SHEMEJI INGIZA POLE POLE (17)

Zephiline F Ezekiel
Mtunzi: Hans Charlz

SEHEMU YA KUMI NA SABA
TULIPOISHIA...
Usiku ulifika na tulipo maliza kula chakula sote tulielekea vyumbani mwetu huku tukiwa tumehakikisha kuwa nyumba yote imefungwa basi nilipokuwa chumbani nilimsubilia Erick mpaka ilipofika majira ya saa 5 usiku nae aligonga mlango.

"hallloooo ni mimi Erick Isabela"

"nakuja"

JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈

SASA TUENDELEE...
Nilifungua mlango nae kuingia ndani na alipoingia ndani nami kuufunga mlango na kurudi kitandani

"Isabela sio kamba nimekuja kwa kuuvuruga usiku wako lakini imenibidi nije maana asubui ulinionesha vitu nami kuvutiwa navyoooo"

"mmmmmmh Erick vitu vipi tena mimi nilikuonesha jana" nilijifanya kuwa nimesahau huku nikitaka nione alivyo shupavu kwenye kutoa madini mdomoni

"Isabela inamaana kwamba ujajua kile kilichotokea kati yangu wakati tukiwa tuna andaa chakula"

"niambie tu Erick uwenda nimesahau"

"okay sawa ni kuhusu hisia zangu ulizifanya kuwa kwenye msukumo ambao sikujua kabisa nifanye nini wakati huo"

Ilinibidi nijiongeze kuwa anataka nini wakati huo na ndipo nilipo mwambia

"Erick nikuulize kitu?"

"ndio niulize Isabela"

"Unanipenda kweli"

"yaah isabela nakupenda kupita kiasi kwani fikira zangu zote zakuwaza wewe kila kukicha?"

"nashukuru kusikia hivyooo lakini ningependa kukufahamisha ukweli juuu yangu kuwa kwa sasa mimi nilikuwa sikai kwa dada Amina"

"mmmmh kivipi yani na ulikuwa ukikaa wapi? aliuliza kwa mshangao sana Erick

"nilikuwa nimepanga na ni storia ndefu sana Erick kwani kulitokea kuto kuelewana kati yangu na dada Amina ndio nikachukua jukumu la kutoka na kwenda mahari kupanga na mpaka sasa niko hapa"

"okay sawa basi tutakuwa wote pamoja sawa"

"lakini naomba kama unanipenda usije nifanyia visa mbeleni nikaja kuumia bure na ni bora kuniambia mapema"

"sitofanya hivyo Isabela kwa maana mimi na mpango wa kuoa na chaguo langu nimelipata ambaye ni wewe isabela naomba uniamini sita fanya hivyo uzaniavyo wewe"

Nae alipo maliza kusema hivyo nae alisogea na kunikumbata huku nikiwa naonekana kuwa dhaifu kwake kwani wanawake tuliumbwa hivyo.

Basi nilimuomba tutakaa chini na kuongelea maswala yote yatakayo tuhusu mimi na yeye.

nili lala na kulipokucha kama kawaida tuliendelea na maisha huku mahusiano yetu na Erick yalianza.

Zilipita siku kazaa huku tukiwa tunaishi vizuri mimi pamoja na Erick huku mahusiano yetu yalianza kushamili kwa kasi kubwa huku nikisahau yale ya shemeji Erinest na ndipo siku moja ilinibidi nitoke na kwenda kwa dada amina huku nikiwa nawaza pindi tutakapo kutanisha sura zetu lakini sikujali kwa hilo kwani nilikuwa naenda kwa ajiri kwenda kupatana na dada kwani nilijiona na makosa japo kuomba samahani kwa yale yaliyotokea.

Nakumbuka siku hiyo ilikuwa ni siku ya wikendi majira ya mchana na kufika kwa dada Amina na kuugonga mlango wake nae Erinest kuufungua mlango na aliponitizama tu allishangaa sana

"mmmmh Isabela karibu"

"asante"

"ingia ndani lakini Amina katoka kidogo"

"okay sawa wala usijali shem"

Niliingia mpaka sebureni na kukaa kwenye kochi nililikuwa nimelizoea na sikukaa saa nae dada Amina aliingia ndani na alipofika na kuniona

"umefata nini hapa naomba utoke kwangu isabela"

Nilishindwa kuongea kwani dada amina alizidi kurusha maneno ambayo yalipelekea mpaka mimi kuanza kulia na ndipo nilipo piga magoti huku nikimfata dada amina na nilipo mfikia nilimshika miguuu nae alinisukuma na kudondoka chini lakini sikutaka kukata tamaa na kurudi tena huku shem Erinest akiwa yuko pembeni akitizama kile kilichokuwa kikiendelea.

Nani nilizidi kumwomba msamahaa dada amina lakini nae alianza kulia tu huku akiishiwa nguvu huku akikosa maneno kwani nae aliangua kilio huku nami pia nikiangua kilio hicho.

Na ndipo dada amina alinyanyuka na kuniangalia sana huku mimi nikiona aibu sana kwa kile nilichofanya nami niliona chochote atakacho hamua kwangu sawa nae alinyayua mdomo wake na kuanza kuniambia

"Isabela isabela wewe wakunifanyia hivi dada yako siamini" alijawa na mtetemo ndani ya mdomo wake na kushindwa kuongea tena na kukimbia chumbani mwake huku akilia.

Nilibaki nikiwa sina Amani kwa kile alichokuwa kaonesha dada amina kwa kunikimbia huku nikifikilia ya kuwa huwenda dada amina ataki kuniona tena au vipi nilibaki nikijiuliza sana kwa kile nilicho jionea lakini nilivuta subira na kujisemea moyoni "huwenda ni hasira"

shem Erinest alikuja na kuninyanyua mahari nilipokuwa nimedondokaaa na ndipo nilipo nyanyuka.

"Isabelaaaa kulikoni tena wala usijali atakusamehee tu okay" Erinest aliongea na kunipa moyo

"mmmmh kweli maana naogopa sasa akitoka ndani itakuwaje" nilimjibu huku nikiwa naagalia mlango wa dada amina endapo akitoka nimuone maana anaweza kutoa uhai wangu niliofia hicho

"wala Isabela usiogope kwani ni vyema umekuja na kuliko kutokuja"

Nilibaki nikiwa nawaza tu dada amina pale atakapo toka ndani nitakuwa vipi endapo akija na kitu cha kunidhuru. sikuwaza sana nae alitoka chumbani na nilipo mwona tu moyooo wangu ulishituka sana kumwona mkono wake uko nyuma huku akija mahari nilipo huku akiniangalia sana na alipofika na kulitaja jina langu "ISABELAAAAAA!!!!!!!!"

nilishituka sana na kubaki nikiwa kimya huku nikimtizama nae aliongea huku mimi nikiwa natetemeka sana kwani nilipatwa na mtetemo mahari nilipo huku nikitega sikio langu kwake

"Isabela nimeumia sana kwa kile ulicho fanya kwa mpenzi wangu na huku ukijua fika hasa navyo mpenda mnoo!! Erinest lakini hakuna jinsi wewe bado utakuwa mdogo wangu"

niliendelea kumsikiliza huku nikiwa makini sana maana dada amina hubadilika ndani ya dakika 1 ya maeongezi nae aliendelea

"Sina budi kuweka chuki kati yangu na wewe kwani inauma lakini moyo wangu kwako uko mweupe kwani umejua kosa lako na kuja kuniomba msamahaa basi nami nimekusameheeee Isabela"

Alipo kwisha kusema neno la mwisho nami nilibadilika na kuwa na furaha na kunyanyuka mahari nilipo na kumfata na kumkumbatia huku nikitwokwa na machozi na kumwmbia

"Asante sana dada kwani alikuwa ni shetani alinipitia kufanya upuuzi huo basi nami sito fanya tena hivyoooo"

"sawa Isabelaaaaa!!!!"

Nilikuwa mwingi wa furaha huku nikiamini kuwa sasa niko free kuwa na Erick mda na mahari popote bila kuwa na buguza au usumbufu hulio kuwa ukipelekea kuwa na hofu na wasiwasi pindi nimuonapo Amina na shem Erinest.

Basi dada Amina aliingia chumbani mwake huku akiniacha sebureni mimi pamoja na Erinest na ndipo Erinest aliponisogerea karibu yangu huku nikiisi kuwa ni mtego uwenda dada amina kaingia ndani aone tena kuwa bado au naendelea na mchezo mchafu.

"Erinest nakueshimu sana naomba kaa mbali nami unataka nini tena kwangu au unataka kunikorofisha tena na dada amina kwa mara nyingine tena au?"

Erinest alibaki akinitizama kwa maneno niliokuwa nimekwisha kuongea mda huo basi

nae alibaki akiwa kwenye mshangao mkubwa lakini mimi sikujali nae akasikika akisema

"usifanye hivyo isabela wajua fika kila kitu"

"Erinest yaliopita sindwereeeeee tugange ya jayoooo hayo ya nyuma achana nayo angalia ya sasa" Nilimjibu Erinest huku nikipatia mafumbo makali mnoooo

"wa maanisha nini hapo Isabela?" aliuliza Erinest

"kwa sasa Erinest mimi na mtu mwingine na siku si nyingi nitamleta kwenu kumtambulisha"

Nilipoongea tu hivyo shem Erinest alibaki akiwa ana shangaaa na ndipo nilipo geuka kuanza kupiga hatua za kutoka ndani ya nyumba Erinest alinishika mkono na kusema

"usemayo ni kweli au?

"ndiyo tena ni ukweli toka moyoni kwa sasa niko na mpenzi" nilimjibu Erinest

Basi nami nilitoka nje ya nyumba hiyo na kugeuka tena kuitizama mara mbili kutokana na kile kilicho tokea ndani ya nyumba hicho kilinifanya kuwa na furahaaa huku nikimuombea dada amina kuwa na ukarimu kama huo tena na tena.

Nilirudi nyumbani kwa Erick na nilipofika niliingia ndani na kumkuta Erick akiwa sebureni basi ilinibidi nikae nae ili kumueleza kila kitu kilichokuwa kikinipa shida na msongo wa mazwazo lakini nae alikuwa muelewa na alinielewa.

Zilipita siku kazaaa na maisha yangu yakawa mazuri na yenye furaha kwani Erick alionekana kunijari na kunipatia kile nilichokuwa nataka na kwa wakati sitahili na ilibidi tufanye mipango ya kufunga ndoa huku kikwazo kikaonekana kuwa baraka za wazazi zinaitajika nami kuwaza kufunga safari na Erick mpaka kijijini kwetu nilipo zaliwa lakini yote nilimuhusisha dada yangu Yolanda kwa yote nilio kuwa naenda kufanya basi Tulisafiri mimi pamoja na Erick mpaka nyumbani na nilipofika tu nilikuta kijiji kimebadilika mpaka kupelekea kupotea nyumbani mpaka mwanakijiji mmoja alitusaidia mpaka kutufikisha kwetu huku Erick akiniona kuwa sikuwa na pakumbuka nyumbani kwetu.

Tulipofika majira ya mchana mama hatukumkuta na kumkuta kaka yangu Gabriel nae aliponiona tu alifurahi sana

Gabriel "dada Isabela karibu sana"

isabela "Asante Gabriel"

Gabriel "mda sana dada mpaka kupelekea kukusahau"

Isabela "yaaaah! kaka lakini sikupata nafasi ya kuja huku"

Gabriel "wasa dada wala usijali japo umerudi hakuna tatizo lolote"

Isabela "mama kaelekea wapi"

Gabriel "Yupo shambani toka asubui lakini mda hiii ndio huwa narudi"

Nilimkaribisha Erick kiti huku mizigo nikiipeleka ndani ili kumsubiria mama arudi toka shamba.

Nae mama alifika kutokea shamba basi nae alipofika karibu na kutuona alianza kuimba kimira huku akitukaribisha kwa shangweeee na alipofika moja kwa moja alikuja kwangu na kunishika huku akiniamgalia sana mwili wangu na kunizunguka.

Mama "mwanagu! mwanangu! mwanangu! isabela karibu sana"

isabela "asante mama"

Mama "mwanangu kipi kilikupelekea mpaka kusahau kwenu"

isabela "mama mambo madogo tu mama lakini nimekuletea mgeni mama umuonae mbele ya macho yao"

Ndipo mama alisalimiana na Erick na kunivuta pembeni na kuniuliza nami nilimwambia ndiye niliye mchagua basi mama alijawa na furaha sana kwani hakutegemea.

Basi niliingia jikoni na kuandaaa chakula ambacho tulijumuika wote mimi pamoja na Erick mama na kaka yangu Gabriel.

Zilipita siku mbili tukiwa nyumbani mimi pamoja na Erick tuliaga huku mama aliweka baraka zake juuu ya ndoa yetu na kurudi mjini.

Erick alifanyaa mpango wa kufunga ndoa nayo mipango ilikuwa ikienda vizuri mpaka hapo siku ilipo wadia nami kwenye shera pembeni yangu Erick akiwa na suti nzuri kupita kiasi chake basi tulifunga ndoa na kuitwa mama huku nikibahatika kupata watoto wawili John pamoja na Heriet.

"Na ndipo ndoto yangu ya kuitwa mama ilitimia siku hiyo!!!!!!!!!!!!!!! nami kujifunza kuto waacha wtoto wangu kutanga tanga na maisha huku nikiwawekea msingi wa kuwa na HEKIMA"

MWISHO

Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi

Chapisha Maoni