SEHEMU YA AROBAINI NA TATU
ILIPOISHIA...
Nikaingia kwenye mgahawa uliopo karibu na hospitali na kuagizia chakula ambacho nitaweza kukila na nikatafuta sehemu ambayo ninaweza kuuona mlango wa kuingilia katika hospitli na kabla sija letewa chakula nikaona taksi ikiwa imesimama kisha nikamshuhudia baba akishuka ndani ya gari akiwa ameongozana na wanaume wawili na katika taksi nikamuona Sheila akiwa amekaa siti ya nyuma.NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
Kwa haraka nikanyanyuka na kutoka nje ya mgahawa na kutokana na magari mengi ikanilazimu kuvunja seheria za barabara na kujikuta nikivuka kwa haraka barabara na kabla sijamalizia nikashtukia nikikumbwa na gari lililo nirusha na kuangukia pembeni ilipo simama taksi aliyopo Sheila
Nikatulia chini kwa muda na kumuona Sheila akifungua mlango kwa haraka na kushuka ndani ya gari na akaonekana kunishangaa baada ya kunijua ni mimi,nikajaribu kujinyanyua ila nikajikuta nikishindwa kutokana na mguu wangu mmoja kutawaliwa na maumivu makali.Nikastuka baada ya kugundua mguu wangu wa kushoto umevunjika japo kichwani na mikononi nimepatwa na michubuko iliyosababishwa na kuaanguka na kuserereka kidogo kwenye barabara ya lami.Sheila akaoanekana kupigwa na bumbuazi kwani hakuzungumza kitu cha aina yoyote zaidi ya kubaki akinitazama hadi watu walipo anza kukusanyika na kuwaomba wauguzi wa hospitalini kunisaidia,
Nikawawekwa kwenye machela na kuingizwa ndani pasipo Sheila kuzungumza kitu cha aina yoyote kwangu,Nikaingizwa kwenye moja ya chumba ambacho ni chaupasuaji na kwa haraka nikachomwa sindano za ganzi kwenye mguu wa kushoto ambao umevunjika na kawanipaka mafuta kisha wakamipitishia kifaa maakumu kinachotoa mwanga mwekundu wenye miyonzi mikali huku dakitazama picha inayopita kwenye Tv ndogo iliyopo ndani ya hiki chumba wakaona ni sehemu ya ambayo mguu umevunjika na wakaanza kazi ya kunihudumia
Ndani ya lisaa moja wakamaliza upasuaji wao na kunifunga bandeji kubwa kisha majeraha madogo madogo wakayapaka dawa kisha wakanihamishia kwenye wodi kitu ambacho ninakiona ni chatofauti ni huku kufanyiwa upasuaji pasiopo kuchomwa sindano ya usingizi.Sikuweza kupata rafiki wa kunijulia afya yangu na kitu kinacho niumiza sana akili yangu ni jinsi hali ya mama ilivyo na kingine sikujua kama ameweza kusalimika mikononi mwa baba ambaye ndio amekuwa adui yetu namba moja kwenye familia yetu.Sikua ya kwanza ikakatika huku nikiwa sijui kitu kinacho endelea ila zaidi nikawa ninahudumiwa na kupewa chakula na wauguzi wa hospitalini.
Wiki moja ikakatika na hali yangu ikaendelea kuwa nzuri zaidi na nikaanza kufanyishwa mazoezi ya kutembea na siku hii nikamuomba muuguzi kunipeleka kwenye sehemu kilipo chumba alichomo mama na hakusita na kwa mwendo wa taratibu tukafanikiwa kufika ila sikuweza kumpata mama na ikanibidi kumuuliza muuguzi huyu kwa lugha ya kingereza
“Hivi huyu mama humu ndani amekwenda wapi?”
“Mama yupi?”
“Kuna mama waziri ambaye alilazwa humu chumbani”
“Sijajua labda tukaulize sehemu zenye rekodi ya wagonjwa kwa maana mimi sihusiki katika kitngo hichi na kama unavyo iona hospitali yetu ilivyo kubwa siwezi kuwajua wagonjwa wote”
“Sawa dada yangu basi nakuomba unifikishe hiyo sehemu wanayo angalizia orodha ya wagonjwa”
Cha kumshukuru Mungu huyu nesi hana makuu zaidi ya alicho kifanya ni kunipeleka hadi sehemu wanayo angalizia idadi ya wagonjwa walipo kwenye hospitali hii na kadri tunavyo litafuta jina la mama kwenye kumputer yao hawakuliona na ikanibidi niweze kuuliza jina la daktari Emmy na jibu nililo lipata kutoka kwa mfanyakazi wa ofisi hii ya takwimu za hospitali likazidi kunichanganya
“Hapa hospitalini kwetu hatuna jina la daktari anaye itwa Emmy na dokta anaye anziwa na herufi ya E ni mwanaume na anaitwa Emmanuel”
“Kweli huyo daktari hayupo....Mbona ana hadi kitambulisho na kitambulisho kinacho muonyesha kuwa yeye ni daktari wa hii hospitali?”
“Wewe ulikutana naye wapi?”
“Tanzania na nikapanda naye ndege moja hadi hapa”
“Mmmm hapa mulikuja lini?”
“Kama wiki moja iliyo pita”
“Ngoja kwanza”
Msichana anayehusika na maswala ya takwimu akanyanyua mkonga wa simy ya mezani kisha akaminya baadhi ya namba na kuiweka simu yake sikioni
“Kiongozi ninashida moja ninakumba unisaidie”
“Kuna tatizo limejitokeza la hawa madaktari feki kuendelea kuivamia hospitali yetu na wanaendelea kufanya matukio ya ajabu”
“Basi ninakuja sasa hivi”
Akakata simu na kuniomba niogonzane naye huku nesi anaye nifanyisha mazoezi akinishikilia vizuri na tukaingia kwenye lifti na ikatupeleka hadi gorofa ya tatu na tukaingia kwenye chumba ambacho nikakuta tivi nyingi ndogo ndogo ambazo idadi yake kwa haraka haraka zinaweza kufika hamsini na kila Tv inaonnyesha sehemu yake na nikagundua zinaonyesha picha za kamera za ulinzi zilizo fungwa ndani ya hii hospitali
“Una rekodi za wiki nzima?”
“Ndio ninazo”
“Ninaomba utuwekee za siku saba za nyuma”
Jamaa anaye onekana ndio muongozaji wa kamera za humu hospitali akaigeukia Tv moja kubwa kama nchi 32 kisha akachuku CD ndogo na kuziingiza kwenye deki ndogo na tukaanza kuangalia video zilizo chukuliwa ndani ya wiki moja na nikajikuta nikinyoosha kidole changu kwenye moja sehemu hii ni baada ya kujiona nikiingia hapa hospitalini siku ya kwanza nikiwa na Emmy na kumfanya jamaa kuisimamisha sehemu hii kisha akaisogeza kwa ukubwa kiasi(ZOOM) na kuiangalia sura ya Emmy ambaye alizidi kunichanganya baada ya kumuona dada wa ofisi ya takwimu akitingisha kichwa huku akiibenua midomo yake
“Mmmm hatuna daktari kama huyu”
“Kaka hembu peleka mbele”
Jamaa akairuhusi CD kutembea na kuanza kuangalia picha za mbele na kujiona nikiingia ndani ya chumba alichokuwa mama kipindi ninatoka kuzungumza na Emmy baada ya kuanza kuhisi hali ya ajabu,Video ikamuonyesha Emmy akizungumza na askari ambaye alikuwepo pale mlangoni kisha yeye akaingia ndani huku akiitazama camera ya ulinzi iliyokuwepo juu.
“Hii ni Camera namba 38 ngoja niweke video zake kwani huu ni mkanda wa jumla”
“Sawa fanya hivyo”
“Na huyo askari hapo ni wa hapa?”
“Askari huyo aliletwa na ubalozi wa Tanzania kumlinda huyo mama.....Kwani wewe huyo mama ni nani yako?”
“Mama yangu mzazi”
Jamaa akaito CD aliyokuwa ameiweka kwenye deki kisha akatafuta CD nyingine ndogo na kuuweka kwenye deki yake na tukaendelea kuona matukio yaliyo endelea eneo la nje ya chumba alicho lazwa mama baada ya mimi kuondoka kuelekea banki.Tukamuona askari akipewa soada ya kopo na Emmy na akaianza kuinywa baada ya Emmy kuingia ndani na baada ya muda akaonekana kama anaumwa na tumbo na akandoka katika eneo la nje ya chumba akielekea sehemu vilipo vyoo na baada ya muda kidogo mlango ukafunguliwa na kumshuhudia Emmy akiwa amevalia koti la kidaktari akikisukuma kitanda cha mama huku mama akiwa amefumba macho yake na kulala kama mtu aliye poteza fahamu
Mapigo ya moyo yakazidi kunienda mbio huku nikiema kwa hasira na kujikutani nikiyang’ata meno yangu kwa hasira kiasi kwamba nikatamani nipone kwa haraka ili niweze kumsaka Emmy sehemu yotote akatakayo kuwepo nchini Afrika kusini.Nikashusha pumzi huku nikiwa macho yangu yamebadilika na kuwa mekundu na kujikuta nikikitazama kioo kilichopo ndani ya chumba hichi kinacho nionyesha vizuri sura yangu na kila mtu akabaki akinitazama kwa umakini pasipo kuzungumza kitu chochote
“Hemu rudisha hiyo CD ya kwanza”
Jamaa akairudisha CD ya kwanza na kipelea mbele kidogo na kumuona Emmy akimuingiza mama ndani ya gari la wagonjwa huku akisaidiana na watu wawili ambao niliwaona wakishuku na baba huku nao kwa sasa wakiwa wamevalia makoti meupe wakionekana kama madaktari.
“Kaka hembu simamasha kidogo hape na zoom kwenye kioo cha dereva wa hilo gari”
Jamaa akafanya kama nilivyo muagiza na akaikuza picha ya dereva na kugundua ni baba japa amevalia miwani huku akiwa amebandika ndevu za bandia na kumfanya aonekane kama mtu wa makamo
“Kwani Flora ina maana hawa jamaa sio wafanya kazi wa hii hospitali?”
“Ndio”
“Mbona wanavitambulisho kwa maana mimi hili tukio linatokea sikustushwa kwa maana ni jambo la kawaida kwa wagonjwa kuhamishwa hapa hospitalini kwetu”
Nikamshuhudia Flora ambaye ndio muhusika kwenye ofisi ya takwimu akikuna kichwa pasipo kuzungumza kitu cha aian yoyote.
“Je daktari wenu mkuu yopoje?”
“Yupoje kivipi?”
“Yaani muonekano wake?”
“Ni mweusi kiasi kiasi na sasa yupo Captown kwenye kikao cha madaktari wakuu hapa nchini”
“Mbona alikuja mzee wa kizungu huyo dada akasema ndio daktari mkuu?”
“Mmmm atakuwa amekudanganya kwani ni wiki ya pili daktari mkuu yupo kwenye kikao cha madaktari kama nilivyo kuambia hapo awali”
Sikuwa na lakuzungumza zaidi ya kuumiza kichwa ni jinsi gani ninaweza kumpata mama yangu na moja kwa moja nikajua ametekwa na baba na sikujua ni wapi alipo mpeleka.
“Tutawasiliana na polisi kuweza kulifwatilia hili tukio”
“Naombeni mufanye hivyo kwani mama yangu ndio kila kitu katika maisha yangu kwa maana nimetoka Tanzania kwa ajili yake na mwisho wa siku mambo yanakuwa kama hivi”
“Usijali wa hilo”
Nikakaa hospitali zaidi ya wiki nne na nikapona kabisa mguu wangu na kufunguliwa bandeji nililo fungwa.Habari za wapi alipo mama kila nilipojaribu kuwaulizia walio sema watalishuhulikia wakadai bado askari wanaendelea na uchunguzi ambao sikujua utaisha lini
“Kaka gharama zako za hospitalini zimesha lipiwa”
“Zimelipiwa na nani?”
“Aliye kulipia ni yule aliye kugonga na gari na yupo nje anakusubiria?”
Nikaanza kujiuliza ni nani huyu aliye ni gonga na kuwa na moyo wa kujitolea kiasi kwamba amenilipia gharama zote za ajali yangu wakati mimi ndio nilikuwa ninamakosa.Nikatoka nje pamoja na daktari aliye niambia habari hii ambayo kwangu ni nzuri kiasi japo bado akilini nimetawaliwa na wazo la wapi alipo mama.
Daktari akanionyesha mzee mmoja aliye valia koti jeusi la suti na alinipa mgongo kwani anazungumza na simu,ikatulazimu kumsubiria amalize ndio daktari amjulishe uwepo wetu.Baada ya muda akakata simu na kugeuka na kujikuta nikihamaki kwa kiasi kikubwa kwani mtu aliyepo mbele yangu anafanana kabisa na baba yangu ambaye kwa sasa ni adui yangu namba moja.
“Habari yako kijana”
“Sh...ikamaoo”
Nilipata kigugumizi cha gafla kiasi kwamba mzee naye akaanza kunitazama kwa umakini huku akionekana kunichunguza kuanzi kichwani hadi miguuni.Daktari akatutizama kwa muda na kuzungumza kitu kilicho tufanya sote tumtimame
“HUYO NI MWANAO?”
HAKUNA aliye lijibu swali la daktari zaidi ya kukaa kimya kimya na tukageukiana na kuendekea kutazama na kadri tulivyo zidi kutazamana ndivyo nilivyohisi ukweli wa maisha yangu juu ya baba yangu kwani kuanzia macho pua midomo na sura hakuna kilicho pishana na mwenzake kiasi kwamba machozi yakaanza kunilenga lenga huku moyoni mwangu nikijihisi amani na furaha iliyo kuba tofauti na ninavyo kuwa na baba yangu gaidi.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com