ROHO MKONONI (3) - CnZ Media

CnZ Media

Jisomee Simulizi Mpya Kila Siku

Jumatano, 6 Julai 2022

ROHO MKONONI (3)

Je unajua kwamba Simulizi zote unazozipata hapa zipo kwenye app ya CnZ Media?

Humo Pia Utakuta:
πŸ“– KUSOMA SIMULIZI
🎬 FILAMU na TAMTHILIA za KITANZANIA
πŸ˜‚ VIDEO za KUCHEKESHA
πŸ“‘ MAKALA za AFYA na MAPENZI

Install app hii GUSA HAPA utavipata vyote hivyo bure kabisa
Mwandishi: Zuberi Maruma

SEHEMU YA TATU
ILIPOISHIA...
"Hizo namba umeshazituma kwa kpl 001?!"

"Ndiyo mkuu!"

"Ok!,wapigie nyumbani Kwanza ujue wanaendeleaje then uwai utanijulisha kila kitakachoendelea,mi nawasiliana na Kpl 001 kujua huyo mtu ni nani ok?!,"

KABLA HATUJAENDELEA NIOMBE KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media BASI INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI
πŸ‘‰GUSA HAPAπŸ‘ˆ

SASA ENDELEA...
"Sawa mkuu"

Akaitikia Butu sambamba na kukata simu,Kpl 001 kilikuwa Ni kitengo cha mawasiliano ndani ya idara ya jeshi la polisi.

Inspekta John Butu baada ya kukata simu alokuwa akiongea na mkuu wake sasa akaelekea upande zilipo bodaboda akapanda akampa ishara aondoe,wakati huo huo akampigia simu mlinzi wake

"Aloo Sam mpo salama?!"

"Ndio mkuu kwani kuna tatizo gani!"

"Kuna hatari cha kufanya funga geti kwa ndani usimfungulie mtu yoyote mi nipo njiani nakuja sawa?!"

"Sawa mkuu" mlinzi alotambulika kwa jina la Sam akaitikia,baada ya maelezo yale Butu akakata simu muda ule ule akamtumia msg mkuu wake kumjulishs kuwa familia ipo salama

Maskin ni kama akujua muda huo anamaliza tu kuongea na simu wakati Sam analifata geti kwa mantiki ya kubana kitasa kwa ndani ghafla alishughudia kageti kadogo cha lile geti kakifunguliwa,vijana wa tano walokuwa wamevaa maski nyeusi usoni kuziba nyuso zao huku mikononi wakiwa na silaha bastola zile ndogo wakazama pale pale wakamweka Sam chini ya ulinzi

Watatu wakaelekea ndani kuichukua familia,wawili walobakia wakaweka silaha zao vibindoni wakasaidiana kumfunga mlinzi yule kamba Kisha wakambeba na kutoka naye nje,ambapo palikuwa na gari lao wakafungua buti ambapo walitoa kamba nyingine wakamweka huko na kulibana buti lile,

Sasa wakabeba ile kamba na kurudi nayo ndani tayari kwenda kuwasaidia wenzao kuikabili ile familia.

Mama na wanaye wawili....

Inspekta wa jeshi la polisi John Butu anapokea simu kutoka kwa mtu asiyemfahamu tena ikiwa ni namba maalumu '15551' ina mtaharifu juu ya watu wanaoingia nchini na madawa ya kulevya hivyo yeye kama afisa wa jeshi la polisi ana amua kufatilia habari ile,

Kitendo cha kuamua kufatilia anajikuta akiyaweka maisha yake hatarini,na si maisha yake tu lah bali mpaka maisha ya familia yake...

Familia yake inatekwa na watu wasojulikana na anaambiwa hili kuipata familia yake ikiwa nzima basi aachiye watu alowakamata pamoja na mzigo wa madawa alokamatwa nao

Je unadhani Inspekta Butu atachukua maamuzi gani?!,ungana nami Zuberi Maruma katika burudani hii itakayokuweka katika hali ya taharuki na maswali mengi ukijiuliza

Hatua ya tano

Inspekta John Butu alifika katika jumba lake la kifahari maeneo ya Msovero,maeneo wanayoishi matajiri,nyumba nyingi zikiwa na fensi,kuta ndefu zenye nyaya za ulizi,pamoja na mageti makubwa yenye cctv camera

Kwanza alishtushwa na giza alokumbana nalo,pale getini kwake palikuwa na taa mbili kubwa zilizo mulika eneo kubwa la nje kivipi pawe giza,wasiwasi ukamvaa,haraka akakaza mwendo kuliendea geti dogo na kulisukuma,mlango wa geti ukafunguka afande akazama ndani...

Kajumba cha mlinzi kalikuwa wazi na ndani hapakua na mtu,haraka akakimbilia ndani ya nyumba walokuwa wakiishi familia yake

Nyumba yote ilikuwa tupu,wakati akiwa bado katika bumbuwazi ghafla simu yake ikaita haraka akaichukua kuangalia ni zilezile namba 0759427653 haraka John Butu akazipokea kwanza akapokelewa na kicheko kikali tena cha majivuni,kicheko kilichotoa sauti ya kukereka kwenye masikio yake...

