
Mtunzi: Halfani Sudy
SEHEMU YA NNE
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
Tena wengine hawakuwepo hata katika ile sherehe yenyewe lakini ndio walikuwa wasimuliaji wakubwa. Vijiwe vyote vya waambea waliipa sana 'airtime ' habari hii ya bwana harusi kukimbia katikati ya sherehe kuliko habari ile ya ajari.
Kule Kilwa Kivinje majeruhi wote sasa walikuwa wodini. Dokta Yusha alifanya kazi kubwa sana usiku ule.
JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈
ENDELEA...
Yeye mwenyewe alifanya kila kitu kuhakikisha majeruhi wote wanapata huduma. Na ile maiti ya mama Nasra ilipelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti na kusubiri taratibu zingine za mazishi ziendelee.
Hadi Asubuhi, Dokta Mkuu wa hospitali ya Kinyonga, Zaidi Kilumba, Dokta Mkuu wa upasuaji Sharifa Juma, na Dokta anayesimamia chumba cha kuhifadhia maiti, Dokta tamaa Karimu walikuwa hawajawasiri kazini, na wala simu zao zilikuwa hazipatikani.
Hospitalini walikuwa wanafanya kazi manesi, wakishirikiana kwa ukaribu mkubwa na Dokta Yusha.
Hadi saa sita mchana, majeruhi wale wanne walikuwa hawajapata fahamu. Hali ilikuwa tete. Dokta Yusha alifanya kazi kama punda, huku akimshukuru Mungu kwa kuwa alikuwa na likizo kwa ajili ya mapumziko ya ndoa yake.
Madaktari wengine katika hospitali ile, hawakuwa na ari kabisa ya kufanya kazi.
Saa kumi na mbili jioni, kazi ya Dokta Yusha ilianza kuleta mafanikio. Mzee Mpaukha alirudiwa na fahamu. Alifumbua macho taratibu akiwa mbele ya nesi aliyekuwa karibu na kitanda chake.
"Niko wapi hapa?"
"Tulia baba, uko sehemu salama"
Nesi alimjibu huku akiweka vizuri dripu ya maji ilikuwa inaingia mwilini kwa Mzee Mpaukha.
Mzee Mpaukha, alifumba macho na kutafakari. Matukio yote yaliyotokea usiku uliopita yalijirudia mithili ya sinema. Tangu wakiwa ukumbini hadi gari lao lilivyoacha njia.
"Tunakufaaaaaaa!"
Mzee Mpaukha alitoa ukelele mkubwa akiwa pale kitandani. Ukelele huo uliokuwa na faida ndani yake. Ukelele ule alifika moja kwa moja katika masikio ya Musa, na kumuamsha Musa, dereva wake, toka katika usingizi mzito aliolala kuja duniani. Musa naye aliunga kumsaidia Mzee Mpaukha
"…..kufaaaaaaa"
Nesi sasa akakimbia kwa kasi kwenda katika kitanda cha Musa. Huku akimshukuru Mungu kwa kuweza kuwaamsha wagonjwa wawili kwa mpigo, tena katika njia ya ajabu.
Nusu saa baadae, Dokta Yusha aliwasiri, alipatwa na furaha isiyo na kifani kukuta wagonjwa wake wawili wamerejewa na fahamu. Ilikuwa faraja kubwa sana kwake. Asilimia hamsini ya kazi alikuwa amefanikiwa. Walipoteza fahamu wagonjwa wanne, wawili walikuwa wamerejewa na fahamu zao na kubaki wawili…
TANO, baada ya kushindwa mpango wake wa kumuua Dokta Yusha usiku ule. Alirudi mafichoni kwa wenzake kujipanga upya. Usiku wa siku uliofuata kundi lile hatari la SIX KILLERS walikuwa na kazi kuu mbili.
Kwanza Kuhakikisha utoaji wa mioyo kwa maiti zilizokuwepo katika chumba cha kuhifadhia maiti unafanyika bila wasiwasi wowote.
Pia kuhakisha Dokta kijana anayejifanya ana morali ya kazi, Dokta Yusha anauwawa.
Kwa kushirikiana na wale madokta wasiokuwa na maadili ya kazi waliamini watafanikiwa katika malengo yao hayo mawili.
Jioni ya siku ile familia ya Dokta Yusha, ilikwenda hospitali kuwaangaalia wenzao. Yalikuwa majonzi makubwa sana baada ya kusikia mama Mpaukha alikuwa amefariki. Na ndugu wengine wa Mzee Mpaukha nao waliwasiri, na waliamua kuuchukua mwili wa mpendwa wao usiku wa siku ile ili kwenda kufanya maandalizi ya mazishi.
