SORRY MADAM (47)
Zephiline F Ezekiel
6 min read
SEHEMU YA AROBAINI NA SABA
ILIPOISHIA...
“Huyu mwanao ni mwenda wazimu nini?’
Sikumjibu kitu cha aina yoyote zaidi ya kumfwata na nilipo sikia swala la uwenda wazimu na mimi nikajichetua sana na ili nionekane ni mwenda wazimu kweli.
NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
Tukaanza kazi ya kukimbizana huku tukimzunguka baba aliye kosa kitu cha kuzungumza,
“Mume wangu mkamate mwanao atanijeruhi”
Na mimi nikaanza kuuigilizia mlio wa Sheila alio kuwa akiningurumia na kumfanua baba kuhamako na kadri muda unavyo kwenda ndivyo nikazidi kujichetua kaisi kwamba baba akaagiza walinzi wake kunikamata na wakashauriana wanipeleke hospitali ya vichaa kwa ajili ya vipimo zaidia.Kwa bahati nzuri tukafika kwenye hospitali tuliyo toka masaa machache yaliyo pita na kwabahati nzuri daktari aliye pewa jukumu la kunipima na yule niliye mpa dola mia mbili na akawa ananishangaa kuniona nikiwa nimeletwa kama mgonjwa
“Dokta wakikuuliza waambie kuwa itanibidi hapa nikae kwa wiki mbili”
Nilimuambia daktari baada ya baba na watu wake kutoka nje ya chumba nilicho ingizwa
“Saaa….saaa”
“Dokta acha kupata kigugumizi wewe waambie hivyo kuwa mimi ni mgojwa na mutaniweka hapa kwa wiki mbili ili kunichunguza zaidi na kama ni pesa mimi nitakulipa ila hili ni dili kati yangu mimi na wewe”
“Sawa nimekuelewa”
Daktari akanipima pima kiuongo ili kupoteza muda kisha akatoka na baada ya muda baba akaingia huku akiwa na sura ya unyongee na kwambali machozi yanamlenga lenga
“Ohhooo Eeeehee baba ukuwaa mkubwaa kamaaaaa John Cennaaaaaa hahaaa…babaaa huuuyoooo katokaaaa kaziiiniiiiiiiii ohooaaooa”
Niliimba nyimbo za kuwehuka na kuzidi kumfanya baba aamini kuwa mimi nimepata kichaa
“Dokta kweli mwangu atapona?”
“Kama nilivyo kuambia hapo awali tunamuweka hapa ndani ya wiki mbili kisha tutaangalia jinsi maendeleo yake yanatavyo endelea”
“Ahahaa doktaaa wiki mbiliiiii hahajhhhaa mimi takaaa kaaaa mwakaa mzimaaaa baaaabaaa lia liaaa kama totojingaaaaaa hahaahaa”
Nikazidi kuzungumza huku nikirusha rusha miguu na mikono na ikawalazimu watu wa baba kunilaza kitandani na kunifunga mikono na miguu kwa kitumia mkanda maalumu uliopo juu ya hichi kitanda nilicho lalia
“Ohoo Mungu wangu sijui ni kitu gani kimempata mwanangu?”
“Usiwe na wasi wasi atapona tuu cha msingi ni kumuomba Mungu aweze kumjalia afya njema”
Baba akanitazama kwa sura ya simanzi na akashindwa kuyazuia machozi yake na akaanza kulia na ikamlazimu mlizi wake mmoja kutoa kitambaa na kumkabidhi baba kisha akatoka naye nje na walinzi wake wengine wawili wakafwatia nyuma
“Dokra wachungulie wamesha ondoka?”
“Ngoja niangalie”
Dokta akafungua mlango na kuchungulia kisha akaufunga na kunifwata kitandani huku akiwa anacheka
“Ndio wamesha ondoka….hivi wewe kijana mbona msanii kiasi hichi?”
“Ahaaa uanajua unapo amua kufanya kitu mtu inabidi uweze kufanya juu chini unakifanikisha hata kwa staily kama hii pia ni vyema si umeona sasa mpaka mzee ame….hahaaaa chipissssisisisisiiii oohoooo”
Nilirudi katika hali yangu ya kuchanganyikiwa baada ya mlango kufungulia na wakaingia majamaa wawili wenye misuli na wamevalia makoti meupe na suruali nyeupe
“Huyo naye dokta ana tatizo gani?”
“Ahaa mchukueni mumpeleke kwenye chumba chake”
Jamaa wakanifungua mikanda na kuninyanyua kwa nguvu na mmoja akanishika mkono wa kulia na mwengine mkono wa kustoto,tukatoka nje ya chumba na kuwaona baba na watu wake wakija kwenye ofisi ya daktari na ikanilazimu nianze kuchetuka kama kawaida huku nikijirusha rusha juu na kuwafanya majama hawa kutumia nguvu zaidi katika kunibana,Baba akawaomba wasimama kisha akasimama mbele yangu na kunitazama kwa muda huku akijikaza kuto kulia.Akanikumbatia na kuwaruhusu jamaa wanipekeleke wanapo nipeleka
Nikaanza kupata woga kwa maana kila nilipo pita vichaa wakiume walianza kushangilia huku wengine wakiwa na sura za ajabu ajabu
“Sasa dokta naye tulimuuliza anatatizo gani huyu hajatujibu sasa tutampeleka kwenye wodi gani?”
“Kwa jinsi ninavyomuona tumuingize wodi namba nano itamfaa”
Jamaa wakashauriana na kweli wakaniingiaza kwenye wodi yenye vitanda vingi na vingi vinawatu ambao kwa muonekano wao ni vichaa walio pitiliza na mbaya zaidi wengi wana miili mikubwa kupita maelezo kiasi kwamba kila nilipo pita walinitazama kwa macho makali.Jamaa wakanionyesha kitanda changu kisha wakatoka kwa haraka huku wakionekana kujishuku.Majamaa matatu yakasimama kwenye vitanda vyoa na kuanza kupiga hatua za kunifwata kitandani huku ikinguruma kama mimbwa inayo gombania mke mmoja,mapigo ya moyo yakazidi kunidunda huku kijsho kikinimwagika kiasi kwamba ubabe wangu wote ukaniishia
Majaa yakanitazama kwa muda huku yakinguruma na yakaanza kunishika shika kichwa changu huku kila mmoja akitaka nimtazama yeye,Nikastukia kofi moja takatifu likitua kwenye sikio langu na kusababisha uwezo wa kuona vizuri ukakata na kuona vitu vyenye alama kama nyota nyota vikielea angani kiasi kwamba nikajikuta nikiona giza lililo endana na ukungu.Nikastukia nikiwa nimelala chini sakafuni wala sikujua nimeshuswaje kwenye kitanda.Makelele ya vichaa wengine yakazidi kunichanganya kiasi kwamba nikawa sielewi nini cha kufanya.Kipigo kutoka kwa haya majamaa ambayo yanaonekana ni mababe kwenye hii wodi kikanifanya nijikunyate huku nikilia kwa uchungu.Nikaingia chini ya uvungu wa kitanda ili kujinusuru kwani inadi ya vichaa wanao nishambulia ikaongezeka,Nikastukia nikivutwa miguu yangu na wakaanza kuniburuza huku wakishangilia kwa nguvu
Maumivu makali yakazidi kuniumiza kiasi kwamba nikajuta kwa uamuzi nilio uchukua.Wakanigongesha gongesha kwenye kwenye vitanda kisha wakanilaza kwenye kordo iliyo tenganishwa na vitanda na wakanizunguka huku wakinitaza na vijamaa viwili vyembaba vikapanda juu ya vitanda nawezao wakaacha nafasi na sikujua wanataka kufanya nini,Nikastukia wa kwanza akijirusha na kunifanya nimkwepe na akapiga kichwa kwenye sakafu na kutulia tuli.Wa pili akafanya kama alivyo fanya mwenzake na akanitulia kwenye tumbo na kunifanya nitoe ukulele mkali wa maumivu huku kicha kizima kikiwa kimejaa manundu ya kipigo nilicho kipata
Nikastukia wakianza kunikojolea huku wakicheka kwa furaha na kupeana mikono na kunifanya nizidi kulia kwa uchungu japo hasira imenipanda sikuwa na uwezo wa kufanya chochote dhidi yao.Wakatawanyika na kuondoka kila mmoja akarudi kawnye kitanda chake na wakaniacha nikiwa nimejilaza chini pamoja na kale kajamaa lalicho nirukia.Nikaanza kujivuta taratibu hadi kwenye kitanda changu huku mwili mzima ukiwa ninanuka mikojo pamoja na kuvimba juu na nikakaa na baada ya muda mlango ukafunguliwa na wakaanza kutoka mmoja baada ya mwengine.Akachugulia daktari mmoja na kutuona ndani ya chumba tumebaki wawili na baada ya muda wakaingia madaktari wanne ambao wawili wakanifwata mimi na wawili wakaenda kwa kale kalicho zimia
“Huyu ni mgeni eheee?”
“Naona”
“Ahaaa wageni huwa wanapata shida sana”
“Kweli kwa maana walivyo mfanya mmmm ni zaidi ya maumivu”
Madtari wakaendelea kuzungumza huku wakinihudumia na kuniweka kwenye machela na kunihamisha kwenye na kuniingia kwenye chumba cha matibabu.
Ndani ya siku nne nikawa nimepona vuzuri japo sio sana kwani kuna baadhi ya sehemu zinamaumivu kidogo.Nikarudishwa kwenye wodi ambayo nilitembezewa kichapo na nikaanza kazi yangu rasmi ya kumtafuta Sheila kwenye kila sehemu ya hospitali hii,Ndani ya siku mbili sikuweza kumuona Sheila na sikujua ni wapi alipo,Nikaanza kuzoeana na vichaa kadhaa ambao ni wanyonge kama mimi kwa maana jinsi watu wanavyo ishi kibabe kwenye hii hopitali inasababisha kuwemo na mgawanyiko wa vichaa wababe na vichaa wanyonge.Wakati wa kuoga ukawadia na kama kawaidi kila wodi ina mabafu yake ambayo muda wa kuoga unapo wadia ni wote tunatakiwa kufanya hivyo.
Nikatafuta sehemu isiyo na mminyano na kusimama na kuwatazama jinsi vichaa wengine wanavyo minyana kwenye kuoga.Wakaoga wote kisha wakatoka na mimi nikanza kuvua nguo zangu na kabla sijamaliza kuzivua akaingia lile jijamaa ambalo lilinizaba makofi pamoja na wezake na baada ya kuniona likaanza kunguruma na kuanza kunifwata na nikajiandaa kwa chochote atakacho hitaji kukifanya kwangu mimi.Likanisimamia mbele yangu huku likinitazama kisha likanitisha kama ninataka kunipiga kofi na kujikuta nikiinama huku mikono yangu nikiwa nimeiweka kichwani kuziba uso wangu na nikastukia likaanza kucheka sana hadi likakaa chini kwa kucheka na ikanibidi na mimi kuanza kucheka
Hata hamu ya kuoga ikaondoka na kujikuta nikivaa nguo zangu na kutoka bafuni.Kama kawaida muda wa michezo ukawadia na kila kichaa anaye penda mchezo wake anakwenda kwenye eneo lenye kiwanja cha mchezo wake.Nikaanza kuzunguka zunguka nikaangalia jinsi vichaa wanavyo fanya mambo ya ajabu kusema kweli inahitaji moyo wa uvumilivu kuishi nao kwa maana kama akili yako ni nzima basi ukishindwa kuvumilia unaweza ukawaambia madaktari kuwa umepona.Nikakuta wasichana watatu vichaa wakiwa wamekaa chini wakichora chora na katika kuwachunguza vizuri nikamuona Sheila akiwa katikati yao
Na mimi nikajisogeza karibu yao na kukaa huku nikimtazama Sgeila jinsi anavyo chora chora cini kwa kkutumia kijiti huku akifuta futa.Wezake wakasimama na kuondoka zao na akabaki peke yake.Sheila hakuinyanyua sura yake kunitazama na akazidi kuchora chini huku akikigandamiza sana kijiti chini na akiwa anaonekana kama anahasira kali.Machozi yakaanza kumwagika kiasi kwamba akafuta alicho kichora kicha akaanza kuandika herufi moja moja kwa uchungu
{I…….L…..O…….V…….E}
Nikabaki nikimuangalia huku kwa mbali na mimi machozi yakinilenga lenga kwani afya yake imedhohifika sana isitoshe mwili wake umetawaliwa na makovu mengi sana ambayo yamemfanya azidi kuonekana mbaya.Akayafuta maandishi yake kisha akachora vikatuni viwili kimoja kikiwa cha kike huku kingine kikiwa cha kiume na akavipatia majina kwa herufi za mwazo ambacho kikatuni cha kike akakiandikia herufi kubwa ya ‘E’ huku cha kike akikiandikia kiherufi cha ‘S’.Hapo ndio nikashindwa kuzizuia hisia zangu na kujikuta nikimwagikwa na machozi na kumuona Sheila akiinyanyua sura yake tartibu na kuniangalia kwa muda kisha akairudisha sura yake chini na akanitazama tena kwa umakini huku akiwa kama mtu anaye jitahidi kuvuta kumbukumbu ya kitu fulani ila anashindwa kujua ni nini anacho kiwazia
“Sheila…..Sheila?”
Akaonekana kustustuka na akanikazima macho hadi akaanza kuniogopesha akajaribu kuzungumza ila akawa kama anashindwa.Aafuta vidoli vyake chini na kuandika maandishi yaliyo nistua zaidi
{MIMI SIWEZI KUZUNGUMZA NIPO SAWA SAWA NA BUBU}
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni