Notifications
  • MY DIARY (34)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA NANETULIPOISHIA...Hapo nikakumbuka kuwa zile zana zangu za kazi nilikuwa nazo ni vile vifaaa vya kupimia ukimwi ambavyo huwa navitumia kabla ya kukutana na mwanaume yeyote nisiyemfahamu. Nikaamua kumkubalia huku nikiamini kuwa hiyo ndo kinga yangu pekee iliyobaki kama mwanaume huyo atataka kuzini na mimi usiku huo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi tuliondoka na kwenda sehemu…
  • MY DIARY (33)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA TATUTULIPOISHIA...Nilikuwa nachanganya staili za kijamaika na hizi za kwetu, sikuacha pia zile za Nigeria hapo nikapata vitu vyangu vya tofauti kabisa. Basi baada ya kujihakikishia kuwa nipofiti kwa mastahili yangu hayo nilisubiri siku ya shindano ifike nikafanye yangu. Siku ya shindano ilifika na mimi nilikuwa miongoni mwa washiriki walioingia tatu bora.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (32)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA MBILITULIPOISHIA...Lakini kuchepuka kwangu na kuingia mgombani haikumaanisha kuwa sheria ingeniacha hivi hivi.Ilifika mahali ikabidi nizime gari na kutulia tulii kusikilizia nini kitafuata.Tayari nilikuwa nimezungukwa na mapolisi ambao walikuwa wakinifuatilia kwa kutumia pikipiki.Kwa bahati nzuri dereva wa lile gari na yeye alishafika hapo na alishawaambia polisi kuwa mimi naugua ukichaa na nilifufuka kutoka mochwari.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA…
  • MY DIARY (31)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA MOJATULIPOISHIA...“marehemu pia alinieleza kuwa ana miliki duka la vitu vya urembo wa kike ambalo pia Leah analisimamia ila hilo apewe mdogo wake Marry ambaye yupo hapa. Mama mdogo huyo mara baada ya kuyasema hayo alikaa zake chini. Baba mdogo ambaye hakurizika na maelezo hayo alisimama na kusema “kwa hiyo kama marehemu alijua kuwa atakufa hivi karibuni kwani nini hakufuata taratibu za kisheria za kuandika wosia na kurithisha mali.IKIWA UNASOMA…
  • MY DIARY (30)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINITULIPOISHIA...Baada ya hapo Nnilimwomba mama mdogo ajikaze na kuwatarifu ndugu wengine habari hizo za msiba.Tulisaidiana hivyo hivyo maana sio siri kila mmoja alikuwa na uchungu sana kutokana na mazingira ya kifo hicho. Habari zilizidi kusambaa kwa kasi na majirani walianza kukusanyika hapo kwa mama mdogo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Msiba ni msiba tu na ukitaka kujua binadamu…
  • MY DIARY (29)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TISATULIPOISHIA...Hapo sasa nikazidi kuchanganyikiwa ikabidi nimuulize mama huyo alikuwa akifanyia shughuli zake za kujipatia kipato sehemu gani.? Yule dada akanambia kuwa anafanyia soko la ndizi huko Korongoni. Sikuwa na jinsi nilimuomba anipeleke lakini na yeye alisita sita kwa madai kuwa alikuwa na kazi nyingi za kufanya na bado anatakiwa ampeleke mtoto shule.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (28)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA NANETULIPOISHIA...Sisi tumesomea mambo haya bhana waliendela kuzungumza wale walinzi huku wakishuka ngazi kwa polepole. Hapo na mimi nikawa nimejifunza kitu kuwa kumbe unaweza kuingia na mtu guest akakuzuru kisha akaondoka zake.Sasa sijui kwenye zile guest zetu za uswahilini kama wanalijua hili.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi nilala japo usingizi ulikuwa hautaki kuja kwa…
  • MY DIARY (27)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA SABATULIPOISHIA...Alinamba eti hayo ya mimi kuolewa tuyaeke pembeni na kwa nini siku hiyo nisilale Moshi tukumbushie enzi zetu. Mwalimu John aliendelea kusema kuwa amenimiss sana na anomba nisahu yaliyopita na turudie yale maisha yetu ya zamani.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilijifanya simwelewi lakini ukweli ni kwamba nyota ya mwanaume huyu ilikuwa ni kali sana zaidi yangu na…
  • MY DIARY (26)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA SITATULIPOISHIA...Joyce alinambia yeye haendi kujipanga foleni kama makahaba wengine hivyo yeye hufanya biashara hiyo kitaalamu zaidi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Alisistiza pia kuwa eti huwa anatumia kinga kuwakinga wengine. Wakati mwingine alinambia acha awaambukize kwa sababu wanaume wangekuwa na akili basi wasingeenda kununua mwanamke. Anasema kuwa laiti biashara hiyo…
  • MY DIARY (25)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TANOTULIPOISHIA...Sikuisha hapo pia nilimpongeza kwa kunijali na kunipenda na kuhakisha kuwa siingii kwenye majanga kama yake mara baada ya kutoka jela. Siku hiyo nilimuelewa sana Joyce na nilikuwa tayari kumsapoti kwa lolote ili mradi tu atimize athma yake hiyo ya kuzaa. Tuliongea mengi sana na baadaye alinionesha picha ya mtu ambaye alitaka kuzaa naye.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…

ROHO MKONONI (1)

Mwandishi: Zuberi Maruma

SEHEMU YA KWANZA
Familia ya afisa wa jeshi la polisi John Butu inaingia katika hatari inayomweka afisa huyo wa jeshi la polisi katika wakati mgumu wa kuipoteza familia yake,sekeseke hilo lilianza baada ya inspekta huyo kupokea simu ya mtu alojitambulisha kama 'raia mwema' na kumpa taharifa za watu waloingiza madawa ya kulevya,kitendo cha yeye kuamua kulivalia njuga swala lile kuna amsha vita kali ambapo anapoamua kuvikimbia anagundua alishachelewa mapema sana.

Ungana na mtunzi mahiri wa riwaya za kijasusi Zuberi Maruma utiririke nayo....

KABLA HATUJAENDELEA NIOMBE KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media BASI INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA👈

SURA YA KWANZA
Alikuwa ni kijana mrefu, mwembamba, maji ya kunde, sura yake ya upole ilipendezeshwa na tabasamu jepesi lililoundwa katika mdomo wake kila mara umtazamapo,alikuwa si muongeaji ila maneno yake machache yalikuwa kivutio masikioni mwa wamsikilizaye kwa kujaa busara,hekima na hata kufuraisha pia kwa utani mwingi...

Huyu ndo John Butu Afisa wa jeshi la polisi aliyekuwa na hari,kasi na nguvu ya kulitumikia taifa lake...

SIKU HII
Alijinyanyua kwenye kiti alichokuwa ameketi mbele ya mkuu wake akampigia saluti ya kumuaga,akageuka na kupiga hatua ndefu kuufata mlango huku akisindikizwa na macho makali ya mkuu wake,akashika kitasa akafungua mlango na kutoka akaelekea moja kwa moja mpaka ilipo gari yake binafsi akafungua mlango na kuzama ndani

Kabla ajawasha gari ghafla akashtushwa na mngurumisho wa simu yake,akasitisha kuwasha gari na kuingiza mkono wake mfukoni akatoa simu yake,akaachia mguno baada ya kuitazama namba ilompigia akakata na kurudisha simu yake mfukoni akawasha gari lake na kuliondoa eneo lile,ila akiwa njiani ghafla simu yake ikawa ikiita tena,hata alipoitazama ni namba zilezile '15551' mwanzo akuzipokea baada ya kuhisi labda ni namba za mtandao,kama si zile za kubashiri michezo,ila kitendo cha kupigiwa sana kikamtia khofu mwisho akaamua kupokea ile simu,huu ukawa ni mwanzo wa safari yake ngumu tena ya kutisha ilo ondoka na furaha yake na kumpa maumivu tele katika moyo wake,bila kusahau kumwachia majuto,..

Sauti alokutana nayo ilikuwa geni katika masikio yake,sauti nzito,ilo ongea kwa kujiamini

"bila shaka naongea na inspekta John butu.."

"yah ndo mimi sijui ni nani mwenzangu?!"

Butu akahoji huku uso wake ukionesha wazi wasiwasi na mashaka tele juu ya simu ile

"hakuna haja ya kulitambua jina langu kwa sasa ila waweza nitambua kama raia mwema,na taharifa nzuri tu kwako"

Kwa kuwa Butu alikuwa katika rafu road haraka akapaki gari yake kusudi amsikilize yule jamaa vizuri...mtu yule baada ya kimya kifupi kusudi maneno yale yasikilizwe vyema na amsikilizaye sasa akaendelea...

"Nina habari ambazo zinaweza kuwa njema kwako,pindi tu utakapoamua kuzifatilia,ila kama utoziamini na uka amua kuzipotezea pia ni juu yako"

Mtu yule baada ya kumaliza kuzungumza maneno yale akaweka tuo,bila shaka ili amsikie mlengwa wake angejibu nini,Butu baada ya kuona anasikilizwa ajibu kitu,basi naye akaona akate ukimya,

"Sawa nakusikiliza ndugu"

"Swadakta,ni kwamba kuna kiasi kikubwa cha mzigo wa unga wa madawa ya kulevya yataingia kesho na ndege ya shirika la ndege la Marekani 'British aerway' utaletwa na vijana wa tano wa kiafrika ambao wote wamevaa suti nyeusi na wamenyoa,vijana hao ushirikiana kwa ukaribu na walinzi pamoja na wakaguzi wa uwanja huo wa DIA,watu hao uwa wakishaweka mzigo yao mashine zote uzimwa hivyo kutowezesha kupiga kelele mara nyingine upeana tu ishara na wakaguzi nao uondoka bila kukaguliwa,ni watu hatari na wenye mbinu zote za mapigano..."

Mtu yule alizidi kumfahamisha inspekta yule na mwisho kukata simu,akiacha kazi kwa Inspekta kuamua kufatilia hiyo kesho au kupuuzia.

Baada ya simu kukatwa Inspekta Butu akawaza kwa sekunde kadhaa,mwisho akawasha gari lake na kuliingiza barabarani kuendelea na safari yake,kuelekea nyumbani.

Ila kichwani mwake alikuwa na maswali mengi sana akijiuliza juu ya mtu yule alojitambulisha kama 'Raia mwema' je habari zile alizo mpa ni za kweli au?!,na kama ni za kweli kwa nini mtu yule amwambie na asitake malipo yoyote?!,akakuna kichwa chake kidogo na kuachia tabasamu jepesi,akajua huyo alompigia pengine ana bifu na mmiliki wa huo mzigo ivyo kaamua kumuunguzia makusudi hili kumtia hasara wazo hili akupingana nalo kabisa,yote kwa yote akutaka kujiumiza sana kufikiria swala hilo,alichoamua ni panapo majaliwa hiyo kesho asbuh aelekee uwanja wa ndege na vijana wake wakaweke mtego...

Inspekta wa Jeshi la polisi John Butu anapokea simu kutoka kwa mtu asiyemfahamu na kumpa habari juu ya kuingia kwa madawa ya kulevya,mtu yule anamwingiza Butu katika mawazo mazito je unahisi nini kiliendelea?

Tusonge katika sehemu hii ya pili kuzidi kutiririka nayo...

Binafsi alijijua kuwa yeye alikuwa ni afisa wa jeshi la polisi ilikuwa ni lazima kufatilia kila habari atakayopewa iwe ya kweli au lah,kwa kujua ilo akajua kesho lazima atakuwa na kibarua kizito...

Akaliwasha gari lake na kuliingiza barabarani,ulikuwa kama ni mwendo wa dakika 15 ulomfikisha nje ya jumba lake la kifahari maeneo ya Tmk Vetenary.

Alipiga honi mara moja kisha geti likafunguliwa na kijana alovaa nguo za mgambo huyu ndo alikuwa mlinzi wa jumba hilo,Butu wakati anaingia alimpungia mkono mlinzi wake ishara ya kupokea salamu alopewa na mlinzi yule kwa kupungiwa mkono Baada ya butu kuingia mlinzi yule akafunga geti na kurudi eneo lake alilokuwa ameketi akanyanyua kikombe chake cha kahawa na kukiweka mdomoni.

Akapiga funda moja na kukirejesha chini,akazidi kusoma kitabu alichokuwa nacho mkononi,alikuwa ni msomaji mzuri wa vitabu vya riwaya hasa za kijasusi na leo hii kitabu kilichokuwa mkononi mwake ni kitabu cha *KUFA TU (HAKUNA NAMNA) cha mtunzi ZUBERI MARUMA

Inspekta John Butu baada ya kupaki gari lake eneo maalumu la maegesho akashuka na kuelekea upande ulipo mlango wa nyumba yake,alipofika akaufungua na kuzama ndani. Ndani pale sebuleni waliketi watoto wawili wakiangalia tv,watoto wale walifanana 'copyright' kama mapapai,usingeweza kuwatofautisha kwa mfanano ule kiumri walikuwa na miaka 19 walijaliwa sura nzuri,ucheshi kitendo tu cha kumuona baba yao wote wakainuka katika makochi na kumkimbilia baba yao wakamkumbatia.

"Shikamoo dady!"

Wote wakasalimia kwa pamoja huku wakiwa wamemng'ang'ania baba yao,

"Marhaba wanangu amjambo?!"

"hatujambo dady"

"mama yenu yupo wapi?!"

"yupo chumbani" Wakaachiana,na kurejea walipokuwa wameketi Butu akaelekea moja kwa moja chumbani...

"alice,katenge mezani uoni dady kashakuja?!"

Katika wale watoto wawili mmoja akamtuma mwenzake,baada ya kutoa kauli ile Alice aligeuza shingo na kumkata jicho kali dada yake kitendo kilicho mfanya anywee ila hakutaka kubaki kimya,

"Hata uniangalie vibaya ndo nishakwambia katenge mezani!..."

"Bwana eeh,usinipigie kelele hata wewe una mikono waweza kwenda kutenga pia si lazima mimi!"

"Nyie mnabishana nini hapo badala mtenge!" Ghafla wakashtushwa na sauti nyuma yao wote wakageuka,

Alikuwa ni mwanamke alojaliwa kila sifa ya kumwita mrembo,kwanzia weupe,urefu wa wastani umbo na hata sura,huyu ndo mama wa watoto wale na mke wa inspekta John Butu basi wakaandaa chakula mezani,John Butu alipotoka bafuni wakaketi na kula kwa furaha na upendo,hakika yeye na familia yake wali ishi kwa amani na upendo.

Baada ya chakula wakaelekea vyumbani mwao kulala wakitakiana usiku mwema watoto wakilala katika chumba chao,baba na mama nao wakaelekea katika chumba chao. Mngurumisho wa alamu aloitegesha katika simu yake ilimuamsha,alipotupa macho yake ukutani kulipokuwa na saa ilikuwa ni saa kumi na mbili kamili akawasha redio yake kusikiliza bbc hii ilikuwa ndo kawaida yake,baada ya kuamka asikilize amka na bbc kisha kumepambazuka na mwisho taharifa ya habari,ya saa moja,hapo ndipo atoke kitandani akakoge anywe chai saa mbili ndo atoke kuelekea kazini ambapo kwa kuwa alikuwa na usafiri na kituo chake cha kazi hakikuwa mbali muda mfupi tu alikuwa akifika kazini...

Hivyo siku hii baada ya kufika kazini alionana na mkuu wake na kumpa taharifa aloipata jana yake juu ya mtu yule alompigia simu kamishna Nurdin akampa askari kadhaa kwa ajili ya kuelekea huko uwanja wa ndege kuisubir hiyo ndege aloambiwa ingeingia saa tano,wakiwa katika nguo za kiraia kama vile wanasubiria wageni wao pale uwanjani zikiwa zimebakia dakika tano ndege kuwasili ghafla simu ya Inspekta Butu ikaita tena,akaitoa,alishtuka baada ya kuona namba ilompigia,aikuwa namba geni kwake '15551' ni namba ilo mpigia jana jioni kumpa habari ilo mfanya muda ule kuwa pale,haraka akaipokea,Kwanza kilitangulia kicheko kizito!,

"Ha ha ha ha ha Butu nafrah kwa kufatilia kile nilichokwambia bado dakika chache ndege iwasili,kuwa makini na watu hao si wakawaida na wanamtandao mkubwa jipange vizuri na vijana wako,"

Baada ya maneno yale simu ile ikakatwa pasina mtu yule kuhitaji jibu lolote kutoka kwa Butu,kitendo hiki kikazidi kumpa mashaka Butu juu ya mtu huyu,maswali kibao yakatawala katika kichwa chake,je mtu yule alikwepo pale uwanjani au?!,kwa nini ampigie kwa namba maalumu?!,ni nani hasa?,ila hakupata wasaha wa kutafakari zaidi baada ya ndege ile kuwasili,ikatua na kwenda kusimama eneo lake mlango ukafunguka watu wakaanza kushuka,wenyeji wao wakijisogeza kuwalaki wenye kukumbatiana wakikumbatiana,wakati askar wale wakitazama walokuwa wakishuka ghafla akashuka jamaa mmoja kweli alikuwa kavaa suti nyeusi mkononi hakuwa na kitu akaenda na kuongea na mtumishi mmoja wa pale ghafla akarudi ndani.Butu alitazama tu,mtumishi yule alienda akazungumza na wenzake ndani ghafla akatoka,sasa watu wale watano wakiwa katika suti nyeusi wakashuka mkononi wakiwa na mabegi makubwa ya kuwekea nguo,wakaweka katika eneo la kupimia wakaenda kuchukua upande wa pili,yani walikaguliwa kama abiria wengine mwisho wakachukua mabegi yao tayari kwa kuondoka,kabla Butu na wenzake kuwafata na kuwaweka chini ya ulinzi wakaonesha vitambulisho vyao na kuhitaji kukagua mizigo..

Kitendo cha kufungua mabegi yale hawakuamini walichokikuta ndani!,pakiti za unga wa madawa ya kulevya yalijaa ndani ya mabegi yale makubwa,palepale wakawekwa chini ya ulinzi,pamoja na watumishi wa pale 'earport' kwa kuwa gari yao awakupaki mbali wakamshtua dereva akaisogeza karibu watuhumiwa wakaingizwa ndani baada ya kunyang'anywa silaha landrover ile ya polisi ikiwa na watuhumiwa ndani ikaanza kutoka uwanja wa ndege huku waandishi wakipiga picha aikujulikana walifika saa ngapi,ila tayari habari zile zilishazagaa...

USIIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUTUMIA AKAUNTI YAKO YA FACEBOOK, LIKE UKURASA HUU USIPITWE NA SIMULIZI NA MENGINE HUKO FACEBOOK

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE TAZAMA VIDEO HII KAMA MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA

KWA TELEGRAM👇BONYEZA HAPA
42 featured Roho Mkononi Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni