
Mtunzi: Richard Mwambe
SEHEMU YA NANE
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
Akatazama kile chumba kwa macho ya kiintelijensia kisha akakiendea kile kitanda kikubwa na kuivuta droo ya kitanda hicho kisha kwa upande wa chini akabandika kidubwasha maalum kisha akafanya hima kutoka katika chumba hicho. Alipofika chini, pale alipoegesha gari lake aliingia na kuketi ndani,
JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈
ENDELEA...
kisha akawasha chombo Fulani kama simu na kuweka vidubwasha Fulani masikioni mwake alibonyabonya vitu Fulani na kutulia, haikuchukua muda Bill alirudi na mwanamke fulani wakikokotana na kuingia ndani ya hotel hiyo. Melchior aliwasha kile kidude chake na kujiwek tayari kisha akalaza kiti cha gari yake na kusubiri, mara baada ya sekunde kadhaa akaanza kusikia mazungumzo ya mahaba yaliyokuwa yakitoka katika chumba hicho, mara alisikia mikoromo ya raha za dunia, akabonyeza kitufe cha kurekodi kila kinachozungumzwa kisha yeye akajitupa katika usingizi akiwa ndani ya gari hiyo.
Katikati ya usiku melchior ndege alishtuka kwa simu iliyomuita ndani ya gari, aliitazama saa yake ilikuwa tayari imetimu saa tisa kasoro robo usiku, aliwasha mashine yake na kusikiliza machache yaliyoongelewa chumbani humo, Melchior alipata habari nyingi ambazo Bill alimshirikisha yule kahaba Rose na kumshawishi aweze kumfanyia kwa malipo ya pesa nyingi za kigeni. Mazungumzo yote melchior alikuwa ameyapata katika chombo chake kile. Alipogundua kuwa tayari ulikuwa ni usiku sana aliamua kuondoka eneo lile.
Asubuhi siku iliyofuata aliwasilisha ripoti kwa boss wake Bw Shikuku na kwa pamoja waliisikiliza kwa makini na kupanga mikakati ya kazi ikiwamo Melchior kusafiri katika ndege ambayo Fr Gichuru angeitumia kwenda Roma kwani huyo bwana Bill naye alipanga kusafiri kwa ndege hiyo ikiwa ni moja ya njama zake za kujiweka karibu na kasisi huyo.
Mpango ukasukwa na kila kitu kikawa sawa kabisa, Melchior Ndege akawa tayari kwa safari hiyo.
Akiwa ujerumani aliweza kumfuatilia vizuri sana mtu mnene Bill nyendo zake zote na kujua ni nini na ni nani aliyekuwa akionana nae mara kwa mara na kwa nia gani, alipolijua na kuhakikisha kuwa hapo cha kuhitaji, Melchior Ndege alichukua ndege na kuelekea Roma Italy ambako alijichanganya na watalii mbalimbali katika viwanja vya Vatican lakini yeye akiwa na lengo tofauti kabisa, alipopata nafasi ya kuingia ndani ya jengo hilo la kihistoria alijariu kutafuta kama anaweza kuona muhusika yoyote labda angemuuliza habari fulani fulani juu ya hiyo Monstrance ambapo sasa ndicho alichogundua kuwa Bill, mtu mnene ndicho hasa kilichomleta.
† † †
Yule mzee aliyekuwa sasa kijana alimtazama Fr Gichuru aliyekuwa amepigwa na butwaa kwa habari hiyo ambayo kwake ilikuwa kama riwaya nzuri masikioni mwake, alimtazama kijana huyu na kumuona hakika ni Malaika kwake.
“Na kuhusu kutekwa kwangu we ulijuaje?” Fr Gichuru alimtupia swali yule kijana.
“Ndiyo maana nakwambia ni stori ndefu sana, mimi nilijua kila kitu mpaka mpango wa wewe kuletwa hapa, anyway, hatuwezi kumaliza yote hapa maana muda nao unatuacha, mpango uliopo sasa kwanza, tunataka tumnase huyu mtu mnene kwani yeye ni jasusi linalotafutwa kila kona ya ulimwengu, kisha wewe tukuweke kwenye usalama, hivyo basi mimi na wewe tutatoka hapa na nitakupeleka sehemu ambayo utakaa huko mpaka amri nyingine itakapotolewa” Melchior Ndege alimaliza kuzungumza na kuinuka pale alipoketi kisha kujikung’uta vumbi katika zile nguo kuukuu.
“Sasa, unajua mimi ni Kasisi, hata kama nakwenda huko lazima viongozi wangu wajue na kuna zana ambazo ni muhimu kuondoka nazo kutokana na mfumo wa maisha yangu” Fr Gichuru alitoa ombi.
“Yeah, najua sana juu ya hilo, lakini kwa sasa kama wameshakuteka ujue hawatashindwa kukuua, kwa hiyo wewe twende na taarifa kwa viongozi wako sisi tutazipeleka kwa njia tunayoijua, maana kwa sasa hatuamini mtu” Melchior aliendelea. Japokuwa alijaribu kumbembeleza fr Gichuru lakini alikataa katakata, alipendekeza arudi kwanza parokiani kwake ndipo afanye taratibu kama hizo. Melchior Ndege hakuona haja ya kupoteza muda, alimchukua fr Gichuru na kupita nae katika vichocjoro kadhaa kisha wakafika nyuma ya jingo moja kubwa, kulikuwako hapo kituka kibanda lakini kilichofunikwa na manyasi marefu yaliyorundikwa baada ya kukatwa. Ndege akapekua pekua na ndani yake kulikuwa na pikipiki kubwa iliyofichwa hapo, akaitoa na kuwasha, muungurumo wake ulieleweka kabisa kuwa pikipiki hilo ni bidhaa ya Mjerumani BMW. Wote wawili wakakaa juu yake na Melchior Ndege akaliongoza kuelekea mjini. Moja kwa moja walifika mbele ya kanisa kuu la familia takatifu, Nirobi mjini na kumuacha hapo,
“Sasa, ukiwa tayari unifahamishe maana tunataka usalama wako fr,” Melchior Ndege alimuasa.
“Sawa Melchior, na Mungu akubariki sana katika hili,” alimalizia fr Gichuru na kuingia ndani ya wigo wa kanisa hilo, wakati Melchior Ndege akiondoka eneo lile na kurudi katika majukumu yake.
† † †
Kijua cha asubuhi kilianza kuchomoka katika maeneo ya viwanda ya Nairobi kandokando ya barabara ya Mombasa, walinzi waliopewa kazi ya kumchunga Fr Gichuru walikwenda kumtazama ili kuhakikisha kuwa yupo salama, walipofika hawakuamini wanachokiona, mlango ulikuwa wazi katika mtindo uleule kama Maria Magdalena alipofika katika kaburi la Yesu alfajiri. Wakatazamana, hawakuwa na lakufanya, wakatoa taarifa haraka kwa wakubwa waliomleta mateka huyo.
“Yaani aisee msilete ujinga, tunakuja sasa hivi” ilikuwa ni sauti ya Blach Cheetah kwenye simu hiyo, na mara simu ile ikakatwa.
Dakika kumi na tano, Black Cheetah, Mellina Wanjiku na Bwana Gichui walifika pale godown na kushuhudia hali hiyo, waliwaita walinzi wote pale laikini mmoja hakuonekana,
“Mwenzenu yuko wapi?” lilikuwa swali kutoka kwa Gichui kwenda kwa wale walinzi, hawakuwa na jibu, walibaki kutazamana tu, “Nawauliza ninyi, walinzi gain mpo hapa na mtu anatoroka? Ninyi mmekula njama,” aliongeza kisha akawasukumia wote kwenye kile kichumba na kuufunga mlango kwa nje.
Taarifa za kutoweka kwa fr Gichuru hazikumfurahisha Bill mtu mnene hata kidogo, alihisi kuwa hiyo ni njama na hasa kwa kuwa mlinzi mmoja hakuonekana kati ya hao.
Pamoja na adhabu walizowapa walinzi wale lakini hakuna kilichozaa matunda.
Bill aliwaita vijana wa kazi katika kivhumba kidogo ndani ya godown hilo na kuwapa kazi ya kumsaka popote alipo Fr Gichuru na atakapoonekana hakuna cha kusubiri ni kumuondoa uhai tu na mambo mengine yatafuatia.
“Sasa tukimuua ndiyo tutapata hiyo monstrance?” Mellina aliuliza.
Bill alibaki kimya kwa swali hilo kisha akamtazama Cheetah na Gichui, akimaanisha watoe wazo hapo cha kufanya.
“Sikia, yule Gichuru ameshajua mengi juu yetu, sasa tukimuacha atatoa siri polisi, halafu mission itashindikana. Hivyo tunamuua kisha tunavamia kanisa ki-ambush na kuchukua tunachokitaka” Black Cheetah aliwaeleza wanzake.
“Safi!” Bill mtu mnene alimpongeza.
Baada ya kikao hicho kifupi, walitawanyika na kuanza kazi ya kumsaka kasisi huyo.
Alfajiri ya siku iliyofuata
“Baba, mimi leo sijisikii vizuri, mwili wote unaniuma sana, naomba unisaidie kigangoni kwa misa mimi nitabaki hapa” fr Gichuru alimuomba paroko wake fr Joe Simith
“Kwa kweli fr inabidi ubaki, kwani hawa maharamia wanaweza kukukamata njiani, ubaki hapa mimi nitakwenda kigangoni”. Baada ya makubaliano hayo fr Joe alichukua gari ya mission na kuondoka zake na kumuacha Fr Gichuru akisubiri muda wa ibada saa kumi na mbili kamili asubuhi.
Fr Gichuru alivalia kanzu yake nyeusi na kofia ya kikasisi nyeusi yenye nyoya jeusi katikati, mkononi akiwa na rozali yake aliterenka ngazi taratibu ili apate muda wa kusali alfajiri hiyo kabla hajaingi katika misa. ‘Moyo wangu una huzuni kiasi cha kufa’ alijiwazia wakati amesimama kwenye ngazi za nyumba yao, kisha kwa hatua za taratibu aliteremka na kukanyaga uwanja wa kanisa hilo kongwe, ‘Baba ikiwezekana kikombe hiki kinipitie mbali,’ aliendelea kupata tafakari hii ya uchungu, hatua chache alisimama, ‘ Lakini si kwa mapenzi yangu bali yako yatimizwe.’
Subaru ya kijivu ilikuwa imesimama karibu kabisa na barabara ipitayo mbele ya kanisa hilo kubwa, hata fr Joe alipopita hapo aliiona lakini hakuitilia maanani. Nadni ya gari hiyo kulikuwa na watu watatu, awili wanaume na mmoja mwanamke. Black Cheetah aliitazama saa katika dashboard ya gari hiyo, ilikuwa tayari ni saa kumi na moja alfajiri akamwambia Gicui aliyekuwa nyuma ya usukani huo, “Twende sasa, mlinzi atafungua tu huu muda ni sawa,” kwa mwendo wa taratibu Gichui aliielekea geti kuu na alipofika getini kwa mbali aliona vivuli kama vya watu, akawasha taa katika mtindo wa full na kuwamulika, alikuwa ni sista na fr, akawasha tena taa mara kadhaa katika mtindo huo. Yule kasisi akalisogelea geti kutazama kulikoni, alifika getini na kusimama akilitazama gari hilo. Milango ikafunguliwa, Black Cheetah akatoka akiwa ndani ya koti lake jeusi na kulielekea geti, sasa uso kwa uso na fr Gichuru.
“Kwa kosa ulilolifanya la kututoroka, jua la leo si halali wewe kuliona” Black cheetah, alimueleza fr Gichuru huku akiondoa usalama wa bastola yake na kuruhusu risasi niingie katika chemba, fr Gichuru aliutazama mdomo wa bastola ile,
“Si kwa mapenzi yangu, bali yako yatimizwe” Fr Gichuru alisema mara hii kwa sauti iliyoweza kusikiwa na Black Cheetah pekee, mkono wa jambazi huyo ulikuwa ukitetemeka hata kutaka kupoteza nguvu.
“Black Cheetah, unachelewaaa!” ilikuwa sauti ya Mellina ikimstua Black Cheetah na bila ajizi vidole vyake vikapata nguvu na kufyatua trigger ya ile bastola, risasi mbili zilipenye katika kifua cha kasisi huyo na kumnyayua kabla ya kumbwaga chini chali na mifereji ya damu kuanza kuchuruzika kutoka mgongoni alaikolalia.
Kwa mwendo wa kasi ile Subaru iliondolewa mahali pale na kusababisha kelele za tairi pindi ilipoingia barabarani.
Fr Gichuru hakuwa na nafasi hata ya kuomba maji, “Yametimia, Baba mikononi mwako naiweka roho yangu” alitamka maneno hayo kwa shida huku damu nyingine zikitoka kinywani na kisha kichwa chake kikaelemea uapnde wa kushoto na kukata roho.
INSPEKTA Saitoti alikuwa akigongagonga kalamu yake mezani kwake huku akionekana wazi kuwa kichwa chake kilikuwa na mambo mengi sana ambayo kwa namna moja au nyingine yalimchanganya kichwa., mara alivuta kabrasha hili mara lile lakini hakujua anachotaka kufanya kwa muda huo, akiwa katika hali hiyo aligutushwa na hodi iliyogongwa mlangoni mwake kisha mwanamama mmoja aliyevalia kiraia aliingia kwa ukakamavu na kubana miguu yote miwili kuonesha nidhamu ya kijeshi.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi