KIJIJINI KWA BIBI (21)

0
Mwandishi: Alex Kileo

SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA
TULIPOISHIA...
"naomba polisi yeyote atakaekuuliza kuhusu yale mambo yaliyötokea

kule, mjibu hujui chochote, sawa?" Sajenti Minja aliwasilisha ombi

lake huku akiwa hana uhakika wa kukubaliwa,

"kwanini tufiche ukweli?" Msaidizi wa mganga aliuliza kwa mshangao,

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
"Ukiongea ukweli utakuwa umeniharibia kila kitu katika maisha

yangu, yaani hata kufungwa nitafungwa" Sajenti Minja aliongea kwa

huruma ili kumshawishi Msaidizi wa Mganga akubaliane nae,

"Kwa maana hiyo wewe umependa lile tukio lililotokea siku ile?"

Msaidizi wa Mganga alimuuliza Sajenti Minja,

"Tukio sasa, maana yalikuwa mengi" Sajenti Minja aliuliza,

"La wenzangu kuuawa kinyama?" Msaidizi wa Mganga aliuliza,

"Hapana, nitalifurahia vipi wakati lilikuja kuharibu tiba ya ndugu

yangu na nikampoteza mtu ambaye ndiye nilikuwa nategemea yeye

atamponya ndugu yangu?" Sajenti Minja aliongea kwa upole na machozi

yakimtoka kwa mbali ili kumshawishi tu Msaidizi wa Mganga asiseme

ukweli mbele ya Polisi wengine,

"Sasa kwanini nifiche?" Msaidizi wa Mganga akauliza tena ila

kipindi hiki aliuliza kwa upole,

"Kuwa na utu ndugu yangu, maana unachotaka kukifanya ni kuniharibia

maisha tu" Sajenti Minja aliendelea kumlalamikia Msaidizi wa

Mganga,

"Sio nakuharibia maisha, mbona mimi maisha yangu yameshaharibika?"

Msaidizi wa Mganga aliongea huku anamkodolea macho Sajenti Minja,

"Yameharibikaje sasa wakati upon hai na upon huru?" Sajenti Minja

alimuuliza,

"Hill sio tatizo, tatizo ni kwamba yule Mganga nilimchukulia kama

mkombozi wangu kutokana na maisha yangu" Msaidizi wa Mganga

aliongea,

" kivipi yaani?" Sajenti Minja alimuuliza,

"Yaani nilikuwa sina mbele wala nyuma, ila yule mzee aliniokota tu

mjini na kunichukua kisha akawa ananifundisha uganga na akawa

ananipa kipato kidogo angalau nikajiona mtu" Msaidizi wa Mganga

aliongea,

"Hilo sio tatizo, ngoja upone tutaongea zaidi, mimi nitakusaidia"

Sajenti Minja aliongea kwa huruma huku akichomoa noti nyingi kutoka

katika mfuko wake wa suruali na kumpa msaidizi wa Mganga,

"Za nini hizi?" Msaidizi wa Mganga aliuliza huku akiwa anaziangalia

zile hela akiwa hataki kuzipokea,

"Zitakusaidia kununua vitu vidogo vidogo kipindi upo hapa

Hospitali" Sajenti Minja aliongea huku akiwa bado amezishikilia

zile pesa,

"Wewe ni ndugu yangu bwana, tusaidiane" Sajenti Minja aliongea kwa

upole,

"Ngoja nitoke hospitali tutaongea vizuri ndugu yangu" Msaidizi wa

Mganga aliongea huku akizitia pesa zile mfukoni,

"Nikununulie chakula gani kabla sijaondoka" Sajenti Minja

alimuuliza,

"Chochote tu, mimi mswahili bwana sichaguagi chakula" msaidizi wa

Mganga aliongea,

"Wewe mgonjwa bwana, itabidi ule minyama nyama, ngoja nikakutafutie

kuku bosi" Sajenti Minja aliongea kwa furaha huku akitoka nje na

akiamini tayari ameshamteka hisia yule Msaidizi wa Mganga.

"*

Babu wa monchwari alivyopigwa ule mtama ile asubuhi kumbe aliteguka

mguu maeneo ya nyuma ya paja chini ya kiuno ila alivumilia na

hakuwaambia kitu chochote wale polisi kwa sababu walikuwa na hasira

muda ule, ila ilivyofika jioni maumivu yalimzidia na Babu wa

monchwari akawaambia polisi ila walimpuuza tu, masikini Babu wa

watu maumivu yalimzidia mpaka akawa Amalia kwa sauti kubwa kama

mtoto, kilio kikamfikia mkuu wa polisi na kuja kuangalia kuna nini,

" mbona huyo mzee analia?" Mkuu wa polisi aliwauliza askari

aliowakuta hapo ambayo walibaki wakitazamana bila kutoa jibu,

"Anamaumivu nadhani" Askari mmoja alijibu,

"Babu una tatizo gani?" Mkuu wa Polisi aliamua amuulize mwenyewe,

"Mguu nahisi umevunjika, nawaambia wanisaidie ila wananitukana"

