Eddy, mbona unanijibu kihasira, kuna kitu nimekuudhi?"
"Hujaniudhi, ngoja nitakupigia"
"Nitumie basi picha sasa hivi, ukiwa na ma.."
Nikakata simu, kabla hata Sheila hajamalizia, sentensi yake
"Mbona unamjibu mwenzako kihasira?"
"Hapana mama, yeye anataka picha ya eneo nililopo, naona ananisumbua"
"Ndio lazima akusumbue, kutoana na mimba aliyo ibeba. Na mwamke akiwa katika kipindi hicho usidhubutu kumuudhi, anaweza kuchukua maamuzi ua ajabu, baadaye ukaja kujutia"
"Nimekuelewa mama"
"Lete, simu yako nikupige picha umtumie"
Nikampa mama simu, akanza kunipiga picha, kadhaa
"Tayari?"
Nilimuuliza mama
"Ndio ngoja nizitazame kama, umetokelezea"
Nikajikuta nikicheka kwani, sikujua kama mama naye anayatambua maneno ya vijana, kama kutokelezea. Nikaiona sura ya mama, ikibadilika taratibu, huku mikonjo kadhaa ikiwa kwenye uso wake.
"Huyu nani?"
"Ahaaa... huyo ni, ni, ni n......."
"Nani?"
Rafiki yangu"
Nilijibu kwa kubabaika sana, mama akanitazama kwa macho makali sana, usoni mwangu.
"Huyu mtoto?"
"Eheee"
"Hujanisikia vizuri au?"
Mama aliniuliza kwa sauti ya ukali, nikajikuta nikikosa cha kujibu.
"Mam..."
"Huyu ni nani kwako?"
"Mama huyo ni Junio"
"Eddy ni ujinga gani umefanya, unazaa na hawa magaidi, Unataka ulipuliwe na mabomu ehee?"
Mama alipo zungumzia swala la julipuka kwa mabomu, moyo wangu ukanza kunienda mbio, kiasi cha kumbukumbu kadhaa za ndoto niliyo iota ndani gari ikanijia kichwani mwangu, kama mkanda wa filamu.
"Eddy, laiti ungejua, binadamu ninao wachukia ni huo waarabu"
"Hivi unawaju vizuri kweli wewe?"
"Ila mama..."
"Edddy hakuna cha ila hapa, kwa nini hujasema, kwba una mwanamke umezaa naye?"
"Mama ninakuomba, utulize jazba, nataka nikuelezee kila kitu juu ya huyo msichana"
"Kwanza ni mtu wa nchi gani?"
"Iraque"
"Mungu wangu, Eddy mwanangu umeingia pabaya"
"Maa sio pabaya ninampenda sana huyo mwanake ni mama wa mwana....."
Kibao kikali kikatua shavuni mwangu, kitendo kilicho mganya hadi mlinzi wa mama akastuka.
"Funga bakuli lako, mbwa wewee. Habari ni hii, simtambui huyo malaya wako wa kiarabu, na wala sikitambui hicho kingurue chako.Ninaye mtambua ni Sheila tuu na mjukuu wangu ajaye."
Mama alizungumza kwa hasira, huku machozi yakimtiririka mashavuni mwake
"Mama, mwanamgu ni ngurue?"
"Kama ulivyo sikia"
Mama akanyanyuka, na kuanza kuondoka huku akitazama chini, ili watuwasiguñdue kwamba analia.
"Mama sinto muoa Sheilaa"
Nilizunguza kwa sauti ya juu, iliyo mfanya mana kugeuka kwa hasira na kurudi nilipo simama
"KAMA MIMI SIJAKUWEKA, TUMBONI MWAÑGU MIEZI TISA, HUTO MUOA SHEILA, ILA KAMA NILIKUZA KWA UCHUNGU, BASI UTAMUOÀ SHEILA."
"HICHO KIBESI CHAKO WAPANDISHIE HAO WASICHANA WAKO, ILA SI MIMI MAMA YAKO. USIPO ANGALIA NITAMPOTEZA HUYO MBWA WAKO NA KITOTO CHAKE"
Mama alizungumza na kupiga hatua tatu mbele akanigeukia na kwaishara ya kidole chake, akaniamrisha nitangulie kwenye gari, huku yeye na mlinzi wake wakifwatia nyuma.
Katika siku ambayo nimejisikia vibaya ndani ya moyo wangu ni siku ya leo, sikutegemea kama mama yangu anaweza kumkataa mwanangu mbele yangu japo sijamuona, ila muonekano wa kwenye picha una dhihirisha kwamba Junio ni mwanangu wa damu. Kila nilipo mtazama aliye keti, pembeni ya siti yangu. Moyo ukazidi kuniuma, kiasi cha kutamani nishuke ndani ya gari, nitembee hata kwa miguu kurudi nyumbani.
Tukaafika nyumbani nikawa wa kwanza kushuka ndani ya gari. Sikuelea chumbani kwangu kuepusha kelele za Sheila, ambaye muda wote, mama anamchukulia Sheila kama mtoto mdogo. Chochote anacho kihitaji anakipata.
"Shem, mbona umekaa huku bustanini, peke yako”
Sauti ya ndugu wa Sheila anaye itwa Blanka, niliisikia ikinisemesha, nyuma yangu
"Hapana nina punga punga upepo"
"Ahaaa, basi nilijua kwamba hjarudi na mama"
"Nimerudi"
Blanka akakaa pembeni yangu, huku akivua viatu vyake na kuvisogeza pembeni
"Shem mbona kama, haupo sawa, unaumwa?"
Nikatingisha kichwa kumjibu Blanka
"Sasa n nini tatizo shem wangu? Sasa hivi ulitakiwa uwe ndani unafuraha"
"Hapana, nina furaha"
"Shem huna furaha, au dada amekudhi?"
"Hapana, kuna maswala yangu yakibiashara kidogo ndio ninayafikiria"
"Ahaaaa, ila shem kuna kitu nahitaji kukuuliza"
"Kitu gani?"
"Unampenda kweli dada Sheila?"
Ikabidi nimtazame Blank vizuri machoni mwake.
"Mbona umeniuliza hivyo?"
"Yaa nà hitaji kujua, kwa maana kuna vitu hapa nyuma vilikua vinaendelea"
"Sijakuelewa, vitu gani vilikua vinaendelea?"
"Kuna mambo alikua anayafanya dada Sheila, kwa upande wangu sijayapenda isitoshe anakwenda kufunga ndoa na wewe, sizani kama anastahili kua mkeo"
Moyo ukaanza kunienda mbio, nikamgeukia vizuri Blanka, kabla sijamuuliza kitu, nikamuona mama akija sehemu tulipo.
"Ina bidi uongeze juhudi kwenye masomo, isitoshe unasoma masomo ya udaktari, ujitahidi sana"
Ilinibidi kubadilisha mada, ili mama asielewe ni kitu gani tunazungumza. Chakumshukuru Mungu Blanka alinielewa maana yangu ya kubadili mada tuliyo kua tukiizungumza.
"B wezako wanakutafuta kule ndani"
"Ahaa sawa mama"
Blanka akanyanyuka na kuondoka, mama akakaa sehemu nilipo. Ukimya wa sekunde kadhaa ukakatiza, sikua na kitu cha kuzungumza.
"Hivi Eddy, ni nani aliye kuroga?"
"Hakuna"
"Nimempigia mchungaji simu, aje kukuombea"
"Ili iweje"
"Eddy wewe si bure, utakua umerogwa"
"Mama na elimu yako hiyo yote yaani una amini kwamba mimi nimerogwa?"
"Tena sana, na aliye kuroga amesha fariki"
Laiti kama añgekua si mama yangu, aliye nibeba tumboni mwake miezi tisa, ningemtandika ngumi, ambayo asinge isahau maisha yake yote.
"Na kama nilivyo kuambia, mtoto uliye naye mimi simtambui, na huyo mama yake naye simtambui. Sasa ole wako unidhalilishe kwa wageni nilio waalika. Haki ya Mungu naapa nitakuachia laana."
Mamà akanyanyuka, nakujifunga tenge lake vizuri.
"Na sitaki siku hata moja huyo mwanangu Sheila ajue, kwamba unamtoto. Akijua na kuchukua maamuzi mabaya utajuta"
Mama à kaondoka na kuniacha nikibaki nikimsindikiza kwa macho, yaliyo jaa hasira.
Kitu kilicho anza kuniumiza kichwa, nikuhitaji kujua ni mambo gani aliyo kua akiyafanya Sheila, kipindi ambacho mimi sikuwwepo. Nikaanza kuamini kwamba Blanka atakua ni msaada mkubwa sana kwangu.
Usiku sikuamini kumuona mchungaji akiwa ameketi kwenye sofa za sebleni, akizungumza na mama. Wakaniita, nikajumuika nao kwenye mazungumzo, mimi na mchungaji tukaingia kwenye chumba cha maombi, kilichopo ndani ya hili jumba jipya la mama.
Bila hata mchungaji kuniuliza swali, lolote akaanza kuniombea huku akiuweka mkono wake juu ya kichwa changu
"Pepo mchafu uliyopo ndani ya kichwa cha huyu kijana toka kwà jina la Yesu kristo"
Mchungaji aliendelea kuniombea huku akinisukuma sukuma kichwa changu. Zaidi ya nusu saa mchungaji aliendelea kunisalia
”Mchungaji, nimechoka kupiga magoti kama mapepo sina si tuachane na hii biashara bwana"
"Ohhhh shagara bagharaa, pepo wewe mchafu huwezi jibizana na mimi mtu wa Mungu, hapo ulipo toka kwa jina la Yesu"
"Mchungaji tuheshimiane bwana, sina pepo wala nini. Hembu fanya jengine la maana"
"Pepo pepo mchafu tokaaaaaa"
Nikaona mchungaji hanielewi, nikasimama, akabaki kunitazama machoni mwangu, huku akizungumza maneno, nisiyo yaelewa.
”Nisikilize mchungaji, nahisi huyo Mungu iyepo ndani yako sidhani kama ni Mungu huyu tunaye muabudu. Hembu rudi ulipo toka kasime vizuri hiyo biblia yako uje tena kuniombea. Matatizo yaliyopo hapa ni kati yangu mimi na mama yangu sawa?"
Nilizungumza kwa sauti ya ukali na yachini, jambo lililo mfanya mchungaji kunitumbulia mimacho. Nikafungua mlango na kwenda chumbani kwangu, na kulala.
Asubuhi na mapema, nikaamka. Nikafanya mazoezi kama kawaida yangu, nikaenda kwenye nyumba wanayo ishi watoto wa kike, na ndipo anapo kaa Sheila, nilitenganishwa nà ye ili nisimuone hadi siku ya harusi yetu. Nikamtafuta Blanka ila sikumuona
"B amekweñda wapi?"
"Wametoka na bibi harusi, leo wamekwenda saloon kuanza kupambwa"
"Saloon gani?"
"Labda mpigie wifi mwenyewe umuulize"
Nikaachana na mdogo wangu, ambaye nilitambulishwa sikujua hata ametokea wapi, ila wote ni ndugu. Nikampigia simu Sheila ila haikupatikana, nikajaribu kupiga simu ya Blanka ñayo haikupatikana. Nikajaribu kupiga ya ndugu mwengine niliye hisi atakua mpambe kwenye msafara huo, simu yake ikaita baada ya muda akaipokea
"Dada upo na hao maarusi?"
"Ndio, tupo Saloon moja inaitwa Rich Power Women au R.P.W"
"Ipo wapi?"
"MÃ eneo ya huku posta"
Akanielekeza walipo, akanieleza simu za Sheila na Blanka, zimezima chaji.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com