Mtunzi: Maundu Mwingizi
SEHEMU YA THELATHINI NA MOJA
TULIPOISHIA...
TULIPOISHIA...
Yule alikuwa Mzee Sufiani Bin Shamhurish aliyekuwa katika umbile lile la kijana ili asiweze kugundulika haraka na Takadiri Al-harabi ambaye alikwishamuona mara ya kwanza akiwa katika lile umbile lake la kiutu uzima, lengo lake safari hii ni kumuwahi na kumuangamiza komando yule
KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO
SASA TUENDELEE...
Cha kuchekesha na kustaajabisha Si Mzee Sufian wala Takadiri aliegundua kua alikuwa akiogelea na hasimu wake, hakika ile ilikuwa ni miamba ya kuotea mbali. Kila mmoja alijibadilisha kiukweli kiasi cha kutomfanya mwenzie ahisi kitu tangu walipokutana kwa mara ya kwanza, hakuna aliyekuwa na mapenzi na mwenzie kwani kila mmoja alikuwa kazini ila ule utowekaji wa kipekee ulitosha kabisa kwa Mzee Sufiani akiwa katika umbile la ujana kuhisi hali ya hatari, akatoka haraka na kuanza kumfuatilia Msichana yule
Kilichomuondoa haraka Takadiri Al-harabi ni Nuru na miale ya Pete(Khatam Budha) iliyokua ikimjia kwa mbali sana huku ikitaka kufifia, miale ile ilikuwa ikitokea katika kituo cha Polisi Kijitonyama alikohifadhiwa Suhail, kama ambavyo Suhail alielekezwa kua atakapoivua kwa muda mrefu Pete ile basi Nuru yake ni kali itaweza kuwafikia wale majini waliokuwa wakiisaka kwa udi na uvumba
Japo haikumdhihirikia waziwazi Komando Takadiri kua Nuru ile inatokea wapi lakini alianza kuifatilia kwa ustadi wa hali ya juu, huku nae kwa nyuma akifuatiliwa na Mzee Sufiani Bin Shamhurish
Katika chumba cha kipelelezi ambacho ndio ofisi ya Inspekta Kenjah, walikuwa wameketi huku wakitazamana, Alikuwa ni Inspekta Kenjah mwenyewe na Kopro Salum Marando alieleta taarifa ya uchunguzi mfupi alioupeleleza, hali aliyokuwa nayo yule Kopro ilimtisha sana Inpekta maana kijana alionekana kujawa na wahka wa hali ya juu
“Enhee Ongea ‘corporal’..” alianza mjadala Inspekta Kenjah
“Afande hali inatisha kiasi…” akakohoa kidogo na kuendelea “..Nimeenda kuonana na mkurugenzi wa ile Bar ya Break down baada ya kujitambulisha kua nimetoka kwako akanipokea vizuri sana na kunipa ushirikiana hatua kwa hatua..”
“Enhee matokeo ua ushirikiano wake..”
“Kabla ya akina Suhail na marehem Msigwa kuwasili pale Bar, Camera zilikuwa zikionesha magari kadhaa yaliyoanza kuwasili pale, magari hayo yalikuwa mengi tu ila kuna magari mawili japokuwa yalikuwa yameegeshwa tofautitofauti tangu yalipowasili hakushuka mtu yeyote na hatimaye tuligundua kua mpigaji wa zile Risasi alikuwa ameketi ndani ya moja ya gari hizo”
“Duh, gari gani hiyo?,” alisaili Inspekta Kenjah kwa wahka
“ilikuwa ni Prado ya rangi ya buluu, namba zake za usajili nimeziandika kwenye Report hapo juu, na hata baada ya tukio lile ile Prado ikatoweka hapohapo huku ikifuatiwa kwa kasi ileile na gari ile nyingine ambayo nayo tulichukua namba zake sa usajili, hii ilikuwa ni Bmw zile Old model”
“Kazi nzuri kopro,” aliongea Inspekta Kenja huku akimpa mkono kijana wake kwa kazi nzito lakini akakatishwa na maneno ya kijana yule
“Zaidi ya hilo Afande… Nimezifuatilia gari zile na nimefanikiwa kupata moja”
“Ipi hiyo?”
“Ile Bmw, alishuka kijana mmoja bila shaka anaeelekea kwenye utu uzima, japo anaonekana ni Bishoo tu lakini anaonekana ni mtu wa kazi yule”
“Kwanini unamuita Bishoo?”
“Japo alikuwa amevaa suti ya kawaida tu lakini kwa mtu wa umri wake asingepaswa kubandika meno ya dhahabu ndani ya kinywa chake”
“Nini? Meno ya dhahabu?,” alisaili kwa hofu Inspekta, Kopro Salum Marando hakujibu akafungua begi lake dogo na kutoa kamera yake aliyotumia kumpigia ile picha, haraka Inspekta akachukua ile Camera na kuiangalia picha ile, hakutaka hata kumalizia akaiweka juu ya meza Camera ile huku akishusha pumzi
“Tumevamiwa Kopro..”
“Kwanini afande?”
“Huyu ni muuaji hatari kutoka Uganda na hua anatumiwa na Mtandao mkubwa sana, anaitwa Joram Ndege, ni hatari huyo mtu..na sasa nimeanza kupata picha ya zile meseji ambazo Suhail alikuwa akilalamika kua zilikuwa zikienda kwa mkewe bila ya yeye kuzituma”
“Sasa anahusiana nini na hizo meseji?”
“Kuna taarifa nilipata kuambiwa kua Mtandao ule una mtambo maalum wa kunasa mawasiliano ya simu hizi za kawaida pia wanaweza kuandika wao meseji wakiwa hukohuko walipo kasha wakaituma kwenye namba yoyote waitakayo na wakaamua iingie kwa jina gani ulilolisevu wewe katika simu yako.. Sasa tukio hilo la Suhail ni la pili kutokea na tuligundua kua kuna uwezo huo kufuatia ile kesi iliyokua kule Msimbazi kuhusiana na yule mwanamke aliyekuwa akilalamika kua kuna meseji za aina ile zilionesha akiwa anawasaliana na namba ambazo hakuwasiliana nazo kamwe..” Kabla Inspekta hajaendelea akadakiwa na Kopro Salum
“.. Ooh nimeikumbuka hiyo kesi, sikia sasa Afande, unajua kua mume wa huyo dada aliyekuwa akilalamika alikuwa ndie huyo mwandishi wa habari alieuawa..Msigwa”
“Kweli eeh?”
“Hakika Afande”
Kikapita kimya cha haja huku kila mmoja akitafakari juu ya kadhia ile kabla ya Kopro kuuliza swali hewani
“Sasa inamaana Msigwa anahusika na mtandao huo?”
“Inawezekana maana jamaa hua wanatumia sana vyombo vya habari, sasa kwa mtu mpenda pesa kama Msigwa itakua walikuwa wakimtumia sasa labda wakatofautiana jambo au pengine alivujisha siri zao”
“Kama ni mshirika wao ikawaje tena meseji hizo za kubumba zikakutwa kwenye simu ya mkewe mpaka wakaachana”
“Hapo ndipo tutakapoanzia upelelezi”
*****
Wakati matukio hayo yakiendelea huko mjini, hali ilikuwa imechemka upande wa pili huko Bagamoyo ambapo Shekhia alikuwa anamalizia kutoa kafara ya damu kwa pete yake ili baada ya hapo sasa arejee tena Dar Es Salaam kuja kumaliza mchezo alioucheza nusu.
“NO, nadhani itakuwa busara kama upelelezi utaanzia kwa Sajenti Rwehumbiza,” alidakia Koplo Marando akimtaja askari mwenzie nd’o achunguzwe
“Rwehumbiza? Kwa lipi hasa?” Alimaka Insp Kenjah
“..Risasi moja aliyopigwa Msigwa haikutosha kuing’oa roho yake hata ikabidi apigwe risasi ya pili bila shaka na mkondo uleule wa wauaji.”
“Mbona sikuelewi Koplo!.. unataka kuniambia Marehemu Msigwa alipigwa Risasi nyingine tofauti na ile ya mwanzo?..”
“Afande, kama utathibitisha kuwa Msigwa alipigwa Risasi moja tu ulipokuwa naye basi akina Rwehumbiza ndio watakaopaswa kutujibu kuwa Risasi ya pili ilitokea wapi?”
“Kivipi?”
“..Iko hivi Afande, baada ya tukio lile la risasi wakati wewe ulipokuwa unaondoka haraka kujaribu kufuatilia muelekeo ulipotokea risasi ile mimi na Afande Chanzi tulikamilisha haraka sana taratibu zote kisha tukawa tunataka kumuwahisha hospitali yule bwana aliye kwenye jokofu muda huu… lakini ghafla akawasili Sajenti Rwehumbiza na kuniamuru kuwa nibaki pale kituoni wakati yeye na Afande Chanzi wakiingia ndani ya gari wakijitwisha jukumu la kumpeleka mgonjwa hospitali.. Majibu niliyatarajia tu kuwa Mgonjwa angefia nje ya hospitali.. na ndivyo ilivyokuwa” Inpekta Kenjah alibaki mdomo wazi asimwelewe vyema kijana wake huyu anayeongea kwa mbwembwe na kujiamini
“Risasi mbili? No, alipigwa risasi moja tu mbele yangu...” alisema Inspekta Kenjah na kuongezea “..Kwanini wewe ulihisi kuwa angefia nje ya hospitali?”
“Mtindo alioutumia Sajent Rwehumbiza kunipokonya jukumu lile la kwenda hospitali japo ni mkubwa wangu tena huku akitaka kushirikiana na Afande Chanzi ndio lilinipa udadisi zaidi maana huyu Chanzi si mtu mzuri sana… kama utakumbuka amekuwa akihusishwa na matukio kadhaa ya kutumiwa na wanasiasa, na hilo ndilo jambo lililomfanya akahimishiwa huku kituoni kwetu akitokea kule Msimbazi. Sasa baada ya kupata habari za kifo cha Msigwa niliwahi haraka Hospitalini nikaonana na daktari ndipo akanionesha vipimo vya uchunguzi wa mwili wa marehemu vinavyoonesha kuwa marehemu alipigwa risasi mbili.. moja kulia na nyingine kushoto mwa kifua chake..”
“E bwana eeh, hakika kuna mchezo mchafu hapa! Rwehumbiza na Chanzi wamehusika kummalizia Msigwa.. Kwanini hasa?!.. Wametumwa tu, na aliyewatuma hatujamjua, Lazima tumjue..” Kikapita kimya cha muda mfupi kabla ya Insp Kenjah kuendelea “..yatupasa kuwa makini sana katika hili lakini ni lazima tuwabaini na kuwatia chini ya chini ya uvungu wa Sheria” kikapita tena kimya cha muda mrefu huku kila mmoja akiwazua yake moyoni
“Sikiliza Koplo hii kazi iliyo mbele yetu ni kubwa kuliko inavyoonekana, kila kinachotokea sasa kinazidi kunithibitishia kua kuna mtandao mkubwa wa Mauaji ndani ya Nchi yetu, Joram Ndege ‘Meno ya dhahabu’ ni kiashiria tosha kua kuna kazi maalum inaendelea humu Nchini hivyo sasa tunaingia kazini, kufa na kupona, Mimi na wewe..”
“Sawa Afande, ila ninashauri tu kua ili kazi hii iwe rahisi hawa akina Rwehumbiza tutawachunguza kimyakimya bila kusema nao jambo lolote wakati tukiwa tunaendelea na upelelezi wa kawaida kwa Suhail, Bucha, Kassa, Lillian, na watakaohitajika.”
“Yeah, hilo jambo la msingi.. hata mimi ninafikiria kwenda kuongea na CP Kibila ili afahamu hatua kwa hatua lakini nahofia kuchanganya samaki mbichi na mchicha maana kama tayari kuna harufu ya wakubwa kuhusika hatuwezi kumjua mwema ni nani kwa sasa.”
Walijadili mengi mwishowe wakakubaliana namna ya kuanza, kwa hatua hiyo wakaafikiana kuwa Insp Kenjah aende akafanye uchunguzi ofisini kwa Suhail wakati huo Koplo Marando yeye atakwenda kufanya uchunguzi wake nyumbani kwa marehemu Msigwa, lakini kabla hawajatawanyika ikaingia simu kwa Inspekta Kenjah
“Hallow,” alipokea Leonard Kenjah kisha akawa akiisikiliza sauti itokeayo upande wa pili wa simu yake. Kadri alivyokuwa akisikiliza ndivyo alivyozidi kuonekana kuchanganywa na taarifa alizokuwa akipatiwa,
“Tukio lina muda gani?,” alisikika tena Kenjah akimsaili mtu aliyekuwa akisema nae na kuongezea tena “..Mmejaribu kunakili namba za gari hiyo?”
Maongezi yaliashiria kua kuna tatizo limeibuka huko itokeako sauti ya upande wa pili wa simu. Koplo Marando alikua akimshangaa tu mkuu wake akiongea kwa wahka japo hakutambua sana kinachojiri ndani ya simu ile
“Tuondoke haraka Koplo, mambo yameshaharibika huko,” aliongea Inspekta Kenjah baada ya kukata simu yake
“Kuna nini Afande?”
“Lillian..”
“Yupi?”
“Yule binti tuliepanga kumuhoji kuhusu Msigwa na Bucha.. ametekwa na maharamia waliomvamia wakati akitoka ofisini kwake, wametoweka naye kusikojulikana.”
“Hakuna waliemjua hata mmoja mmoja kati ya hao watekaji?”
“Hata namba ya gari ilikua ni ya kichina achilia mbali wao watekaji..”
“Aisee hii kali, nani amekupigia wewe?” Koplo Marando aliendelea kumuuliza Inpektah Kenjah wakati wakiwa wameshatoka nje ya ofisi kwa ajili ya kuanza msafara wao
“Kanipigia yule Mkurugenzi wa pale, Bwana Kassa, dah tumepoteza shahidi mwingine huyo.”
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi