KIJIJINI KWA BIBI (35)

0
Mwandishi: Alex Kileo

SEHEMU YA THELATHINI NA TANO
TULIPOISHIA...
…"duh!, sawa babu, malipo ni kiasi gani",Sajenti Minja akamuuliza Mganga,

"weka kiasi chochote",Mganga aliongea huku akimuelekeza Sajenti Minja sehemu ya kuwekea hela,

Sajenti Minja akaingiza mkono mfukoni na kutoa shilingi elfu kumi, na kuiweka juu ya ungo wa Mganga,

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
"haya babu tunaenda",Sajenti Minja akaaga kwa niaba ya wenzake,

"haya karibuni tena, ila mnatakiwa muwahi kumpeleka, kwa sababu mkichelewa kidogo inaweza kuwagharimu zaidi",Mganga alitoa msisitizo huku akiwa awaangalii na badala yake alikuwa akizipanga panga vizuri dawa zake,

"hamna shida Babu, tutaenda wiki ijayo",Sajenti Minja alisema kwa sauti ya unyonge,

"Wiki ijayo?, Mimi ndio ningekuwa nyie, yaani ningeenda muda huu kupanda gari" Mganga aliendelea kuongea,

"Kwani mzee ni hatari sana tukienda wiki ijayo?" Sajenti Minja aliuliza huku akisimama kabisa, kwa maana mwanzo alikuwa anaongeo huku anatembea,

"Mwenyewe fikiria kwenye kchwa chako alafu utaamua uende wiki ijayo au uende haraka iwezekanavyo" Mganga alitoa jibu lililomfanya Sajenti Minja akae kimya na kutoka zake nje.

Baada ya hapo, wakina Sajenti Minja wakaondoka zao kurudi nyumbani.

Walipofika, wakamkuta Mama Kayoza yuko sebuleni anaangalia kwaya,

"karibuni jamani, za uko?",Mama Kayoza aliwakaribisha,

"uko ni yale yale tu",Sajenti Minja alijibu katika sauti iliyokata tamaa,

"yale yale yapi, ina maana na huyo Mganga ameshindwa?",Mama Kayoza aliongea kwa upole,

"ndio, ila nae amesema dawa ipo",Sajenti Minja akasema kiunyonge,

"si angewapa kama ipo",Mama Kayoza aliongea kwa mshangao,

"amesema ipo KIJIJINI KWA BIBI yake Kayoza",Sajenti Minja alijibu,

"mh, kweli ni yale yale",Mama Kayoza nae akawa mnyonge ghafla.

Ikawabidi wajipange, na mwisho wakakubaliana kuwa, Sajenti Minja achukue likizo fupi kwa ajili ya safari ya Bukoba.

Yule kijana aliyepewa kazi ya upelelezi alukuwa ni mpelelezi haswa, unaweza kujiuliza kwanini asingepewa kazi usalama wa utaifa?

Maana sio kufuatilia tu nyendo za Omary, ila mpaka baadhi ya maneno waliyokuwa wanaongea wakina Omary alikuwa anayapata kwakutumia ujanja anaoujua yeye.

na hapa alikuwa ameyasikia maneno yanayohusu safari ya Bukoba, sasa alipoyasikia haya, akaenda hadi kwa Mkuu wa Polisi,

"vipi bwana mdogo, kuna mafanikio?",Mkuu wa Polisi alimuhoji yule Kijana,

"yapo mengi sana mkuu. Kwanza pole kwa msiba kwa maana kipindi kile nilikuja ila nilishindwa kuonana na wewe",Suma alijibu kwa kujiamini, na pia akatoa maneno ya pole,

"Siwezi kusema asante kwa maana uchungu bado ninao, tena mkubwa tu, na ukizingatie mtoto mwenyewe alikuwa mmoja tu" Mkuu wa polisi alijibu,

"Tatizo lilikuwa nini, maana Mimi nilisikia juu juu tu kuwa mlivamiwa?" Suma aliuliza,

"Ndiyo hayo hayo mambo ambayo nilikuagize uyafuatilie ndio yamenirudia nyumbani kwangu" Mkuu wa polisi aliongea kwa unyonge,

"Aisee pole sana. Sasa nimekuja hapa kukueleza nilipofikia" Kijana Suma aliongea huku akiweka note book yake mezani,

"ehe, niambie kijana wangu",Mkuu wa Polisi aliongea huku akibadilisha mkao katika kochi,

"kwanza kabisa, yule kijana unayemtambua kama Remmy, jina lake halisi ni Omari Mkwiji, ni mwenyeji wa Tanga, pia mwanafunzi wa UDOM pale Dodoma, na pale hana undugu na yeyote kati ya wale, ila anaishi pale kama rafiki wa mjomba wake Sajenti Minja, ambae anaitwa Kayoza. Na mahali walipokutana nae ni Dodoma pale Chuo kikuu.

Huyu Kayoza ndio mwenye matatizo sasa, yeye ndio mnyonyaji wa damu, na Siku binti yako anafariki ni yeye ndio aliyemuua na hiyo habari niliisikia kwa Dada yake Sajenti Minja wakati wakiwa wanajadili kuumaliza ugonjwa wa Kayoza unaosababisha yeye kuwa katika hali ile ya kunyonya damu watu, na hapa ninavyokuambia ni kuwa Sajenti Minja atakuja kukuomba likizo ya muda kwa sababu walienda kwa mganga, wakaambiwa waende kijijini kwa bibi yake Kayoza ambapo ni Bukoba, uko ndipo waliambiwa kuwa kuna dawa ya kumponya Kayoza, kwa hiyo Sajenti Minja ataongozana na Kayoza na Omari kwa ajili ya Safari",yule Kijana alimaliza hivyo,

"kwa hiyo Minja anajua mchezo mzima, hata ile kesi kumbe ni ujanja ujanja tu!",Mkuu wa Polisi aliongea kwa sauti yenye mawazo yaliyoificha hasira yake,

"mimi nafikiri kazi uliyonituma nimeshaimaliza",sauti ya yule Kijana ilimshtua Mkuu wa Polisi aliyekuwa kazama ndani ya kina kirefu cha mawazo,

"sawa, asante, ngoja nikuletee mzigo wako",Mkuu wa Polisi aliongea huku akinyanyuka na kuelekea ndani.

Baada ya dakika chache alitoka na bahasha kubwa ya kaki, akamkabidhi yule kijana, yule Kijana akazitoa pesa ndani ya bahasha, akazihesabu, kisha akaagana na Mkuu wa Polisi.

"Kijana uliniambia huna kazi?" Mkuu wa polisi alimuuliza Suma ambaye alikuwa ameshaanza kuondoka,

"Ndio Mkuu" Suma alijibu huku akisimama,

"Jiandae basi, maana nakuandalia barua itayokufanya uende moshi ukachukue mafunzo ya uaskari" Mkuu wa polisi alitoa maneno yalimfanya Suma amshukuru sana,

"Asante sana, nine lini?" Suma aliuliza,

"Nitaakutaharifu kupitia simu, we kaa tayari tu kwa maana itakuwa muda wowote kutoka sasa" Mkuu wa polisi alimjibu,

"nashukuru sana mzee wangu.

Ubaki salama", Suma aliongea na kuondoka sake na kumuacha Mkuu wa polisi akiwa sebuleni,

"Sajenti Minja, Joel Minja, Minja, Minja, lazima nikuue kwa mkono wangu, wewe ndio umesababisha mwanangu amekufa kifo cha aibu",Mkuu wa Polisi aliongea kwa sauti ndogo huku akiwa ameuma meno kwa hasira,

"Kwa hiyo Omary sio muuaji, Kayoza ndiyo kamuua binti yangu?, Minja unajua kila kitu ila umeficha mpaka mwanangu ameuwawa kinyama? Hakuna atakayesalimika kati yenu" Mkuu wa polisi aliongea na kisha akagida kinywaji kikali chenye rangi ya maji kilichokuwa katika chupa kubwa kama ya waini (wine) ila chenyewe ubavuni kiliandikwa MAGIC MOMENT.

Siku iliyofuata, Sajenti Minja alipanga akaombe likizo, akajitayarisha vizuri, na kuwa nadhifu kama kawaida yake. Akachukua gari yake na kwenda nayo moja kwa moja mpaka ofisini.

Ofisini aliingia saa nne asubuhi, alipokelewa na pole nyingi sana kutoka kwa askari wenzake, kwa sababu toka apate ajali ndio kwa mara ya kwanza alikuwa anaingia ofisini, baada ya salamu za hapa na pale, akawa anaelekea katika ofisi ya Mkuu wa Polisi, alipofika akagonga mlango,

Mkuu wa Polisi alikuwa ndani,

"nani?",Mkuu wa Polisi akauliza,

"Minja",Sajenti Minja akajibu kwa nje,

"leo ndio mwisho wako mshenzi na msaliti mkubwa wewe",Mkuu wa Polisi aliongea huku akijaza risasi katika bastola yake ndogo, alipomaliza, akamwambia Sajenti Minja aingie…..