Sauti ile sasa aikuwa ngeni kwake

"Nadhani utakuwa umeshaijua nguvu yangu ni kubwa kiasi gani,afande wewe ni mtu mdogo sana kwangu usitake makuu ya kushindana nami utaipoteza familia yako nawe kuteketea pia sasa Ni saa tatu kasoto nakupa nusu saa nenda usiku huu kawa achie watu wangu sambamba na kete zote za mzigo wangu tofauti na ivyo tusije kulaumiana"

Sauti ile ikamaliza na simu ikakatwa,Butu akajikuta akikaa Sofani pasina kuamini kile akisikiacho wala akionacho,Ni ukweli usiopingika kwamba aliipenda familia yake na pia aliipenda kazi yake,ni kipi afanye?!....

Akakumbuka alishakula kiapo kulitumikia taifa lake kufa na kupona kutolisaliti hata ikiwezekana kuipoteza familia yake,ila kwa wasaa ule katika hali alokuwa nayo hapana hakuwa tayari japo kulikuwa na baridi iloletwa na 'ac' ilokuwepo pale sebuleni lakini mwili wake wote uliloa jasho

Ghafla akakurupuka,Akasimama kwenye lile kochi na kuelekea ulipo mlango akafungua na kutoka akaelekea kunako eneo anapoegeshea magari yake akaliendea gari moja lililokwepo Pale na kushika mlango kabla ajaufungua akakumbuka gari yake iloteketea masaa machache yalopita,gari yake aloipenda akaliangalia eneo anapoliegeshea akapeleka mkono wake usoni na kufuta machozi yalomtiririka...

Butu alikuwa na gari mbili moja yake nyingine ndo haka ka Artaza cha mke wake,akafungua mlango na kuzama ndani...

Akaliwasha na kuliondoa kuelekea getini alipofika akaanza kupiga honi kusudi mlinzi amfungulie....

Ni wazi alishasahau kuwa muda huu mlinzi wake hayupo,au ni kutokana na kuchanganyikiwa na kujua kuwa kitendo cha kushuka kwenda tena kufunga geti ni kuzidi kupoteza muda katika zile dakika alizopewa.

Alipokumbuka haraka akashuka huku akikimbia akaelekea kufungua geti,akatoa gari na kurudi akafunga geti kwa kurudishia kwa nje akarudi kwenye gari lake akaingia na kuliwasha akaliondoa tena kwa mwendo wa kasi.

Butu saa tatu hii ya usiku alizidi kukanyaga mafuta na katu akuangaika wala kuitilia shaka gari moja nyeusi aina ya pajero ilopakiwa pembeni ya barabara,Butu alipopita tu,aliyekuwa dereva wa gari ile akashika simu yake na kubonyeza namba kadhaa akaweka masikioni akasubiri kwa nukta kadhaa kisha akaongea...

"Ndiyo katoka,katupita hapa kwa kasi ya ajabu bila shaka ndo anaenda kuwaachia"

"Sawa mkuu"

Mtu yule akaitika na kukata simu akawageukia wenzake,ndani ya gari ile jumla na yeye walikuwa watano,siti ya nyuma walikaa wawili,mbele pamoja na yeye walikuwa watatu...

"Mkuu kasema tumsubiri,akiwaachia watu wetu tumpeleke ilipo miili ya familia yake"

Dereva yule aliongea kwa majivuni, wenzake wakatingisha kichwa ishara ya kukubali,nyote wakiwa wameficha nyuso zao kwa kofia maalumu zilizoacha tu macho,kofia hizi utumiwa sana na majambazi kuibia kusudi sura zao kutotambulika kiurahisi, wakaendelea na stori zao huku wakimsubiri mzee wa kazi inspekta John Butu 'JB' kama bosi wao alivyo waagiza...
***
Inspekta alifika kituoni akashuka kwenye gari yake na kuelekea zilipo mahabusu ndogo za watuhumiwa akafungua na kuwatoa wale watano pamoja na wale watumishi wa uwanja wa ndege akawapeleka ofisini kwake...

Akawaambia wasubiri,akaelekea katika chumba kilichokuwa kina ifadhia ushahidi akatoa zile begi za madawa akawapelekea wenyewe

Polisi walokuwa zamu usiku ule walibaki tu wakishangaa kila kilichokuwa kikiendelea hakukuwa na aliye mzuia

"Haya ondokeni"

Palepale akawaruhusu watu wale waka anza kuondoka.

"Mkuu mbona umewaruhusu tena watuhumiwa utaeleza nini kwa kamishna?!"

"Nailinda familia yangu"

"Lakini jua umeenda kinyume cha sheria na utashtakiwa kwa hili....

Kabla Butu ajajibu ghafla simu yake ikaita Kutazama ni bosi wake Cp Nurdin kabla ajapokea ghafla namba nyingine zikaingia 0759427653 haraka akakata zile za bosi wake na kuzipokea zile namba ngeni...

"Vizuri sana kijana kwa chaguo zuri ulochagua sasa nenda nyumbani kwako nje utakuta pajero nyeusi ingia watakupeleka ilipo familia yako wahitajika uende peke yako"

Baada ya maelezo yale simu ile ikakata,

Butu palepale akanyanyuka na kuelekea nje alipopaki gari yake alipofika ile anaingia ndani ya gari yake ghafla nyuma yake akasikia sauti sambamba na milio ya kukokiwa risasi...

"Tafadhali John Butu upo chini ya ulinzi,usiingie kwenye gari na tupa silaha tofauti na ivyo sitosita kutoa ruksa kuusambaratisha ubongo wako ulolala,ikiwa ni amri kutoka kwa kamishna...

John Butu akaganda sauti ile ali ifahamu fika ni ya Inspekta mwenzake aitwaye Jonathan,taratibu akageuza shingo sauti ile ilipotokea akakutana na mitutu mitatu iloshikwa vema na wale askari alokutana nao ndani,walokuwa zamu usiku ule...

Butu akaachia tabasamu,na kutaka kuongea kitu ila Jona akampa ishara kwamba asiongee kitu zaidi ya kufanya alivyoambiwa...

Kweli akatupa silaha yake na kuonesha mikono mbele tayari kwa kufungwa pingu,

Kumbe ile alipoingia tu huku akionekana wazi kuchanganyikiwa na kuelekea zilipo selo Insp Jona alimpigia simu mkuu wao na kumjulisha kuwa Butu anataka kuwatoa wale watuhumiwa wa madawa alowakamata asubuh,haraka Kamishna akampigia Butu,kitendo cha kukataa kupokea akawapa amri wamweke chini ya ulinzi kwenda kinyume na sheria pasina kujali Butu yupo katika hali ya kuikomboa familia yake...

Insp Jonathan akaweka bastola yake ndogo kibindoni na kuitoa pingu taratibu akawa akimsogelea Butu kutaka kumfunga bado bastola mbili za makoplo zikiwa zimemwelekea!

Hakika alikuwa katika mtihani mzito,tena mtihani wa maisha...

Na ilikuwa ni lazima aufahulu kuikomboa familia yake,

Kivipi sasa!....

Lilikuwa ni swali lisilojibika

Inspekta John Butu analazimika kuwaachia watuhumiwa kadhaa alowakamata na madawa ya kulevya,lengo la kuwaachia ni ili familia yake ilotekwa na watu

wasojulikana ipate kuwa huru....

Kufanya ivyo ni kwenda kinyume na sheria,wakati anaondoka anajikuta akiwa chini ya ulinzi wa Askari wenzake anasamli amri na Inspekta Jona anamsogelea kwa lengo la kumtia pingu ikiwa ni amri kutoka kwa kamishna wao Cp Nurdin Kyango je unadhani nini kiliendelea?!....

Tusonge ujifunze na kuburudika zaidi...

*HATUA YA SITA*

Inspekta Butu alijua kuendelea kusimama pale ni kupoteza muda hali ya kuwa ajui familia yake ipo katika wakati gani kwa muda ule,machozi yakaanza kutiririka katika macho yake,alijua ndiyo kaenda kinyume cha sheria kuachia watuhumiwa ila sasa angefanyaje,

"Jonathan rafiki yangu,tambua nimefanya hayo kwa ajili ya familia yangu,...

Palepale akatoa ile simu yake mfukoni na kwenda upande aliposevu audio mbalimbali alizorekodi,akaanza kumsikilizishia afisa yule mwenzake,huku akimsimulia toka mwanzo jana alipopokea simu kutoka kwa namba 15551 na leo kuamua kufatilia,jinsi alivyo wakamata wale watuhumiwa,simu za vitisho alizokuwa akipigiwa,mabalaa alokumbana nayo barabarani ikiwemo kukoswa koswa na bomu na hata kuikosa familia yake mpaka kufikia pale kuwa achia wale wahalifu,

Inspekta Jonathan kiukweli alijikuta akimuonea huruma askar mwenzake,alijua hata yeye yale yangeweza kumtokea,palepale akawahamuru askar waweke silaha chini,na kumruhusu Butu kuondoka baada ya yeye kukataa msaada wake,Butu akaingia ndani ya gari yake tayari kurudi nyumbani akiacha zogo huku nyuma kati ya inspekta Jona na mkuu wake
***
Inspekta Butu aliwasili nyumbani kwake akaliweka gari lake na kutoka nje ambapo alielekea mpaka kwenye

USIIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUTUMIA AKAUNTI YAKO YA FACEBOOK, LIKE UKURASA HUU USIPITWE NA SIMULIZI NA MENGINE HUKO FACEBOOK

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE TAZAMA VIDEO HII KAMA MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA

KWA TELEGRAMπŸ‘‡BONYEZA HAPA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni