NILIFANYA MAPENZI NA MAITI 20 ILI NITAJIRIKE (5)

Zephiline F Ezekiel

SEHEMU YA TANO
TULIPOISHIA...
Wakati ikiwa imefika saa nane usiku, hapo ndipo mganga yule akatokea hapo ndani na kunifuata. Kabla ya kuzungumza lolote, akaniangalia machoni, aliiona hofu niliyokuwa nayo.

“Upo sawa?” aliniuliza.

JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈

SASA TUENDELEE...
“Ndiyo! Nipo sawa na nipo tayari kwa kazi,” nilimwambia.

Alichokifanya mganga yule ni kuuchukua usinga wake, akaanza kuimba wimbo ambao sikuwa nikiuelewa. Aliimba kwa sauti kubwa iliyonifanya nione kama wale walinzi wangesikia lakini haikuwa hivyo.

Waliendelea kupiga stori huku mganga yule akiendelea na wimbo wake. Alipomaliza, akalifuata sanduku moja, akalitoa pale lilipokuwa. Nilibaki nikiwa nimeduwaa tu, sikuamini kilichokuwa kikiendelea, sanduku lilikuwa zito lakini yeye alivyolishika ilikuwa ni kama mtu aliyeshika kikaratasi.

Akaliweka chini, akalifungua na kisha kuiangalia maiti ile. Niliogopa, hata kusogea kule sikuweza. Wakati nimesimama huku nikiwa nimeduwaa, yule mganga akachukua unga fulani na kuipaka maiti ile kisha kuanza kuzungumza maneno ambayo sikuyaelewa, ghafla, katika hali iliyonishtua, nikaiona maiti ile ikiinua mkono wake.

“Mungu wangu!” nilisema kwa mshtuko, sikuamini kile nilichokiona. Mganga yule hakunyamaza, aliendelea kuzungumza maneno yale, mbali na mkono, ile maiti ikainuka na kisha kukaa kitako mulemule kwenye sanduku. Mpaka kufikia hatua hiyo, nilitamani kukimbia. Jasho lilinitoka.

Kuna kipindi nilihisi kile kilichokuwa kikitokea kilikuwa ni ndoto, nilitamani kukimbia lakini miguu ilikuwa mizito.

Kadiri muda ulivyozidi kusonga mbele ndivyo nilivyozidi kushikwa na hofu. Kumbuka kwamba hiyo ilikuwa usiku wa manane, tena tukiwa mochwari, najua umeshapata picha ni jinsi gani nilikuwa na hofu moyoni mwangu.

Yule mganga hakunyamaza, akawa anazungumza maneno ambayo sikuyaelewa kabisa. Aliponitupia macho niliyahamisha yangu na kuiangalia ile maiti iliyokuwa imeketi kitako kama mtu aliyekuwa akitaka kuzungumza na yule mganga.

“Usiogope Zakia,” aliniambia huku akiniangalia lakini nilikuwa na hofu.

Nikaanza kuyakumbuka maneno ya yule mganga aliyoniambia kipindi cha nyuma kwamba kama kweli nilitaka kuwa tajiri basi ilinibidi nikubali sharti la kufanya mapenzi na maiti ishirini, kwa hiyo ile maiti iliyokuwa mbele yangu ilikuwa ya kwanza.

Nilikubali lakini ndani ya mochwari ile lilionekana kuwa jambo gumu mno, kufanya mapenzi na maiti. Tena kama ile iliyokuwa ikitisha iliyoonekana kabla ya kuwa maiti, mtu huyo alipata ajali mbaya, kama si gari, basi ilikuwa treni kwani mwili wake ulikuwa na majeraha mengi.

“Njoo huku,” aliniambia yule mganga, nikaanza kusogea kule alipokuwa.

Akaniambia nikae kwanza, nilitakiwa kuvuta pumzi na sikutakiwa kuogopa. Nilikuwa kimya, nilikuwa na hofu sana nikiogopa.

Maiti ile ikafumbua macho yake na kuanza kuniangalia, kuna kipindi nilikuwa nikijiuliza kama kweli ile ilikuwa maiti au nilikuwa nikichezewa mchezo. Majibu ya Swali langu hilo lilipatikana kila nilipokuwa nikiuangalia mwili wake, ilionesha dhahiri kwamba ilikuwa maiti.

“Upo tayari?” aliniuliza mganga.

“Ndiyo! Ila….”

“Ila nini tena?”

“Nitaweza kweli?”

“Usijali! Utaweza. Kwani hujawahi kufanya mapenzi na mwanaume?” aliuliza mganga huku akiniangalia usoni.

“Nimewahi!”

“Basi jua hakuna tatizo,” aliniambia.

Nilibaki nikimwangalia tu, kuna kipindi nilijuta kwa nini nilitaka kuwa tajiri na wakati masharti ya utajiri wenyewe yalikuwa magumu kiasi hiki. Nilibaki nikisononeka lakini kumbuka kwamba nilitamani kuwa tajiri hivyo chochote kilichokuwa kinatokea mbele yangu, nilikubaliana nacho.

“Vua nguo zako,” aliniambia.

Wakati hayo yakiendelea ndani ya mochwari, wale walinzi hawakuwa wakijua kitu chochote kile, hawakutuona hivyo kufanya kila kitu kwa kujiachia. Baada ya kumaliza kuvua nguo zangu na kubaki kama nilivyozaliwa, akaniambia nipande juu ya meza, nikafanya hivyo, nikalala chali.

Ndugu yangu, ninachokwambia hapa ni kweli kabisa, kilinitokea katika maisha yangu, kipindi kile nilipokuwa nikisaka utajiri kwa udi na uvumba. Ghafla nikaiona maiti ile ikisimama kutoka ndani ya sanduku na kuanza kuvua nguo zake zilizokuwa zimechanikachanika kutokana na ajali, baada ya hapo, akapanda pale juu.

“Mkimaliza, utatoka nje, hili sanduku usiwe na hofu nalo, litarudi tu lilipokuwa,” aliniambia yule mganga na kisha yeye kutoka ndani ya mochwari ile na kwenda kunisubiri nje.

****

Kilichoendelea ndani, ni kufanya mapenzi na maiti ile. Huwa ninasikia maumivu mno moyoni mwangu kila ninapokumbuka mambo haya ambayo yalinitokea. Ninaamini kwamba mtu anapokufa, kuna roho huwa inabaki na ndiyo maana unapofika makaburini usiku, kuna sauti huwa zinasikika, mbali na roho iliyokufa, kunakuwa na roho nyingine ambayo bado ina uhai.

Hiyo ndiyo roho aliyokuwa nayo ile maiti, roho yake ya kwanza ilikuwa imekwishatoka na kwenda kwenye hukumu, iliyokuwa ikifanya yote hayo ni roho ya pili ambayo ilimpa pumzi.

Pale juu, niliendelea kufanya mapenzi na maiti ile, ilikuwa ni kama nafanya mapenzi na binadamu aliyekuwa hai. Nilisikia maumivu makali chini ya kitovu, nilipiga kelele lakini haikujali, iliendelea kama kawaida yangu.

Kitendo kile kilichukua dakika arobaini, ilipomaliza, ikasimama, ikavaa na kisha kuingia ndani ya sanduku lile. Sikuvaa, nilibaki kuangalia nione kitu gani kingetokea. Wakati imeingia kwenye sanduku lake, likajifunga na kuanza kuinuka, likajiingiza katika sehemu yake na kutulia.

Sikutaka kubaki humo, nilichokifanya ni kuinuka, kuvaa nguo zangu na kutoka ndani ya mochwari ile. Walinzi walikuwa wakipiga stori, sikujali, nikatoka mpaka nje, nilipofika huko, nikamkuta mganga akiwa na tabasamu pana kabisa huku akitingisha kichwa chake juu chini, chini juu kuonyesha kukubaliana na kile kilichofanyika.

****

Mganga alinipa uhakika kwamba kila kitu kingekuwa kama kilivyotakiwa kuwa. Kwa kweli nilimwamini sana na kuona kuwa hivi karibuni ningekuwa tajiri mkubwa mno nchini Tanzania na hivyo kurudi kijijini nikiwa shujaa.

Siku iliyofuata, mganga akaniambia nirudi nilipokuwa nikiishi ambapo sikutakiwa kumwambia mtu yeyote juu ya kile kilichokuwa kimetokea. Sasa ratiba ikawa ni kwenda kwa mganga kila siku, ananichukua kimazingara na kunipeleka mochwari ambapo kama kawaida nilikuwa nikiendelea kufanya mapenzi na maiti.

Siku ya kwanza niliogopa sana lakini siku zilivyoendelea kwenda, hofu ikaniondoka na hivyo kuwa na ushujaa mkubwa moyoni mwangu. Nilipitia mengi kipindi hicho, wakati mwingine nililetewa maiti zilizoungua moto, zilitisha sana lakini ilikuwa ni lazima nifanye nazo mapenzi, wakati mwingine nililetewa maiti zilizopata majanga mengine, zote hizo, nilivumilia.

Siku zilikatika mpaka nilipobakiza maiti moja. Mganga akaniambia kwamba hiyo sikutakiwa kufanya nayo kule mochwari bali nilitakiwa kufanya nayo sehemu nyingine kabisa, tena makaburini.

Kwa kweli niliogopa sana, sikujua kitu kilichonitisha kwani kiukweli kati ya makaburini na mochwari, mochwari kulitisha zaidi. Usiku, mganga akanichukua na kuniepeleka katika makaburi fulani yaliyokuwa jijini Dar. Nilipofika karibu na makaburi hayo, akaniambia niingie ndani ya eneo la makaburi na kisha kuelekea katika kaburi moja la jamaa mmoja aliyekufa miaka kumi iliyopita, huyo jamaa aliitwa Samweli Ramadhani.

“Nitalijuaje?”

“Utalijua tu, una uwezo mkubwa wa kulijua kaburi hilo, wewe nenda,” aliniambia mganga.

Wakati nimeingia ndani ya eneo la kaburi hilo, kwa macho yangu niliweza kuwaona wachawi, walikuwa zaidi ya ishirini, walisimama pembeni ya kaburi moja la mtoto ambapo maiti yake ilikuwa ikihitajika sana.

Sikujua kwa nini, sikufika pale kuwafuatilia achawi wale niliowaona ila wao hawakuniona, nilifika pale nikiwa na mambo yangu, hivyo sikujali. Nilitembea kwa tahadhari, makaburini kulitisha sana, kulisisimua kupita maelezo.

Nilipofika katika kaburi moja, nikasimama, sikujua kama lilikuwa lenyewe au jingine, nikasogelea kuangalia jina, nikakuta limeandikwa Samweli Ramadhani, nikashangaa, nimejuaje kama hilo kaburi ndilo lenyewe.

“Ila kwa nini maiti hii?” nilijiuliza, ghafla nikasikia mganga akinijibu.

“Kwa imani zetu wanadamu, tunasema jina la Samweli ni la Kikristo na Ramadhani ni la Kiislamu, hivyo ukifanya mapenzi na maiti hii, Wakristo na Waislamu wote watakuheshimu, na utajiri wako utamsisimua kila mtu,” nilimsikia vema mganga huyo.

Nilisimama huku nikiwa sijui nini cha kufanya, nilisubiri maelekezo, nikaisikia sauti ya mganga ikiniambia nisubiri, nikafanya hivyo, ghafla, katika hali ambayo sikuitarajia, nikaona hirizi kubwa ikiwa imefungwa kiunoni mwangu, ilikuwa nzito, kilichonishangaza, hirizi ile kama ilikuwa na moyo, kwani niliweza kuyasikia mapigo kama ya moyo yakidunda kutoka katika hirizi hiyo.

Mara ghafla, upepo mkali ukaanza kuvuma mahali hapo, matawi ya miti iliyokuwa makaburini hapo yakaanza kuyumbishwa huku na kule. Nikasikia kelele za watu wengi, sikujua zilitoka wapi lakini nilizisikia masikioni mwangu.

Nikaanza kutetemeka, mara nikahisi kama kuna mtu alikuwa nyuma yangu, sikugeuka kuona alikuwa nani, mtu huyo akanisogelea, na kunishika bega kwa nyuma, pumzi zake nilisikia vema karibu kabisa na masikio yangu . Nikashindwa kuvumilia, nikageuka nyuma, cha kushangaza sikuona mtu.

Wakati nikiendelea kutetemeka kaburini pale, ghafla nikaliona lile kaburi likianza kujifukua lenyewe na ndani yake kuona jeneza likiwa limefunguliwa na ndani yake hakukuwa na maiti yoyote ile, nikashangaa sana.

Mara ghafla mwili wangu ukaanza kusisimka sana, nikahisi tena kwamba nyuma yangu kulikuwa na mtu, nilitaka kugeuka, nikashindwa kufanya hivyo, nikahisi nikishikwa bega kwa nyuma, nilitetemeka zaidi, kijasho chembamba kikanitoka mno.

“Unanukia vizuri mpenzi wangu!” nilisikia sauti hiyo nyuma yangu, nikazidi kutetemeka.

“Wewe nani?” nilijikuta nikiuliza huku mihemo ya mtu huyo ikisikika vema nyuma yangu.

Niliuliza swali hilo huku nikitetemeka sana, nilitamani nipotee na kutokea sehemu tofauti na hiyo. Mwili haukuacha kusisimka, kuna kipindi niliyasikia kabisa mapigo yangu ya moyo yalivyokuwa yakidunda kwa nguvu.

“Mimi ni mpenzi wako uliyemfuata hapa makaburini, una ngozi laini sana, hakika wewe ni mwanamke wa ndoto yangu,” niliendelea kuisikia sauti hiyo.

Mara mguso wa mtu huyo ukahama kutoka begani mwangu na kuanza kuelekea chini, nilizidi kutetemeka mno, mikono yake ikahamia katika mgongo wangu na kuanza kuushikashika, baadaye akahamia katika kiuno changu,

USIKOSE SEHEMU IJAYO

Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi

Chapisha Maoni