Babu alijibu huku akiendelea kulia,

"Umevunjikaje, umeanguka?" Mkuu wa Polisi aliuliza,

"Hao wenyewe walinipiga asubuhi" Babu alijibu,

"Hata mambo ya kuwapiga watuhumuwa si tulishawakataza?, tena

mnampiga mzee kabisa..ebu chukueni gari ya doria mumpeleke

hospitali" Mkuu wa Polisi aliongea kwa ukali na vijana wake

wakanyanyuka haraka,

"Kwani yupo hapa kwa kosa gani" Mkuu wa polisi akauliza,

"Huyu ndiye yule mlinzi wa monchwari" Askari mmoja akajibu,

"Hata mumpeleke hospitali akapatiwe matibabu na mumrudishe hapa,"

Mkuu wa polisi aliongea na kuondoka huku akiwaacha vijana wake

wakimbeba Babu monchwari na kumpeleka kwenye gari na safari ya

hospitali ikaanza.

Iliwachukua dakika chache kufika hospitali, walimshusha Babu na

kumpeleka kupata matibabu.

Babu akapatiwa huduma kisha kwa Saa nzima na akaonekana ni mfupa tu

ulikuwa umehama eneo lake, madaktari wakafanya jitihada na kumtibu

bila tatizo na kuwaruhusu askari waondoke nae.

Askari walipotoka nje walienda moja kwa moja mpaka kwenye gari yao,

wakapanda gari ili warudi kituoni, kwa bahati mbaya gari yao

ilipata itilafu ikawa haiwaki, ikabidi wapige simu kwa mkuu wao ili

wapate msaada, mkuu wao akawapa namba ya sajenti Minja na kuwaambia

yuko pale hospitali kwa hiyo wampigie awape msaada wa kuwarudisha

kituoni kwa maana Sajenti ana gari.

Sajenti Minja baada ya kupigiwa simu akawaelekeza mahali gari lake

lilipo, wale askari na Babu wa mochwari wakafika mahali gari

lilipo, kisha wakawa wanamsubiri sajenti Minja atoke ndani ili

awarudishe kituoni, na Babu wa monchwari ndio kabisa alikuwa

anaangalia katika mlango wa kutokea hospitali ambayo ndio njia

anayokuja nayo Sajenti Minja..

…Sajenti Minja wakati anatoka ndani ya hospitali, akawaona wale

polisi na yule babu wa mochwari kupitia dirishani, akasita, kisha

akili yake ikafanya kazi haraka.

akarudi kisha akawapigia simu wale askari na kuwaambia kuwa yeye

bado ana shughuli anazifanya katika eneo like la hospitali, kwa

hiyo askari mmoja amfuate ndani ili akampe ufunguo,

mmoja kati ya wale polisi akaenda alipoelekezwa na sajenti Minja,

akapewa ufunguo, kisha akaambiwa arudishe gari pale hospitalini

baada ya kazi zao

Sajenti Minja aliingia katika nyumba ya dada yake saa mbili usiku,

baada ya salamu wakakumbushana mambo yaliyowakuta usiku uliopita,

wakafurahi na kuhuzunika pia,

Ila habari iliyowashtua wote ni kupatikana kwa wale maiti na mtu

mmoja akiwa mzima, pia sajenti Minja akawaambia namna

alivyofundisha yule msaidizi wa mganga kukana kujua lolote.

Mama kayoza kidogo akashusha presha baada ya kusikia hivyo,

"Kitu kingine kibaya ni kwamba hata yule babu wa monchwari

aliyetusaidia kuiba ile maiti nae amekamatwa ila sijajua kwa kesi

gani?" Sajenti Minja aliendelea kutoa habari mbaya,

"Ni hiyo hiyo ya kupotea kwa maiti, asubuhi si nilikuwa hospitali

nilienda kumuona mtu, ndio nikakutana na hizo habari, ila maiti

yenyewe imeshapatikana uko makaburini ilikutwa pamoja na hiyo miili

ya waganga wenu" Mama Kayoza aliwapa habari,

"Kama maiti imepatikana itakuwa afadhali kwa Babu" Kayoza aliongea,

"Hujui sheria mjomba, Babu hawezi kuachiwa mpaka ipatikane au

ijulikane sababu za kuuza ile maiti" Sajenti Minja aliongea huku

akimuangalia Kayoza,

"Sababu iliyomfanye auze si ni pesa?" Kayoza alijibu kiutani na

wenzake wacheke,

"Haya mambo mazito msiyachukulie kiutani utani hivyo" Mama Kayoza

aliongea huku akionekana kutofurahishwa na jibu la Kayoza,

"Mama inabidi tujifurahishe tu, ukisema uegemee sana upande wa

yanayotukuta, tutakuwa watu wa machozi kila siku" Kayoza alimwambia

Mama yake,

"Ujinga huo, badala uangalie namna ya kujisaidia unakalia kuongea

vitu visivyo na kichwa wala miguu" Mama Kayoza aliendelea

kumshambulia mwanaye,

"Vitu vya maana kama vipi?, ngoja nijiandae niende kanisani" Kayoza

aliongea kwa hasira huku akiondoka sebuleni,

"Ana hasira kama babu yake, mzee John Minja" Sajenti Minja aliongea

huku akicheka,

"Mjinga tu, hasira ananiletea Mimi badala ya kumpelekea bibi yake

uko kijijini" Mama Kayoza aliongea,

"Kayoza anaenda kanisani?" Sajenti Minja aliuliza,

"Leo kuna maombi, tena na wewe itabidi uende ili bwana akakupe

wepesi uenda kazi ya kumsaidia mjomba wako itatimia haraka" Mama

Kayoza alimwambia Sajenti Minja,

"Sawa itabidi tuongozane, kwani maombi yataisha saa ngapi?" Sajenti

Minja akauliza,

"Tunakesha" Mama Kayoza alijibu,

"Mh..sasa si itabidi niende nyumbani nikabadili nguo" Sajenti Minja

aliongea,

"Kwani hizo ulizovaa zina ubaya Gani? Mama Kayoza aliuliza,

"Mimi naona sio vizuri kwenda Nazi kwa sababu nimeshinda nazo kutwa

nzima" Sajenti Minja alijibu,

"Hiyo sio sababu, nenda kaoge uende kanisani" Mama Kayoza aliongea,

"Sawa basi, nirudi baada ya muda gani?" Sajenti Minja aliuliza huku

akiinuka,

"Hakuna kuondoka, nilipokwambia ukaoge nilimaanisha uingie bafuni,

sasa unavyotaka kuondoka unadhani bafu lipo kwako tu?" Mama Kayoza

aliuliza,

"Sawa bwana, basi ngoja nikajitayarishe" Sajenti Minja aliongea

huku akielekea vilipo vyumba vya wakina Kayoza,

Baada ya saa moja na nusu wote walikuwa wamejiandaa mpaka Omary

wakaanza kwenda eneo la maombi.

Walienda kwa miguu tu kwa maana ni eneo jirani na wanapoishi.

Walifika na muda ulipofika waumini walikuwa wengi sana kanisani,

walianza kwa kuimba nyimbo mbalimbali za kutukuza.

Baada ya saa zima Mchungaji Wingo aliingia, akakaa katika kiti

anachopaswa kuwepo. Nyimbo ziliimbwa kisha waimbaji wakamaliza,

sala zilianza, walisali muda mrefu sana mpaka kayoza akachoka

kutokana na kwamba yeye sio mtu aliyezoea sana kwenda kanisani,

"oya kaka, tusepe" kayoza alimwambia Omari ambae alikuwa anasinzia

tu muda wote.

"wapi sasa" Omari akauliza kivivu huku akijinyoosha,

"maskani dogo, we unasinzia tu bila ya mpango, usije ukaharibu hewa

bure" Kayoza aliongea kwa utani.

"aah wapi, mimi nina kontroo wewe" Omari akajibu kisha wote

wakacheka.

Wakatoka nje ya kanisa wakawa wanaelekea nyumbani, ilikuwa kama saa

saba usiku hivi, kwa mbali wakaona msichana anawakimbilia, alikuwa

yule binti wa mchungaji,

"habari jamani" Binti akawasalimu.

"nzuri" wakajibu kwa pamoja.

"Kaka unaweza kutupisha kidogo?" Binti Mchungaji aliongea huku

akimuangalia Omary,

"Sawa" Omary alijibu huku akitangulia mbele na kuwaacha Kayoza na

Binti Mchungaji wakiwa wamesimama,

"vipi jibu langu Kayoza" Binti Mchungaji alimuuliza kayoza huku

akiwa hana chembe ya aibu.

"kesho nitakujibu" Kayoza akajibu kwa ufupi.

"jamani mbona unanifanyia hivyo, au kwa kuwa nimekwambia

nakupenda?" Binti Mchungaji alilalamika kwa huruma.

"sikia binti, hapa unapoteza muda wako bure, kiukweli kabisa mi

siwezi kukubalia ombi lako" Kayoza aliongea kwa ujasili kwa maana

aliona bora amueleze ukweli tu kuliko kumpotezea muda,

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)