Hadi muda huo, madaktari wakuu katika hospitali hiyo walikuwa hawajulikani walipo. Nia yao ilikuwa ni kukaa mafichoni muda mrefu ili idadi ya watu watakaofariki waongezeke, ili mradi wao wa kupata mioyo kumi na tano kila siku ukamilike. Walijua wasipokuwa kazini wao, wagonjwa wengi watakufa.
Saa nne kamili usiku, mganga Mkuu wa hospitali ya wilaya ya Kilwa, ndugu Zaidi Kilumba, Daktari Mkuu wa upasuaji Dokta Sharifa Juma, Mkuu wa chumba cha upasuaji, Dokta Tamaa Karimu, wale manesi watano, na kundi zima la SIX KILLER waliwasiri katika eneo la hospitali ile, kwa magari aina mbili tofauti. Madokta na manesi walipanda gari yao na lile kundi hatari walipanda gari yao. Walitofautiana kufika eneo la hospitali kwa dakika kumi tu, wakitangulia wale madaktari. Walikuwa wamekuja kufanya kazi ya kutoa mioyo ya maiti, wakifuatiwa na gari la kundi la hatari la Six Killers waliokuja kulinda hali ya usalama pale hospitali, na kumuua daktari aliyeonekana kizuizi kwa kazi yao, Dokta Yusha.
Wale madaktari waliposhuka tu pale hospitali, walilakiwa kwa furaha na bashasha kubwa sana toka kwa Dokta Yusha. Lakini wao hawakuonesha kabisa sura za furaha, haikuwa kama ilivyo kawaida yao kila walipokuwa wanakutana hapo kabla. Madaktari wale walionesha sura zilizoonesha dharau na kiburi.
Madaktari wote watatu walikataa kushikana mkono na Dokta Yusha wakati wa kusalimiana ! Waliuacha mkono wa Dokta Yusha ukielea hewani.
"Hivi wewe hiki ni kituo chako cha kazi, au unataka kutuaminisha kwamba wanaopanga vituo hawana akili?" Dokta Sharifa alimuuliza swali kwa dharau Dokta Yusha.
Dokta Yusha hakujibu swali lile, alitumbua macho kuonesha mshangao wake. Aliwaangalia kwa zamu madaktari wale. Wote walionesha kutojari kabisa mshangao wake.
"Au unahamu…..?" Dokta Kilumba nae aliuliza swali lililoelea hewani, bila kutanabaisha Dokta Yusha alikuwa na hamu ya nini.
"Mbona siwaelewi ndugu zangu" Dokta Yusha aliongea kwa sauti ndogo iliyokuwa ikiashiria kutoelewa kinachoendelea.
"Naitwa Tamaa Karimu, unaitwa Yusuph Shaweji, sina undugu na wewe na wala sijawahi kuwa na undugu Na wewe, labda hawa wenzangu ndio ndugu zako"
"Nani, mimi nitakuwa na ndugu kama huyo?" Dokta Sharifa alirukia kwa mtindo wa swali.
"Lazima niwe makini, kuna kitu kinaendelea" Dokta Yusha alijionya mwenyewe kimoyomoyo.
Wakati wanaongea na Dokta Yusha, lile kundi la wauaji walikuwa wamejipanga vizuri kule katika chumba cha kuhifadhia maiti. Tayari kwa kulinda usalama ili wale madaktari waje kufanya mchezo wao hatari. Mchezo wa kutoa mioyo ya maiti ! Pale walikuwa wanamchanganya tu Dokta Yusha ili kupoteza umakini wake, na kuwapa nafasi kundi la Six killers wajipange vizuri kule katika chumba cha kuhifadhia maiti.
Na walifanikiwa !
Usiku uleule wa saa nne, familia ya Mzee Mpaukha walijipanga kwenda kuchukua mwili wa mpendwa wao kule chumba cha kuhifadhia maiti. Walikuwa wanamsubiri Dokta Yusha tu ili waende kuchukua mwili wa marehemu. Walikuwa wameshaongea na Mkuu msaidizi wa mhifadhi wa chumba cha maiti. Bila kujua Mpango hasi uliokuwemo katika chumba kile…..Balaa !
Alivyotoka kuongea na madaktari wale waliombadirikia, Dokta Yusha moja kwa moja alienda wodini. Hali aliyoiacha wodini ndiyo aliyoikuta. Hadi muda ule. Ni Mussa na Mzee Mpaukha tu ndio waliorejewa na fahamu. Dokta Yusha alisogea hadi kitanda alicholazwa mke wake kipenz, Nasra, alikaa pembeni ya kitanda kile. Huku akimwangalia mkewe aliyekuwa amefumba macho. Akiwa amehama kabisa katika Dunia hii. Mwanamke aliyekuwa nusu mfu kwa sasa. Aliangalia jinsi dripu ikivyotiririka taratibu katika mishipa laini ya Nasra.
Wakati Dokta Yusha akiwa pale na mkewe, Dokta Kilumba aliingia mle wodini. Alisogea taratibu hadi pale kitandani alipokuwa amekaa Dokta Yusha. Taratibu Dokta Yusha aliacha kuiangalia ile dripu na kumwangalia Dokta Kilumba. Dokta waliyetoka kugombana naye punde tu kule nje.
Dokta Kilumba alipofika pale naye hakuongea. Alikaa pale kitandani, karibu kabisa na Dokta Yusha, kiasi kwamba magoti yao yaligusana. Hali ya ukimya iliendelea kama dakika tatu, ndipo Dokta Yusha alikiharibu kimya hiko.
"Vipi Dokta, mbona umekuja kimya kimya halafu hauongei ?"
"Tusamehe Dokta, haikuwa dhamira yetu hali ile itokee"
"Msijari mambo ya kawaida tu kupishana kauli"
Baadae walielewana. Na kuanza kuongea mambo mbalimbali.
Dokta Kilumba alikuja kuongea na Dokta Yusha kwa dhamira maalum. Dhamira mbaya kabisa. Ni kuchelewasha muda kwa Dokta Yusha kwenda kule chumba cha kuhifadhia maiti kuchukua maiti ya mama Mpaukha. Kwa kuwa na maiti ya mama Mpaukha ilikuwa katika orodha ya maiti zilozotakiwa kutolewa moyo siku ile !
Kule nje familia ya Mzee Mpaukha walikuwa wanamsubiri Dr Yusha atoke wodini kuangalia hali za wagonjwa, ili waende naye kwenda kuchukua maiti yao kule katika chumba cha kuhifadhia maiti.
Bila kujua lengo la Dokta Kilumba, Dokta Yusha aliendelea kuongea nae. Alifurahi sana kuelewana na daktari yule Mkuu, alijua itakuwa rahisi sana kuwasimamia wagonjwa wake kwa kuelewana na Dokta yule.
Kule katika chumba cha maiti hali ilikuwa ya kutisha. Ilihitaji mtu jasiri kuangalia kilichokuwa kinaendelea. Mioyo kumi na nne toka katika maiti kumi na nne ilikuwa imeshapatikana tayari, na kuhifadhiwa katika deli moja kubwa jekundu!
Sasa ilikuwa zamu ya kutolewa moyo wa kumi na tano, ili kukamilisha idadi yao ya siku ile. Kisha baada ya hapo wakachungulie katika akaunti zao kitaongezeka nini. Waliikumbuka sana ahadi ya Don Genge.
Hali ndani ya chumba cha kuhifadhia maiti ilikuwa ya utulivu sana. Kila mtu akifanya kazi yake kwa umakini mkubwa. Utafikiri walikuwa katika operesheni moja muhimu sana ya kuokoa maisha ya mtu. Kumbe walikuwa wanafanya vitendo vya kinyama sana!
Dokta Sharifa alikuwa ameshika kisu maalum kwa ajili ya upasuaji, mbele yake kulikuwa na kitanda kidogo kikichotumika kulaza zile maiti wakizozitoa mioyo!
Dokta Sharifa alikuwa anapasua maiti na kutoa moyo kisha kuishona tena miili ya marehemu. Wale manesi walikuwa wanafanya kazi ya kubeba maiti na kuzileta pale kitandani, kisha kuzirejesha katika sehemu zao baada ya kufanyiwa upasuaji na kushonwa na Dokta Sharifa. Dokta wa kike katili !
Dokta Tamaa yeye alikuwa anasimamia kazi kama inaenda vizuri, ndiye alikuwa Mkuu kwa muda ule, wakati Dokta Kilumba hakuwepo.
Nje kulikuwa na ulinzi imara. Walinzi wote sita wakiwa na bunduki, walikuwa wamekizunguka chumba cha kuhifadhia maiti , tayari kwa kupiga mtu au kitu chochote kitakachosogelea chumba kile. Walikuwa makini, Kuhakikisha hawafanyi kosa lolote la kiufundi.
Manesi wawili walienda kufungua kabati moja la kuhifadhia maiti. Walivuta droo taratibu. Sura ya maiti yule ilikuwa inaonekana vizuri. Sura tulivu kabisa, sura ya kipole, sura isiyokuwa na hatia yoyote, sura ya mama Mpaukha. Wale manesi wawili waliitoa maiti ile na kuilaza vizuri kwenye machela. Waliisukuma machela ile kuelekea pale alipokuwa Dokta Sharifa, ili Dokta afanye kazi ile ya kikatili !
Kazi ya kuutoa moyo mwili ule, mwili wa mkwe wa Dokta Yusha.
Mwili wa mama Mpaukha ukawekwa katika kile kitanda maalum kwa kazi hii ya kikatili!
Dokta Sharifa alinyanyua mkono wake wa kulia ulioshika kisu juu,
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi