MAHABA NIUE (39)
Zephiline F Ezekiel
6 min read
SEHEMU YA THELATHINI NA TISA
ILIPOISHIA...
Wote walitoka nje na kumuomba lOydah apunguze jazba kwani ana lotaka kuli fanyab lina takiwa umakini wa hali ya juu sana, vinginevyo wana weza waka mkosa huyo mtu na kumpelekea akabadili namba.
KABLA HATUJAENDELEA NIOMBE BURUDIKA NA VIDEO HII
SASA ENDELEA...
"Subiri"!
kway alitoa jibu hilo huku akiweka simu masikioni.
"Yes kamuhanda Willson"!
"naam bwana Kway"
"kuna tatizo kidogo hapa, naweza nika kuona"?
"upo wapi"?
"nipo sayansi"
"wahi haraka, nataka nitoke"
"sawa Wilson"
Baada ya Ramsey kukata simu alimchuka LOydah na kuingia nae ndani ya gari na safari ya kuelekea central kuanza
"huyo ni nani, uliye kuwa unaongea nae"?
"uyo ni IGP wilson Kamuhanda"
"weeee, una fahamiana nae"?
"tena sana, ni rafiki yaangu mkubwa sana!"
"sasa tutaenda kumwambia nini"?
"wewe subiri"
safari ili zidi kuendelea huku kila mtu akiwa kimnya,
baada ya kufika waliingia na kuomba waonane na IGP moja kwa moja walipita ndani ya ofisi hiyo na kukutana na mkuu wa kituo huyo Wilson Kamuhanda, baada ya kutoa maelezo yake,
zili tolewa Deffender mbili na kazi moja tu kuanza kumtafuta Abdul , ambapo baada ya kuingia katika mitambo yao waliweza kumuona alipo wakitumia kifaa maalumu cha GPRS ,shukrani ya Loydah kumpa Kway haikuelezeka,
******
Majibu ya Don CHuwa kuwa mbwa wake ana umwa yali mkera sana Mr, Mwasha kupita maelezo,
"hakuna jibwa lingine"?
"hakuna Mwasha, ila subiri mpaka kesho hivi, nita kua tayari nime kupa jibu"
"okay!."
Mr, mwasha alisogea karibu ya RAmsey na kumpiga na kitako cha bunduki cha kichwa na kumfanya damu zianze kumtoka tena sababu alimtonesha kidonda usoni ambacho, kilianza kuka uka. alimuangalia bila huruma alichukua chupa iliyo kuwa mezani na kumpiga nayo kichwani na kumpasukia kichwani na kufanya damu zizidi kutapakaa juu ya malu malu,kweli mwasha likua na hasira sana, na kufanya mwili wake uanze kutetemeka sana, na kufanya macho yake yawe mekundu, kweli hakuwa yeye wakati, zili kua ni hasira mbaya sana, ambazo zakuweza kuelezeka hata kidogo!
alimshika na kumpiga kichwa cha puani na kumfanya Ramsey aanze kuvuja tena damu puani,
maumivu aliyo kua akisikia Ramsey hakuwahi kuya sikia tangu azaliwe, hakuwahi kuyasikia wala kuota, kweli alistaili kufa ili pengine apumzike kutokana na kipigo kikali anacho pigwa.
Roho ya huruma ili muingia Josephine pale alipo alikuwa akilia machozi , hakuwahi kuumia roho kama siku hiyo,
hakuwahi kulia kama siku iyo, alihisi moyo una muuma sana, alitamani amvae mume wake ampige ila hakuwa na uwezo huo hata mara moja, alibaki tuu akibubujikwa na machozi, na kufanya kifua kizima kiloe machozi na lowanisha nguo yake ya juuu, yalikua ni machozi ya uchungu kupita kiasi,
"hivi sija kwambia kwanini na kupiga Ramsey, subiri"!
Mr, mwasha aliingia chumbani na baadae kurudi na baasha ya kaki ambapo aliifungua na kutoa picha wakiwa na jOsephine, wame kombatiana ki mahaba,,
japo kuwa alikua haoni vizuri kwa mbali aliweza kuta mbua zile picha., picha ya Doreen wakiwa wote kitandani inaanza kuji jenga kama mkanda wa filamu na kuanza kukumbuka maneno yake , hakuelewa zili mfikia vipi mr,
mwasha, alijiuliza maswali kichwani ila alishindwa kupata jibu kamili, licha ya kufiikria hayo yote hakujipa tena matumaini ya kuishi duniani alijua kifo ndo kina kuja na wala sio kitu kingine chochote kile, na kuamini kuwa muda
mfupi angeenda kuungana na Doreen huko alipo na kuanzisha tena mapenzi mengine, hilo ndilo alilowaza kichwani mwake.
na kuji kuta tena akilia machozi,
"una lia nini sasa KIDUME mzima"?
aliulza Mwasha huku akitupa baasha ile juu ya meza ya kioo.
"okay, machozi yako haya tazuia kifo chako, nisikilize. mimi ni mtu wa watu,izi picha , nili pewa na mume wake Doreen, , HAKutaka kuku bali kuona ushenzi ushenzi una fanyika, lakini pia izi picha zili kutwa ndani ya kabati la Marehemu Doreen mke wake, Mungu ailaze mahali pema peponi roho yake, ina elekea kuna mambo mengi sana alitaka kuniambia, ila namimi nita fanya juu chini nijue hao majambazi walimfanyia huo unyama wa kumuuwa."
kwa mara ya kwanza Josephine kusikia kuwa picha zile zilikua kwa Doreen,aliingiwa na wasi wasi sana kusikia maneno yale kutoka kwa mume wake, alimtazama RAmsey na kuta mani
kuongea kitu ila alikaa kimnya, hakujua kwanini Doreen alimpiga zile picha na kumkumbuka mpiga picha aliye kuwa akiwa piga picha bichi, hakuelewa kwanini doreen alifanya kitendo kile, ila alielewa si kingine bali ni wivu wa mapenzi, ila kwa upande mwingine alifurahi sana na
kujiona mshindi kwa kitendo cha kumtumia watu wamuuwe,
Kwa Ramsey alijua vizuri zile picha alijua kila kitu na kuanza kujilaumu kwanini hata haku zichukua ile siku,
"Naaa....ombbaaa niiuuuue"
"uta kufa tuu, hilo usiombe, wewe jihesabie ni mfu,Abubakari niletee lile kopo la spirit kule stoo, au ukikosa leta ile chupa ya VALUER"
baaada ya dakika chache ili letwa chupa ya valuer pamoja na spirit na kumiminiwa Ramsey juu ya mwili wake ambao ulikua na vidonda donda, kelele nyingi zili sikika, hakika alisikia maumivu makali sana, alihisi kama mwili wake unakatwa katwa na viwembe, alipiga kelele nyingi, ila ili kua kama wana chochea moto, sababu Mwasha alizidi kumimina spirit ile juu ya mwili wa Ramsey, huku nyingine akimwagia machoni,
kopo la Spirit lilivyoisha alichukua chupa ya Valuer na kuanza kumimina tena, yalikuwa ni zaidi ya mateso ambayo bina damu yoyote yule ange omba aionje mauti, yaani afe aepukane na kikombe kile,
"grriiii griiii"
ili kua ni simu ya mwasha iikiita aliitoa mfukoni na kuiweka sikioni ambapo anaambiwa kuwa kuna dharura ivyo ana hitajika mara moja,
Ramsey alirudishwa stoo na kufungwa kamba, Josephine alizidi kulia sana, asijue la kufanya.
baadae kidogo alihisi mlango una gongwa hakutaka kuamini baada ya kumuona Abdul akiwa mlangoni alimfungulia mlango haraka haraka,
"MAMa mbona kimnya, hupatikani, ile pesa vipi sasa"?
"nita kumalizieni sasa hivi nina matatizo sana, kwanza naomba nisaidie na simu yako"
"subiri kwanza, kazi yako tume ifanya tayari, mtu uliye taka tumuuwe tayari kesha kufa, si nili kwambia mimi mtu wa kazi, piga mapanga sana,"
"nisaidie simu yako kwanza"
Maneno yale yalipenya moja kwa moja ndani ya ngoma za masikio ya RAmsey, tena kwa mbali sana akiwa stoo, sauti ile haikuwa ngeni kwake, alizidi kujiuliza maswali mengi, ila hakutaka kujiuliza sana sababu haya toweza kumsaidia kutokana na kifo ambacho alijua kita fuata muda mfupi,
"shika hiyo hapo"
Abdul alitoa simu yake na kumkabidhi Josephine, alikimbia moja kwa moja stoo na kumkuta Ramsey akiwa hana nguvu hata kidogo.
"Ram, Rammsey baba, taja namba yoyote una yo ijua kichwani"
JOsephine aliongea huku akimpiga piga Ramsey mashavuni ili aweze kumzindua.
"Lo..yydddaaah. m,,pig,,iie Loooydah dada nipe niongee nae kwa mara. yayaya mwiiii sho nimwambie nakuf,,,a"
Ramsey alitaja namba za LOydah, baada ya kufunguliwa kamba kwa kutumia kisu na Josephine, wana ongea machache na simu ile kukata, hakuelewa kwanini ime kata,
"na,,,omba kisu hiko"
"chanini"?
"niipe"
Ramsey alichukua kisu kile kilichokua chini na kuki shika vizuri kwa mikono miwili, huku akikiweka usawa wa tumbo, alishusha pumzi ndefu, na kuanza kuhesabu, hakutaka kuishi tena duniani, alilia sana, aliki vuta kwa juu huku ncha ya kisu hiko kikiwa
usawa wa tumbo, alivyo taka kuji choma josephine alimrukia na wote kudondoka chini na kisu kile kudondoka pembeni.
Hiyo ndiyo nafasi pekee JOsephine aliamini ata itumia kumtorosha Ramsey nayeye kutoroka pia,
alitoka mpaka seblen na kichuma kizito na papo hapo kumpiga nacho Abdul utosini na kumfanya adondoke chini, alimfuata Ramsey na kuanza kumkokota,
tayari giza lili kua limeshatanda , walivyo taka kutumia gari ili watoroke Ramsey alikataa katakata kweli Josephine alizungusha mkono mmoja wa RAmsey juu ya shingo yake, na kuanza kumkokota taratibu, sababu Ramsey hakuwa na nguvu tena.
Licha ya RAmsey kuokolewa ila bado kichwani alitaka kufa tu wala sio kitu kingine, walizidi kutembea na kufika bara bara kubwa ambapo magari yalikua yakienda kasi sana.
RAmsey japo alikua haoni vizuri alipiga hesabu huku akiyaangalia magari yaendayo kasi, Josephine hakuweza kujua nini ana cho fikiria RAmsey kwa wakati ule hata kidogo. alicho jua yeye ni kumtorosha RAmsey waende popote pale, sababu alimpenda sana RAmsey,
Ghafla katika hali ya kushangaza alimsukumiza Josephine pembeni na kuji tupa kati kati ya bara bara,kelele za matairi vikikwaruzana na lami vili sikika. kila mtu alishiika kichwa, wengine walishika midomo yao baada ya kumuona
Ramsey akitupwa hewani kama karatasi, na gari ambalo lili kuwa liki toka kasi sana aina ya NISAAN MURANO, ili kua ni ajali ambayo hakuna aliye amini kuwa Ramsey ata pona, kila mtu alibaki kushangaa na watu kuzidi kuku sanyika
JOsephine akiwa chini aliangua kilio na kukosa nguvu za kusimama aliishuudia Ramsey akitua chini na damu nyingi ziki mtoka, watu wengi walianza kumzunguka, na wezi kaunza kumsachi na mmoja wapo kuchukua simu iliyopo mfukoni mwa RAmsey ambayo ni ya Adul na kutokomea nayo,
Bado msako una zidi kuendelea , hawa kukata tamaa ya kuendelea kumsaka Ramsey ambae waliamini kuwa ame tekwa na watu wasio fahamika watu ambao ni wabaya kivyovyote vile!, bila kujua Ramsey amegongwa na gari na
kuumia vibaya mno, na kupata majeraha pengine yange weza kusababisha kifo chake mara moja!
, hakuna mtu yoyote aliepata taarifa izo, Kway ili bidi amtumie Binamu yake ambae alikua na mkono serikalini na mwenye cheo kikubwa JENNIFER KAUWEDI na jeshi kuzidi mara fudu,
hapo walita futiwa RPC wa mkoa wa Dar es salaam Cosmas MKUMBO, moja kwa moja taarifa za kupotea kwa RAmsey zili anza kuta pakaa katika vyombo vya habari mbali mbli.
mpka magazetini.
kila mtu aliji uliza mara mbili mbili Ramsey ana cheo gani, wengi walidhani wenda ni mbunge, kila kona na pembe ya mkoa ili bandkwa picha yake huku Mkumbo akitoa jeshi lake lingine ili kazi ya kum tafuta RAmsey aliye aminika ametekwa ifanyike mara moja bila kupoteza muda,
"Ramsey bado haja onekana"?
ili kua ni sauti ya Esta akiwa anaangalia habari na ghafla tangazo ilo kupita huku iki ambatana na picha yake
*****
askari walizidi kuifatilia ile simu kwa njia maalumu ya GPRS na kuzidi kuifatilia taratibu sana,
"huyu hapa,, yupo TANDALE Kwa TUMBO"
"lazima leo tumu weke ndani,"
"tuki shuka pale ina bidi , wewe MUdi uende sawa"
"sawa mkuu"
yalikua ni maongezi ya maaskari hao wakiwa ndani ya deffender yao, kweli walifanya kazi iyo kwa hali ya umakini wa juu sana kutokana na vitisho walivyo pewa kutoka ngazi za juu,
na kufanya waanze kuhaha kupita kiasi, huku nyuma kukiwa kuna deffender nyingine kweli ulikuwa msako wa kutisha sana ambapo nyuma ya msako huo kulikua na mkono mkubwa kutoka serikalini ,
USIIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUTUMIA AKAUNTI YAKO YA FACEBOOK, LIKE UKURASA HUU USIPITWE NA SIMULIZI NA MENGINE HUKO FACEBOOK
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni