MAUAJI YA KASISI (20)

Zephiline F Ezekiel

SEHEMU YA ISHIRINI
ILIPOISHIA...
Maria alimsimulia Otho juu ya Yule kichaa na maneno tata aliyomueleza na pia jinsi alivyomtoweka kimiujiza. Otho alimsikiliza bosi wake mpaka alipomalizia mkasa huo.

“Ila majamazi sio watu aisee, kinachonichanganya wakati wa mapambano yetu, kuna gari nyingine ilikuja na kumchukua cheetah na hilo begi kisha wakaondoka zao,

JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈

ENDELEA...
akiwa amegubikwa na mawazo, hasira na chuki kwa mtu asiyemjua, aliona wazi kuwa mtu huyo amekwamisha harakati zake zote.


MEZA MOJA iliyokuwa mbele ya kijana mtanashati, Melchior Ndege, ilibeba bia aina ya tusker na vitafunwa kadhaa. Kijana huyu aliyekuwa akinywa bia yake taratibu kana kwamba hana haraka katika hilo alionekana akipepesa macho yake huku na kule kuona kama Yule anayemsubiri amefika au la. Pembeni kukiwa na wateja wengine lakini yeye halikumfanya kujali hali hiyo, aliendelea taratibu kubarizi kwa macho akina dada warembo wanaojipitisha mbele yake, wakizani kuwa labda wangeitwa lakini wapi, hakukuwa na muito wala mruzi. Muda ulizidi kwenda, Ndege hakumuona mgeni wake, akili ikaanza kumzunguka, nini kimetokea maana muda wa ahadi yao ulishapita kwa dakika arobaini na tano na zaidi.

§§§§§

Mwanamke mmoja wa makamo kidogo aliteremka kwenye tax hatua chache kutoka katika jingo la mikutano la Kenyatta (KICC), alipokwishamlipa dereva tax alivuta hatua chache kulielekea jingo hilo, akaingia ndani na kutazama huku na kule, usalama ulikuwepo, akaiendea lifti na kubofya kitufe Fulani, dakika moja baadae mlango ule wa alluminium ulifunguka na Yule mwanamama kujitoma ndani, kidole chake cha kati kilichobeba pete kubwa ya haja, kikabonyeza namba 5 na 0 yaani 50, ile lifti ikamnyanyua na kumfikisha ghorofa ya juu kabisa, akashuka na kuiendea kaunta.

“Tusker tafadhali,” aliitisha tusker ambayo ilikuja maramoja na kuanza kuimiminia tumboni mwake, huku akiangalia kwa makini Yule mwenyeji wake asiyemjua. Hapa na pale alianza kumuhisi kijana mmoja aliyeketi pembeni kabisa katika meza ya peke yake, akashuka na kuielekea ile meza huku akimuambia mhudumu amletee bia yake pale.

“Naweza kujiunga nawe? Maana naona u mpweke sana,” Yule mwanamama alimueleza Ndege. Melchior alimtazama Yule mwanamama kwa makini, macho yake yalipanda na kushuka mpaka kifuani ambako hakuona matiti ya asili isipokuwa ya kuchonga, akacheka na kutikisa kichwa, “Kamanda Amata, salute kwako. Jinsin ulivyojiweka sikukutambua kabisa, hakika hakuna anyeweza kukutega kwa ubaya maana unajua jinsi ya kukwepana na kifo,” Ndege alimueleza Kamanda Amata ambaye alijitupia ndani ya vazi maridadi la kike na kuonekana wazi kuwa ni mwanamke, akiwa ameondoa ndevu zote kidevuni mwake, vipodozi na mekap alizojipaka zilimfanya aonekane mmoja kati ya wanamama mashangigi wa kutoka Mombasa.

“Wewe ni nani?” Amata aliuliza sasa kwa sauti yake ya kawaida, huku mkono wake wa kulia ukiwa ndani ya pochi ambayo ililazwa mezani. Melchior Ndege alielewa ishara hiyo alijua wazi kuwa Kamanda Amata ndani ya pochi hilo amekamata bastola tayari kwa lolote, alimtazama macho yake na kuyaona hayana masihara hata kidogo.

“Melchior Ndege, idara ya usalama wa taifa Kenya,” Ndege alijibu.

“Umenifahamia wapi?” Amata aliuliza

“Kamanda, tulikutana Arusha kwenye kozi ya kiintelijensia pamoja na watu wa Cuba na USA” Ndege alijieleza.

“Sasa naanza kukumbuka, kijana wa Bwana Shikuku, siyo?”

“Hapo umenena,”

“Inaonekana umekuwa ukinifuatilia sana, kwa nini?” Amata aliuliza.

“Hapana, sikufuatilii, ila nilikuona mara moja katika hali ambayo nilijua wazi upo katika hatari, tangu hapo nikaanza kukulinda kuhakikisha hushuriki na nilijua wazi kuwa umekuja kwa ajili ya Bill Van Getgand,” Ndege alipoeleza hayo, Amata alikunja sura kidogo kwa mshangao.

“Wapi?” Amata akauliza.

“Ujio wako kamnda ulijulikana tangu ukiwa JNIA pale Dar es salaam, watu wa Bill ambao walitapakaa kila kona iliyotia wasiwasi walikuona na kutoa taarifa huku kwa Bill, mpaka unatua JKIA hapa Nairobi walikuwa wamekuweka kwenye target yao, hawakupenda kukumaliza ila walitaka wajue hasa kuna nini ulichokifuata, watu wangu niliowatega pale uwanja wa ndege wa Jommo Kenyatta walinipa taarifa kuwa watu wa Bill wapo pale na inaonekana kuna mtu wanamsubiri, bahati mbaya hawakufahamu wewe. Hivyo nilifika na kuwafuata kwa nyuma, nilitazama ratiba ya ndege kujua ndege ile ilikuwa ikitoka wapi, nikaambiwa ni kutoka Dar es salaam, hisia zikaanza kunicheza juu yako. Ulipoingia hotelini pale Plazza wale jamaa walibaki nje wakisubiri labda kukuvamia au sijui kufanya nini, mimi niliondoka kwa kuwa niliitwa ofisini ambako nilipewa taarifa iliyonikosesha raha kabisa.” Ndege alitulia na kupiga funda moja la bia.

“Taarifa gani?” kamanda aliuliza

“Niliambiwa na Bwana Shikuku kuwa FBI wamesema sisi tuachane na Bill, wao ndio watakaofanya kazi ya kumnasa, nilihuzunika sana, nikaamua kuondoka zangu kwenda kutafuta sehemu ya kutuliza mawazo kwa muda, ndipo nilipopita pale Safari Park Hotel, na kukuona wewe pamoja na wale jamaa wane na mwanamke mmoja, kwa jinsi walivyojipanga tu nilielewa umetekwa, nikabadili mawazo nikaingia hotelini humo mpaka casino walipokupeleka na kufuatilia kila kitu. Pole sana Kamanda, Bill alidhamiria kukuua, hakukupa sumu kwenye pombe kwa maana nyote mlikunywa chupa moja, bali sumu ilikuwa kenye vipodozi vya Yule mwanamke aliyekupa akustareheshe, vuta kumbukumbu Kamanda, nilikuwa nafuatilia kila kitu, kila hatua na kila kipengele. ”

Kamanda Amata alitulia kwa muda, akavuta kumbukumbu ya tukio hilo akakukumbuka kitu,

Ilivyokuwa…

Muziki laini ulikuwa ukipigwa katika casino ile, watu walikuwa wakiendelea kucheza kamali na michezo mbalimbali inayofanana na hiyo. Alipepesa macho na kushuhudia tu dhambi mbalimbali zilizokuwa zikiendelea katika jumba hilo. Kamanda Amata hakuwa na linguine alijivuta taratibu kuelekea kaunta, hakuweza kutoka nje wala kufanya nini, kwa maana Bill alimuwekea ulinzi wa nguvu, Amata alijuwa wazi kuwa yupo mtegoni. Mara Yule mwanamke aliyemfuata chumbani akaja kwake na kumkumbatia,

“Mmm Sweetie, fanya haraka tukalale, Bill amesema nikakuburudishe usiku wa leo,” Yule mwanamke alimueleza Amata ambaye hakuonekana kuwa na hari ile iliyozoeleka, kichwa chake kilikuwa kimevurugika kikitafuta njia ya kujinasua. Alimkumbati Yule mwanamke kwa mkono mmoja na kumvutia mlango wa kutokea nje,

“Tunywe kidogo hubby” Yule mwanamke aliendelea kumbembabemba Amata, akaingiza mfukoni mwake mkono na kutoka na pafyumu iliyoandikwa ‘Sunset’ kwenye kopo lake.

“Nini hiyo?” Amata aliuliza.

“Pafyumu, beibi, inanukia vizuri sana, check” baada ya Yule mwanamke kumueleza hayo aliifyatua ile pafyumu na kumpulizia usoni kiasi. Kisha akajipulizia kwapani huku nakule na kuirudisha pochini, akatoka na Amata na kuelekekea kwenye gari huku nyuma akifuatiwa na mtu mwingine. Wakaingia garini na kuondoka, Kamanda Amata alishangaa badala ya kuelekea hotelini ile gari ilikuwa ikichukua barabara ya kuelekea Embu, akawauliza wakamwambia kuna mzigo wanafuata kisha watarudi, mara akaona nguvu zinamuishia, mwili unachokia, macho yanakuwa mazito, kila alipojaribu kupambana na hali ile alishindwa kabisa, aliwaona wale jamaa kama madudu ya kutisha mbele yake, mpaka alipokutana na usingizi mzito wa kutokujitambua kabisa…

Rejea KICC …

“Niliwafuatilia kwa gari niliyoiba pale hotelini kwa mwendo mrefu mpaka nilipoona panafaa ndipo nikasababisha ajali ya makusudi na kukuokoa, lakini nilikukuta ukiwa na hali mbaya, povu zito likikutoka puani na mdomoni, nikakuwahisha klatika hospitali yetu pale Nairobi, kwa matibabu, ndipo bwana Shikuku akamtafuata boss wako Madam S na kumpa taarifa. Ofisi yako ilikodi ndege hapa Nairobi na kukuchukua mpaka Dar es salaam,” Ndge alitulia akimtazama Amata, kisha akafungua kinywa chake na kumwambia, “Ni mimi nilikutana nawe pale Nakumatt, Westland kama mbwia unga, ni mimi tulikutana pale kwenye bustani ya ufufuko ndani chumba cha kitubio, najua unamsaka Bill lakini Bill ametoweka, hayupo Nairobi na hajulikani alipo, ila Rose anajua kila kitu.”

“Ndege, Rose ameuawa kikatili,” Amata alimwambia kwa kifupi. Ndege alishtuka sana kwa habari hiyo, “Unasema Rose ameuawa? Lini na wapi?” aliuliza.

“Rose ameuawa nyumbani kwake, jioni hii, baada ya kukutana na wewe pale kwenye bustani ya ufufuko na kuniambia nikamuulize Rose kuwa anajua habari za Bill nikakuta kauawa kwa kukatwa kichwa ndani ya nyumba yake mwenyewe. Sikumkuta aliyemuua lakini nishuhudia gari iliyotoka hapo nje kwa kasi ilikuwa ya rangi ya kijivu, sikuweza kuisoma namba, lakini pia sikuona haja ya kuifuata,”

“Dah! Rose, hivi nilikuwa nasubiri upate habari toka kwake kisha tuone tunafanya nini, bwana Shikuku amenambia nifanya kazi hii kwa siri sana.” Ndege aliongea kwa masikitiko.

“Ok! Kuna watu wawili, Wambugu na Mellina, nawahitaji sana, kutoka kwao nitajua wapi pa kuanzia, lakini kifo cha Rose kimenikwamisha kwa mengi sana, watu wengi wanajua mi ni Malaya sana lakini svyo, kutoka kwa wanawake ndio mara nyingi tunapata habari za wahalifu tunaowafuata lakini pia tunaweza kuwakamata kwa urahisi wahalifu kwa kuwatumia wanawake hawa, Masikini Rose, lazima niilipe damu yake kwa damu.” Amata aliongea kwa masikitiko.

“Usijali kaka, nilikujengea mazingira bila kujua, twende kwa Rose sasa hivi, mengine tutaongea mbele,” Ndege alimwambia Amata.

“Ok, sawa, sikia Ndege, nimekuja hapa mimi binafsi, najua ofisi inanitafuta lakini usimwambie mtu kama niko hapa hata bosi wako usimwambie.” Amata alimsihi Ndege,

“Dah! Samahani sana kaka, nilishamwambia Shikuku kama upo hapa,”

Kamanda Amata alimtazama Ndege kwa jicho bay asana, “Tuyaache, hukuwa unajua, ila usimwambie mtu mwingine, na leo hii lazima tuonane na Shikuku tulidhibiti hilo haraka,” Kamanda Amata aliufungua mlango wa gari na kuketi upande wa kushoto, Ndge akaukalia usukani na kuondoka zao.

“Imekuwaje ukavaa kama mwanamke leo?” Ndege aliuliza

“Na we ilikuwaje ukajifanya teja au kasisi?” Amata nae aliuliza

“Ah ah ah ah!!! Trust no one kaka,” Ndege alijibu.

“Umeona ee? Muwinda huwindwa!”.

Kwanza kabisa walifika hotelini mwa Kamanda Amata, kamanda akabadilisha nguo na kuingia ndani ya suti kama kawaida yake kisha wote wawili wakionekana vijana nadhifu wakarudi kwenye gari yao na Ndege akatulia nyuma ya usukani wakaendelea na safari.

“Wewe unamtaka Bill? Lakini kuna kesi nyingine hapa inaungana nay a Bill. Kiasi kwamba lazima na hiyo uifanyie kazi ili upate picha kamili,” ndege alimwambia Kamanda.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi

Chapisha Maoni