…Sajenti Minja akaingia ndani,

"vipi tena mkuu, mbona kifaa umekiweka mezani?",Sajenti Minja aliuliza baada ya kuiona bastola iko juu ya meza ya Mkuu wa Polisi,

"nilikuwa naisafisha, karibu Minja",Mkuu wa Polisi aliongea huku akibasamu kwa tabasamu batili,

"Tunatishana bwana, hivyo vyombo vya moto vinafichwagwa bwana" Sajenti Minja aliongea huku nae akitabasamu,

"Kweli kabisa.. Vipi mbona umekuja leo kabla likizo yako haijaisha? Au uliwamisi wenzako?" Mkuu wa polisi alimuuliza Sajenti Minja,

"Hata hiyo ni sababu pia, ila sababu juu iliyonileta ni kuja kuomba kuongezewa likizo" Sajenti Minja aliongea kauli ambayo mkuu wa polisi aliitegemea,

"Haina shida Minja, je ungetaka likizo ya muda gani?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"Ningepata kama wiki mbili nyingune, ingekuwa safi sana" Sajenti Minja aliongea,

"Mi nitakupa likizo ya mwezi mzima, najua hali yako haijatengemaa vizuri" Mkuu wa polisi aliongea,

"Nashukuru sana, sasa ngoja nikaandae barua ili niiwasilishe baadae" Sajenti Minja aliongea,

"Hapana, hakuna haja ya barua, we nenda tu Minja" Mkuu wa polisi alimzuia Sajenti Minja kuandika barua,

"Haiwezi kuleta matatizo baadae?" Sajenti Minja alimuuliza mkuu wake,

"Hakuna Shida Minja, Mimi ndiyo nimekuruhusu, usiwe na wasiwasi" Mkuu wa polisi alimwambia Sajenti Minja.

Baada ya Sajenti Minja kuongea kilichompeleka, haikuwa ngumu kukubaliwa, alipewa likizo ya mwezi mzima,

"utakuwa hapa hapa au utarudi Dodoma?",Mkuu wa Polisi alimuuliza Sajenti Minja,

"hapa hapana, nitaenda Moshi kwa wazazi, alafu wiki mbili za mwisho nitazimalizia Dodoma",Sajenti Minja alijibu,

"haya bwana Minja, mi nakutakia likizo njema, na safari njema pia",Mkuu wa Polisi alihongea kwa sura aliyoibandika huzuni wa bandia,

"shukrani sana Mkuu, tukijaaliwa",Sajenti Minja alisema wakati ananyanyuka kutoka kwenye kiti,

Kisha akauendea mlango na kwenda zake.

Mkuu wa polisi alisitisha zoezi la kumuua Sajenti Minja ofisini kwa sababu angekamatwa na kufungwa kwa sababu ushaidi ungekuwepo wa kutosha, aliamua kwenda kumuua Sajenti Minja huko huko Bukoba, Mkuu wa Polisi na yeye akajipa likizo.

Likizo iliyokuwa maalum kwa ajili ya kisasi, likizo ambayo aliibatiza jina na kuiita LIKIZO YA MALIPO YA KIFO.

Siku ya safari ilipofika, Mama Kayoza aliwasindikiza mpaka stendi kuu ya mkoa, walipofika, wakafanikiwa kupata usafiri wa haraka haraka,

"Jamani safari njema" Mama aliwaambia,

"Lakini Dada kumbuka sisi tunaenda sehemu ambayo hatuhijui, kama una namba za wenyeji wetu ni bora uwape taharifa juu ya safari yetu" Sajenti Minja alimuambia Dada yake,

"Kayoza anapajua huyo, au na wewe umepasahau?" Mama Kayoza aliongea huku akimuangalia Kayoza,

"Mama ni muda sana, hata kumbukumbu sina vizuri" Kayoza alijibu,

"Mimi na wewe ni nani ambae ametoka muda mrefu kule? Mbona mimi bado napakumbuka?" Mama Kayoza alimuuliza mwanae,

"Tatizo sio kila sehemu naikumbuka, kuna njia sizikumbuki kabisa" Kayoza alijibu Mama yake,

"Bwana nyie wanaume, mtafika tu, maana Mimi sina mawasiliano na mtu yoyote wa uko" Mama Kayoza aliongea,

"Tutafika tu" Omary aliongea na kufanya wenzake wamuangalie,

"Unavyoongea utasema unapajua, au umeshawahi kufika?" Sajenti Minja alimuuliza Omary,

"Tuwe na imani tutafika tu" Omary alijibu na kufanya wenzake wacheke,

"Achana na huyu mwendawazimu, ebu nichoree ramani kwenye karatasi" Sajenti Minja alimwambia Dada yake,

"Nipe hiyo karatasi na kalamu" Mama Kayoza akaongea na kumfanya Sajenti Minja ajisachi na kutoa kalamu na kitabu chake kidogo cha diary na kumpatia Mama Kayoza kisha akaanza kuwachorea ramani huku pia akiwaelekeza, alipomaliza akawaachia ile karatasi yenye mchoro.

Wakaendelea kuongea na maongezi mengine mpaka muda wa kuondoka basi ulipofika ndipo mama Kayoza akaagana na wenzake hao na kuachana hapo huku wakipungiana mikono kipindi basi inaacha eneo la kituo kikuu cha mabasi ya mikoani.

Baada ya gari kupotea machoni pake, Mama Kayoza aliondoka zake eneo hill huku akiamini Wakina Sajenti Minja watakaa wiki tu kisha watarudi.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)