MKONO WA JASUSI (22)
Jina: MKONO WA JASUSI Mtunzi: Richard Mwambe SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI ILIPOISHIA... “Tungemmaliza lakini sijajua anatuzidi vipi akili, kila tukipanga hili, yeye yupo sekunde kadhaa mbele,” Robinson akaeleza. Kikao hicho cha dharula kikaendelea kwa dakika kadhaa na kumalizika kisha kila mtu kurudi katika shughuli zake. JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media ? IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI 👉 GUSA HAPA KU-INSTALL 👈 ENDELEA... KAMANDA AMATA aliegesha gari yake nje ya jengo kubwa la ofisi za shirika moja la simu, katikati ya jiji la Ontario . Mbele yake alikuwa akiitazama gari iliyombeba Lereti na watu wake ambao waliingia Ontario kwa tofauti ya saa tatu tu na Amata. ‘Ni yeye!’ alijiwazia alipomwona Lereti akiingia ndani ya gari hiyo huku walinzi wake wakimlinda kama kawaida. Walipoondoka naye akawafuatia nyuma nyuma bila wao kujua mpaka pembezoni kidogo mwa jiji hilo ambapo kumesheheni mahoteli makubwa ya kifahari. Ontario Paradise , ilikuwa hoteli ya kisasa nje kidogo ya jiji h…