SEHEMU YA AROBAINI NA MOJA
ILIPOISHIA...
Nesi akatoka na kukiacha kisinia chake na askari akanyanyuka na kutoka nje na nikapata wazo la haraka nikaanza kutafuta kifaa kidogo kinachoweza kuingia kwenye shimo la funguo la pingu na kuchukua kijikifaa kidogo kilichopo kwenye sinia na sikujua kina kazi gani na kuanza kuifungua pingu niliyo fungwa kwa utulivu wa hali ya juu na chakumshukuru Mungu ikafunguka kisha nikashuka kitandani japo mwili umetawaliwa na maumivu makali ila nikajikaza na kuufwata mlango wa kutokea kwenye chumba nilichopo na kuwaona watu wakiwa wanaendelea na mishe zao.NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
Nikatoka ila kitu kilicho nichanganya sikujua askari ni wapi alipo elekea,nikaanza kutembea kwa umakini huku nikifwata sehemu yenye mlango wa kutokea na kwabahati nikamuona kwa mbali askari wa magereza akija kwa mwendo wa haraka huku mkononi mwake akiwa ameshika kifuko cheusi.Nikajibanza kwenye ukuta na akapita pasipo kuniona na kwaharaka nikatoka huku miguuni nikiwa sina hata kitu chohote,Nikafanikiwa kuondoka eneo la hospitali na safari hii moja kwa moja nikaelekea nyumbani kwetu
Japo kuna umbali kidogo ila nikajikaza kutembea na nikafanikiwa kifika na kukuta geti likiwa limefungwa,nikakumbuka kwenye sehemu ya nyuma ya ukuta wetu kuna matofali yaliyo pagnwa ya mtu mwenye kiwanja chake aye taka kujenga.Nikazunguka na kuyakuta matofi kama nilivyo tarajia
“Hivi mwenye haya matofali amefariki dunia au?”
Nilijisemea huku nikianza kuyapanga matofali karibu na ukuta wetu ambao ni mrefu kiasi kisha na kitu kingine kilicho niogopesha ni nyaya za umeme za ulinzi zilizo zungushiwa kwenye ukuta wa nyumba yetu sehemu ya juu.Ikanichukua kama dakika kumi na tano kutengeneza urefu wa ngazi za kuingilia kwenye nyumba yetu na nikafanikiwa kupanda ukutani huku kwa hahadhari kubwa nikizikwepa nyaya za umeme na nikafanikiwa kurukia kwa ndani na ukimya mwigi umetawala ndani ya nyumba,nikafika kwenye mlango wa mbele na kukuta umefungwa na kawaida mlango ukiwa umefungwa huwa funguo tunazificha kwenye vyungu vya udongo vyenye mau.Nikanza kutafuta kwenye chungu kimoja baada ya kingine wala sikuzikuta
“Huyu shetani ameondoka na hizi funguo nini?”
Nikaendelea kutafuta na kwabahati nzuri nikaziona zikiwa nimefichwa kwenye kindoo kidogo chenye maua ambayo mama siku zote huwa huyapenda na kwamadai yake ameyanunulia nchini Canada na aliyanunua kwa gharama kubwa kubwa sana.Nikafungua ndani na kukukuta vitu vikiwa vimeshanguliwa sana huku kukiwa na chupa nyingi za pombe zikiwa zimezagaa zagaa kwenye sakafu huku vijimito vidogo vya masofa vikiwa vimetupwa tupwa.Nikapanda ngazi hadi chumbani kwangu na kuingia bafuni na kuoga kisha nikapanda kitandani na kulala kutokana na uchovu mwingi sana.
Nikaamka mida ya saa mbili usiku huku niikiwa nimechoka nikaelekea jikoni na sikukuta kitu chochote cha kula hata mafriji yote hayakuwa na kitu chochote,Nikakumbuka kwenye nyumba ya uwani kuna handaki ambalo mara nyingi nikiwa nipo likizo nilikuwa nikamuona mama akiingia na sikujua ni kitu gani anacho kifwata ndani ya handaki hilo.Nikaingia kwenye nyumba ya nyuma katika chumba ambacho kuna kitanda kimoja na kiti kisha nikasogeza pembeni kitanda na kulisogeza kapeti lilolopo ndani na kuukuta mlango wa chuma ambao ni mlango wa handaki.Nikaufungua na kukuta ngazi za kushuka chini ambapo kunagiza la kutisha sana ikanibidi nirudi tena juu kutafuta tochi.Nikafanikiwa kuiona tochi yenye uwezo mkubwa wa wa mwanga.Nikaingia tena ndani ya handaki huku tochi ikiwa inawaka,nikaanza kuona picha nyingi za kutisha zikiwa zimebandikwa kwenye kuta za handaki hili huku kukiwa na vitu vichache sana ikiwemo majoho matatu moja likiwa jeusi la pili likiwa na rangi nyeupe na jengine ni la rangi nyeusi.Sikujua ni ya kazi gani nikakifwata kitabu kikubwa kilicho jaa vumbi nilicho kikuta na kukifungua na kukuta maandishi ambayo sikujua ni ya lugha gani iliyo andikwa ndani yake
Nikakiacha na kukiona kisanduku kidogo cha wastani kikiwa kimefungwa na kuwekwa kwenye kona ya handaki na nikakisogelea na kukifungua,Sikuamini macho yangu baada ya kukuta cheni na pete za dhahabu pamoja na vipande vaya madini.Na nikaanza kuchangua changua na kukuta pete moja ya madini ya Tanzanite ikiwa imetengenezwa kwa ustadi mkubwa huku kukiwa na vipande vingine vingi vya madini yenye dhamani kubwa na hata madini mengine sikuwahi kuyaona maishani mwangu.Nikakibeba kisanduku huki nikiwa nina furaa kubwa na nikaingia ndani ya chumba changu na kuvimwaga vitu vyote kitandani na furaha ikazidi kunitawala hata njaa sikuweza kuihisi tena na kujikuta nikiaanza kuimba nyimbo za aina mbali mbali huku nikicheza kiduku kisicho na mpangilio maalumu.
Nikazikusanya na kuziweka kwenye kisanduku chake kisha nikaviweka chini ya uvungu wangu wa kitanda na kwenda sebleni na kuwasha Tv na kuangalia angalia miziki hadi usingizi ukanipitia.Cha kwanza baada ya kuamka asubuhi nikaoga na kuvaa nguo nyingine zilizo nipendeza na kuingia chumbani kwa mama na kuzikuta baadhi ya funguo za magari zinapo wekwa kwenye kabati na kuchukua moja kisha nikichukua dini moja la kuliweka mfukoni na kutoka nje na kuingia kwenye gari moja aina Verosa ambayo mama aliinunu kipindi zinatoka.Moja kwa moja nikaenda kwa sonara na kukutana na muhindi mmoja na tukakubaliana biashara na nikamuuzia kwa milioni kumi ambazo zinanitosha sana kwenye matumi ya kwenda nchini Afrika kusini kumuona mama.Nikaingia saluni moja kiume na kunyolewa vizuri kisha moja kwa moja nikaelekea benki ya backrays kwenye akaunti yangu ambayo ni siku ningi niliifilisi hadi ikabaki kilinda akaunti na kukiweka kiasi cha milioni saba na kubaki na tatu na nikaanza mipango ya kutengenezewa hati yangu mpya ya kusafiri
Na ndini ya masaa machache nikawa nimefanikiwa kutokana na kuhonga sana pesa kwa watu wanao husika na utengenezaji wa hati za kusafiria na hadi ninafanikiwa kuipata nikajikuta nikiwa nimebakiwa na laki tano na nusu nusu na nikakata tiketi ya ndege ya shirika la South Africa Aur ways.Na nikaelekea kwenye ofisi za wizara ya afya na kukutana na mmoja wa masekretari wa mama ambaye nina fahamiana naye vizuri na akaonekena kunishangaa.
“Eddy si nimesikia umefariki wewe?”
“Nani amekuambia?”
“Eddy kila mtu anajua kuwa wewe umeuawa kwa kuchomwa sindano ya sumu kitendo kilicho mpa mama yako mstuko na tumemkimbiza Afrika kusini kwa matibabu zaidi”
“Tena hilo ndilo nililokuwa nimekuja kulijua mama yangu amelazwa hospitali gani?”
“Amelazwa hospital moja inaitwa Louis Pasteur ipo mji wa Pestoria”
“Ahaaa asante kwa hilo”
“Ila Eddy niambie ni kitu gani kilicho kupata hadi ukafufuka kwa maana mimi mwenye kwa macho yangu niliiona maiti yako ikiingizwa mochwari ila cha kustaajabu leo hii ninakuona hapa?”
“Ni historia ndefu ila Mungu akibariki nikipata nafasi nitakuja kukusimulia ila nashukuru kwa masaada wako”
“Usijali nakutakia safari njema”
Kutokana tiketi ya ndege niliyo kata inaondoka saa Mbili usiku ikanilazimu kurudi nyumbani na kubeba nguo kadhaa na kurudi uwanja wa ndege kwa kutumia taksi ya kukodi.Nikatafuta sehemu yenye mgahawa na kujipatia chakula cha kutosha kwani kutokea asubuhi sikuweza kuingiza chochote kutokana na mizunguko ya kuandaa safari.Imebaki lisaa limoja kabla ya safari nikaendelea kusubiri kwenye sehemu za abiria.
“Samahani kaka hii sehemu kuna mtu?”
“Hapana unaweza kukaa”
Dada mmoja aliye valia suruali ya kubana na kuyafanya makalio yake makuwa kujichora vizuri huku akiwa amejiremba na kuonekana mrembo zaidi alianiambia na baada ya kumjibu akakaa pembeni huku akiwa na pochi yake kubwa kiasi na kujikuta nikimtazama kwa jicho la kuiba.Nikaendelea kusoma gazeti hadi tulipo tangaziwa abiria shirila la ndege la South Afrika Air ways tujiandae kwa safari na tukapanga foleni na kuanza kuingia sehemu maalumu ya kukaguliwa kisha nikaingia kwenye ndege na kutafuta sehemu ilipo siti yangu na kukaa baada ya mida kidogo akingia dada aliye niuliza kuhusiana na sehemu ya kukaa kisha na yeye akakaa siti ya pembeni yangu na baada ya muda safari ikaanza pasipo kusemeshana kitu cha iana yoyote hadi katikati ya safari ndipo akaanza kuniongelesha
“Samani kaka unaelekea wapi?”
“Afrika kusini”
“Ahaa mimi ninaitwa Emmy”
“Mimi ni Eddy”
“Ahaa nashukuru kukufahamu”
“Na mimi pia”
“Unakwenda South kufanya nini?”
“Ninakwenda kumcheki bi mkubwa ni mgojwa”
“Ahaa mimi kule ndio ninaishi ila mimi ni Mtanzania
“Kwa hiyo wewe ni mwenyeji kule”
“Ndio....mama yako amelazwa hospitali gani?”
“Inaitwa Louis Pasteur”
“Ahaa ndipo ninapo fanyia kazi na nidaktari pale”
“Kweli?”
“Ndio ila nilikuwa nipo likizo ndio ninarudi hivi nilikuja kuwaona wazazi mara moja”
“Eheee asante Mungu nimepata mwenyeji kwa maana hapa nilikuwa ninajiuliza ni jinsi gani ninaweza kumpata mama yangu”
Safari ikaendelea kwa masaa kadhaa huku nikiwa nina amani moyoni mwangu kwani nimempata mwenyeji wangu.Ndege ikatua kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Maputo.Emmy akaniomba kwanza niende kwake ili kukipambazuka vizuri tuweze kwenda hospitali kwani yeye amebakisha siku tano za kurudi kazini.Tukafika nyumbani kwake kwenye gorofa refu moja ambalo alinieleza kuwa watu wangi wamepanga na yeye sehemu yake ni gorofa ya saba kutoka chini.
“Eddy karibu ndani?”
“Asante”
Emmy akanikaribisha kwenye sehemu anayo ishi ambayo yenye vitu vingi vya dhamani ya hali ya juu.Taratibu Emmy akaanza kuvua nguo zake moja baada ya nyingine na kunifanya nibaki nikiwa nimemshangaa kwani sikujua ana maana gani na imekuwaje amevua nguo mbele yangu na kubakiwa na chupi wakati mimi na yeye hatuna mahusiano ya namna yoyote
Emmy akachukua taulo na kujifunga kisha akaingia bafuni na kuniacha mimi nikiwa nimekaa kwenye sofa nikiyatadhimini mazingira ya ndani kwake.Baada ya muda kidogo Emmy akatoka bafuni
“Umeshindwa hata kuwasha Tv?”
“Ahaa hakuna tatizo sana”
“Ok ngoja nivae nguo tuelekee hospitalini ukamuone mama”
“Sawa”
“Ila unajua wodi aliyo lazwa?”
“Hapana siijui”
“Ok basi tutajua huko huko”
Emmy akaingia ndani kwake na akatoka akiwa amevalia mavazi mazuri kiasi kwamba tama za mapenzi zikaanza kunitawala na kujikuta nikimtazama Emmy kwa macho ya matamanio
“Eddy twende zetu”
“Mmmmm”
“Twende zetu mbon unanishangaa?”
“Ahaa hakuna kitu”
Nikanyanyuka na nikatangulia kutoka nje ila kutokana na baridi kali ikanilazimu kumuomba Emmy koti na akarudi ndani na kunichukulia koti lake kubwa na sote tukaingia kwenye Lifti na kushuka chini gorofani.
“Twnde huku kwenye maegesho ya magari”
Tukafika sehemu yenye maegesho ya magari mengi na Emmy akafungua gari moja na kuniomba niingie.Safari ikaanza huku kila mmoja akiwa kimya ndani ya gari ila Emmy akaamua kuvunja ukimya
“Hivi Tanzania wewe unafanya kazi?”
“Mimi ni mwanafunzi wa A leve bado”
“Ohh kumbe unasoma?”
“Ndio”
“Kombi gani?”
“PCB”
“Mungu wangu PCB wewe....Mbona unaonekana kama HKL?”
“Hahaa PCB halisi...Aafu mbona ndege leo imetua kwenye uwanja wa Maputo international airport imekuwaje kutokana tumetua Mozambique?”
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com