MAHABA NIUE (42)
Zephiline F Ezekiel
6 min read
SEHEMU YA AROBAINI NA MBILI
ILIPOISHIA...
Kweli wali fanya kazi kwa kuhaha sana wakitumia umakini wa hali ya juu sana, japokua KIKUNDANKYALO, alikua katili ila alimuogopa sana mwasha sababu alikua katili wa chini chini.
KABLA HATUJAENDELEA NIOMBE BURUDIKA NA VIDEO HII
SASA ENDELEA...
"Aisee tukimkosa huku sijui itakuaje!..."
alisika akisema kijana mmoja liyekua akiendesha gari hilo.
"ni lazima tumpate"
KIKUNDANKYALO alisema kwa ghadhabu kubwa huku akitoa mimacho, ilionesha alipania kumuua Ramsey kwani hakutaka kumuangusha bosi wake aliyemuweka mjini.
walifika hospitali hapo na kufanikiwa kumkuta Ramsey aliyekua amelazwa hapo. pia walifanikiwa kumuhonga daktari mmoja aliye waahidi kuwapatia mavazi na vitambulisho vya kidaktari ambavyo vingewawezesha kuingia hospitali kwa urahisi na bila kuulizwa na mtu yeyote.
wakati yule daktari akishughulika na kufoji vyeti vya kumhamisha Ramsey hospitali uroho wa hela ukiwa umemjaa kama fisi ajavyo mate aonapo mzoga, vijana wale walienda kutafuta ambulance ya kukamilishia kazi yao.
"saini fomu hii ya kumhamisha mgonjwa wodi namba 11 kwenda hospitali nyingine"
dokta Godbless aliongea huku akimwekea zile fomu mezani dokta aliyekua zamu usiku ule.
"haiwezekani, huyu mgonjwa ana hali mbaya na haruhusiwi kuhamishwa ndio maana ameletwa hapa"
"hivi unajua unaongea na nani?
nitakuharibia kazi sasa hivi. kama unataka kibarua kisiote nyasi saini hizo fomu, sasa hivi!"
ilibidi dokta Godbless afoke maana aliona dokta yule anamwekea kiwingu na kutaka kumuondolea dili la hela ndefu. baada ya kutishiwa aliogopa na kusaini zile fomu bila kuuliza swali au kitu kingine chochote kile.
"mipango yote ipo tayari njooni mchukue mzigo wenu, "
alisikika akiongea dokta Godbless kwenye simu. baada ya dakika ishirini KIKUNDANKYALO alifika hospitali pale, na vijana wake, akiwa na ambulance,
walipewa makoti ya hospitali na vitambulisho vya madaktari huku wakielekezwa alipokua amelazwa Ramsey. walimchukua Ramsey huku akiwa hajielewi kwani fahamu zake zilikatika kipindi alipopata ajali. moja kwa moja
kweli hakua ana elewa lolote lina loendelea duniani, laiti angeelewa wenda angekurupuka na kutoa mbio ndefu.
walimwingiza kwenye ambulance hiyo huku ikitoa mlio kuashiria kuwa wana dharura na kuondoka hospitalini hapo kwa spidi ya ajabu kuelekea kusikojulikana ili kumtokomeza kabisa Ramsey.
kweli wali panga kumuaa.
"si tumkabe na mto tu huyuu, maana hawezi hata kupigana ni kama mfu"
kijana aliyekaa kilipo kichwa cha Ramsey alisema kwa majigambo makubwa. wote walikubaliana na kuamua wafanye hivyo, baada ya kuchukua mto huku akijiandaa kumkaba nao juu ya mdomo na pua .
ghafla mbwa alionekana akikatiza barabara mbele ya gari ambapo ilisababisha gari lile kupoteza uelekeo...........
“Kobelo huyo bado hajataka kusema kitu chochote kile?”
Rpc MKUMBO aliuliza baada ya kupita maabusu pale na kumuona Mwasha anavyo pokea mateso ya kipigo kikali lakini bado hakuwa tayari kufungua mdomo wake kuongea chochote kile,ilibidi RPC Mkumbo aingie ndani ya maabusu
na kumuangalia Mwasha ambae bado alionesha sura ya kutotoa jibu lolote lile,
“Mr, naomba ushirikiano wako”
“ushirikiano gani, nisha ongea kila kitu,”
“mwasha nisikilize kwa makini, mkeo kaongea kila kitu, naomba nijibu swali langu moja tu, RAMSEY yuko wapi?”
“mimi sijui, mkamuulize huyo huyo, na nina muhitaji mwana sharia wangu, sitoongea chochote kile”
“okay”!
Rpc Mkumbo alitoka nje na baadae kurudi akiwa amekasirika sana sura yake ili onesha dhahiri kuwa ameka sirika sana , kweli alitaka kujua Ramsey alipo kwa wakati ule na wala si vinginevyo, maana vitisho vilizidi kutoka kwa JENNIFER KAUWEDI kutoka serikalini akipigwa mikwara kuwa endapo hawa to mpata Ramsey ita pelekea yeye
kushushwa cheo, alirudi ndani ya maabusu ile na kumvuta Mwasha akitupia nguvu nyingi.
“uta niambia tu,, nasema hivi uta niambia kile nacho taka kujua.
“kobelo, niletee huyu mtu ofisini kwagu”
Msobe msobe Mwasha aliinuliwa na kuingizwa ndani ya ofisi ya Rpc Mkumbo, ambapo pembeni ya ofisi iyo kulikua na chumba kidogo sana, moja kwa moja alitupwa humo ndani.
Muonekano wa chumba kile ulimfanya jasho jembamba lianze kumtoka, aliona pembeni yake kuna kiti cha umeme, alivyoangalia juu ya meza aliona nyundo, visu vidogo, na viwembe alikadhalika na vitu vingine vyenye ncha kali sana, alijua kivyovyote vile ana enda kupokea mateso makali sana, ila hakuwa tayari kuongea lolote lile aliapa,
Sababu jambo alilokua akisubiri muda mchacche ujao ni kupewa taarifa za kifo cha Ramsey kutoka kwa kijana wake na si vinginevyo, hilo aliamini lita tokea ,
Baadae ana ingia RPC Mkumbo akiwa na mkasi mkononi na kuka pembeni yake.
“una ona ivyo vifaa hapo pembeni yako”?
“nakuuliza una ona ivyo vitu?, hata kama haujibu, napenda kuku hakikishia , utasema, wapo waliiokua wabishi kama wewe, ila waki fika humu , wana sema, usijidanganye hata kidogo”
“mimi sijui chochote”
RPC mkumbo ambae mwenye sifa moja tu ugaidi, kweli alikua gaidi hasa katika swala la kazi yake, hakuwahi kutokea hata mtu mmoja kujaribu kuficha siri endapo ata fika mikononi mwa Mkumbo,
Alimvuta mwasha na kumfunga juu ya kiti cha umeme,
Na kuzungusha switch, na kumfanya Mwasha aanze kupiga kelele za maumivu sana kweli alipiga kelele sana huku jasho likianza kumtoka mwili mzima,
“sema Ramsey yuko wapi”?
“yuyuyupo yuyupo subiri”
“niambie yupo wapi”?
Mkumbo alifoka huku akizidisha kasi ya umeme ule na kumfanya Mwasha azidi kutetemeka, kwa hasira Mkumbo alizidisha tena mpaka mwisho na kufanya mpaka kiti kile kianze kutoa Moshi mwingi sana,
Sana pamoja na mvuke
Ukimnya ulitawala ndani ya chumba hiko Mwasha akiwa ametulia , mateso yale yali mfanya apoteze fahamu zake na kuzirai juu ya kiti kile, aliinuliwa na kulazwa pembeni, Maji ya baridi sana yali letwa na Mwasha kumwa giwa,
“amka amka amka, Ramsey yuko wapi, leo leo utataja KUNGUNI wewe”
“mimi sijui, mara ya mwisho, mara ya mwisho, aaa aaaah”
“una nitania naona”
RPC mkumbo alisimama na kuiendea meza hiyo iliyo kuwa na kila aina vitu vyenye ncha kali, alionekana kuta futa kile ana cho kitaka na kuona KOLEO ya kuka tia vitu vigumu, alimfuata moja kwa moja Mwasha na kufungua mdomo wake,
kwa nguvu sana alimfungua mdomo na kuingiza koleo lile ndani ya mdomo wa Mwasha na kumtoa jino moja la mbele bila ganzi, hakika yalikua ni zaidi ya maumivu sababu alivyo toa koleo, zili ruka na damu nyingi sana kutokea mdomoni
“nita fanya ivyo mpaka meno yote yaishe mdomoni. Ubaki kibogoyo!”
Mr, Mwasha alilia sana huku RPC akizidi kutoa meno yale mdomoni mwa Mwasha tena bila ganzi yoyote ile, hakika hakuna bina damu yoyote angeweza kustahimili mateso yale,
Alijitahidi kukaa kimnya ila aliji kuta uzalendo una mshinda hakika yalikua mateso ambayo hayakua na mwisho hata kidogo.
“KIKUNDIYANKALO,kikiiki kundyankalo”
Mwasha aliongea huku akilia machozi sana akiwa ame fungwa mikono nyuma. Huku damu nyingi zikiwa zina mtoka mdomoni kama mchuzi, RPC mkumbo ili bidi asitishe zoezi lile.
“ndo kilugha gani hiko, una zungumza una nitukana,”?
“kikikikundiyakyalo, ndo ndo nime muagiza, ameniambia Ramsey yyuuuupo st, Theresa,”
“una tudanganya”!
“siwezi kuku danganya afande, siwezi kusema uwongo”
“endelea kusema”
“nili watuma waka muuwe, naomba usiendelee kuni tesa ukweli wangu ndio huo, AFANDE naomba nisamehe mimi, “
Kweli Mwasha alilia kama mtoto siku hiyo, alihisi maumivu ya kifo
Hakuona sababu ya kukaa kimnya na kuendelea kupokea mateso yale kutoka kwa RPC ambaye alionesha hali ya kutokua na masihala wala mzaha hata punje,
“Afande Moza, chukua Deffender. Nenda st, THERESA sasa hivi”
Rpc Mkumbo alitoa agizo hilo huku akitoa simu akiwa pigia Kway na LOYDAH akiwaambia waende st, Theresa huko ndipo Ramsey alikua ana patiwa matibabu, bila kujua tayari Alisha tekwa nyara , kama
ange jua asingesema maneno hayo kutoka mdomoni mwake, upande wa pili Loydah na Kway walionekana kuwa wenye furaha kupita kiasi, na hapo hapo kuanza safari ya kuelekea hospitalini st Theresa iliyo kua nje kidogo na mji wa Dar es salaam,
*********
“para panda italia, paranda, wata kua wame kwisha nyakuliwa, kweeeenda kumlaki bwana yesu mawinguni, … tuonane paradiso, tuo tuonane para disooo, tuonane”
“uwii Ramsey mdogo wangu”
Ili kua ni nyumbani kwa Loydah dada yake na Ramsey, kili kua ni kilio chenye simanzi sana, hakuna hata mmoja aliye kua ana kubali kuwa leo hii Ramsey ame fariki dunia, kili kua ni kilio cha kuuzunisha sana,
Loydah, alilia na kuzimia mara saba, kila akizinduka ana zimia tena, hakika hakutaka kuamini kama leo hii Ramsey
kafariki dunia, alitamani iwe ndoto, alitamani jambo lile liba dilike, ali tamani japo kumuona Ramsey kwa mara ya mwisho, ila alikuwa kasha chelewa, watu walilia sana, hakika Loydah alilia mpaka sura yake ikabadilika rangi, machozi yote yalika uka kabisa.
“Ramseeey mdogoo waaaangu, ume niacha mwenyeweee, ume niacha eeeh Mungu weeee, eeeh Mungu wangu, mrudishe mdogo wangu”
Kway aliye kua pembeni yake wakisaidiana na mume wake Loyda walikua na kazi kubwa sana ya kumbeleza Loydah kwa wakati ule bil,a mafanikio yoyote yale ili kua ndo kama wana chochea azidi kulia, hakika ulikua ni msiba wa kuuzunisha sana, kila kona ya pembe zilisikika sauti za watu wakilia,
Hata Esta pia alikuwepo akilia kama mwenda wazimu, watoto wa kike wengi walilia sana , walilia kwa mengi ndani ya mioyo yao, Monanlisa nae alikuwepo na Fetty hawa kutaka kuamini kama kweli Ramsey katoweka duniani, katoweka kwenye sura ya dunia, hawa tomuona tena, hawa topewa penzi kama la Ramsey tena, hakika walikua na maumivu mioyoni mwao.
Kilikua ni kilio kikubwa sana watu walizidi kufurika katika msiba huo, na kwenda kumpa pole Loydah na kujumuika katika msiba huo.
“Loydah usilie sana, kwani hatuna uhakika kama Ramsey kafa kweli”!
Aliongea Kway huku akijaribu kumfariji Loydah kwa wakati ule
Baaada ya gari lile kuja ribu kukwepa mbwa Yule aliye katiza barabarani, gari lile ambulance
lilionekana kumshinda dereva na kuhama bara bara liki poteza uelekeo na kuingia bondeni ambapo kuliku na korongo kubwa na kuanza
kubiringika kama mpila, mlango wa nyuma wa gari hilo uli funguka na Ramsey kuchomoka juu ya kitanda kile na kutoka nje akiwa hana fahamu yoyote ile, alibiringika akielekea chini kwa kasi na kudondoka juu ya gari kubwa aina ya canter lililo kua lina safirisha magodoro mkoani MOROGORO, alidondoka juu ya magodoro yale bila dereva wa gari lile kujua lolote lile,
Dereva Yule alizidi kuondoa gari bila kujua chochote kitu, baada ya kufika MSAMVU mkoani MOROGORO aliegesha gari ili ashushe magodoro yale, ila nusura akimbie baada ya kumkuta mtu akiwa juu ya magodoro huku akiwa na bandeji nyingi usoni.
USIIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUTUMIA AKAUNTI YAKO YA FACEBOOK, LIKE UKURASA HUU USIPITWE NA SIMULIZI NA MENGINE HUKO FACEBOOK
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni