SORRY MADAM (49)
Zephiline F Ezekiel
6 min read
SEHEMU YA AROBAINI NA TISA
ILIPOISHIA...
Nikabaki mdomo wazi huku nikimuangalia baba kwa macho ya mshangao hulu machozi yakinitiririka.
“Eddy anacho kifanya yule mwanamke ni haki yake…..tangu mimi nimchukue sijawahi kufanya naye chochote….Ndio maana mara ya kwanza nikakuambia kuwa mama yako ni katili sana na mimi ninajua kila kitua anacho kifanya mke wangu”
“Oohh baba kwanini eeehee umemchukua wa nini sasa yule mwanamke?”
NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
Nilizungumza kwa sauti ya chini iliyo jaa unyonge wa hali ya juu
“Eddy nilihitaji kuficha aibu yangu kama mtu mwenye pesa zake”
Nikajukuta ninakosa la kuzungumza na kumfanya kunyanyuka kwenye kiti alicho kaa kilichopo pembezoni mwa kitanda changu cha hospitali kisha akanifwata kwenye kitanda nilicho kaa kisha na yeye akakaa
“Eddy nakuomba unitunzie siri hii ambayo sipendi mtu yoyote aijue zaidi ya yako wewe na yule mwanamke”
“Nitakutunzia baba yangu lakini nakuomba yule mwanamke aondoke pale nyumbani”
“Eddy siwezi kuondoka kwa maana atanichafua sana kwani siri yangu sio hiyo niliyo kuambia”
“Kwani kuna siri nyingine zaidi ya hiyo?”
“Ndio”
Ikanibidi nikae vizuri kitandani nimtazame baba huku nikiwa na hamu ya kusikiliza ni nini anaco taka kuniambia
“Kipindi ambacho nilichomwa sindano ya sumu madaktari wakanitoa sehemu zangu za siri ili kuepuka kupatwa na ugonjwa wa kansa…..ila wakanishauri kitu ambacho sikuweza kubisha kwani ningekataa nisinge weza kuwa hai hadi leo”
“Kitu gani hicho?”
“Wakalinipandikiza sehemu za siri za jinsia ya kike kwahiyo nipo sawa na mwanamke……”
Moyo wangu ukapiga PWAAaaa huku macho yangu nikihisi yakitaka kunichomoka usoni kwani katika maisha yangu sikuwahi kusikia kitu kama hichi ambacho baba yangu mzazi ndio ananiambia.Kulia ninatamani kuzungumza ninashindwa nikawa kama nimegandishwa kwenye Tv.Mapigo ya moyo yakaanza kupiga kwa nguvu kiasi kwamba moyo ukaanza kuniuma
“Eddy…..Eddy”
Baba aliniiita kumsikia ninamsikia ila kuitikia nikajikuta nikishindwa kwani kuna kitu kimenikaba koo kiasi kwamba hata kufumbua mdomo ni shuhuli pevu kwangu.Akaingia nesi akiwa ameshika kisahani cha bati huku kikiwa na vichupa pamoja na bomba la sindano hadi anaviweka juu ya meza ndio kidogo nikaanza kurudi kwenye hali yangu ya kawaida.Baba akanyanyuka na kutoka nje ya chumba na ni nikabaki na nesi na akaniomba nilale kifudi fudi na akanichoma sindano ya kutuliza maumivu kabla hajatoka nikamzuia
“Ehee”
“Kuna dada mmoja nilikuja naye anaendeleaje?”
“Yupo vipi vipi?”
“Amekondeana kidogo na mwili wake kidogo umejaa makwaruzo”
“Ahaa…yule anaendelea vizuri tuu japo kidogo madaktari wanadai kuwa amepoteza kumbukumbu zake”
“Eheee haya asante”
Nesi akatoka na kujikuta akili yangu ikikosa hata cha kufikiria na ndani dakika kumi nzima sikuweza kuwaza kitu chochute.Nikajinyanyua kitandani na kuufungua mlango wa chumba na kuchungulia nje na sikumuona baba wala walinzi wake ambao aliwaacha nje.Nikatafuta sehemu yanye viti vya watu kupumzika nikapumzika huku mara kwa mara macho yangu yakielekea mlangoni mwa chumba changu,Nikamumba jamaa mmoja gazeti lake baadaya kuona taarifa ya michezo iliyo nivutia juu ya timu ya brazili kupigwa goli saba kwa moja na wajerumani.Kidogo akili yangu ikaanza kuchangamka kila nilipo yatazama makatuni yanayo fanana na wachezaji wa kibrazili yaliyo chorwa kwa utaalamu mkubwa ambao mtu ukiyatazama lazima ucheke
“Ndugu mbona unacheka?”
“Ahaa ni hawa makatuni walio chorwa humu kwenye hiili gazeti ndio wananifurahisha”
“Ahaa”
Nikiwa nineandelea kusoma gazeti nikamuana jamaa aliye valia nguo za udaktari akiingia kwenye chumba changu na kwa haraka kumbukumbu ya wale watu walio mteka mama ikanijia kwani kichwa chake amanyoa upara na nimweusi sana.Akakaa ndani kwenye chumba kama dakika mbili kisha akatoka huku macho yake yakitazama huku na huku na ikanibidi kwa haraka nipandishe gazeti juu na kuiziba sura yangu.Nikajikaza nisitetemeke kwa woga ili jamaa mwenye gazeti lake asigundue kitu chochote kinacho endelea
“Hembu ninaomba gazeti hilo”
“Ehee”
“Naliomba mara moja kuna namba ya simu nimeiandika kwenye moja ya kurasa hapo sasa sijajua ni kurasa ipi niliiandika”
Jamaa akazidi kunichanganya kiasi kwamba nikajikuta nikiling’ang’ania kwama langu hadi jamaa akaanza kunishangaa.Nikachungulia na kumuona jamaa akizungumza na mmoja wa manesi nahisi anamuuliza ni wapi nilipo na kwa ishara nikagundua nesi alimjibu kuwa hajui ni wapi nilipo kwenda kisha jamaa akaondoka kidogo nikashusha pumzi na kumpa mwenyewe gazeti lake huku nikinyanyuka nikilichungulia jijamaa na nikamshuhudia akijichanganya kwenye watu wanao toka nje.Nikaanza kupiga hatua za kwenda kumtazama ni wapi alipo elekena nakumkuta akizungumza na mwanamke mmoja ambaye nikamtambua kuwa ni Emmy
Wasiwasi ukaanza kunijaa kiasi kwamba amani ikatoweka moyoni mwangu kwani sikujua wamejuaje kuwa mimi nipo hapa kwenye hii hospitali.Wakaendelea kuzungumza kisha wakaanza kupiga hatua za haraka kurudi ndani.Nikajificha kwenye ya ukata na wakapitiliza na wote wakaingia kwenye chumba changu na baada ya muda wakatoka na kila mmoja akaenda upade wangu huku Emmy akija upande wangu na macho yake yakawa na kazi ya kuwachunguza watu waliomo kwenye sehemu za kupumzikia.Nikaanza kupanda ngazi za kwenda gorofani na kwabahati mbaya Emmy akaniona na ikanilazimu niweze kuongeza mwendo wa kupandisha ngazi na yeye akafanya hivyo hivyo.
Nianza kukimbia kwenye kordo iliyo ndefu na yenye vyumba vingi na sehemu hii haina watu kabisa na Emmya naye akazidi kuongeza mwendo wa kukimbi na kwabahati mabaya mbele yangu ndipo mwisho mwa wa ukuta na hapakuwa na sehemu yoyote ya kukunja zaidi ya vyumba vilivyopo pembezoni.Nikashika kitasa cha chumba kimoja na kukuta kikiwa kimefungwa na ikanilazimu kukimbilia kwenye chumba cha mbeleni ambacho ni cha mwisho kwenye hii kordo na kwa bahati nzuri nikakuta kipo wazi na kitu cha kwanza kukiona ni bomba la chuma linalo tumika kuning’inizia dripu lililo anguka chini huku pembeni kukiwa na mgonjwa akiwa amemelala sakafuni huku kichwa chake kikiwa kimefunikwa na shuka.Nikaliokota bomba na kuchomo kipande kimoja na nikajianza kwenye mlango.
Taratibu mlango ukaanza kufunguliwa huku mdomo wa bastola ukiwa umetangulia mbele.Kwa haraka nikaipiga mikono ya Emmy kwa kutumia bomba na bastola yake ikaanguka pembeni,nikarusha bomba ili limpiga usoni ila akaikwepa na sikujua amelichukuaje chukuaje mikononi mwangu na nilicho kistukia mimi ni mikono yangu ikiwa haina chochote.Ikawa ni kazi ya mimi kuanza kuyakwepa mabomba anayo nirushia japo kuna baadhi yalinipata vizuri ila nikajikaza na nikabahatika kumpiga ngumi ya pua na kumfanya ajishike pua na ikawa nafasi yangu kumshambulia kwa ngumi za fujo amabozo mara nyingi tunaziita ni ngumi za mtaani kwa maana hazina mfumo maakumu
Emmy akashindwa kuhimili mashambulizi yangu kiasi kwamba akaanguka chini na nikaendelea kumshindilia magumi mfululizo yalio changanyikana na uchungu kwa uzalilishaji walio ufanya juu ya mama yangu
“Yupo wapi mama yangu?”
“Yupoo Yuupo?”
Nikaishusha ngumi kwa kasi kabla haijafika usoni mwake akaniomba huku machozi yakimwagika na damu zikimtoka kwenye maeneo ya kwenye jicho.
“Usinipige usinipige Eddy,Mama yako yupo hapa hapa Afrika kusini?”
“Eneo gani?”
“Kwenye hii hii hopitali ika kwa chini ndipo kuna handaki…”
Nikashtukua kitu kizito kikitua kichwani kwa nyuma yangu na nikaanguka pembeni na macho yangu yakaanza kuingia ukungu na kwa mbali nikaliona jinamaa lenye upara likiwa limesika bomba nililokuwa nimelitumia kupambana na Emmy na nikashuhudia akitoa bastola yake na kuikoki na macho yangu yakafumba na sikujua ni nini kilicho endelea
Nikaanza kusikia kwa mbali sauti ya vyuma vikigogwa kila nilipo jaribu kufumbua macho kutokana na ukungu ulio tawala kwenye macho yangu,nikatingisha kichwa ili kuyaweka macho yangu sawa ili kuweza kuona kitu kilichopo mbele yangu,Nikashuhudia watu wengi wakiwa wanaendelea na shuhili za utengenezaji wa magari yaliyo aribika.Nikasimama na kuhisi maumivu kwenye kichwa changu na nikajaribu kupiga hatua mbili mbele na nikastukia kitu kikinizuia kwenye mguu na nilipo chunguza vizuri nikagundua ni mnyororo ndio unao nizuia na umefungwa kwenye mguu wangu wa kuliaa.Hakuna aliye shuhulika na mimi na kila mmoja akawa anaendelea na shughuli yake na kila nilipo jaribu kumuongelesha aliye pita karibu yangu hakunisemesha kitu cha aina yoyote
Nikaaendelea kulichunguza eneo hili na kugundua ni gereji kubwa kwa maana kila eneo limejaa magari yanayo tengenezwa na yaliyo na tayari kwa matumiazia.Baada ya muda watu wawili wanye vifua vikubwa wakanifwata sehemu nilopo na kunifungua myororo na tukaingia kwenye kitorori kinacho pita kwenye reli na tukaondoka na kuondoa kwenye eneo tulilopo huku tukupita kweye miaamba iliyo pasuliwa na sikujua ni wapi wanapo tupeleka na kila nilipo waomba wanieleze ni wapi tunapo elekea wakabaki wakinitazama huku kitoroli tulicho panda kikizidi kuongeza kasi.Ndani ya muda mchache tukafika sehemua ambayo nikakuta watu wengi wakiwa matumbo wazi,huku miili yao ikiwa imedhohofika kiasi kwamba wanatia huruma na wengi wao wanafanya kazi ngumu za kupasu miamba na wamechanganyikana wanaume na wanawake.Miili ya watu hawa imechanika chanika kama ilivyo kwa Sheila
Wakanishusha kwenye kitorori na tukaanza kupandisha kwenye mawe yaliyo tengenezwa kama ngazi na kila nilipo pita watu nilio wakuta ndani ya hili pango kubwa wakawa na kazi ya kunisikitikia kiasi kwamba nikaanza kupata wasiwasi na walinzi waliomo kwenye hili pango wakawa na kazi ya kuwachapa kwa kutumia mkia wa taa kila mtu aliye jaribu kuniangalia.Tukaingia kweny moja ya kibanda kilicho jengwa na mawe na kukutana na jitu lililo jazia mwili na akawaamrisha wanikalishe kwenye kiti na kuwaomba jamaa walio nileta kunitoa nje
“Eddy” aliniita na sikujua jina langu amelijuaje
“Umelijuaje jina langu?”
“Hahaaaa ni kitu rahisi sana kulijua jina lako kwa maana wewe tumekutafuta kwa muda mwingi sana hadi leo tumekupata kwangu ni furaha kubwa sana”
“Wewe nani na unampango gani na mimi?”
“Mpango wangu kwako ni ule”
Jamaa akanyoosha kidole kwenye kiio na kunionyesha watu wanaoendelea na kazi ngumu ya kupasua miamba kwa kutumia yundo huku wakiwa wamejaa vumbi jingi hata sura zao zikiwa hazionekanani vizuri.
“Kuanzia sasa wewe utakuwa ni mtumishi wa humu ndani”
“Wewe unaumwa nini hembu nirudisheni sehemu muliyo nitoa”
Jamaa akagonga meza yake na wakaingia majamaa nilio kuja nao kisha wakaninyanyua kinguvu na kunivua shati langu na kubakiwana suruali yangu kisha wakanitoa ndani ya ofisi huku wakiwa wemeibeba juu juu.Wakanikabidhi kwa askari mmoja ambaye anaonekana ndio mkubwa wa humu ndani na moja kwa moja askari niliyo kabidhiwa kwake akanipeleka kwenye mango jengine huku akiwa amenibebe begani
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni