ROHO MKONONI (2) - CnZ Media

CnZ Media

Jisomee Simulizi Mpya Kila Siku

Jumapili, 3 Julai 2022

ROHO MKONONI (2)

Je unajua kwamba Simulizi zote unazozipata hapa zipo kwenye app ya CnZ Media?

Humo Pia Utakuta:
πŸ“– KUSOMA SIMULIZI
🎬 FILAMU na TAMTHILIA za KITANZANIA
πŸ˜‚ VIDEO za KUCHEKESHA
πŸ“‘ MAKALA za AFYA na MAPENZI

Install app hii GUSA HAPA utavipata vyote hivyo bure kabisa
Mwandishi: Zuberi Maruma

SEHEMU YA PILI
ILIPOISHIA...
...pamoja na watumishi wa pale 'earport' kwa kuwa gari yao awakupaki mbali wakamshtua dereva akaisogeza karibu watuhumiwa wakaingizwa ndani baada ya kunyang'anywa silaha landrover ile ya polisi ikiwa na watuhumiwa ndani ikaanza kutoka uwanja wa ndege huku waandishi wakipiga picha aikujulikana walifika saa ngapi,ila tayari habari zile zilishazagaa...

KABLA HATUJAENDELEA NIOMBE KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media BASI INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI
πŸ‘‰GUSA HAPAπŸ‘ˆ

SASA ENDELEA...
Butu hakiwa ndani ya gari ghafla simu yake ikaita tena kucheki namba ni zile zile '15551' haraka akapokea "vizuri sana afande kwa kazi nzuri,ila nyuma yako kuna gari ilotumwa kuja kuwachukua hao watu inawafatilia kazi iliyopo mbele yao ni kuwashambulia,na siyo hiyo tu hata mbele yenu kuna tipa la mchanga linakuja lengo kuwagonga ikiwezekana kuwaokoa wenzao nanyi mko wachache ivyo yatakiwa mfanye kitu haraka tofauti na ivyo amtofika hata hapo kituoni!

Inspekta wa jeshi la polisi John Butu anapokea simu kwa mtu asiyemjua,mtu huyo alotumia namba maalumu '15551' anampa taharifa za watu wanaoingiza madawa ya kulevya,Butu anaamua kufatilia na kweli anafanikiwa kuwakamata ila wakati wakiwa njiani wanarudi kutoka uwanja wa ndege mtu yule anampigia tena haraka Butu anapokea...

Mtu yule kwanza anampa pongezi kwa kazi nzuri aloifanya,ila pia anamwambia awe makini kwani nyuma kuna gari imetumwa kwa lengo la kuwashambulia,na siyo ivyo tu pia mbele yao kuna tipa la mchanga linakuja kwa lengo la kuwagonga,je unadhani nini kiliendelea?! Tusonge katika sehemu hii ya tatu kujua kitakachojiri....

Inspekta Butu alitoa macho ya mshangao pasina kuamini kile alichokisikia wenzake walimwangalia kwa mantiki ya kumsikiliza nao wajue mwenzao alichoambiwa.

Macho yalipotua kwa wale majamaa watano walionesha kuwa katika matabasamu mazito yamkini pengine walijua mkuu wao ndio atakayekuwa kampigia simu Inspekta yule kumuomba awaachie huru.

"Kwa habari nilizopata ni kwamba tunafatiliwa mbele na nyuma,mbele kuna tipa la mchanga linakuja kwa lengo la kutugonga na nyuma kuna gari linakuja kutushambulia hivyo wekeni silaha zenu tayari ngoja nipige simu makao makuu kuomba msaada zaidi"

Butu aliongea huku akishika simu yake tayari ku mpigia mkuu wake ila kabla ajapiga akapata wazo,ni baada ya kukumbuka mita kadhaa mbele yao kuna matrafki na mmoja wapo wa matrafiki walokuwepo pale ni rafiki yake Hamza

Kijana huyo waliwahi kuwa nae katika mafunzo ya upolisi ila mwishoe huyo rafiki yake wakabadilishwa vitengo,yeye akapelekwa 'ffu' mwenzake akapelekwa askar wa usalama barabarani 'trafki' na kituo chake kilikuwa tu mita kadhaa mbele,haraka akashika simu yake na kumpigia,akisitisha kwanza kumpigia mkuu wake,

"Hamza swahiba naomba uzuie kila tipa la mchanga linalokuja huku mpaka tutakapopita,"

Baada ya maelezo yale hapohapo akakata simu na kumpigia mkuu wake kamishna Nurdin,na kumpa taharifa juu ya taharifa aloipokea,kamishna akamuomba asubiri hapo hapo kando ya barabara anatuma askari wa kutosha wakuja kuwapa msaada!

Mpaka dakika kumi zinakata gari tatu zilizojaza polisi wa kutosha wengine wakining'inia wote wakiwa na silaha zilizojaa risasi za kutosha,mpaka wanawasili hiyo gari ya kuwashambulia ikuwa imewasili,ivyo watu wale wakazidi kuwekwa kwenye ulinzi mkali,safari ikaendelea.

Walipofika pale eneo walipo ma trafki hawakukuta tipa hata moja kwa mantiki hiyo hakukuwa na tipa ilopita,maswali yakajizalisha katika kichwa cha Inspekta yule,je habari alopewa ni ya uongo?!,ah! akutaka kuzidi kujiumiza kwa maswali mengi yasiyo na majibu.

Hatimaye baada ya safari ya takribani dakika 20 waliwasili makao makuu ya jeshi la polisi,hiki ndo kilikuwa kituo cha Inspekta huyu akawaingiza watuhumiwa 'lock up' Kisha akaenda kuonana na mkuu wake kamishna Nurdin na kumjulisha kila kilichotokea

Mkuu wake alimpongeza ila alimuomba afanye mahojiano nao na kila kitu akikamilishe siku hiyo hiyo kusudi siku inayofatia watuhumiwa wafikishwe mahakaman ikiwezelana wahukumiwe siku hiyo hiyo kama sheria ilivyosema akutwaye na madawa ya kulevya lazima afikishwe mahakamani na kuhukumiwa kabla ya masaa 48 kukatika toka kukamatwa kwao,ivyo kwa kuwa muda ule ulikuwa ni saa nane na alihisi njaa alipotoka ofisini kwa mkuu wake akaenda kantini kula,aliposhiba sasa akaelekea ofisini kwake,akamuagiza askari mmoja amletee mtuhumiwa mmoja mmoja ndani kwa ajili ya mahujiano

Wakati hayo yakiendelea nje iliingia gari fulani mpaka maeneo ya maegesho,ikapaki pembeni ya gari ya Inspekta Butu zikapita dakika kadhaa bila mlango kufunguliwa Wala kutoka mtu ndani ya gari ile,ila ghafla mlango ukafunguliwa na kwa haraka akashuka mtu na kuzama chini ya mvungu wa gari ya Butu pasina kuonekana na mtu,hata dakika moja aikuisha hakatoka na kuingia ndani ya gari yake,akapandisha vioo juu,akarudisha gari nyuma na kulitoa,akaelekea kunako geti kutoka ndani ya jengo lile,alishakamilisha kazi alopewa

Mpaka inatimia mida ya kuondoka,watu wale wa tano hapakuwa na alodiriki kufungua mdomo wake kusema mzigo ule wa metumwa na nani,hata baada ya vipigo vikali kutoka kwa askari polisi,bado walikuwa kimya wakicheka tu,ni kama walikula kiapo cha usiri,mwisho Inspekta akaamua tu waachwe wakafie segerea,

Baada ya kutoka katika ofisi ya bosi wake kufikisha ripoti akaingia ndani ya gari yake tayari kuelekea nyumbani sasa akakae na familia yake,kimuonekano alionekana wazi kuchoka,dakika kadhaa alikuwa katika barabara kubwa "double rod" na sasa alikuwa katika foleni kama mjuavyo foleni nyakati za jioni katika barabara kubwa jijini Dar

Wakati akiwa hana hili wala lile ng'afla simu yake ikaita,kuangalia ni namba ngeni '0767433106' haraka akaipokea

"Inspekta John Butu,askari ufanyaye kazi yako vyema,na mwenye uchungu na nchi yako,una watu wangu nakuomba uwaachie kwa usalama wa maisha yako,nakupa dakika moja na sekunde 15 tu piga simu kituoni achia watu wangu na mizigo yangu tofauti na ivyo ohooo tusilaumiane hati!"

Palepale simu ikakata,Butu hakuweza kuongea kitu mdomo ulikuwa mzito,mshangao ulimvaa akabaki kaganda...

'tik,tik,tik,tik,tik'

Ghafla akashtushwa na mlio kama wa saa,

"Huu ni mlio wa bomu rimonti ya kulipulia au kutegua anayo huyo ulo ongea naye,ndani ya dk alizokupa fanya kama ulivyo ombwa tofauti na ivyo sina msaada na wewe"

Ghafla ikasikika sauti ambayo bila shaka ilirekodiwa ikasetiwa ndani ya gari yake akujua iliwekwaje,hakuwa na muda wa kuitafuta,kabla ajafanya kitu gari ya mbele yake ikaanza kuondoka hii ilimaanisha gari za upande wao ziliruhusiwa honi zikaanza kupiga nyuma yake,wazo alilopata haraka ni kufungua mlango na kurukia upande ule mwingine gari zilizo simama nyuma kukafatia mlipuko mkali...

Hakika ilikuwa ni hatari

Kelele zikazagaa,gari ilokuwa nyuma yake aikusalimika kwani moto uliruka,dereva akawahi kutoka...

Hali ya sintofahamu ikazuka,wakati hayo yakiendelea kule alipoangukia Butu simu yake ikaita kucheki namba ni zilezile 0767433106 haraka akapokea ila awakuelewana kutokana na makelele,mtu yule baada ya kuona awakuelewana akatuma sms...

"Butu,ongera kwa kuokoa maisha yako,ila niku ulize je vipi utaweza kuiokoa familia yako?!,una dakika 15 tu za kufikiria uzitumie kwa kupiga simu kituoni watu wangu waachiwe,au uwai nyumban kwako ukaiokoe familia yako,maamuzi yapo mkononi mwako'

SMS ile ikaishia hapo...

Inspekta John Butu anapokea simu kwa mtu asiyemjua,mtu huyo alijitambulisha kama 'Raia mwema' anampa taharifa ya watu kuingia wakitokea nje ya nchi wakiwa pamoja na mihadarati ya madawa ya kulevya....

Butu akishirikiana na Askari wake kadhaa wanaamua kufatilia uwanja wa ndege na kweli wanawakamata ila wakati wakirudi Butu anapigiwa simu na mtu yule yule na kumwambia wanafatiliwa ivyo awe makini....

Hatimaye wanafika kituoni salama Butu anamweleza mkuu wake kila kitu,Nurdin anampongeza ila anamuomba amalize uchunguzi wake siku hiyo hiyo na siku inayofatia watuhumiwa wafikishwe mahakamani.

Mahojiano yanafanyika mpaka jioni washtakiwa awakusema chochote juu ya mkuu wao,Butu anaamua kufunga faili lao akiadhimia kesho kuwafikisha mahakamani wakapate hukumu yao

Wakati akielekea nyumbani anapokea namba ngeni nyingine anapewa dakika moja na sekunde 15 za kupiga simu kituoni na kuwaruhusu wale watuhumiwa tofauti na ivyo hana maisha,mlio wa bomu unasikika Butu anawahi kuruka na gari linalipuka.

Akiwa upande wa pili wa barabara aliporukia ghafla simu yake inaita anapopokea kutokana na makelele wanashindwa kuelewana na upande wa pili,simu inakatwa punde inaingia sms

"Butu,ongera kwa kuokoa maisha yako,ila niku ulize je vipi utaweza kuiokoa familia yako?!,una dakika 15 tu za kufikiria uzitumie kwa kupiga simu kituoni watu wangu waachiwe,au uwai nyumban kwako ukaiokoe familia yako,maamuzi yapo mkononi mwako"

SMS ile ikaishia hapo...

Je unadhani nini kiliendelea?!........

Tusonge kuburudika zaidi...

Inspekta Butu akuamini kile alichokisikia kwa sekunde kadhaa aliganda akiwa katika bumbuwazi,ila ghafla akazinduka na kuanza kukimbia hovyo mara aende mbele mara arudi nyuma,Wakati hakiwa katika hali ya kutojielewa walifika askari kadhaa wakamkamata kwa nguvu na kumzuhia kwani kwa wenge alilolipata angeweza hata kugongwa na magari...

"kuna tatizo gani afande mbona ujatulia mara uende huku mara kule kuna nini alafu mbona wahema ivyo?!"

Mmoja wa maaskari alimuhoji inspekta yule,hata ivyo Butu akujibu kitu zaidi ya kuitazama saa ilokuwa katika simu yake

"Butu,ongera kwa kuokoa maisha yako,ila niku ulize je vipi utaweza kuiokoa familia yako?!,una dakika 15 tu za kufikiria uzitumie kwa kupiga simu kituoni watu wangu waachiwe,au uwai nyumban kwako ukaiokoe familia yako,maamuzi yapo mkononi mwako"

Kumbukumbu ya sms aloisoma dakika chache zilizopita ikajirudia katika akili yake akamwangalia mmoja wa wale askari walomshika

"embu niachieni kwanza"

Butu akaachiwa palepale akabonyeza tarakimu kadhaa za simu yake na kuipachika sikioni...

"Hallow mkuu,nimekoswa koswa na bomu hapa nyerere road,..ndiyo,katika gari yangu,nilipigiwa simu na mtu nisiye mjua akanambia niwa achie wale watuhumiwa huru ndani ya dakika moja na sekunde kumi na tano tofauti na ivyo wataniua alipokata simu tu nikasikia mlio wa bomu nikawahi kuruka,..limeleta mahafa bosi,trafki wapo hapa,wakanipigia tena na kunipongeza kwa kusalimika kifo ila wamenipa tena dakika kumi na tano familia yangu itakuwa hatarini sijui nifanyaje mkuu?!"

Wazo alilopata nikumpigia Kwanza mkuu wake na kumjulisha kila kilichomkuta.

"Hizo namba umeshazituma kwa kpl 001?!"

"Ndiyo mkuu!"

"Ok!,wapigie nyumbani Kwanza ujue wanaendeleaje then uwai utanijulisha kila kitakachoendelea,mi nawasiliana na Kpl 001 kujua huyo mtu ni nani ok?!,"

USIIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUTUMIA AKAUNTI YAKO YA FACEBOOK, LIKE UKURASA HUU USIPITWE NA SIMULIZI NA MENGINE HUKO FACEBOOK

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE TAZAMA VIDEO HII KAMA MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA

KWA TELEGRAMπŸ‘‡BONYEZA HAPA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni